Kuna anayewafahamu vizuri ForePlan Clinic ya Dr. Mwaka?

Kuna anayewafahamu vizuri ForePlan Clinic ya Dr. Mwaka?

Huyu dk nasikia kazi yake kubwa ni kuongezea wanawake utamu huko chini kwa kokwa la embe na mgagani, hili la kutibu ugumba ni part time
 
Wazungu wameharibu akili za wengi kwa kukariri bila kufikiri. Simfahamu huyu anayeongelewa wala siwezi kutoa maoni yangu kama anaweza au la. Nitachangia kufuta ujinga wa kudhani kuitwa Dr. Lazima upitie shule zenye mfumo wa wazungu. Nitatoa mifano miwili tu. Hakuna hospitality yeyote inaweza kutibu jino zaidi ya kung'oa au kuziba. Waafrika nje ya mfumo wa wazungu wanatibu hata leo. Mkoa wa Tanga leo hii kuna watu wanaunganisha mifupa iliyovunjika na hospitali zikawaandikia kuikata maana hawawezi kuiunga. Jukwaa hili nina uhakika lina wapo wanaoweza kukiri haya.Hawa waitweje?

Panaitwa kibiboni mkuu,wagonjwa wanatoka hospital ya mkoa bombo wanakwenda kwa mganga wa kienyeji na wanapona
 
Jambo la msingi hapa ni kuwadhibiti hawa waganga na serikali kuhakikisha kwamba kweli tiba zao zinawasaidia wananchi na sio dili za kujipatia tu fedha.
Kuwa mganga wa mitishamba sio kosa, ukizingatia hospitali zetu za serikali ni kama majumba ya makumbusho..Huduma zao ni Duni mno. Nafikiri hili ndio tatizo letu kubwa.

Lazima tujiulize ni kwa nini wananchi wanakimbilia zaidi tiba mbadala?? Ni sawa na issue ya shule binafsi na zile za serikali.

You can not strengthen the poor by weakening the rich..
 
Mimi huwa sikubaliani sana na waganga wa mitishamba. Lakini si kwa sababu wanavaa makoti am kujiita kama unavyolalamika.

Utabibu siyo kuvaa makoti ishengom. n awala siyo kujjita jina au kupata degree. Utabibu ni uwezo wa kutibu wagonjwa na kuwafanya warejee katika afya yao sahihi.

Nilitegemea ungesema juu ya utendaji wake wa kazi kwamba anayosema anayafanya hafanyi. Ungetuambia kwa research kwamba umebaini hana uwezo wa kusaidia tusema matatizo ya uzazi ila anaongopa. nk nk. Au ungetuambia anayofanya ni scientifically disapproved AU ina madhara makubwa kwa mgonjwa kwa namna moja ama nyingine, au ungesema hafuati ethicks za tiba kwa abc.

Lakini ukisema anavaa makoti, anajitngaza, bila sababu za msingi, unaonyesha wivu wa kijinga. Matangazo ya makoti yanakuathiri nini wewe kwenye taaluma yako ama wateja wake?

Pengine labda kama hujui, tiba mbadala imepanda kasi baada ya hao unaowaita medical dr kuprove failures. Wemebaki na hayo makoti, na mashine za kupimia watu shingoni lakini hakuna tiba. Mtu yuko diabetic na wanajua halafu wanamtundikia drip za glucose. Hao ndio wanamwuliza mgonjwa anataka aandikiwe dawa gani wakati yeye hata anachosumbuliwa nacho hakijui zaidi ya maumivu; Hao wanaoitwa mgonjwa kazidiwa wodini wanasema "nisubiri nitakuja" halfu wanatoroka au kusema subiri dr wa zamu ijayo yeye muda wake umekwisha. Hao hao wanaotaka wapewe rushwa ili mgonjwa apate huduma za karibu n.k. Hao wanao prescribe wrong medicines and dose kwa wagonjwa wanaend up kufa, hao wanaoona wagonjwa ni tatizo badala ya ajira.

Wangeonyesha competitiveness kwa uhai wa wagonjwa, bila shaka watu wasingehangaika na tiba mbadala. Huji ni kwa kiasi gani imesaidia watu kipindi chote ambacho hakuna serikali. Ninamshauri regulator kuwawekea mazingira mazuri zaidi ya kazi na kuwapa support inayotakiwa ili huduma zao ziwe bora zaidi ili Watanzania wasife kwa kutegemea makoti.

WIVU WAKO WA KIJINGA USIOKUWA NA HATA SCIENTIFIC REASONS BAKI NAO KWENU.

TENA UMENIUDHI KWA SABABU KAMA VILE NAKUONA ULIVYOVIMBA ETI KWA KUWA NAYE ANAVAA MAKOTI MEUPE. UPUMBAVU. MASUALA YA KITAALAM HAYABISHANWI KIPROPAGANDA ishengom. Ukitenda mema hutapata kibali?

Mkuu Tabby, nimechukua tu sehemu uliyoongelea weakness za professional Mds umeandika ukweli mtupu maana bila hayo mapungufu watu wasingekimbialia kikombe cha babu au hao wengine, THUMB UP ila hayo mengine ya kum-attack muanzisha thread kama hayakustahili maana yanapunguza nguvu ya hoja uliyoielezea kwa kina juu ya mapungufu ya Mds
 
Acha mambo ya kimbea mtoto wa kike....ukishaona mtu amefanikiwa basi wew povu linakutoka maisha yako kuwa magumu sio sababu ya wew kukaza mishipa kutaka kuwaharibia wengine maisha yao waliofanikiwa...jitume sio kutokwa povu kwenye mafanikio ya wengine

Wewe ndiye dokta mwezi nini mbona unachachawa sana. Tulia ukamuliwe jipu
 
Doctor kikwete amesoma miaka mingapi ili aitwe dr?
!

Mkuu kuna tofauti kati ya dr wa kutibu watu na dr phd,wote wanaitwa dr. Kikwete ni phd,kina mengi na wengine.

Phd unaweza kutunukiwa kwa heshima kama ilivyo kwa kikwete au ukaseomea kama ilivyo kwa dr mwakiembe.

Dr wa kutibu watu lazima uende shule miaka kadhaa.

Sema tatizo siku hizi kujiita dokta hapa kwetu imekua kama fasheni,waganga wa kienyeji nao ni dokta na wengine profesa kama maji marefu.
 
Nadhani watu wanachanganya honorary doctorate, medical doctor na doctor of philosophy. Yeyote kati ya hao anatumia title ya Dr. Sasa sijui huyu Mwaka ana uDr upi kati ya hizo ila kama hana hata aina moja basi ni straight forward hafai kutumia title ya Dr. Tusipindishe maneno

Wewe TU ndio nmekuelewa... Hawa wengine naona wanajibu hoja kwa kejeli na matusi na ukosefu wa maarifa ya kutosha juu ya neno DR.
 
Ukiumwa unachotafuta ni kupona Mara nyingi hao madoctor fake inakuwaga plan B baada ya A kufeli nao Wanalijua hilo ndio maana ukienda huko huwezi kukosa sababu ya tatizo lako but all in all is KAMARI kupoa au kutopona,
 
Kilichomponza ni ile issue ya kudhamini wimbo wa diamond. ..

Ila kihalali ajiite mganga. ..jina la Dr. Awaachie wenzake.

Pia serikali isimamie afya za watu wake.

Kwani Dr kwa kiswahili anitwaje?
 
Hapa kuna watu kweli vichwa vyao vigumu ishengom amekuja na hoja ya maana kwanini aitwe doctor? Wakati yeye ni mganga wa kienyeji. Kuwa doctor lazima usomee kwa miaka 4 hadi 8. Lakini mganga wa jadi unapata maelezo ya kienyeji enyeji tu.
Udaktari ni nini?
 
Hapa tatizo ni lugha iliyotumika tu ajiite mganga wa Kienyeji basi watu wanatoka sana mapovu wakisikia Dr.Mwaka wanahamishia ubongo wao Moi au Aga Khan, huyu jamani udoctor wake kaupata Kienyeji enyeji koti lisiwachanganye hata wauza nyama wanavaa mbona.
 
Jaman wanajamvi,

Napenda kuuliza huduma za huyu bwana anajiita Dr. Mwaka kwa yeyote aliyewahi kutibiwa naye!Juzi nilimpigia simu akapokea mdada akasema nitume pesa ili huduma!

Je, huduma zake zikoje maana me nna tatizo la kutopata mtoto kwa muda mrefu!

kuna madam ninafundisha nae huku kijijini.yeye alikuwa na tatizo ujauzito ukitunga baada ya mwezi mmoja miwili unatoka wenyewe.lakini alipata msaada kwa njia ya cm.aliwasiliana na dk mwaka akatuma pesa kisha akatumiwa dawa na sasa ni mjamzito mwezi wa sita huu.

Lakini kwa usalama zaidi fika mwenyewe pale ilala bungoni maana isije ukawa umewasiliana na wahuni.

pia mwandishi wa huu uzi apunguze mihemko na kukurupuka.dr mwaka kashawasaidia watu wengi.
 
Back
Top Bottom