Kumbe wanaume ndio wapo hivi!?

Kumbe wanaume ndio wapo hivi!?

When I was a young me & my mama had a beef 20 years old kicked out on the street.

Pole sana ndugu yangu muombe mungu atakusaidia.
 
habari za maisha wana jf! naombeni kushare na nyie kuhusu hichi kitu kinachonikabili kwan naamini naweza kuelewa maisha jinsi yalivyo kwa kuwa kila siku tunajifunza.
Mimi nmeolewa miaka 6 iliyopita n am 31 now! mume wangu ndio kila kitu kwangu nampenda sana namhurumia namthamini pia...vile sina wazazi na nmezaliwa peke angu bas mume wangu nmemchukulia km ndo kaka, baba, mama, dada na kila kitu!
yaan jinsi nilivyo yaan simfichagi hata kitu ktk maisha yangu...furaha huzuni kila kitu anajua....napenda sana kupiga nae stori huzuni kila kitu anajua....napenda nmezoea kwake tukihuzuni kila kitu anajua....napenda nmezoea kwake weeeeee! nmezoea kwake kwan sinaga hata rafiki wa karibu sina mazoea na watu saaaanaaa..
Lakiniiii kitu ambacho kinaniumizaa bwana ni life style yy na bi mkubwa wake...mama ana tabu huyo cjapata ona! nmpenda sana lkn hapendeki! yaan sielewi ana tatizo gani....anamwekea mtoto ake biz sana kiasi kwamba ile furaha yangu nahisi inatoweka! na mtoto nae (mume) yy na mamake humuelezi kitu! anatupangia tuishi vile anavyotaka yy...sisi tukiplan kitu chetu yy anaenda anaharibu...hafla unamuona mtu hakupatilizi tena!
ni mda mrefu hili tatizo nmelifanyia uchunguzi nmegundua ni mama ndie anaharibu!
ni stori ndefu sana cpendi kuwachosha lkn sasaiv mume wangu sina stori nae....anaongea na mamake na sim mda wote! hata sokoni wanaenda wote napangiwa budget na ma mkwe tena anambia kabisaa nyanya hizo mwezi mzima!
kwanini imekuwa hivi ikiwa me ni mke nna kazi nna biashara najua kutafuta na mume wangu kipato chake kidogo sana! nikijaribu kumuuliza anakasirika ndo ctoongeleshwa cku tatu mtu kanuna!
mara mama mtu amfate mwanae asbh cjui wanaenda wapi!!? siambiwi wala siulizi! utakuta tumekaa watatu hafla wanaanza kunong'onezana...jamaniiii!!!??
baadhi ya watu wameshaiona hii picha naskiaga ckiaga tu wanasema mhhhh yule kaka anamsikiliza sana mamake naskia hata rafiki zake wanamwambia awe na msimamo na maamuzi yake...lakn wapiiiii!!!! jamani sina furaha...
hivi ndio wanaume wote walivyo au ni huyu wangu tuu?? naombeni ushauri kwani naumia sana hlafu nahisi kupoteza mapenzi na huyu mama...nmevumilia mengi sana kwake!
Duuh mnasema na watu
 
Hilo ni tatizo la wakwe wachawi anataka kumrithisha mwanae uchawi
 
kusema kweli sijamaliza kusoma mana maneno mengi nilikata tamaa ulivyosema kuwa mume wako umemfanya mama yako,kaka yako,dada yako, kwann usimfanye mama yako huyo mama mkwe wako?nijibu kisha mimi nimalizie kusoma ndio nikupe ushaur mwengine
 
Ni ngumu sana kuishi na mama anayeingilia Nyumba yako.
Na hapo hutaelewana na mumeo abadani hata akiondoka lazima amkotroo na simu.
Pole sana kwa maisha unayoishi, asipoangalia atapoteza mke huyo kijana.
 
Huyo jamaa kuna siku moja alikua anatupa mbinu za kuwapata mademu masta inster maana huwa wanatabia ukimutumia msga hawJibu sasa mkuu the boss siku moja akanipa mbinu za kuwapata na kujibu hizo msg nikazitumia zike mbinu zake alizonipa aisee sikuamini kuona staa mmujo akijibu coment zangu

Huyo jamaa ni hatar sana the boss we mkali maujanja yako yamefanya saiv nina namba ya nandy na shilole
Usiwe mnyimi wa fadhila mkuu! Share hiyo knowledge..! Nataka nikatest kwa bossylady!
 
Kwanini mkiolewa mnawachukia Wakwe zenu?
 
Kwanini mkiolewa mnawachukia Wakwe zenu?
Kwani kasema amemchukia??
Sawa sawa na wewe uoe halafu mke akalale chumbani kwake kwenye nyumba ya baba na mama ake. Ni sawa?? Msipende ku comment vitu Itakavyowakera watu hasa wenye kuhitaji misaada yenu. Sio kila post ni ya kujibu upuuzi buana. Jf ya siku hizi hii bana.
 
Mmh hapa unaweza uka-reply kitu ukaonekana wa ovyo!

Yawezekana kuna mahaba kati yao, si bure.
Eti jamani.... Nimeshangaa sana... How ever am a silent killer.. Nyanya za mwezi mzima natumia week mbili tatu afu nasema wazi kuwa zimeisha wakanunue zingine maana wao ndoto wanunuzi...eboooo
 
Duh!!! Pole sana.
I try to wear you shoes but cha kushoto kimenibana na kingine cha kulia kimenipwelepweta.
And you mention being an orphan, hadi chozi limenitoka.

My dear, talk to your husband. Muulize mnanong'onezana nini ambacho hamuwezi ongea mbele yangu? Na kwanini mama akuoangie nyumbani kwako?Si abaki mpenzi mtazamaji, Au mnanisema vibaya? Au pengine wanataka uondoke uende mbali uwaache wenyewe. Na hii hali ya kuwa yatima huna hata wa kumwambia. Aisee, pole sanaa. Tena sanaa.

Nimejisikia vibaya as if nimetendewa mimi.
Mkuu maserati. Kwenye ndoa sisi yatima hatuna cha kushika jamani acha tu.
 
Inaonekana wewe ndio mkosaji, unasemaje wanaume tupo hivo, hii inadhiirisha kua unachepuka au una experience na wanaume maana huwezi kutumia uwingi wetu kumzungumzia mumeo.....

But kwa maelezo yako, kosa kubwa ulilolifanya ni kuonyesha wazi upendo wako asilimia 100% kwamba bila yeye huwezi fanya kitu,,

Wanasaikolojia wanasema The only way to get some one attention is to stop giving them yours,, jaribu hii kitu, I mean na wewe punguza mihemko kulialia kwa sababu yake au kujionyesha kua umekufa umeoza, trust me ukifanya hivi lazima ataona tu kuna kitu ana ki miss na ataanza kujirudi,, kama hamna tatizo lotote lililosababishwa na wewe,, au pia kama source sio mambo ya watoto trust ni lazima atajirudi.

hivi mleta mada umemuelewa kweli?

Hajasema wanaume mpo hivyo ameuliza kama je wote mpo hivyo?

Pili shida hapa ni mama mkwe kamganda mwanae as ni mke mwenzie kumbe ni mama wa mume, hivi mpaka mama mkwe anapanga bajeti ya nyumba ya mwanae, sasa hapo kweli kuna mihemko gani kama sio wazima wa huyo mama, hata ingekuwa mimi ningewehuka huwezi kumpitia mume wangu asubuhi bila sababu, huwezi panga bajeti ya nyumba yangu, huwezi kuja kwangu tumekaa wote sebuleni unanong'onezana na mwanao as if mimi ni kinyago hapo mbele yenu
 
Ni ngumu sana kuishi na mama anayeingilia Nyumba yako.
Na hapo hutaelewana na mumeo abadani hata akiondoka lazima amkotroo na simu.
Pole sana kwa maisha unayoishi, asipoangalia atapoteza mke huyo kijana.
Angalau wewe umeona kitu ambacho wengi wetu hatukionagi. "Atampoteza mke wake", while wengi wetu tunaonaga ni mwanamke tu ndo ana cha kupoteza kwenye ndoa
 
Tatizo wew ulimpenda saana ,ukamwamini sana,ukaonyesha huna msaada bila yeye, yaani miaka sita ni michache sana bado mnasomana na kuna suala hujalitaja au sikusoma vizur issue ya watoto,kama huna mtoto du, itakusumbua sana.
Nashauri
1. Uanze maombi ya nguvu, Mungu atakufunulia namna ya kunusuru ndoa yako.
2. Endelea kuwa mwaminifu ukimvumilia huyo mwanaume ,mtatoka ktk hiyo hatua
3. Usimchenjie ma mkwe, endelea kumheshimu kwa kila hali.
Pole sana Dada,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom