Kuna kiongozi yeyote wa BASATA ambaye ni msanii?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
879
4,109
Nikitafakari katika jicho la kiuchumi na kibiashara, nikitafakari katika jicho la roho mbaya, nikitafakari katika jicho la asiye na uchungu najiuliza watumishi wa BASATA ni wasanii au ni watumishi wa umma?

Naomba anayejua compositions ya watendaji wa BASATA atusaidie tujue may be tunaweza kutambua tatizo lao ni nini! Inaweza kutusaidia kujua kwanini msanii atumie mamilioni kufanya kazi yake wao watumie wino kuiweka Kalama kazi hiyo bila kumsikiliza wala kuhojiana naye.

Lakini itatupa nafasi ya kufahamu wapo kwa ajili ya wasanii au wapo kw ajili yao wenyewe na ofisi zao. Sijawahi kusikia wakisaidia msanii jambo lolote hata mawazo na mafunzo, sina taarifa za wao kwa namna yoyote kiuinua wasanii wala kuwapa connection nje ya mipaka yetu. Hawa kazi yao ni nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom