Kumekucha Bungeni - PICHA za wabunge wapya wakiwa Dodoma

Status
Not open for further replies.
View attachment 16689 CHENGE NA SITTA USO KWA USO.JPG
Hii picha uliyoonyesha siyo ya leo, hiyo ilikuwa kipindi cha kampeni.
 
Jamani mbona tunafundishwa kwenye dini kwamba tuwapende adui zetu? Sasa nyie mlitaka wasisalimiane eti kwa kuwa Chenge alimsema vibaya Six?

Hapana, kwa mawazo yangu ilikuwa halali kusalimiana na kuchekeana hata kama hicho kicheko ni cha kinafiki.

Tiba
 
sidhani km ni picha ya leo hii. inataka uvumilivu wa ziada kusalimiana kwa bashasha namna hii.
 
maendeleo Tanzania hayawezekani kwa sababu viranja wetu badala ya kufikiria kubana matumizi, wanafikiria kutanua. Hao wameenda kuendeleza huduma ya viburudisho. Subili mtaona!
 
Huyo wa pembeni ya Vicky Kamata ni kimwana wa kukata na shoka mbunge wa viti maalumu wa CCM Catherine Magige, aisee hivi ni macho yangu au ndio uhalisia naona Vicky kavaa kipete che kidole cha mguu baada ya dole gumba mweh
 
Hatimaye mpinzani wa Marehemu Amina Chifupa kaingia bungeni.... hope atafata nyayo za marehemu Amina.RIP Amina.
 
Naona Vick yuko na Mbunge mpya wa Umoja wa Vijana wa CCM, mkoa wa Arusha, Catherine Magige. Ama siyo yeye?

Kama ndiye magazeti ya Shigongo yalimripoti hivi:

Kwa mujibu wa vyanzo makini vya Risasi, baada ya Catherine ‘Catty’ kutwaa nafasi hiyo, anaingia bungeni kwa nia moja tu, kuhakikisha sera za CCM zinafanya kazi kwenye uwakilishi wake, UV-CCM.

“Yale ambayo uliwahi kusikia marehemu Amina Chifupa akiyafanyia kazi, atayachukua yote na kwenda nayo mpaka mafanikio yake,” kilisema chanzo chetu.


Mheshimiwa huyo mtarajiwa ambaye jina lake la utotoni ni Pamela inaelezwa kwamba, kifo cha Amina ndicho kilichomsukuma kuchukua maamuzi magumu ya kujitosa kwenye ubunge ili kuyaendeleza mazuri yote ya marehemu.


“Unajua marehemu (Amina) alikuwa mwanaharakati wa kufanya mapambano ya kutetea jamii, hasa vijana, kifo chake kikakatisha mafanikio yake, sasa ilikuwa lazima azaliwe Amina mwingine ili kuyaendeleza, ni Catty,” kilisema chanzo kingine cha Risasi.


Ikazidi kuwekwa kweupe kwamba, Catherine ambaye aliandika barua ya kuacha kazi rasmi katika Benki ya Barclays jijini Dar, Desemba 2009 (Risasi lina nakala yake) ili kujipanga na Ubunge na mapambano ya kutetea jamii husika huku ikielezwa kwamba siyo mtu wa kurudi nyuma katika harakati zake.


Chanzo hicho kiliendelea kuweka wazi kwamba, wako waliokuwa na dalili ya kumvunja moyo, “lakini pia wapo waliokuwa wakimtia moyo,” kilisema chanzo hicho.


Kwa mujibu wa ‘dokumenti’ zinazoshikiliwa na Risasi bila ridhaa yake, Catty alimaliza masomo ya Uandishi wa Habari mwaka 2004 katika Chuo cha Dar es Salaam (DSJ).


Hata hivyo, Risasi Jumatano lina ‘kopi’ za vyeti vyake vyote ambavyo havina chembe hata moja ya ‘kufojiwa’, kuanzia vile vya shule ambapo kuhusu elimu ya Sekondari, ilibainika kwamba, mwaka 1999 alimaliza Sekondari ya Mtakatifu Joseph (Saint Joseph), Ngarenaro, Arusha.


Mwaka 2004 alisoma Chuo cha Institute for Information Technology (IT), Dar kabla ya mwaka 2006 kusomea masomo ya Biashara (CBE), pia jijini Dar. Kote huko alitunukiwa vyeti vya kufuzu (Risasi lina nakala zote).


Mheshimiwa Catty ana mtoto mmoja wa kike aliyemzaa mwaka 2002, ambapo kwa mujibu wa chanzo chetu, kama kuna watu wanadhani ‘amefoji’ vyeti, ni vyema wakaenda kwenye taasisi hizo ili kupata ukweli, lakini kwake, “anaendelea kupambana kwa nafasi yake hiyo,” kilisema chanzo hicho.


Mheshimiwa Catty alizaliwa mwaka 1981 kama marehemu Amina huku wote wakipata mtoto mwaka 2002. Wana ‘nafsi’ moja ya kutumikia vijana huku wote kauli mbiu yao ikiwa moja, ‘mapambano mbele daima’.


Marehemu Amina alikuwa mbunge wa Viti Maalum kupitia Umoja wa Vijana wa CCM kati ya mwaka 2005-2007 alipofariki dunia. Alizikwa mkoani Njombe (wakati huo wilaya) kwenye Kijiji cha Lupembe ambapo ameacha mtoto mmoja.
 

Attachments

  • Catherine1.jpg
    Catherine1.jpg
    36.9 KB · Views: 595
Dah, mbichi huiva na mbivu huoza.
Sishangilii move hata moja ya ccm mie nazidi kuiombea imegeke megeke mpaka ishindikane kuiunga kwa supa glu
 
attachment.php


Naona yuko na Mbunge mpya wa Umoja wa Vijana wa CCM, mkoa wa Arusha, Catherine Magige. Ama siyo yeye?

Kama ndiye magazeti ya Shigongo yalimripoti hivi:

Kwa mujibu wa vyanzo makini vya Risasi, baada ya Catherine ‘Catty' kutwaa nafasi hiyo, anaingia bungeni kwa nia moja tu, kuhakikisha sera za CCM zinafanya kazi kwenye uwakilishi wake, UV-CCM.

"Yale ambayo uliwahi kusikia marehemu Amina Chifupa akiyafanyia kazi, atayachukua yote na kwenda nayo mpaka mafanikio yake," kilisema chanzo chetu.


Mheshimiwa huyo mtarajiwa ambaye jina lake la utotoni ni Pamela inaelezwa kwamba, kifo cha Amina ndicho kilichomsukuma kuchukua maamuzi magumu ya kujitosa kwenye ubunge ili kuyaendeleza mazuri yote ya marehemu.

"Unajua marehemu (Amina) alikuwa mwanaharakati wa kufanya mapambano ya kutetea jamii, hasa vijana, kifo chake kikakatisha mafanikio yake, sasa ilikuwa lazima azaliwe Amina mwingine ili kuyaendeleza, ni Catty," kilisema chanzo kingine cha Risasi.


Ikazidi kuwekwa kweupe kwamba, Catherine ambaye aliandika barua ya kuacha kazi rasmi katika Benki ya Barclays jijini Dar, Desemba 2009 (Risasi lina nakala yake) ili kujipanga na Ubunge na mapambano ya kutetea jamii husika huku ikielezwa kwamba siyo mtu wa kurudi nyuma katika harakati zake.


Chanzo hicho kiliendelea kuweka wazi kwamba, wako waliokuwa na dalili ya kumvunja moyo, "lakini pia wapo waliokuwa wakimtia moyo," kilisema chanzo hicho.


Kwa mujibu wa ‘dokumenti' zinazoshikiliwa na Risasi bila ridhaa yake, Catty alimaliza masomo ya Uandishi wa Habari mwaka 2004 katika Chuo cha Dar es Salaam (DSJ).


Hata hivyo, Risasi Jumatano lina ‘kopi' za vyeti vyake vyote ambavyo havina chembe hata moja ya ‘kufojiwa', kuanzia vile vya shule ambapo kuhusu elimu ya Sekondari, ilibainika kwamba, mwaka 1999 alimaliza Sekondari ya Mtakatifu Joseph (Saint Joseph), Ngarenaro, Arusha.


Mwaka 2004 alisoma Chuo cha Institute for Information Technology (IT), Dar kabla ya mwaka 2006 kusomea masomo ya Biashara (CBE), pia jijini Dar. Kote huko alitunukiwa vyeti vya kufuzu (Risasi lina nakala zote).

Mheshimiwa Catty ana mtoto mmoja wa kike aliyemzaa mwaka 2002, ambapo kwa mujibu wa chanzo chetu, kama kuna watu wanadhani ‘amefoji' vyeti, ni vyema wakaenda kwenye taasisi hizo ili kupata ukweli, lakini kwake, "anaendelea kupambana kwa nafasi yake hiyo," kilisema chanzo hicho.


Mheshimiwa Catty alizaliwa mwaka 1981 kama marehemu Amina huku wote wakipata mtoto mwaka 2002. Wana ‘nafsi' moja ya kutumikia vijana huku wote kauli mbiu yao ikiwa moja, ‘mapambano mbele daima'.


Marehemu Amina alikuwa mbunge wa Viti Maalum kupitia Umoja wa Vijana wa CCM kati ya mwaka 2005-2007 alipofariki dunia. Alizikwa mkoani Njombe (wakati huo wilaya) kwenye Kijiji cha Lupembe ambapo ameacha mtoto mmoja.


Tutamkabidhi Sugu ateme mashairi ili aingie tunduni kama Zitto kwa marehemu Amina ha ha ha

Btw nyimbo zake na kutumikia viongozi kumemsaidia kuingia mjengoni
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom