Kuna kitu hakipo sawa kwenye Ulinzi wa Rais

Kuna kitu hakipo sawa kwenye Ulinzi wa Rais

IMG_5763.jpg

Huyu dada namuelewa sana...anaijua kazi yake vyema! Kongole nanii ...
 
Usiogope kusema,funguka hapa tujadili kwa maslahi mapana ya nchi na Rais wetu.
 
Jana nilipoona video anashuka kwenye ndege nikaendelea kuamini ulinzi wake ni wa kawaida.

Rais anashuka kwenye ndege na watu kibao nyuma wanamzonga, sijui utaratibu wetu ukoje ila kwa wenzetu sijawahi kuona rais wa nchi yoyote anashuka ndege na nyomi kwa wakati mmoja. Anashuka au kupanda mwenyewe peke yake.

Rais anashuka wakati huohuo na mpambe wake anashuka mbio. Pale ilibidi mpambe atangulie kwanza afike, then utulivu kidogo rais ndio ashuke.

Kuna wale watatu waliovaa reflectors nyuma. Sijui ni walinzi au wafanyakazi wa uwanjani wanashangaa. Kama si walinzi hawakustahili kuzubaa pale.
 
binafsi hilo nimeliona, sio hapo tu, ktk matukio mengi nimeona udhaifu.

inaonekana wazi kabisa ulizi wa Rais wetu kama vile hauko sawa(not organized),

either hakuna mawasiliano baina ya walinzi wao kwa wao sijui ni ugeni au nini?!

lkn kwa uelewa wangu mdogo sana, nijuavyo mimi Ulinzi wa Rais wa nchi yeyote ile lazima uwe well organized, wala sio jambo geni, tuliona ulinzi wa Hayati Magufuli ulikuwa sio tu tight lkn ulikuwua well organized.

Tunaomba Ulinzi wa Rais wetu Uwe makini kwa kiwango kinacho takiwa kulindwa AMIRI JESHI MKUU, inatia kichefu chefu na aibu kubwa inapo onekana KASORO KUBWA.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Tazama vizuri picha hii, Rais Samia akiwasili Dar Es Salaam mara baada ya kutoka Uganda.

Picha hii inaonyesha kuna mambo hayako sawa hasa kwa walinzi wa Rais. Wataalam watakuwa wamenielewa, naomba wahusika walifanyie kazi, tunampenda mno Rais wetu.
View attachment 1750281
Walinzi wapo wa kutosha tu,security details imekamirika,chini kila upande wapo TISS wawili,na hapo JNIA muda Raisi anaingia,hiyo sehemu inakuwa imejaa security kila kona mpaka vyooni,mpaka kwenye paa,eneo zima linawekwa chini ya ulinzi.
Raisi anaposafiri sio Swala la kushitukiza linapangwa na watu wenye weredi sana.
Ukitaka kujua weredi wa hao security nenda uhamiaji uone Ana Makakala anavyolindwa.
 
Back
Top Bottom