Kumekucha CCM, hii ni aibu ya mwaka

Kumekucha CCM, hii ni aibu ya mwaka

Huu ni mkutano wa ccm jioni hii Segerea mwisho,wamejikuta ni viongozi na wamama wa kuhesabu kama tunavyoona,viti vyote viko wazi pamoja na kupiga muziki kutwa nzima ya leo,Nyie watu someni alama za nyakati......

MPAKA TUNATOKA ENEO LA TUKIO HAKUKUWA NA MWANANCHI YOYOTE ALIE JITOKEZA ZAIDI YA VIONGOZI WA CCM NA WAKEZAO.

TIZAMA JUA LINAVYO SOGEA BILA MATUMAINI

Hata Ritz alishindwa kupeleka UDA kusomba watu? Majanga!
 
it takes empty brains to think insults can outweigh obvious facts. Nilikuwa nimelaa sasa nimeamka. Vipi, wajumbe hawajafika tu? Weka basi picha. Watakuja saa ngapi na saasa ni saa sita usiku?

What is the highest level of education completed by your father?
 
hiyo ID nimeitilia mashaka kitambo sana !

jana mtu mzima kaumbuka...alipost comment kwa jina lake halisi alafu akajichangaja akarudi kujibu comment ya BENSaanane kwa ID ya Imebidi. Hiyo thread hadi mda huu ipo na inachangiwa na magreat thinker lakini yeye Imebidi alipoona amejichanganya ajatia pua yake tena hadi leo
 
Last edited by a moderator:
Huu ni uongo mkutano ulikuwa saa 10 jioni ,picha umechukua saa 2asubuhi.

Yeye alikuwa anawahi kanisani akawahi kupiga picha hiyo saa 2.Wewe uliyepiga saa 10 wakati wa mkutano,tunaomba picha yako hapa tuamue.
 
nashukuru sana ila dhibitisha uongo wangu.
Mkuu Pisto Lero, asante. Nimetanguliza neno "too good to be true!", kwa vile ulicholeta ni picha, seeing is believing, yaani ukileta picha watu waone, kuona ni kuamini, na yale maneno yako yalioandamana na hiyo picha ni maneno ya "make believe!" kuwaaminisha watu humu kuwa sasa CCM ndio imechokwa kiasi hiki! kitu ambacho ni kweli CCM imechokwa ila sio kwa kiwango hicho cha totally empty seats kiasi hicho!.

Mtaji mkubwa wa CCM ni mtandao wake wa wanachama kuanzia mabalozi wa nyumba kumi kumi, mashina ya wakereketwa yanayohusisha wale ma joblesshata vibaka, matawi kila pahali, haiwezekani waitishe mkutano wa hadhara alafu wawe wachache kiasi hicho!. Kwanza wanachama wao tuu wa eneo husika wangetosha kujaza nusu ya viti!.

Thanks.
Pasco
 
Jamaa alipiga picha akiwa anjiendaa zake kanisani asbh anataka kudanganya watu,
 
Mbona hapo mapema sana cku ilikuwa mbichi sana wakati picha inapigwa aisee.....leta picha kuanzia yaa SAA nane mchana halo utajua uhalisia watu wanavyo nunuliwa au kuletwa kwa mafuso na mabasi nii wazee na majimamaa tuu na green guard yao
 
Zile Fuso za kubebea watu hazifanyi kazi pande hizo.
Naona segerea wanaanza kurudiwa na akili

Mimi kama mpiga kura wa jimbo la segerea pamoja na wananchi wengi sana wa jimbo hili tulishikwa na butwaa siku ilipotangazwa kuwa mshindi wa kiti cha ubunge ni mbunge wa sasa! Kwahiyo segerea tulishajitambua siku nyingi ipo siku KITAELEWEKA TU.
 
kiwango cha elimu ya baba yangu hakitakusaidia ila shule ameenda sana kuliko unavyojifikiria na kuona kuwa ukiandika kwa kingereza hapa jf ndo ujiko wengine tunakuona mburula tu jenga hoja zenye mashiko acha kutaradadi

I wasn't arguing with you.Ngorope.Stop reading into everything as if it's a formal debate.It's just the internet and it's a randomness forum on a world of warcraft website.If you want to act like an intellectual,this is not the best place to do it.
 
Mkuu big in, huyu jamaa ni kauzu sana hizi picha zinaonyesha kwanza kama ndio wamemaliza kuandaa kwa kuanza na hao wamama hapo chini kama vile wanabadilishana mawazo machache huku wakisubiri wageni wakuu, mbona sioni picha ya mgeni rasmi hapo, inaonyesha kwamba ndio wapo wanawasubiri,ccm inapendwa sana na watanzania wa rika zote ndio maana umeona wameandaa viti vya kutosha kwa umati mkubwa unaotarajiwa kuhudhuri, huyu pimbi mleta mada anakwenda kupiga picha wakati wa maandalizi kweli chadema kuna vijana wehu

Chama CCM namba moja
 
Sikuwepo kwenye tukio mkuu asubuhi umekunywa chai?
No, huwa nakula baada ya kuingiza siku and not before, nile na-celebrate nini...consumtion?
Ambayo ningekula walishaichukua kwenye mshahara wangu as income tax na kuipeleka kwenye posho na kubebea watu kwenye malori na kuwapeleka kwenye mikutano, kukodishia vipasa sauti bungeni.......!
 
zile fuso za kubebea watu hazifanyi kazi pande hizo.
Naona segerea wanaanza kurudiwa na akili
mkuu hujajua kuwa ni warushi? Hapa town ni ngumu mno kila mtu mjanja anajuwa kuwa atarushwa malipo yake
 
Back
Top Bottom