lucley
JF-Expert Member
- Jun 15, 2016
- 728
- 2,007
Ingawa ndiyo kwanza naanza maisha ila gari ni miongoni mwa vipaumbele vyangu pale 'mishemishe' zitapokaa vizuri. Kuna kipindi mzee wangu alikua anaumwa sana na safari za kwenda na kurudi kutoka hospital zilikuwa ni za kila siku, sio siri tulipata shida sana kwani tulikuwa tunatumia 35-40 kila siku za kukodi gari, bado na za kumlipa dereva na hali ilikua hivi kwa takribani miezi miwili. Sasa hivi 'mzee' amepata nafuu ameapa huu mwaka haumalizi lazima aweke hata 'babywalker' uani ili kupunguza karaha.