Bibie King'asti angalia Wazungu wanavyojitangazia mambo ya Uchawi ingelikuwa huko kwetu watu wanamkamata na kumuuwa mchawi wakati ulaya mtuanajiona fahari kujitangazia mimi ni Mchawi tuache jamani mambo ya kuhisiana mtu mchawi ukiwa upo uchi nje ya nymba yako watu wakikuona usiku au asubuhi utaambiwa wewe ni mchawi kwa ushahidi gani jamani?Angalia website za kichawi za kizungu bonyeza hapa British Traditional WitchcraftFrom all your descriptions, wote ni mule mule and.you cant tell a difference?
Gosh!
Mkuu Jodoki Kalimilo Umezungumza vizuri ila umekosea kusema kuwa ( wale wanaotumia ramli uchawi) neno (Ramli) kuwa ni uchawi na (Ramli na Uchawi) ni vitu viwili tofauti kabisa.Neno Ramli ni neno la kiarabu kwa kiswahili ni mchanga wa
kutizamia mambo yako ya maisha au tunaweza kusema kupiga bao kwa lugha ya kiswahili sasa unaweza kujuwa
kutizamia kwa kutumia hiyo (Ramli) Kupiga Bao lakini ukawa hujuwi kufanya uchawi wala mambo ya uganga unaweza kuwa ni Mtabiri wa kupiga ( Ramli) lakini usiweze kutibu watu wala
kuroga watu .Na neno (Uchawi ) Uchawi kazi yake Mtu huwa anadhuru watu kwa huo uchawi wake mchawi hajuwi mambo ya Ramli wala mchawi
hajuwi kutizamia kwa aina yoyote ile Mchawi anachojuwa yeye ni kudhuru watu sasa usituchanganye kati ya mpiga
Ramli na mchawi ni vitu 2 tofauti kabisa.
Mkuu nivea mimi ni Mtaalamu na Mchunguzi wa Dawa za miti shamba ukija kwangu unaniambia Matatizo yako ninakupa dawa. Hiyo ndio kazi yangu mkuu nivea.Hahaha nilijua tu MziziMkavu hukosekani hii ni moja ya mada ambayo unawezatolea ufafanuzi kwa aslilimia mia,swali je unajihusisha nakimoja wapo?
Mkuu nivea mimi ni Mtaalamu na Mchunguzi wa Dawa za miti shamba ukija kwangu unaniambia Matatizo yako ninakupa dawa. Hiyo ndio kazi yangu mkuu nivea.
Bibie charminglady Kwa sasa mimi sipo Tanzania nipo nje ya nchi ukiweza wasiliana na mimi kwa njia ya Email nitumie barua ya Pepe Address yangu ni hii hapa fewgoodman@hotmail.comunapatikana wapi mkuu???
wewe ndye umesema kweliMganga wa kienyeji na mchawi ni sawa na Malaika na Shetani. Malaika ndie anaeweza kupambana na Shetani kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu. Vile vile Mganga wa kienyeji anaweza kupambana na Mchawi kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu.
Mganga yoyote ili awe mzuri zaidi lazima ajue mbinu za kichawi. Ili uweze kutibu ugonjwa , lazima uujue na ujue tiba yake. Hivyo basi, Mganga sio Mchawi, ila anaujua uchawi ili aweze kukabiliana nao.
Je Polisi na Wanajeshi ni Majambazi kwasababu tu wanajua mbinu za Majambazi na kutumia silaha za moto?.
Huyo mkaka alie kutibu kama yupo hai naomba nambaMkuu bornagain Mganga ambaye anayekwambia ukitaka mafanikio yako itabidi umuuwe mtoto
wako, mganga huyo kwangu mimi nina muita Mchawi sio Mganga mimi Babu yangu alikuwa ni mganga maarufu huko
kwao Uzaramuni hakuna mtu hata mmoja aliyesema kuwa babu yako aliwahi kuwaambia wateja wake Eti ukitaka kufanikiwa mambo yako lazima Umuuwe Mwanao hicho kitu kamwe sitoweza kukubaliana nacho huyo
atakuwa sio mganga bali ni Mchawi mganga kamwe hawezi kukwambia ukitaka kufanikiwa Umuuwe mwanao eti ufanikiwe Mganga
akisema hivyo mimi huwa ninamuita Mchawi sio mganga kazi yake ni kuwatibu watu maradhi na matatizo yao
sio kuuwa watu anaye uwa watu huyo sio Mganga huyo ni Mchawi. Kwenye Miaka ya 1980 mpaka 1986 mimi
binafsi yangu nilisha wahi kwenda kwa Waganga hapo Dares-Salaam zaidi ya Waganga 20 nilikuwa ninaumwa
maradhi ya ajabu Homa za mara kwa mara kichwa kisicho pona Moyo kwenda mbio kiuno na mambo mengine
siyawezi kuyataja hapa ni Siri yangu nilikwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kupima vipimo vyote yaani kupiga picha ya
EX-Ray,kupima mkojo na Damu hawakuona kitu ndio nikamuwa kwenda kwa hao Waganga na nilipoona mambo
mengi wanayoyafanya Waganga mengine ni ya ukweli na mengine ni ya uongo na nilijifunza mengi mpaka nlipona
nili Rogwa na kutupia pepo mbaya na nilimaliza Waganga mpaka akaja kijana mmoja kutoka Mwanza kunitibia
ndipo nilipo pona kwa hiyo nina wafahamu kwa undani baadhi ya Waganga wanatumia mbinu ili waweze
kupata pesa nyingi kwa wateja wao kwa mfano wewe unaweza kuumwa na kichwa tu sababu hupati usingizi
vizuri au una mawazo au una matatizo ya kutopata choo ukienda kwa mganga akikupigia Ramli kitu cha kwanza
atakuambia umerogwa na mtu wako wa karibu ukikubali hapo umeingia kwenye mtego wake kwa leo
ninakuacha hapo......