Kwetunikwetu
JF-Expert Member
- Dec 23, 2007
- 1,535
- 408
Leo jioni nilipitia pale tawi la Yanga buguruni adjacent na shule ya msingi Buguruni kumsalimi mzee mmoja anaitwa Makumbi. Nikawakuta jamaa wawili wamekaa kwenye benchi wanapiga story. Nikawasalimu, then nikawauliza;
"Jamani samahani nilikuwa namuulizia mzee Makumbi sijui naweza kumpata wapi"
Wale jamaa wakabaki wameduwaa, nikaona labda hawajanielewa, nikabadilisha swali;
"Jamani Mzee Makumbi mmemuona jioni hii, nilikuwa nataka kumsalimu"
Duh, jamaa mojawapo akaniuliza;
"Kwani mara ya mwisho umemuona Makumbi lini"
Nikamjibu "Ni muda mrefu sana inawezekana mwaka mmoja na zaidi umepita"
Basi jamaa akajibu "Basi kipindi hicho hicho ndio huyu mzee amefariki, ilikuwa mwaka jana mwezi wa pili"
Kwa kweli nilihisi baridi ghafla! Mungu amlaze mahali pema peponi, amini!
"Jamani samahani nilikuwa namuulizia mzee Makumbi sijui naweza kumpata wapi"
Wale jamaa wakabaki wameduwaa, nikaona labda hawajanielewa, nikabadilisha swali;
"Jamani Mzee Makumbi mmemuona jioni hii, nilikuwa nataka kumsalimu"
Duh, jamaa mojawapo akaniuliza;
"Kwani mara ya mwisho umemuona Makumbi lini"
Nikamjibu "Ni muda mrefu sana inawezekana mwaka mmoja na zaidi umepita"
Basi jamaa akajibu "Basi kipindi hicho hicho ndio huyu mzee amefariki, ilikuwa mwaka jana mwezi wa pili"
Kwa kweli nilihisi baridi ghafla! Mungu amlaze mahali pema peponi, amini!