Asprin
Platinum Member
- Mar 8, 2008
- 68,272
- 96,398
Sio siri kuwa mzalendo ni kitu kizuri, ila lazima kuwe na vipaumbele katika uzalendo. Si busara kua mzalendo katika kila kitu eti kwakua kimefanywa na wazawa.!
Katika uchumi kuna kitu kinaitwa "Scale of Preference" na kingine "Opportunity Cost".
Sidhani kama mapema hii Jembe lingepelekwa uwanjani kushangilia mpira na wakati sehemu kibao nchini bado hazijalimwa. Mstaafu angeenda uwanjani pekeake bila kubebelea jembe letu.
Jamani jamani ninasisitiza bado mapema!
Limelima Dar kidogo sana, Mikoani na Visiwani nako kuna magugu jamani!
Lingelima kwanza afu wakati wa kusubilia mavuno ndo wangeenda nalo viwanja.
Mdogo mdogo Tingatinga lishaanza kutolewa kwenye malengo, kesho kutwa utasikia limesepa mambele kufanyiwa service.
Jembe limetiwa mpini wa mbao...... hamna lolote. Juzi hapa limepigwa stop na wenye chama chao. Tangu litoke Muhimbili jembe linapalilia ukoka ikulu....
Hapana cheza na system wewe.... chama kimeshika hatamu. Mwenye chama chake jana katia timu Lumumba kupiga kazi.
Jembe litakuwa la kwanza tangu tupate uhuru kushuhudia wapiganaji wakilambishwa magoli kadhaa.... siku chache tu baada ya kukabidhiwa nyumba.
Poor jembe!!