Habarini!
Poleni kwa mtikisiko huu wa korona na Mwenyezi Mungu atuepushe, amina! tuendelee kuchukua hatua stahiki tafadhali!
leo ni siku ya 3 kama sikosei nyimbo ya alikiba inatrend namba 01 views ni kama 1.4M. kuna mambo kidogo yananishangaza:
1. Kwanini views za huyu lazima mara zigande au zishushwe? tangu alipovunja rekodi 2017 na 'seduce me' ni kama kuna mtu 'asiyejulikana' anamfuatilia kwa karibu sana......alipojaribu kutoa mvumo wa radi 2018 kuna mambo kama hayo yalitokea.....zikisogea basi husogea taratibu sana. nina uhakika, siku tatu kitu kutrend namba moja kwa upande ule stori ingekuwa kubwa sana na views zingesogea kwa kasi mno. kuna nini?!!!!
2. Akitoa nyimbo watu humfuata sana na kujaribu kumponda kwa kila namna tofauti na wengine. alipotoa seduce me na wengine nao wakaachia muda huo huo ili kujaribu kuipoteza. alipotoa mvumo wa radi mtu fulani alisikika akisema, 'tunamkaushia ili ibume'.....baadae views zikaanza kuganda. ametoa dodo juzi, kuna mtu sijui meneja au prodyuza analeta vijembe na mafumbo eti 'kipindi hiki cha corona watu wanahitaji za kucheza na hatutaki maqaswida' sijajua ye inamuathiri vp na kwanini afuatilie. ukiacha hilo, kuna mtu alikuwa anatambulishwa siku hiyohiyo alipokuwa anazindua nyimbo yake. sijawahi kusikia alikiba akisema chochote kuhusu wao wanapotoa kazi zao au hata bila kutoa kazi zao zaidi ya kujaribu kujibu tu pale anapotajwa. humu leo umefunguliwa uzi ukisema, 'huyu ndo!' zimemwagwa sifa zake humo kedekede. thread ililetwa km jaribio la kutaka kupoteza habari za dodo!
3. Kuna ajabu gani ya kumtumia mobeto?!! eti nyimbo imepata umaarufu sababu ya mobeto. nikikumbuka mwaka jana alikiba alipofanya ziara kule tabora na umati ambao ulikuwa unampokea na kumsimamisha humo njiani, nabaki najiuliza hivi na hamisa mobeto nae ni hivyo hivyo? haya tufanye mobeto ni maarufu kuliko kiba, sasa kuna ubaya gani wa kumtumia mtu maarufu ili nawe upate umaarufu? kwani muziki si biashara jamani?!!! sasa mnataka amtumie joanah wa jf ili nyimbo yake iambulie 1k mwaka mzima?!!!
4. Kwanini watu wahangaike na mtu asiyejua kuimba/aliyeishiwa/aliyechuja kama inavyosemwa? ninapata hisia kuwa kuna mtu ana roho mbaya kwelikweli licha ya mafanikio lukuki aliyonayo. hapendi kabisa kuwaona wengine nao wakijipatia ugali wao. inawezekana yale malalamiko ya penseli yana maana kubwa sana!. hii ni hatari sana!
Many are the plans in a man's mind, but it's the God's purpose that prevails! tutajikuta tunaendelea kushangaa tu jamaa hapotei kama matamanio yetu yanavyotaka!
Poleni kwa mtikisiko huu wa korona na Mwenyezi Mungu atuepushe, amina! tuendelee kuchukua hatua stahiki tafadhali!
leo ni siku ya 3 kama sikosei nyimbo ya alikiba inatrend namba 01 views ni kama 1.4M. kuna mambo kidogo yananishangaza:
1. Kwanini views za huyu lazima mara zigande au zishushwe? tangu alipovunja rekodi 2017 na 'seduce me' ni kama kuna mtu 'asiyejulikana' anamfuatilia kwa karibu sana......alipojaribu kutoa mvumo wa radi 2018 kuna mambo kama hayo yalitokea.....zikisogea basi husogea taratibu sana. nina uhakika, siku tatu kitu kutrend namba moja kwa upande ule stori ingekuwa kubwa sana na views zingesogea kwa kasi mno. kuna nini?!!!!
2. Akitoa nyimbo watu humfuata sana na kujaribu kumponda kwa kila namna tofauti na wengine. alipotoa seduce me na wengine nao wakaachia muda huo huo ili kujaribu kuipoteza. alipotoa mvumo wa radi mtu fulani alisikika akisema, 'tunamkaushia ili ibume'.....baadae views zikaanza kuganda. ametoa dodo juzi, kuna mtu sijui meneja au prodyuza analeta vijembe na mafumbo eti 'kipindi hiki cha corona watu wanahitaji za kucheza na hatutaki maqaswida' sijajua ye inamuathiri vp na kwanini afuatilie. ukiacha hilo, kuna mtu alikuwa anatambulishwa siku hiyohiyo alipokuwa anazindua nyimbo yake. sijawahi kusikia alikiba akisema chochote kuhusu wao wanapotoa kazi zao au hata bila kutoa kazi zao zaidi ya kujaribu kujibu tu pale anapotajwa. humu leo umefunguliwa uzi ukisema, 'huyu ndo!' zimemwagwa sifa zake humo kedekede. thread ililetwa km jaribio la kutaka kupoteza habari za dodo!
3. Kuna ajabu gani ya kumtumia mobeto?!! eti nyimbo imepata umaarufu sababu ya mobeto. nikikumbuka mwaka jana alikiba alipofanya ziara kule tabora na umati ambao ulikuwa unampokea na kumsimamisha humo njiani, nabaki najiuliza hivi na hamisa mobeto nae ni hivyo hivyo? haya tufanye mobeto ni maarufu kuliko kiba, sasa kuna ubaya gani wa kumtumia mtu maarufu ili nawe upate umaarufu? kwani muziki si biashara jamani?!!! sasa mnataka amtumie joanah wa jf ili nyimbo yake iambulie 1k mwaka mzima?!!!
4. Kwanini watu wahangaike na mtu asiyejua kuimba/aliyeishiwa/aliyechuja kama inavyosemwa? ninapata hisia kuwa kuna mtu ana roho mbaya kwelikweli licha ya mafanikio lukuki aliyonayo. hapendi kabisa kuwaona wengine nao wakijipatia ugali wao. inawezekana yale malalamiko ya penseli yana maana kubwa sana!. hii ni hatari sana!
Many are the plans in a man's mind, but it's the God's purpose that prevails! tutajikuta tunaendelea kushangaa tu jamaa hapotei kama matamanio yetu yanavyotaka!