Kumbe Tingatinga letu ni Manual na sio Automatic..!

Kumbe Tingatinga letu ni Manual na sio Automatic..!

IQ Warehouse

Senior Member
Joined
Apr 21, 2014
Posts
136
Reaction score
53
Sio siri kuwa mzalendo ni kitu kizuri, ila lazima kuwe na vipaumbele katika uzalendo. Si busara kua mzalendo katika kila kitu eti kwakua kimefanywa na wazawa.!

Katika uchumi kuna kitu kinaitwa "Scale of Preference" na kingine "Opportunity Cost".
Sidhani kama mapema hii Jembe lingepelekwa uwanjani kushangilia mpira na wakati sehemu kibao nchini bado hazijalimwa. Mstaafu angeenda uwanjani pekeake bila kubebelea jembe letu.

Jamani jamani ninasisitiza bado mapema!
Limelima Dar kidogo sana, Mikoani na Visiwani nako kuna magugu jamani!
Lingelima kwanza afu wakati wa kusubilia mavuno ndo wangeenda nalo viwanja.

Mdogo mdogo Tingatinga lishaanza kutolewa kwenye malengo, kesho kutwa utasikia limesepa mambele kufanyiwa service.
 
Watanzania kwa kushabikia mambo bila kitafakari, MTU kwenye akili timamu huwezi kuona utendaji wa MTU ndani ya wk moja na kuanza kushangilia. Wengine wameshaanza kusema 2020 atashinda kwa 90%!
 
Yani sisi watanzania sijui tunataka nini!!!!

Ilo jembe kwenye kampeni zake alitoa ahad za ku support na kuinua michezo (sanaa).
 
Sidhani kama huko sahihi, inamaana hii siku moja atakayo kwenda Taifa ingemtosha kuitembelea nchi nzima?

Ni jambo la faraja kuona Rais anaungana na Watanzania wengine kuishangilia team ya Taifa.
 
Sijui kwa Kikwete msoga hakukaliki!
 
hauko sahihi mkuu, maana jamaa lazima aisapoti timu ya taifa maana ni moja ya ahadi zake tkt kampeni kuinua wanamichezo na wasanii, na hiyo ni mechi kubwa sana hapa tz, ni faraja kuona rais anaisapoti timu yake, kwani ni dhambi kuisapoti timu ya taifa?? hiyo siku moja ni vibaya kuonesha watanzania kuwa nae anasapoti michezo?? ni moja ya nafaisi yake muhimu kama rais kutoa sapoti kwenye National Team yetu Taifa Stars Versus Algeria,
 
sio siri kuwa mzalendo ni kitu kizuri, ila lazima kuwe na vipaumbele katika uzalendo. Si busara kua mzalendo katika kila kitu eti kwakua kimefanywa na wazawa.!

Katika uchumi kuna kitu kinaitwa "scale of preference" na kingine "opportunity cost".
Sidhani kama mapema hii jembe lingepelekwa uwanjani kushangilia mpira na wakati sehemu kibao nchini bado hazijalimwa. Mstaafu angeenda uwanjani pekeake bila kubebelea jembe letu.

Jamani jamani ninasisitiza bado mapema!
Limelima dar kidogo sana, mikoani na visiwani nako kuna magugu jamani!
Lingelima kwanza afu wakati wa kusubilia mavuno ndo wangeenda nalo viwanja.

Mdogo mdogo tingatinga lishaanza kutolewa kwenye malengo, kesho kutwa utasikia limesepa mambele kufanyiwa service.

chunga sana kinywa chako huyu ni rais wetu uwe na lugha ya staha utaishia segerea. Muda wa kampeni umeshaisha ni wakati wa kazi na wala si muda wa kubeza. Chunga sana nakuonya tu. Tumia lugha ya staha kumzungumzia rais wako.
 
Kwenda uwanjani ndio kuinua michezo???

Ww kusoma haujui!!! Ku support"

Kufika kwake uwanjani kutawapa hamasa wachezaji wa Taifa stars na kutojisikia kufanya vibaya mbele ya Raisi wao wa awamu ya Tano.
 
sasa mnadhani uwepo wake utabadilisha matokeo anaenda kujiaibisha tu. Watanzania tuwekeze kwenye elimu kwanza labda kidogo kilimo michezo bado sana maana hatuna nidhamu ya mchezo wachezaji wanywa viloba na kukurubia wanawake kwa sana wakati huo msosi ugali dona dagaa unadhani tutafika?. hivi sisi tupo nafasi ya ngapi kwa watu wenye IQ duniani?.
 
Ww kusoma haujui!!! Ku support"

Kufika kwake uwanjani kutawapa hamasa wachezaji wa Taifa stars na kutojisikia kufanya vibaya mbele ya Raisi wao wa awamu ya Tano.

Kama ingekua rahisi ivo, mbona kufika kwake hospitali hakujawafanya wagonjwa wapone??
ku support michezo sio kushangilia michezo! ku support michezo ni kutengeneza mazingira ya kuboresha viwanja, kuibua vipaji na kuving'alisha, kutengeneza pato la taifa kutokana na michezo, kutengeneza ajira kupitia michezo, nk...
 
Hizi movements zinaashiria usanii wa hali ya juu na huenda zikatia nuksi matokeo ya mchezo japo hakuna apendaye hilo!
 
Kama ingekua rahisi ivo, mbona kufika kwake hospitali hakujawafanya wagonjwa wapone??
ku support michezo sio kushangilia michezo! ku support michezo ni kutengeneza mazingira ya kuboresha viwanja, kuibua vipaji na kuving'alisha, kutengeneza pato la taifa kutokana na michezo, kutengeneza ajira kupitia michezo, nk...

Yani wewe sijui unaishi Tanzania gani!!
Hivi hauoni kwenda kwa magufuli Muhimbili kumeokoa maisha ya wengi!!

Kwa kuagiza zile mashine zipone na imepona bdo CT scan ndio imebainika tatizo na linatafutiwa solution na philips.
Na pia imeingeza umakini kwa madaktari na Wauguzi kwa ujumla.

Kufika kwake uwanjani ndio kutamfanya kuzijua na kuziona changamoto za mchezo wa mpira wa miguu.

Kisha atapata fursa ya kujadili na viongozi wa shirikisho la soka kwa kujadili changamoto hizo na kutafuta ufumbuzi wake.

Hiyo na awali tu, Dr.JPM ni jembe kama ulivyo sema utaiona kazi yake.
 
Kama ingekua rahisi ivo, mbona kufika kwake hospitali hakujawafanya wagonjwa wapone??
ku support michezo sio kushangilia michezo! ku support michezo ni kutengeneza mazingira ya kuboresha viwanja, kuibua vipaji na kuving'alisha, kutengeneza pato la taifa kutokana na michezo, kutengeneza ajira kupitia michezo, nk...

Duh kweli kila mtu na akili zake, Sisi wanamichezo hususani soka AKA kabumbu au kandanda tunaamini, mashabiki Ni wachezaji wa 12 mshinde au mshindwa haijalishi ila wechezaji hupenda kuona mashabiki wapo. Dada iwapo rais wa nchi anapoingia uwanjani, huko kuja kwake Ni hamasa kwa hai mashabiki watakuingia wengi zaidi uwanjani, pia wachezaji hucheza kwa kujituma zaidi mbele ya rais wao. Kuhusu kutendo cha kutembelea Muhimbili na kitendo hicho kutoponyesha wagonjwa, mkuu usitokwe na ufahamu kiasi hicho, ukienda hospital zinazolaza wagonjwa unadhani kwanini huweka muda wa kitizama wagonjwa, au hai wanaokuja kusalimia wagonjwa huponyesha wagonjwa? Ina maana mpaka sasa hujui nini kimetokea baada ya rais kutembelea Muhimbili.
 
Sidhani kama huko sahihi, inamaana hii siku moja atakayo kwenda Taifa ingemtosha kuitembelea nchi nzima?

Ni jambo la faraja kuona Rais anaungana na Watanzania wengine kuishangilia team ya Taifa.

huyu ni mtumishi wa umma anafanyakazi jaumatatu hadi jumamosi saa saba anapumzika na kufanya mambo binafsi kama kutizama mpira na kwenda kanisani. Labda wasiwasi ni adha ya kukaguana milangoni ukizingatia shari iliyotokea ufaransa.
 
Watanzania kwa kushabikia mambo bila kitafakari, MTU kwenye akili timamu huwezi kuona utendaji wa MTU ndani ya wk moja na kuanza kushangilia. Wengine wameshaanza kusema 2020 atashinda kwa 90%!

Hakuna anaekuelewa now
lakini wape mda....mwaka tu unatosha
 
hauko sahihi mkuu, maana jamaa lazima aisapoti timu ya taifa maana ni moja ya ahadi zake tkt kampeni kuinua wanamichezo na wasanii, na hiyo ni mechi kubwa sana hapa tz, ni faraja kuona rais anaisapoti timu yake, kwani ni dhambi kuisapoti timu ya taifa?? hiyo siku moja ni vibaya kuonesha watanzania kuwa nae anasapoti michezo?? ni moja ya nafaisi yake muhimu kama rais kutoa sapoti kwenye National Team yetu Taifa Stars Versus Algeria,

Angetaka kusapoti basi angetoa mkwanja wakati wa maandalizi ili timu ya taifa icheze mechi za maana. Badala ya kuacha timu inaenda South halafu inacheza na wanafunzi wa vyuo huko, eti Leo Tingatinga linajifanya kusapoti Taifa.
Aache kuiga tabia za u-Msoga.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom