Kulikoni Polepole kukaa kimya sakata la CAG?

Kulikoni Polepole kukaa kimya sakata la CAG?

CcM hawawezi kujisafisha na kashfa hizi za wizi kwenye ripoti ya CAG.Wao ndio waliounda Serikali,sasa asije kutuhadaa kwamba CcM haihusiki.

Sent using Jamii Forums mobile app
" si haki kukilaumu chama au Serikali kwamba havifanyi kazi zake barabara kwa kosa ambalo limefanywa na kiongozi mmoja wa Chama au wa Serikali au wa shirika la Umma". Edward Sokoine, Oktoba 12, 1983.
 
Katika sakata la 1.5 Trillion Polepole alijitokeza kwa ushujaa kufundisha taifa hesabu na kuonyesha hakuna fedha imepotea.

Polepole ni katika watu walio mstari wa mbele kuunga lolote lifanywalo na Rais hata kama halina maslahi kwa nchi.

Lakini kabla ya haya yote, kabla ya Polepole kupata vyeo CCM alikuwa kijana mahiri mwenye kulitetea taifa na kusimamia maslahi ya taifa na alivuma sana kipindi cha katiba mpya.

Kimya chake cha ghafla baada ya watu kuanza kumuandama mitandaoni Je kuna jambo kashtukia sivyo alivyotegemea au kashaona muelekeo mbaya wa taifa na anaanza kujitoa taratibu na kukabidhi kazi kwa akina Musiba.

Polepole tumjuae asingeacha ripoti ya CAG imchafue Magufuli lazima lawama zingepelekwa kuwa kuna vibaraka wa mabeberu.

Je, nini kimemsibu?
Kapigwa ganzi na ujio wa Lowassa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nimeguswa na hii mada kwa maswali lukuki kuwa je ni huyu mzee kijana tu alie kimya wakati huu? je kwanini yuko kimya? yupo ofisini? busy? lakini mbona na wakubwa zake pia nao kama wamemwagiwa maji wako kimyaaa, ripoti hii imetaja mafisadi wote ofisi walipo na kiasi walichoiba, ni aibu sana kwa nchi na serikali kwa ufisadi huu wa kutisha uliofanyika na wenye ushahidi, je mahakama ya mafisadi ofisi zao ziko wazi au wapo likizo? je kwanini hawaanzi kukamata na kuwahoji wahusika wote simply kuanzia na all budget holders na signatories wa kila wizi ulioandikwa na CAG, ni aibu na kichekesho kikuu kusema serikali inapambana na ufisadi na kuwaacha mafisadi wenye ushahidi wakidunda mitaani , shime sana mahakama ya mafisadi ifanye kazi yake sasa kuwakamata mafsadi wote walioainishwa kwenye ripoti ya CAG , ni bora tutafute kauli mbiu ingine!!
Alipo anzisha mahakama ya mafisadi, aliamini kuwa ufisadi unafanywa na wapinzani hasa baada ya mamvi kuhamia upinzani. Amekuja kugundua kwamba unafanywa na wanaCCM hasa wasaidizi wake anao waamini sana, mahakama haina kazi tena. Kilangila.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chama Cha Taifa CCM kipo Pamoja Na CAG

CCM ndio imeamuru Wabunge wake wapuuze Azimio la Bunge la kumsusia CAG
Duuhhh, kwa hiyo wabunge wa CCM na CCM kwa ujumla imempuuza speaker Job Ndugai. Hivi waliopitisha Azimio la kumkataa CAG wakati wabunge wa upinzani wakitoka nje walikua wabunge wa chama gani!!??? Mkuu nadhani hapa umetupia tu ili uone watu wanasemaje. This is a joke kiongozi. CCM hoyeeeeeee.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duuhhh, kwa hiyo wabunge wa CCM na CCM kwa ujumla imempuuza speaker Job Ndugai. Hivi waliopitisha Azimio la kumkataa CAG wakati wabunge wa upinzani wakitoka nje walikua wabunge wa chama gani!!??? Mkuu nadhani hapa umetupia tu ili uone watu wanasemaje. This is a joke kiongozi. CCM hoyeeeeeee.

Sent using Jamii Forums mobile app

Wabunge wa CCM hawakukutana Kwenye Kamati ya Wabunge wa CCM kupata ridhaa ya Chama kwa Azimio Hilo

Walikurupuka ndio sababu Chama kimewaamuru kutupilia mbali Azimio linalovunja Katiba

CCM ipo kusimamia Na kuelekeza Wabunge wake sio Wabunge kuelekeza CCM
 
Polepole hana uwezo wa kuona mwelekeo wa taifa, hata yeye akisoma uzi wako atakushangaa
 
Katika sakata la 1.5 Trillion Polepole alijitokeza kwa ushujaa kufundisha taifa hesabu na kuonyesha hakuna fedha imepotea.

Polepole ni katika watu walio mstari wa mbele kuunga lolote lifanywalo na Rais hata kama halina maslahi kwa nchi.

Lakini kabla ya haya yote, kabla ya Polepole kupata vyeo CCM alikuwa kijana mahiri mwenye kulitetea taifa na kusimamia maslahi ya taifa na alivuma sana kipindi cha katiba mpya.

Kimya chake cha ghafla baada ya watu kuanza kumuandama mitandaoni Je kuna jambo kashtukia sivyo alivyotegemea au kashaona muelekeo mbaya wa taifa na anaanza kujitoa taratibu na kukabidhi kazi kwa akina Musiba.

Polepole tumjuae asingeacha ripoti ya CAG imchafue Magufuli lazima lawama zingepelekwa kuwa kuna vibaraka wa mabeberu.

Je, nini kimemsibu?
bado yuko bize anafanya yale mahesabu yake ya kukokotoa ili atoke vizuri
 
Chama Cha Taifa CCM kipo Pamoja Na CAG

CCM ndio imeamuru Wabunge wake wapuuze Azimio la Bunge la kumsusia CAG
Mhu mbona sijaagiza wine saa hivi, hivi huyu ni Pohamba au amedukuliwa? Yaliyopo yanashangaza.
 
Chama Cha Taifa CCM kipo Pamoja Na CAG

CCM ndio imeamuru Wabunge wake wapuuze Azimio la Bunge la kumsusia CAG
Kwani nani aliyetoa azimio la kutofanya kazi na CAG? Vibaraka mnapata tabu sana kutetea ujinga

Sent using Boeing 737-MAX 8
 
Yuko busy anaatafuta ni mbunge gani anamiliki NISSAN Patrol akirudi atakuja na jina...
 
Anaona aibu yeye na boss wake jinsi wanavyochezea box la kura kwa kisingizio cha kuunga juhudi za jpm kisha wizi wa kutisha bado upo.
 
Wabunge wa CCM hawakukutana Kwenye Kamati ya Wabunge wa CCM kupata ridhaa ya Chama kwa Azimio Hilo

Walikurupuka ndio sababu Chama kimewaamuru kutupilia mbali Azimio linalovunja Katiba

CCM ipo kusimamia Na kuelekeza Wabunge wake sio Wabunge kuelekeza CCM

KUB alidai na kutahadharisha ndani ya Bunge kuwa Wabunge wa ccm walijiandaa kutekeleza kusudio la kumsusia CAG kama njia ya kumshinikiza kujiuzulu.Tunajua kuna Wabunge wa ccm wazuri sana na bila shaka walijua uamuzi huo ulikuwa batili kikatiba. Yupo pia AG! Naye kweli hakuona tatizo? Haiwezekani. Nadhani wote hao waliamua kunyamaza kuona mwisho wa hizo mbio za farasi. Kwa watu wenye uelewa ni ccm pekee ndiyo yenye ubavu kuagiza wabunge wake cha kufanya; kiutaratibu serikali (rais) haina huo ubavu ( ingawa tunajua siku hizi linafanyika nyuma ya pazia). Officially, agiizo la kumsusa CAG lilikuwa la ccm. Hata hili la kutenğua azimio la Bunge nalo la ccm! This is how some people have decided to prostitute this once great country!
 
Wabunge wa CCM hawakukutana Kwenye Kamati ya Wabunge wa CCM kupata ridhaa ya Chama kwa Azimio Hilo

Walikurupuka ndio sababu Chama kimewaamuru kutupilia mbali Azimio linalovunja Katiba

CCM ipo kusimamia Na kuelekeza Wabunge wake sio Wabunge kuelekeza CCM
Mkuu, twende taratibu. Baada ya kamati kumhoji CAG na kutoka na Azimio la kumkataa ambalo kiukweli lilishakua limeandalia na Job Ndugai kabla hata ya CAG kuhojiwa, kamati ilileta mapendekezo yaliyo kwenye Azimio ndani ya Bunge kuungwa au kukataliwa na wabunge. Utakumbuka wabunge wa upinzani walilipinga hilo Azimio na baada ya hoja za mh Lema kulipinga kwa nguvu na kumuunga mkono mh Mdee juu ya hoja ya kukubaliana na CAG ambayo maana yake Lema pia alikubaliana na hoja za CAG, speaker alimtoa mh Lema nje ya Bunge na baada ya hapo wabunge wa upinzani walitoka kumuunga mkono Lema.

Wakiwa nje, speaker Job Ndugai alipiga marufuku vyombo vya habari kuwahoji wabunge waliotoka ndani ya Bunge.

Huku nyuma wabunge wa CCM waliendelea kujadili Azimio la kutofanya kazi na CAG Prof Mussa Assad na mwisho kwa umoja wao walilipitisha Azimio lao.

Mzee Pohamba, tulia fuatilia matukio ya Azimio na hata kabla ya Azimio, fuatilia kauli za speaker Job Ndugai, utaelewa ni nini CCM imekifanya juu ya hili sakata.

Inawezekana walifikiri rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM angeungana nao, lakini hali haijakua hivyo ndiyo maana nyuso zimewashuka na ndiyo sababu ya huu ukimya.

Mkuu, uje na hoja zingine kama unazo, lakini kwa hizi, watanzania siyo wajinga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom