Kuna anaewafahamu sagaci research?

Aisee, Mimi ndio ile iliyoenda Mbeya. Wenzetu wanasoma wakiwa na age ndogo sana....sisi tukiwa na 25+ ndio tunaanza kutumikia ajira, hatari sana!.. Mtoto kama yule kutuelekeza sisi watu wazima hahahaa!, na hipsi zake
Ha ha ha na lips nyekunduu, kuna siku tulimtolea macho had akajishtukia
 
Halaf kuna co-ordinator wetu akapita na Tablet zote baada ya project aiseeee sisi wabongo bhana noma sana, akachange na namba kabisaaa
 
Ni wetu wa Arusha mkuu, yule jamaa alikuwa ninja, yaani alizikusanya zote,akahakikisha pesa tumelipwa halaf akapita hv
Dah!, walioenda Arusha karibia wote walikuwa marafiki.....nitakuwa namjua huyo. Mm yule wakwangu aliwarudishia.....jamaa alikuwa mstaarabu sana
 
wameniambia niende kwenye training ya siku mbill dar.je nauli yangu ya kunitoa huku nilipo to dar watanirudishia?
 
Nilifanya nao mwaka juzi Mbeya...kazi ni Ku collect data kwa kutumia Tablets 'GPS'... Kazi ya mwezi mmoja, niliachiwa tablet miezi sita baadae nikapigiwa simu kwamba wanaihitaji.....wakanifata Dom wakaniachia kama laki mbili then wakachukua chao....kazi yao ni ya luxury sana kama huta complicate.....usiwe muongo maana coordinates zinaaibisha. Mm niliitwa nikafanya interview Dar Oysterbay jioni nikaanza kazi wakatupeleka Sinza kwa mafunzo ya wiki moja then tukatawanywa mikoani kufanya kazi....wao walibaki Dar hotelini sisi mikoani, kila ukimaliza kazi jioni una sinc results then kesho yake unaendelea na kazi....tablet zina database imesetiwa tayari 'questionnaires' kwa kila eneo unalokusanya data. Kama huna kazi we nenda wanalipa vizuri tu, kwa USD.

Training kufanyika Sinza, hao hawana ela
 
kwa hiyo ili waonekane wana pesa walitakiwa wafanyie wapi?
Nakumbuka mwaka Jana kabla sijaacha kazi mahali Fulani, training zao zilikuwa zinafanyika Snow crest hotel Arusha, Mara Gold crest Mwz, Nashera Moro, etc ulikuwa ni mradi wa serikali magu akaingilia kati akaamuru semina na mafunzo yote yawe yanafanyika ofisini kwa kumbi za serikali....Mara ya mwisho kabla sijaacha kazi..tulienda fanyia ukumbini kwa mkuu wa mkoa mwanza ile semina....lakini pesa zikalipwa kiwango kilekile!..........huyu jamaa yetu naomba atujibu kwanza mm nilipotezea sasa nimepata nguvu upya....na pesa zilikuwa ndefu tu..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom