Kuna tabia zinakera sana katika jamii zetu

Kuna tabia zinakera sana katika jamii zetu

Unaishi wapi?...huku kwetu hata mboga pia tunaomba kwa JIRANI na sio tatizo
Hama bhana nenda kaishi kwa hao wenye migeti mikubwa na vibao vyenye tahadhari kali
 
Nijitathmini nini Sasa? Ni lazima kusalimia? tunapenda kukuza Mambo ambayo wala sio muhimu

kaka yangu Mtingijoli,nimekuelewa na naheshimu msimamo wako ni kweli jamii yetu ina tabia za ajabu moja wapo ni hili suala la salamu,ila nashindwa kuafikiana na ww kwa upande wa kazini...Tukumbuke kazini ni mahali nyeti na muhimu sana ili ufanikiwe kikazi ni vyema ukawa na ushirikiano mzuri na wafanyakazi wenzio,hata wale ambao hauko nao department moja..suala muhimu hapa ni kuthamin kazi uliyonayo na kujenga uhusiano mzuri na wafanyakazi wenzio salamu inahusika hapa I think it's a matter of attitude.
 
Tabia ya kukopa pesa kwa mtu halafu unajidai umesahau kama umekopeshwa miaka 3 inapita, mfyuuuuuuuuu!!!!!
 
80% ya mada yako ni kuchukia kuazimana vitu!!!

Lazma unakaa uswazi sana. Bado mnaazimana chilisosi, chumvi, pasi, ungo, ... dah!!!

Hahaaa.., maisha ya uswazi raha sana ukiyazoea! Hakuna stress wala complication!
Ukitaka kutumia vyako peke yako basi wapanga maeneo wanayoishi middle class vingenevyo hutoeleweka!
 
Kibongo bongo wengi tu huwawekea wenzao vifundo kwenye makoromeo hahaaaa yao bila sababu either, kwa kumhisi vibaya, kumuona ana ringa bila sababu, na ukimzidi mtu kitu nalo ni kosa.
Hilo la kusalimia ndo sijui wanaona ni nini kuna mtu alikua anauliza kitu baada ya kutoa msaada wakaanza kumshambulia mbona husalimii, sijui nini? Hivi hapa mjini utasalimia wangapi.
Na tabia ya jamii kutaka uishi wao wapendavyo na kupangia wengine life style. Kuna vtu vingi Jamii ibadilike sasa.

Bongo, tatizo uelewa wa wengi ni mdogo sana (niko tarari kusahihishwa ktk hili)!
Hii si ktk kuazimana vitu tu..., bongo ukimzidi watu kielimu, kimaisha n.k., tayari kwao huo ni uhasama/uadui!

Wale maadui watatu (Ujinga, Maradhi na Umasikini) bado umewakaa wengi kiasi cha kwamba ukitoka tu kimaisha inakuwa kama umejenga uadui kuanzia kwa ndugu, jamaa, marafiki n.k.

Tubadilikeni jamani, hizi roho za kwanini hazitufikishi popote zaidi ya kututia vijiba vya roho!
 
Bongo, tatizo uelewa wa wengi ni mdogo sana (niko tarari kusahihishwa ktk hili)!
Hii si ktk kuazimana vitu tu..., bongo ukimzidi watu kielimu, kimaisha n.k., tayari kwao huo ni uhasama/uadui!

Wale maadui watatu (Ujinga, Maradhi na Umasikini) bado umewakaa wengi kiasi cha kwamba ukitoka tu kimaisha inakuwa kama umejenga uadui kuanzia kwa ndugu, jamaa, marafiki n.k.

Tubadilikeni jamani, hizi roho za kwanini hazitufikishi popote zaidi ya kututia vijiba vya roho!

Ushaona jinsi watu waishio ughaibuni wanavyoandamwa humu?

Utadhani maisha ya hao waishio ughaibuni yanawahusu watu wanaowaandama.
 
Kuna vitu vingine watu wanajiendekeza tu kuomba wakati kuna mbadala.Mfano mtu ana shughuli yake anakuja kukuomba kamera na wakati angeita mpiga picha akampiga hata picha tano( kama ndo izo ana uwezo nazo.)Au mwingine anakuomba gari aende nalo club ucku na wakati angekodi tax au pikipiki kulingana na uwezo wake.

Ushauri wangu ni bora hata umwambie huyo muombaji kitu changu hiki kibovu siwezi kukuazima au kipo kwa flani.Ukiwa na kifua unamwambia live sikupi.
 
Hahahah ilinikuta hii

Nilikuwa nafanya ofisi fulani...asubuhi moja na hataka haraka zangu za kuwahi ile napanda ngazi tu nyuma wamama watu wazima wakaanza kunisema na kuniteta.... nikaamua heri nichelewa, nikaweka ustaarabu kwenye pochi nakuwarudia....nikawapa za uso za kutosha.

Toka siku hiyo ilibidi wawe wanatabasamu wanaponiona hata kama nipo mbali...hadi nilipoondoka


Hahaa umenikumbusha kuna ofisi kuna dada hana cheo chochote
lakini anaogopwa kupita maelezo sababu ya kuwapa watu makavu live
hata kama wamemzidi umri na vyeo wakiingia anga zake ni makavu live
yaani akipita utaona wamama wote kimyaa hata kama walikuwa wanapiga umbea
inachekesha sana ukiona live
 
lol...nimecheka hiyo ya "nikumbushe"kila nikitembelea home nakutana na watu wao wananikumbuka mimi nimewasahau basi nawaulizaga straight "hebu nikumbushe" wanakasirika sana kumbe ninakua nimewasahau kweli.

Ndo walivyo baadhi ya watu
ukiwaambia umewasahau tu kosa
 
teh teh teh...bwenga weeeee!.,we unajitosheleza?

unaweza sema kwa hekima sio kutusi watu ambao huwajui.sijajitosheleza lakini siazimi kitu kwa mtu na wala nafasi hiyo hakuna kwani hata jirani yangu simjui anafananaje.
 
No 3 ukiishi uswazi ukijifanya huazimishi watu vitu vyako basi hata msiba wanaweza kukususia

au ukawa wezi wanakuibia wewe tu

kuna mitaa uswahilini hadi wali wanaiba....linaibiwa sufuria la wali na jiko lake la mkaa...


Dawa ya yote hayo tafuta hela uhame tu mitaa hiyo.....
umeandika kitu nilichotaka kusema,
dawa ni kuhama maeneo hayo tuu maana ndo maisha yao hapao wewe hamia kule mnapoamka asubuh mnasalimiana kisha kila mtu na lake, mambo ya kukaa barazani hakuna.
Polee
 
kaka yangu Mtingijoli,nimekuelewa na naheshimu msimamo wako ni kweli jamii yetu ina tabia za ajabu moja wapo ni hili suala la salamu,ila nashindwa kuafikiana na ww kwa upande wa kazini...Tukumbuke kazini ni mahali nyeti na muhimu sana ili ufanikiwe kikazi ni vyema ukawa na ushirikiano mzuri na wafanyakazi wenzio,hata wale ambao hauko nao department moja..suala muhimu hapa ni kuthamin kazi uliyonayo na kujenga uhusiano mzuri na wafanyakazi wenzio salamu inahusika hapa I think it's a matter of attitude.


Asante, Nimekuelewa ndugu
 
unaweza sema kwa hekima sio kutusi watu ambao huwajui.sijajitosheleza lakini siazimi kitu kwa mtu na wala nafasi hiyo hakuna kwani hata jirani yangu simjui anafananaje.

teh teh teh teh...hujui kama kuna watu wanaazima vitu karne hii ya 21 maana hata jirani yako hujui anafananaje!...
Mbona wewe unadanganya watu ambao huwajui?!!
 
Umenikumbusha mkasa uliowahi kunikumba kisa kumwambia mtu nimekusahau!Wacha akanitangaze eti najidai,mtu unakuwa na mambo mengi kichwani na ushakutana na watu wengi ktk sehemu tofauti,inakuwa vigumu kumkumbuka kila mmoja ht km ni ndugu yako,watu wanabadilika,kuna kunenepa na kukonda,kukua na kuzeeka utamkumbuka yule ambaye kila siku mnaonana,hamjaonana century lbd tangu utotoni anategemea umkumbuke!
Yaani siku hizi naogopa ht kumwambia mtu nimekusahau nabaki kukisia tu cjui fulani! Khaaa kazi kweli kweli.
 
Uswahilini ndio wapi??

Hahahahaaaaaaaaaaaaaa hahahahahaaaaaaaaaaaa daaaah nimecheka kwa kweli...!

Ok,anyway uswahilini ni kule ambapo kuna vijumba vilivyo bananabanana na havikujengwa katika utaalamu, viwanja havijapimwa mtu anajijengeajengea tu bila utaratibu vichochoro ndo usiseme...,Kumejaa majungu fitina na Umbea..
Ukiamka asubuhi unakuta watu wamekakaa tu hawajishughulishi kazi kukalia majungu, umbea na fitina.

Mfano mzuri manzese,mbagala kwa bibi nyau, temeke uswahilini,vingunguti, Buguruni ndanindani n.k
 
Back
Top Bottom