Jamani hatupaswi kuwa na hasira hapa bali nimepost kuwapa taarifa no matter nimetumwa au la! the issue is ni lichokisema ni kweli au nimetoa wrong habari? niwape habari zaidi ni kuwa baada ya selelii kuzomewa sana jana katika kikao cha tathmini jioni selelii amelalamika kwa viongozi juu ya hali hiyo hivyo yakatoka maamuzi kuwa ni marufuku kwa wananchi kumshangilia mgombea mmoja na yametoka maamuzi kuwa kuanzia leo mikutano isifanyike sehemu zenye mikusanyiko mikubwa ya watu, kwa maana hiyo mkutano wa kwanza wa leo umefanyika kata ya puge lakini nje kabisa ya kitongoji cha puge japo haijasaidia kwani watu wamekodi baiskeli( gana gana) kuufuata mkutano na hali iliyojitokeza jana imejitokeza leo pia japo kidogo imedhibitiwa na viongozi wa msafara kwa kumfanya Bashe awe mzungumzaji wa mwisho. huyo aliyesema yupo Nzega sina hakika sana na taarifa zake kwani kwa sasa tuna malizia mkutano wa Mwisho kata ya Magengati inayopakana na wilaya ya Uyui na watu wamemshangilia sana Bashe nipo kwenye msafara! mwenye swali aulize
By definition, mkutano ni mkusanyiko wa watu wengi. Sasa wanakwepa mikusanyiko mikubwa ya watu ili iweje? Hapa kuna doubts za kutosha kuhusu hizi taarifa unazozitoa.
Tamko kama hilo sidhani kama ni sahihi. Lengo la mikutano hiyo ni kumwaga sera kwa wapiga kura, sasa ukipeleka mkutano huo nje ya makazi/kitongoji unakwenda kuhutubia miti? Sometimes unapopika stori tumia basi akili kidogo maana siyo kila mtu atakubaliana na stori ambayo inaonekana ina elements za uongo/uzushi.