Kulikoni Polepole kukaa kimya sakata la CAG?

Kulikoni Polepole kukaa kimya sakata la CAG?

singojr

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2014
Posts
5,314
Reaction score
6,896
Katika sakata la 1.5 Trillion Polepole alijitokeza kwa ushujaa kufundisha taifa hesabu na kuonyesha hakuna fedha imepotea.

Polepole ni katika watu walio mstari wa mbele kuunga lolote lifanywalo na Rais hata kama halina maslahi kwa nchi.

Lakini kabla ya haya yote, kabla ya Polepole kupata vyeo CCM alikuwa kijana mahiri mwenye kulitetea taifa na kusimamia maslahi ya taifa na alivuma sana kipindi cha katiba mpya.

Kimya chake cha ghafla baada ya watu kuanza kumuandama mitandaoni Je kuna jambo kashtukia sivyo alivyotegemea au kashaona muelekeo mbaya wa taifa na anaanza kujitoa taratibu na kukabidhi kazi kwa akina Musiba.

Polepole tumjuae asingeacha ripoti ya CAG imchafue Magufuli lazima lawama zingepelekwa kuwa kuna vibaraka wa mabeberu.

Je, nini kimemsibu?
 
Anahangaika kutafuta fedha wanazodaiwa na NSSF maana kwa jinsi wanavyojinasibu na uzalendo lakini wanakula hela za wanyonge bila kuzipeleka mahali husika ameona bora wazipeleke halafu aje na propaganda kuwa zilicheleweshwa na mifumo ya kibenki
 
Chama Cha Taifa CCM kipo Pamoja Na CAG

CCM ndio imeamuru Wabunge wake wapuuze Azimio la Bunge la kumsusia CAG
 
Katika sakata la 1.5 Trillion Polepole alijitokeza kwa ushujaa kufundisha taifa hesabu na kuonyesha hakuna fedha imepotea.

Polepole ni katika watu walio mstari wa mbele kuunga lolote lifanywalo na Rais hata kama halina maslahi kwa nchi.

Lakini kabla ya haya yote, kabla ya Polepole kupata vyeo CCM alikuwa kijana mahiri mwenye kulitetea taifa na kusimamia maslahi ya taifa na alivuma sana kipindi cha katiba mpya.

Kimya chake cha ghafla baada ya watu kuanza kumuandama mitandaoni Je kuna jambo kashtukia sivyo alivyotegemea au kashaona muelekeo mbaya wa taifa na anaanza kujitoa taratibu na kukabidhi kazi kwa akina Musiba.

Polepole tumjuae asingeacha ripoti ya CAG imchafue Magufuli lazima lawama zingepelekwa kuwa kuna vibaraka wa mabeberu.

Je, nini kimemsibu?

Bado anamalizia kuandaa ' Propaganda ' itakayobadili upepo wote wa ' Sakata ' zima. Vuta subira!
 
Back
Top Bottom