Kumbe Mzee Makumbi amefariki dunia!

Kwetunikwetu

JF-Expert Member
Dec 23, 2007
1,535
408
Leo jioni nilipitia pale tawi la Yanga buguruni adjacent na shule ya msingi Buguruni kumsalimi mzee mmoja anaitwa Makumbi. Nikawakuta jamaa wawili wamekaa kwenye benchi wanapiga story. Nikawasalimu, then nikawauliza;

"Jamani samahani nilikuwa namuulizia mzee Makumbi sijui naweza kumpata wapi"
Wale jamaa wakabaki wameduwaa, nikaona labda hawajanielewa, nikabadilisha swali;

"Jamani Mzee Makumbi mmemuona jioni hii, nilikuwa nataka kumsalimu"

Duh, jamaa mojawapo akaniuliza;
"Kwani mara ya mwisho umemuona Makumbi lini"

Nikamjibu "Ni muda mrefu sana inawezekana mwaka mmoja na zaidi umepita"

Basi jamaa akajibu "Basi kipindi hicho hicho ndio huyu mzee amefariki, ilikuwa mwaka jana mwezi wa pili"

Kwa kweli nilihisi baridi ghafla! Mungu amlaze mahali pema peponi, amini!
 
Mambo haya hutokea. Yalikuta mara mbili:

(a) Nilikuwa na rafiki yangu wa karibu sana, ambaye kama mimi alikuwa pia mvivu sana wa kuandika barua. Kuna wakati nilikuwa nje ya nchi kwa mwaka mmja, niliporudi Dar, nikasema ngoja nikamwoen mshikaji wangu tuingine kwenye moja moto moja baridi. Nilipofika nyumbani kwake na kuulizia nikakutana na swali kama uliloulizwa.

(b) Nilikuwa na mpenzi wangu poa sana mwishoni mwa miaka ya themanini. Nikatokea kuwa nje ya nchi kwa miezi sita tu, ila wakati nikiwa kule nilikuwa namtumia kadi ambazo zilikuwa hazijibiwi. Niliporudi Dar, nikakimbia haraka sana kwenda kumwona mwandani wangu huyo, nikakutana na swali kama hilo hilo uliloulizwa.


Hiyo ni sehemu ya maisha.
 
Sio yule mchezaji, bali ni shabiki mmoja mashuhuri sana wa Yanga pale buguruni. Alikuwa mcheshi sana na mtu wa sound kweli kweli. Alikuwa al-watan fulani, mambo ya mjini-mjini alikuwa makini kuukuunganishia mishemishe
 
Mambo haya hutokea. Yalikuta mara mbili:

(a) Nilikuwa na rafiki yangu wa karibu sana, ambaye kama mimi alikuwa pia mvivu sana wa kuandika barua. Kuna wakati nilikuwa nje ya nchi kwa mwaka mmja, niliporudi Dar, nikasema ngoja nikamwoen mshikaji wangu tuingine kwenye moja moto moja baridi. Nilipofika nyumbani kwake na kuulizia nikakutana na swali kama uliloulizwa.

(b) Nilikuwa na mpenzi wangu poa sana mwishoni mwa miaka ya themanini. Nikatokea kuwa nje ya nchi kwa miezi sita tu, ila wakati nikiwa kule nilikuwa namtumia kadi ambazo zilikuwa hazijibiwi. Niliporudi Dar, nikakimbia haraka sana kwenda kumwona mwandani wangu huyo, nikakutana na swali kama hilo hilo uliloulizwa.


Hiyo ni sehemu ya maisha.

Kichuguu, hiyo pia mimi imeshawahi kunitokea. Kuna jamaa zangu niliokuwa nafanya kazi nao ambao tuliishi vizuri. Basi niliporudi bongo miaka ya karibuni nikaamua kuwachukulia vijizawadi vidogo vidogo. Nikapita pale ofisi kuwajulia hali. Nilikuwa nafahamiana na watu wengi sana pale ofisini lakini hawa tulikuwa tuko kaibu mno. Basi katika kusalimia mwishi nikaingia ofisi ya mmoja wa waliokuwa karibu na hao jamaa zangu. Nikauliza dada fulani na fulani wanakaa ofisi zipi? Akanijibu hao wameshafariki kwani hukusikia? Nikapata mshtuko ambao sikutegemea maana nilikuwa sijasikia vifo vyao. Miaka hiyo mawasiliano na Bongo yalikuwa ni shida kubwa sana siyo kama ilivyo sasa baada ya utandawazi na simu za mkono kurahisisha sana mawasiliano. Nikaambiwa watu wengi wamefariki nikaanza kutajiwa majina basi nikabaki nimepigwa na mshangao na kuwa na mshtuko wa hali ya juu. Madada wawili walikuwa wamefariki na njemba 6 kati ya wanane niliokuwa nimewachukulia vijizawadi nao walikuwa wamefariki. Kilichonisikisha zaidi wengi wao walikuwa bado wana maisha marefu mbele yao. Basi nikaishia kugawa zawadi zangu kwa watu ambao hawakuwemo kwenye list yangu.
 
kama sikosei makumbi juma (homa ya jiji) naye alikwishatangulia
mbele za haki. aligongwa na gari akitokea uwanja wa taifa
kuangalia mechi. kama nimekosea, nawataka radhi ndugu
na jamaa wahusika.


Unayemsema hapo ni KIZOTA!
 
kama sikosei makumbi juma (homa ya jiji) naye alikwishatangulia
mbele za haki. aligongwa na gari akitokea uwanja wa taifa
kuangalia mechi. kama nimekosea, nawataka radhi ndugu
na jamaa wahusika.

Mkuu usije kuwa unachanganya na Said Mwamba Kizota!
 
Aliyegongwa na gari na kufariki ni Said Kizota naye alikuwa ni mchezaji wa Yanga.
 
Siku hizi nikirudi kijijini nasita kuulizia watu niliokuwa nawafahamu zamani. Nisipomwona mtu au kupata salamu zake huwa nakaa kimya.
 
Siku hizi nikirudi kijijini nasita kuulizia watu niliokuwa nawafahamu zamani. Nisipomwona mtu au kupata salamu zake huwa nakaa kimya.

Jasusi inaelekea huulizii kabisa mademu zako wa kale...hutaki pressure! looooooh
 
kama sikosei makumbi juma (homa ya jiji) naye alikwishatangulia
mbele za haki. aligongwa na gari akitokea uwanja wa taifa
kuangalia mechi. kama nimekosea, nawataka radhi ndugu
na jamaa wahusika.

Du! Mzee isijekuwa unataka kumtoa kafara!!Ingekuwa busara zaidi ukaminya tu imya kinywa kama huna uhakika.maana kama bado yupo unaweza zua kilio kwa jamaa zake wa mbali ambao hawajamuona siku nyingi
 
(b) Nilikuwa na mpenzi wangu poa sana mwishoni mwa miaka ya themanini. Nikatokea kuwa nje ya nchi kwa miezi sita tu, ila wakati nikiwa kule nilikuwa namtumia kadi ambazo zilikuwa hazijibiwi. Niliporudi Dar, nikakimbia haraka sana kwenda kumwona mwandani wangu huyo, nikakutana na swali kama hilo hilo uliloulizwa.QUOTE]


Du mshikaji

Umenikumbusha mbali sana nyuumaaa mwaka 1997 nikiwa ni mwenye shauku ya kumuona kipenzi changu cha roho huko Morogoro baada ya kuwa safari ya mbali kwa takribani miaka 2, nilifunga safari ya kwenda kumuona niliyempanga kuwa mahbuba wangu wa milele aliyekuwa akifundisha mitaa ya Pangawe.

Baada ya kukaribia na kwa kuwa nilikuwa sijajitambulisha rasmi, nilimsimamisha mdada mmoja kwa nia ya kumuulizia habari za mpenzi wangu na ikiwezekana akaniitie. Jibu nililopata ni swali "Kwani huna taarifa kuwa alifariki mwaka 1995 au nikakuoneshe kaburi lake?

Kwa siku hizi ni mambo ya kawaida kabisa kukutana na taarifa kama hizo.
 
Mwenzenu ilinitokea mwaka jana (2008). Nilikuwa nimepanga kwenda kumuona baba mdogo ambaye tulikuwa hatujaonana miaka mingi. Ila kwa kuwa nilikuwa na muda kidogo na sehemu hiyo wanayoishi pia usafiri wa shida hasa masika basi niliomba tukutane naye mji mkubwa wa karibu. Binamu yangu alinijibu .."haiwezekani, baba mdogo amefariki tangu mwaka 2006".

Nilimpigia simu mtoto wake na ndugu wote kuwauliza imekuwaje ni mimi tu sijapata taarifa za msiba wa baba? Kila aliyepata simu alipata kigugumizi na kusema "wala sijui imetokea vipi..."
 
Mwenzenu ilinitokea mwaka jana (2008). Nilikuwa nimepanga kwenda kumuona baba mdogo ambaye tulikuwa hatujaonana miaka mingi. Ila kwa kuwa nilikuwa na muda kidogo na sehemu hiyo wanayoishi pia usafiri wa shida hasa masika basi niliomba tukutane naye mji mkubwa wa karibu. Binamu yangu alinijibu .."haiwezekani, baba mdogo amefariki tangu mwaka 2006".

Nilimpigia simu mtoto wake na ndugu wote kuwauliza imekuwaje ni mimi tu sijapata taarifa za msiba wa baba? Kila aliyepata simu alipata kigugumizi na kusema "wala sijui imetokea vipi..."

Mkuu Sikonge, uwezekano mkubwa mpaka usisikie kifo cha Baba yako mdogo ulikuwa nje ya nchi. Manake kweli miaka karibia miwili usiwe na mawasiliano na Baba yako mdogo. Pole lakini mkuu. Hii habari ya Mzee Makumbi nilipoiona mwanzo nikajua ni Makumbi Juma.
 
...kwa hali hii ya "huna habari alishafariki mwaka uleee...!" kuna haja hapa Jamvini ifanyike Roll-Call,

isijekuwa wenzetu tayari wamesha Rest in Peace! ilhali sie twadhani wameuchuna tu!
 
Du! Mzee isijekuwa unataka kumtoa kafara!!Ingekuwa busara zaidi ukaminya tu imya kinywa kama huna uhakika.maana kama bado yupo unaweza zua kilio kwa jamaa zake wa mbali ambao hawajamuona siku nyingi

naona umelishikia bango hili kosa pamoja na kumba radhi kwangu.
ngoja basi nifute kabisa maneno yangu isje ikawa issue bure.
 
Kichuguu, hiyo pia mimi imeshawahi kunitokea. Kuna jamaa zangu niliokuwa nafanya kazi nao ambao tuliishi vizuri. Basi niliporudi bongo miaka ya karibuni nikaamua kuwachukulia vijizawadi vidogo vidogo. Nikapita pale ofisi kuwajulia hali. Nilikuwa nafahamiana na watu wengi sana pale ofisini lakini hawa tulikuwa tuko kaibu mno. Basi katika kusalimia mwishi nikaingia ofisi ya mmoja wa waliokuwa karibu na hao jamaa zangu. Nikauliza dada fulani na fulani wanakaa ofisi zipi? Akanijibu hao wameshafariki kwani hukusikia? Nikapata mshtuko ambao sikutegemea maana nilikuwa sijasikia vifo vyao. Miaka hiyo mawasiliano na Bongo yalikuwa ni shida kubwa sana siyo kama ilivyo sasa baada ya utandawazi na simu za mkono kurahisisha sana mawasiliano. Nikaambiwa watu wengi wamefariki nikaanza kutajiwa majina basi nikabaki nimepigwa na mshangao na kuwa na mshtuko wa hali ya juu. Madada wawili walikuwa wamefariki na njemba 6 kati ya wanane niliokuwa nimewachukulia vijizawadi nao walikuwa wamefariki. Kilichonisikisha zaidi wengi wao walikuwa bado wana maisha marefu mbele yao. Basi nikaishia kugawa zawadi zangu kwa watu ambao hawakuwemo kwenye list yangu.

Ushukuru ulikuwa nje huenda hayo mavuno yangekupitia. Pole sana kwa kuwapoteza swahiba zako. Endelea kula maisha.
 
Back
Top Bottom