Kuna kitu hakipo sawa kwenye Ulinzi wa Rais

Kuna kitu hakipo sawa kwenye Ulinzi wa Rais

Sasa PSU si wapo chini ya TISS? Hata kazi za TISS huzijui? Moja kati ya kazi zao ni VIP protection, ni kama jeshini au polisi kuna mgawanyiko wa kazi, wengine trafiki, wengine wapelelezi na wengine kutuliza ghasia. Vivyo hivyo kwa TISS wapo undercover informers, walinzi wa viongozi, deep covers nk.
Una uhakika PSU iko chini ya TISS au umedhania. Sina hakika kama sisi tunaziunganisha, nilitumia comparison na nchi nyingine nyingi ambazo hutofautisha sana hivi vitengo hasa hizi ambazo hazijakomaa kiusalama na kiutawala. Nchi nyingi hazichanganyi ili mmoja akiharibu mwingine arekebishe.

Refer jaribio la mapinduzi nchini Uturuki dhidi ya Erdogan mwaka 2016. Presidential guard yao ilikutwa na washiriki 300 kati ya watu 2500 kwenye regiment wakati intelligence agency yao ndio ilizima mapinduzi. Hata wanamapinduzi walishambulia HQ za usalama wa taifa baada ya mkuu wa usalama kupata briefings mapema ikabidi wanamapinduzi watekeleze jaribio masaa matano kabla walipojua wameshtukiwa na hawana control uko.
 
Una uhakika PSU iko chini ya TISS au umedhania. Sina hakika kama sisi tunaziunganisha, nilitumia comparison na nchi nyingine nyingi ambazo hutofautisha sana hivi vitengo hasa hizi ambazo hazijakomaa kiusalama na kiutawala. Nchi nyingi hazichanganyi ili mmoja akiharibu mwingine arekebishe.

Refer jaribio la mapinduzi nchini Uturuki dhidi ya Erdogan mwaka 2016. Presidential guard yao ilikutwa na washiriki 300 kati ya watu 2500 kwenye regiment wakati intelligence agency yao ndio ilizima mapinduzi. Hata wanamapinduzi walishambulia HQ za usalama wa taifa baada ya mkuu wa usalama kupata briefings mapema ikabidi wanamapinduzi watekeleze jaribio masaa matano kabla walipojua wameshtukiwa na hawana control uko.
Nakubaliana na wewe kua nchi nyingi za wenzetu ulaya na wengineo wanatofautisha hizo taasisi mbili, hata USA kuna FBI, Secret services, na CIA japo hao walinzi wa rais wanatokea kati ya taasisi hizo za kiulinzi na usalama kuunda taasisi ya ulinzi wa rais

Kwa nijuavyo mimi wale walinzi wa PSU wanapitia vyuo vile vile vya TISS, wao wanapata mafunzo maalumu ya kiulinzi zaidi. Mfumo wa kuwa recruit ni ule ule wa maafisa wengine wa TISS. Hili linanipa uhakika PSU ipo chini ya TISS. na kwa nchi yetu idara ya usalama ina wajibu wa moja kwa moja kwenye usalama na ulinzi wa rais na serikali yake, hata muundo wake Wanaripoti moja kwa moja kwa 'sponsor' wao ambaye ni Rais.
 
Nakubaliana na wewe kua nchi nyingi za wenzetu ulaya na wengineo wanatofautisha hizo taasisi mbili, hata USA kuna FBI, Secret services, na CIA japo hao walinzi wa rais wanatokea kati ya taasisi hizo za kiulinzi na usalama kuunda taasisi ya ulinzi wa rais

Kwa nijuavyo mimi wale walinzi wa PSU wanapitia vyuo vile vile vya TISS, wao wanapata mafunzo maalumu ya kiulinzi zaidi. Mfumo wa kuwa recruit ni ule ule wa maafisa wengine wa TISS. Hili linanipa uhakika PSU ipo chini ya TISS. na kwa nchi yetu idara ya usalama ina wajibu wa moja kwa moja kwenye usalama na ulinzi wa rais na serikali yake, hata muundo wake Wanaripoti moja kwa moja kwa 'sponsor' wao ambaye ni Rais.
Kwa kifupi PSU ni TISS ila hao wapo kitengo cha ulinzi wa viongozi waandamizi
 
Hii ni tasnia maalum kwa watu maalum. Ulinzi wa Rais ni siri kubwa. Ulinzi wa kiongozi wa caliber yake huwa ni wa rings zaweza kuwa tatu mpaka nne. Ring ya ndani walinzi huwa hawa display silaha zoa kama regime iliyopita. Hii unawezekana ni kubadili tu style ya ulinzi ambayo inaweza kuwa nzuri isiyo attract attention kubwa kwa watazamaji. May be comment ya huyu bwana ni crowding the president while disembarking from the plane mimi sio mtaalam wa haya mambo.
 
Tazama vizuri picha hii, Rais Samia akiwasili Dar Es Salaam mara baada ya kutoka Uganda.

Picha hii inaonyesha kuna mambo hayako sawa hasa kwa walinzi wa Rais. Wataalam watakuwa wamenielewa, naomba wahusika walifanyie kazi, tunampenda mno Rais wetu.
View attachment 1750281
BWANA asipoilinda nyumba wailindao wanafanya kazi bure. Yule aliyekuwa analindwa na brigade nzima kwa mitutu minene, vingora vya kutisha, msafara wa magari elfu.....yuko wapi.

Tanzania ni nchi njema sana kutawala, raia wake hawana noma mradi uwahakikishie usalama, amani na wale wakashida. Ukiwatendea vibaya Mungu wa mbinguni anakushughulikia.,,,,,ova and auti
 
Kwa kiasi nimepitia komenti za wadau hapa ka ilivyo kawaida yangu[emoji1787][emoji13][emoji13]. Nimejifunza yafuatayo [emoji116].
1.ukiwa unajua mambo kwa upana wake utaitwa mjuaji(kwa chuki binafsi)
2.watu huishi kwa mazoea na kukariri baadhi ya mambo kwenye mazingira yanayowazunguka
3.ukiwa unajua mambo mengi na yenys mantiki sana automatically utachukiwa.
Back to the topic
Hata kama mleta mada amebezwa kama ni mjuaji fulani hivi wa kujipendekeza uzuri mmoja ni kuwa wahusika naamini washapitia huu uzi na kuufanyia kazi .
 
Jana nilipoona video anashuka kwenye ndege nikaendelea kuamini ulinzi wake ni wa kawaida.

Rais anashuka kwenye ndege na watu kibao nyuma wanamzonga, sijui utaratibu wetu ukoje ila kwa wenzetu sijawahi kuona rais wa nchi yoyote anashuka ndege na nyomi kwa wakati mmoja. Anashuka au kupanda mwenyewe peke yake.

Rais anashuka wakati huohuo na mpambe wake anashuka mbio. Pale ilibidi mpambe atangulie kwanza afike, then utulivu kidogo rais ndio ashuke.

Kuna wale watatu waliovaa reflectors nyuma. Sijui ni walinzi au wafanyakazi wa uwanjani wanashangaa. Kama si walinzi hawakustahili kuzubaa pale.
Unawafundisha kazi wenye kazi yao!!?? Acheni ujuaji wana Jf
 
Tanzania na Afrika kiujumla kwenye ulinzi wa viongozi wetu bado tuko kishamba na kizamani. Ulinzi wa viongozi wetu umejaa mbwembe na ujinga wa kizamani sana. Hatujui kutofautisha kati ya ulinzi na mbwembe, au walinzi na wapambe au kulinda na kuzongazonga. Sisi bado tunaamini wapambe ndio walinzi, kuzongazonga ndio kulinda!

Mifumo ya kisasa ya ulinzi kidunia kwa viongozi imebadilika sana, sisi bado tunaamini ulinzi ni kujaza wapambe kibao kumzunguka rais, huku tukisahau wabambe hao hao sio watu salama sana kwa rais, adui anaweza kupenya na kuwa miongoni mwa wapambe hao hao!

Ngoja twende kwa mifano.
-Rais akiwa kwenye himaya yake (eneo lililoandaliwa na kikosi chake cha usalama kabla ya rais kuwepo eneo hilo), hakuna sababu ya wapambe au walinzi kumsogelea karibu hata mita mitano. Wakae mbali kabisa.

-Rais akiwa Ikulu, hakuna sababu ya walinzi au wapambe kumsongasonga.

-Rais akiwa eneo la kiitifaki chini ya protokali mahususi (mfano bungeni, kwenye mikutano ya wakuu wa nchi, dhifa za kitaifa na kimataifa nk) hakuna sababu ya wapambe kumzonga zonga.

-Rais akiwa amezuka mtaani katika ziara binafsi ya kijamii 'iliyotengenezwa' hapaswi kuzungukwa na wapambe.

Mifano ni mingi, na wajuzi watakuwa wamenielewa, kama mtu huwezi kuelewa hilo basi jaribu kutazama namna wakuu wa nchi zenye vitisho vikubwa vya kiusalama wanavyolinda viongozi wao. Tazama USA, UK, Israel, Germany, France, Spain nk. utaelewa ninachokisema.
Huwezi kuwafundisha kazi wenye kazi yao, hizo story za movie baki nazo.
 
Umetoa Hoja nzuri na pia ni angalizo sahihi kabisa juu ya Mashaka yako makubwa.

Ni ukweli usiopingika kuwa kuna Udhaifu mahala na najua Watu wa PSU nao wameshauona pia.

Kifo cha ghafla cha Rais Dkt. Magufuli kimechangia sana Udhaifu huo ( huu ) unaouna.

Mara nyingi Rais ajaye akijulikana basi hata PSU nao huanza Kusaka Walinzi wake ambao ni Mahiri.

Kilichotokea kwa Rais Mama Samia ni kumtafutia Kwanza wa muda na wale Mahiri wakiandaliwa Kiitifaki.

Kwa Jicho la Kiulinzi na Kiujasusi binafsi sioni faida ya hawa Walinzi Wawili Wadada kutoka PSU.

Najua Rais Mama Samia hataki Kuwaacha kwakuwa katoka nao mbali hasa huyo Mmoja mrefu.

Siwadharau Wanawake na Mnisamehe, ila Rais Mama Samia alindwe hasa tu na Wanaume.

Sina shaka na Training za PSU, ila kwa Rais wetu Mama Samia kulindwa na Wanawake ni hapana.

ESCORT 1 hofu yako itatatuliwa upesi na tegemea kuona mabadiliko au ukaimarishwa zaidi.

Kuangalia sana Movies zao zaweza Kukufanya uyajue mengi hata kama ni Raia Mwema tu na hujaariwa nao.
Usichokijua: hao wanawake si walinzi ni wasaidizi wa Rais. Walinzi wako pembeni na mbali kidogo ya Rais.
 
Usichokijua: hao wanawake si walinzi ni wasaidizi wa Rais. Walinzi wako pembeni na mbali kidogo ya Rais.

Siku zingine usibishane na Mimi katika hii Medani kwani Wewe ni Mtoto mdogo ( Njuka ) sana Kwangu sawa?

Kwa Kukusaidia tu na huo Upumbavu wako ni kwamba Kiitifaki Msaidizi wa Rais ( Mpambe ) ni huyo tu ADC ( Aide de Camp ) ambaye huvalia Sare za Kijeshi.

Wengine wote wanaobakia hapo siyo Wasaidizi wa Rais bali ni Walinzi wa Rais kutokea Kikosi cha Ulinzi cha Rais cha PSU kilicho chini ya Idara ya Usalama wa Taifa ( TISS )

Na ili Kukuthibitishia hili ( hilo ) na uone kuwa hawa Wanawake siyo Wasaidizi wake ni kwamba Mheshimiwa Rais akitaka Msaada wowote hapo huyo Mpambe ( ADC ) wake tu ndiyo anatakiwa Kushughulika nalo, ila hao akina Dada huendelea na Jukumu lao Kuu ( Mama ) la Kiulinzi na ndiyo maana Wao wana Vifaa vya Mawasiliano Masikioni mwao vya Kuratibu Ulinzi mzima wa Rais lakini kwa huyo Mpambe ( ADC ) yeye hana.

Jikite sana tu kupata zaidi Maarifa haya.
 
..nasubiri kuona kama Mama Samia atavaa camouflage uniforms za jwtz kama mtangulizi wake alivyokuwa akifanya.
 
True hii biashara ya maonesho wakati kila sehemu anapoenda Rais panakuwa pameandaliwa na usalama umehakikishwa haina tija
 
Mimi sio mtaalamu, lakini ningependa niseme kitu kidogo, kama mtoa mada alivosema hapo juu, naunga mkono, wataalamu mtamuelewa, lakini kama nilivosema hapo mwanzo mimi sio mtaalamu, sina cha kusema.
Well said mkuu
 
Tatizo la ujuaji limekuwa kero sana siku hizi!
Watu wamekuwa wajuaji kupindukia hadi kero!

Kwa taarifa yenu ANAEMLINDA NI MUNGU! hata hawa walinzi waliopo ni Auxiliary security tu!
MNABOA SANA NA UJUAJI WA KIPUUZI
Wakuangalia Movie za kuigiza
😅
Naomba msamaha kwa niaba ya Wajuaji wote kwa ujumla wao.
 
Kwamba mbele yake anapaswa kuwepo bodyguard, nyumba yake na pembeni yake

Kama wame secure perimeter vizuri haina haja hiyo, maana ni old school style ya ulinzi

Sent from my M2004J19C using JamiiForums mobile app
 
Nakubaliana na wewe kua nchi nyingi za wenzetu ulaya na wengineo wanatofautisha hizo taasisi mbili, hata USA kuna FBI, Secret services, na CIA japo hao walinzi wa rais wanatokea kati ya taasisi hizo za kiulinzi na usalama kuunda taasisi ya ulinzi wa rais

Kwa nijuavyo mimi wale walinzi wa PSU wanapitia vyuo vile vile vya TISS, wao wanapata mafunzo maalumu ya kiulinzi zaidi. Mfumo wa kuwa recruit ni ule ule wa maafisa wengine wa TISS. Hili linanipa uhakika PSU ipo chini ya TISS. na kwa nchi yetu idara ya usalama ina wajibu wa moja kwa moja kwenye usalama na ulinzi wa rais na serikali yake, hata muundo wake Wanaripoti moja kwa moja kwa 'sponsor' wao ambaye ni Rais.
Naunga mkono hoja zako
 
BWANA asipoilinda nyumba wailindao wanafanya kazi bure. Yule aliyekuwa analindwa na brigade nzima kwa mitutu minene, vingora vya kutisha, msafara wa magari elfu.....yuko wapi.

Tanzania ni nchi njema sana kutawala, raia wake hawana noma mradi uwahakikishie usalama, amani na wale wakashida. Ukiwatendea vibaya Mungu wa mbinguni anakushughulikia.,,,,,ova and auti
Watu wangu huangamia kwa kukosa maarifaaa, haina maana tahadhari kutochukuliwa eti kisa BWANA anaulinda mji
 
Back
Top Bottom