Apologise lady
JF-Expert Member
- Sep 16, 2013
- 5,980
- 3,115
Habarini?
Jamani ukweli kuna tabia za watu zina kera sana, sijui nikukosa ustarabu, sijui ni ushamba, sijui nini ila zinakwaza sana.
Jamani ukweli kuna tabia za watu zina kera sana, sijui nikukosa ustarabu, sijui ni ushamba, sijui nini ila zinakwaza sana.
- Tabia ya mtu anakuja nyumbani kwa mtu(mgeni) lakini ni mjuaji hadi kero, ukigeuka kidogo tayari kaparamia vitu hata visivyomuhusu kama: simu, pc, flash n.k
- Tabia ya mgeni kila akija anapoondoka anaazima kitu na kuondoka nacho alafu harudishi ila akija anaazima kingine inanikera sana.
- Tabia ya watu kuazima vitu kama fagio la ndani, ungo, CD, pasi,chillsource, n.k inakera sana.
- Tabia ya mtu anaazima kitu unampa kwa moyo wote, baada ya siku unakuta kile kifaa chako kinaburuzwa na kuchezewa hovyo hovyo na watoto wake, yaani kimetupwa tupwa, inanikera sana.
- Hii ndio inakera sana, mtu anaazima kitu cha mtu cha thamani tena anapewa kikiwa kizuri lakini mtu harudishi hadi udai na siku yakukirudisha unaweza lia baada ya kukiona, unakuta kimerudi kimeharibika na kuchakaa, alafu yeye anaona sawa tu, inakera sana.