Kujenga nyumba na kununua magari ni sababu mojawapo ya Umasikini

Lofefm

Senior Member
May 22, 2011
126
72
Habari,

"Tafuta kiwanja, Jenga, Oa/Olewa, nunua mkoko", njia hii na mawazo haya yamekuwa kwa vijana wengi wanaoanza maisha, hususani waliobarikiwa kupata ajira au biashara zao binafsi ambazo zinawapa kipato flani cha kuendesha maisha yao. Kwa uzoefu wangu hii imekuwa kati ya sababu moja kubwa zinazosababisha watu kuwa maskini na kushindwa kufikia uhuru wa kifedha.

Lakini tujiulize swali la msingi, kwanini watu wengi wameamua kuchagua njia hii ya maisha. Nimefanikiwa kuwahoji watu wengi kidogo kuhusu hili na majibu niliyoyapata mengi yalikuwa kama ifuatavyo:

  • Gharama ya kupanga nyumba ziko juu sana, ni bora kujenga ya kwako.
  • Nyumba ni asset.
  • Usafiri ni shida sana eneo niliko jenga ni bora kuvuta gari yangu.
  • Mama/baba mwenye nyumba ana gubu sana.
  • Nikiwa na kwangu nakuwa na uhuru mkubwa sana.
  • Siku nikifukuzwa kazi au biashara ikiyumba nibaki na pakulala na familia yangu.

Sababu hapo juu nyingi ni za maana kabisa ila tatizo ni kwamba njia zilizotumika kutatua hizo changamoto zinaongeza changamoto zaidi, kivipi?. Ngoja tujadili mambo machache kuhusiana na maisha ya watu wengi hususani mijini (e.g. Dar):

- Wengi wananunua viwanja maeneo ya mbali kutoka mahali wanapofanyia shughuli zao zinazowapa kipato.
- Baadhi ya hayo maeneo yana changamoto za miundombinu ya maji, umeme, barabara na hata kiusalama.
  • Wengi wanajenga kwa kuunga unga sana, unaweza jenga nyumba hata miaka sita au zaidi. Kuna msemo wanasema "nyumba haiishi".
  • Nyumba nyingi wanazojenga watu kukaa zinakuwa ni kubwa na za kifahari bila kukumbuka lengo la mwanzo lilikuwa ni makazi tu na sio jengo la maonesho (Hapo utajibiwa kuwa tunajenga mara moja ya kuzeekea)

Kuzingatia hizo hoja hapo juu, yafuatayo yanakuwa ni matokeo ya gharama za maisha baada ya huyu mtu kuhamia kwake:

  • Gharama za usafiri au mafuta zinakuwa juu ukilinganisha na awali.
  • Mazingira yanakuwa sio rafiki kwa familia kuishi, maana nyumba nyingi zinakuwa bado hazijaisha (Wengine wanasema unakuwa unaishi site).
  • Kama una gari, gharama za matengenezo zinakuwa juu kwa sababu ya pengine barabara kuwa mbaya, lakini kwa kuwa unasafiri umbali mrefu kila siku, basi hata service ya gari utafanya mara nyingi zaidi.
  • Pia kama una gari utalazimika kuendesha gari umbali mrefu kila siku, hii si nzuri kwako kiafya.
  • Gharama za umeme na maji pia zinaweza kuongezeka kwa kuwa nyumba ni kubwa sasa na pengine maji hayajafika.
  • Maeneo mengine hata watu hawajahamia wengi hivyo hata usalama unakuwa hatarini.
  • Mara nyingi unaweza ukajikuta mbali na huduma bora za kijamii ikiwemo hospitali, shule, n.k.

***NOTE: Gharama zinaweza kuongezeka ukilinganisha na mwanzo.

Kwanini kuna hofu ya kuwekeza hizo pesa?

Tujiulize swali hili la msingi. Ni kweli baadhi ya watu wanatamani sana kuffanya biashara, lakini wengi wanasema, BIASHARA HAZITABIRIKI. Ni kweli kabisa, lakini ukweli ni kwamba hilo sio tatizo la watu kutokuwekeza.
SHIDA KUBWA NI WATU KUTOKUWA NA ELIMU YA FEDHA. Hili ni jambo la muhimu sana kwa vijana kupata elimu. kwanza kabisa sio kweli kwamba ukitaka kuwekeza ni lazima ukafanye biashara fulani kama kuuza nguo, vinywaji au duka la mangi. Unaweza ukafanya uwekezaji kwa njia nyingi sana ambazo hazitahitaji your active time kuweza kusimamia ila mwisho wa siku ukaja kuwa na uchumi mkubwa kabisa. Uwekezaji huu ni kama mifano ifuatayo:

  • Kununua viwanja na mashamba (Kumba muda unavyokwenda ardhi inapanda thamani lakini nyumba inashuka thamani)
  • Kununua hisa za makampuni
  • Tressury Bonds and Bills
  • Mifuko ya uwekezaji ya pamoja (e.g. UTTAMIS)
  • Fixed deposits accounts
  • Kuwekeza kwenye elimu (Hii sio lazima zile za darasani, inaweza kuwa hata kujiendeleza katika fani flani)
  • N.k.

La muhimu ni kupata elimu sahihi ya mambo ya fedha ili ujue jinsi ya kufanya maamuzi ni vipi utumie pesa yako.


Ngoja nitoe mfano halisi mmoja ulio hai kabisa kwa lengo la kupata uhalisia wa ninacho kisema:

Mwaka 2013 niliajiriwa mahali na tulikuwa kama waajiriwa sita wapya katika hiyo kampuni, mwenzetu mmoja alikuwa na uelewa mkubwa sana wa mambo ya fedha, na mara nyingi alikuwa anatushauri kuhusu haya mambo lakini tulikuwa tunamuona kama kachanganyikiwa: Mimi na wenzangu wengine wa tano tulikwenda mahali tukanunua viwanja na kuanza kujenga kwa kasi sana na badae tukachuku na mikopo kuongeza kasi hiyo. Kwa haraka haraka kwa wastani tuliweza kutenga kama milioni moja kwa mwezi kila mmoja wetu kwa ajiri ya miradi ya ujenzi. Mungu si athumani baada ya miaka mitatu paka minne wote watano tukawa tumehamia kwenye site zetu huku tukiendelea na finishing.

Jamaa alikuwa kila mwezi anaweka milioni moja kwenye mfuko mmoja wa uwekezaji wa pamoja na alikuwa anapata average interest kama ya 11.85% kwa mwaka. Badae akawa ananunua na bond za serikali pamoja na mambo ya kununua mashamba mbali kidogo na mji yakichangamka anakata na kuyauza. Kiufupi jamaa ana zaidi ya milioni 200 kwenye mfuko anaoweka pesa pamoja na kuwa na asset ya viwanja na mashamba na benki ana pesa chafu.

Turudi kwetu tuliojenga na sasa tuna mikoko yetu, umbali wa kwenda na kurudi nyumbani ni 50 Km kila siku. Na pia siwezi pata picha ile hofu ya kwamba nikiachishwa kazi bado ipo maana siwezi nikala nyumba.

Kwa ajili ya muda niishie hapa kwa leo, nipate mawazo ya watu wengine pia. Kiufupi mimi naona kuna mitaji mingi ya biashara na uwekezaji inapotea kwa huu mwamvuli wa kujenga na kununua hii mikoko.

Ahsanteni!!!
 
Ulitumia miaka mitatu kujenga means by 2016 ulikuwa umemaliza. Kuanzia 2016 hadi leo miaka zaidi ya sita bado haujawa stable, kama ulijenga kwa miaka mitatu imagine hii miaka sita ungekuwa makini ungesave kiasi gani!! Inaonekana ni wewe ndio mwenye shida.

Kujenga bongo ni rahisi sana, na ni risky sana kufanya biashara au kuinvest hilo halipingiki (of course ukitoboa umetoboa).. hizi principle za usijenge invest kwanza zinafaa Marekani na Ulaya ambako kujenga ni ghali sana. Bongo ukipata pesa jenga uepushe aibu za hapa na pale.
 
Habari,

"Tafuta kiwanja, Jenga, Oa/Olewa, nunua mkoko", njia hii na mawazo haya yamekuwa kwa vijana wengi wanaoanza maisha, hususani waliobarikiwa kupata ajira au biashara zao binafsi ambazo zinawapa kipato flani cha kuendesha maisha yao. Kwa uzoefu wangu hii imekuwa kati ya sababu moja kubwa zinazosababisha watu kuwa maskini na kushindwa kufikia uhuru wa kifedha.

Lakini tujiulize swali la msingi, kwanini watu wengi wameamua kuchagua njia hii ya maisha. Nimefanikiwa kuwahoji watu wengi kidogo kuhusu hili na majibu niliyoyapata mengi yalikuwa kama ifuatavyo:

  • Gharama ya kupanga nyumba ziko juu sana, ni bora kujenga ya kwako.
  • Nyumba ni asset.
  • Usafiri ni shida sana eneo niliko jenga ni bora kuvuta gari yangu.
  • Mama/baba mwenye nyumba ana gubu sana.
  • Nikiwa na kwangu nakuwa na uhuru mkubwa sana.
  • Siku nikifukuzwa kazi au biashara ikiyumba nibaki na pakulala na familia yangu.

Sababu hapo juu nyingi ni za maana kabisa ila tatizo ni kwamba njia zilizotumika kutatua hizo changamoto zinaongeza changamoto zaidi, kivipi?. Ngoja tujadili mambo machache kuhusiana na maisha ya watu wengi hususani mijini (e.g. Dar):

  • Wengi wananunua viwanja maeneo ya mbali kutoka mahali wanapofanyia shughuli zao zinazowapa kipato.
  • Baadhi ya hayo maeneo yana changamoto za miundombinu ya maji, umeme, barabara na hata kiusalama.
  • Wengi wanajenga kwa kuunga unga sana, unaweza jenga nyumba hata miaka sita au zaidi. Kuna msemo wanasema "nyumba haiishi".
  • Nyumba nyingi wanazojenga watu kukaa zinakuwa ni kubwa na za kifahari bila kukumbuka lengo la mwanzo lilikuwa ni makazi tu na sio jengo la maonesho (Hapo utajibiwa kuwa tunajenga mara moja ya kuzeekea)

Kuzingatia hizo hoja hapo juu, yafuatayo yanakuwa ni matokeo ya gharama za maisha baada ya huyu mtu kuhamia kwake:

  • Gharama za usafiri au mafuta zinakuwa juu ukilinganisha na awali.
  • Mazingira yanakuwa sio rafiki kwa familia kuishi, maana nyumba nyingi zinakuwa bado hazijaisha (Wengine wanasema unakuwa unaishi site).
  • Kama una gari, gharama za matengenezo zinakuwa juu kwa sababu ya pengine barabara kuwa mbaya, lakini kwa kuwa unasafiri umbali mrefu kila siku, basi hata service ya gari utafanya mara nyingi zaidi.
  • Pia kama una gari utalazimika kuendesha gari umbali mrefu kila siku, hii si nzuri kwako kiafya.
  • Gharama za umeme na maji pia zinaweza kuongezeka kwa kuwa nyumba ni kubwa sasa na pengine maji hayajafika.
  • Maeneo mengine hata watu hawajahamia wengi hivyo hata usalama unakuwa hatarini.
  • Mara nyingi unaweza ukajikuta mbali na huduma bora za kijamii ikiwemo hospitali, shule, n.k.

***NOTE: Gharama zinaweza kuongezeka ukilinganisha na mwanzo.

Kwanini kuna hofu ya kuwekeza hizo pesa?

Tujiulize swali hili la msingi. Ni kweli baadhi ya watu wanatamani sana kuffanya biashara, lakini wengi wanasema, BIASHARA HAZITABIRIKI. Ni kweli kabisa, lakini ukweli ni kwamba hilo sio tatizo la watu kutokuwekeza.
SHIDA KUBWA NI WATU KUTOKUWA NA ELIMU YA FEDHA. Hili ni jambo la muhimu sana kwa vijana kupata elimu. kwanza kabisa sio kweli kwamba ukitaka kuwekeza ni lazima ukafanye biashara fulani kama kuuza nguo, vinywaji au duka la mangi. Unaweza ukafanya uwekezaji kwa njia nyingi sana ambazo hazitahitaji your active time kuweza kusimamia ila mwisho wa siku ukaja kuwa na uchumi mkubwa kabisa. Uwekezaji huu ni kama mifano ifuatayo:

  • Kununua viwanja na mashamba (Kumba muda unavyokwenda ardhi inapanda thamani lakini nyumba inashuka thamani)
  • Kununua hisa za makampuni
  • Tressury Bonds and Bills
  • Mifuko ya uwekezaji ya pamoja (e.g. UTTAMIS)
  • Fixed deposits accounts
  • Kuwekeza kwenye elimu (Hii sio lazima zile za darasani, inaweza kuwa hata kujiendeleza katika fani flani)
  • N.k.

La muhimu ni kupata elimu sahihi ya mambo ya fedha ili ujue jinsi ya kufanya maamuzi ni vipi utumie pesa yako.


Ngoja nitoe mfano halisi mmoja ulio hai kabisa kwa lengo la kupata uhalisia wa ninacho kisema:

Mwaka 2013 niliajiriwa mahali na tulikuwa kama waajiriwa sita wapya katika hiyo kampuni, mwenzetu mmoja alikuwa na uelewa mkubwa sana wa mambo ya fedha, na mara nyingi alikuwa anatushauri kuhusu haya mambo lakini tulikuwa tunamuona kama kachanganyikiwa: Mimi na wenzangu wengine wa tano tulikwenda mahali tukanunua viwanja na kuanza kujenga kwa kasi sana na badae tukachuku na mikopo kuongeza kasi hiyo. Kwa haraka haraka kwa wastani tuliweza kutenga kama milioni moja kwa mwezi kila mmoja wetu kwa ajiri ya miradi ya ujenzi. Mungu si athumani baada ya miaka mitatu paka minne wote watano tukawa tumehamia kwenye site zetu huku tukiendelea na finishing.

Jamaa alikuwa kila mwezi anaweka milioni moja kwenye mfuko mmoja wa uwekezaji wa pamoja na alikuwa anapata average interest kama ya 11.85% kwa mwaka. Badae akawa ananunua na bond za serikali pamoja na mambo ya kununua mashamba mbali kidogo na mji yakichangamka anakata na kuyauza. Kiufupi jamaa ana zaidi ya milioni 200 kwenye mfuko anaoweka pesa pamoja na kuwa na asset ya viwanja na mashamba na benki ana pesa chafu.

Turudi kwetu tuliojenga na sasa tuna mikoko yetu, umbali wa kwenda na kurudi nyumbani ni 50 Km kila siku. Na pia siwezi pata picha ile hofu ya kwamba nikiachishwa kazi bado ipo maana siwezi nikala nyumba.

Kwa ajili ya muda niishie hapa kwa leo, nipate mawazo ya watu wengine pia. Kiufupi mimi naona kuna mitaji mingi ya biashara na uwekezaji inapotea kwa huu mwamvuli wa kujenga na kununua hii mikoko.

Ahsanteni!!!
Umetoa elimu kubwa sana hapa
Big up mkuu
 
Watanzania tunahitaji kubadili mentality na kuondoa uoga kuhusu kufanya biashara. Mtu anafanya kazi posta anaanza ujenzi Madale, akimaliza nyumba anahamia kwake, anaanza kuendesha gari kilometer 60 kwenda kazini na kurudi, wastani wa mafuta ya elfu 25 Kwa siku na masaa manne njiani kwenda na kurudi. Wakati huo ana familia, mke na watoto wawili wanaosoma English medium. Unakuta nyumba na gari vimemcost kati ya milioni 40 hadi 60, kama angepata ushauri na kuwa na elimu nzuri kuhusu uwekezaji na financial management ya kutosha. Hiyo pesa ndani ya miaka miwili anakuwa anaongea story tofauti. Lakini unakuta vijana wengi wana nyumba nzuri na usafiri, ila kiuhalisia wamekwama kiuchumi kila mwisho wa mwezi unamkuta na madeni. Sababu ya haya yote ni tunaishi kwa kuigana na kutafuta status kwenye jamii. Kwa watanzania walio wengi ni bora aishi kwenye nyumba yake yenye thamani ya milioni 50 hata kama hana kazi, ila kwangu mimi ni bora kuishi nyumba ya kupanga ila nina akaunti iliyonona na nina biashara inayozungusha pesa na nina backup ya pesa kwenye akaunti kulinda/au kuanzisha biashara nyingine wakati wowote. Mleta mada upo sahihi sana.
 
Kuna jamaa yangu Kaenda jenga bonge la mjengo mbondole. Katumia pesa nyingi sana kupambania mjengo ule. Kazi anafanyia posta. Jamaa kashindwa kabisa kuhamia mjengoni badala yake kamuweka mtu amtizamie.

Angetumia ile pesa kuinvest angekuwa mbali. Sasa hivi analalamika maisha yanamchapa anashindwa kula bata kumbe pesa alikopa na anakatwa pesa ndefu ya mkopo.
 
Ulitumia miaka mitatu kujenga means by 2016 ulikuwa umemaliza. Kuanzia 2016 hadi leo miaka zaidi ya sita bado haujawa stable, kama ulijenga kwa miaka mitatu imagine hii miaka sita ungekuwa makini ungesave kiasi gani!! Inaonekana ni wewe ndio mwenye shida.

Kujenga bongo ni rahisi sana, na ni risky sana kufanya biashara au kuinvest hilo halipingiki (of course ukitoboa umetoboa).. hizi principle za usijenge invest kwanza zinafaa Marekani na Ulaya ambako kujenga ni ghali sana. Bongo ukipata pesa jenga uepushe aibu za hapa na pale.
nilitaka kuongea point kama hii,kufanikiwa kwa yule jamaa yao aliyetumia principles za finance haiwezi kuwa formula kwa watu wote,kama hiyo formula inasaidia watu wote ilitakiwa na wao baada ya kumaliza mijengo yao wangeitumia pia ili watajirike.
Kuna formula zingine zinafaa zina application ulaya huko kwa bongo ni ngumu sana.
Bongo kuna factors nyingi sana ambazo zinaleta variations kwenye business aspects kwa mfano utawala ukibadilika na mifumo yote inabadilika,miundombinu,mambo ya kodi,rushwa yote haya yana affect business na kufirisika ni rahisi sana.
Refer wale wafanyabiashara wa kariakoo walivyotoa vilio vyao na baadhi mitaji yao ilikuwa ni billions of money.
 
Ulitumia miaka mitatu kujenga means by 2016 ulikuwa umemaliza. Kuanzia 2016 hadi leo miaka zaidi ya sita bado haujawa stable, kama ulijenga kwa miaka mitatu imagine hii miaka sita ungekuwa makini ungesave kiasi gani!! Inaonekana ni wewe ndio mwenye shida.

Kujenga bongo ni rahisi sana, na ni risky sana kufanya biashara au kuinvest hilo halipingiki (of course ukitoboa umetoboa).. hizi principle za usijenge invest kwanza zinafaa Marekani na Ulaya ambako kujenga ni ghali sana. Bongo ukipata pesa jenga uepushe aibu za hapa na pale.
Uzi umeufunga
 
nilitaka kuongea point kama hii,kufanikiwa kwa yule jamaa yao aliyetumia principles za finance haiwezi kuwa formula kwa watu wote,kama hiyo formula inasaidia watu wote ilitakiwa na wao baada ya kumaliza mijengo yao wangeitumia pia ili watajirike.
Kuna formula zingine zinafaa zina application ulaya huko kwa bongo ni ngumu sana.
Bongo kuna factors nyingi sana ambazo zinaleta variations kwenye business aspects kwa mfano utawala ukibadilika na mifumo yote inabadilika,miundombinu,mambo ya kodi,rushwa yote haya yana affect business na kufirisika ni rahisi sana.
Refer wale wafanyabiashara wa kariakoo walivyotoa vilio vyao na baadhi mitaji yao ilikuwa ni billions of money.
A
Ulitumia miaka mitatu kujenga means by 2016 ulikuwa umemaliza. Kuanzia 2016 hadi leo miaka zaidi ya sita bado haujawa stable, kama ulijenga kwa miaka mitatu imagine hii miaka sita ungekuwa makini ungesave kiasi gani!! Inaonekana ni wewe ndio mwenye shida.

Kujenga bongo ni rahisi sana, na ni risky sana kufanya biashara au kuinvest hilo halipingiki (of course ukitoboa umetoboa).. hizi principle za usijenge invest kwanza zinafaa Marekani na Ulaya ambako kujenga ni ghali sana. Bongo ukipata pesa jenga uepushe aibu za hapa na pale.
Atasevu vipi pesa wakati alikuwa na deni benki la huo ujenzi usiozalisha chochote + gharama kubwa za usafiri?
 
Kuna jamaa yangu Kaenda jenga bonge la mjengo mbondole. Katumia pesa nyingi sana kupambania mjengo ule. Kazi anafanyia posta. Jamaa kashindwa kabisa kuhamia mjengoni badala yake kamuweka mtu amtizamie.

Angetumia ile pesa kuinvest angekuwa mbali. Sasa hivi analalamika maisha yanamchapa anashindwa kula bata kumbe pesa alikopa na anakatwa pesa ndefu ya mkopo.
Kuna uhakika gani ange invest angekua mbali?

Usiwaze tu kua mbali kuna kupoteza
 
Habari,

"Tafuta kiwanja, Jenga, Oa/Olewa, nunua mkoko", njia hii na mawazo haya yamekuwa kwa vijana wengi wanaoanza maisha, hususani waliobarikiwa kupata ajira au biashara zao binafsi ambazo zinawapa kipato flani cha kuendesha maisha yao. Kwa uzoefu wangu hii imekuwa kati ya sababu moja kubwa zinazosababisha watu kuwa maskini na kushindwa kufikia uhuru wa kifedha.

Lakini tujiulize swali la msingi, kwanini watu wengi wameamua kuchagua njia hii ya maisha. Nimefanikiwa kuwahoji watu wengi kidogo kuhusu hili na majibu niliyoyapata mengi yalikuwa kama ifuatavyo:

  • Gharama ya kupanga nyumba ziko juu sana, ni bora kujenga ya kwako.
  • Nyumba ni asset.
  • Usafiri ni shida sana eneo niliko jenga ni bora kuvuta gari yangu.
  • Mama/baba mwenye nyumba ana gubu sana.
  • Nikiwa na kwangu nakuwa na uhuru mkubwa sana.
  • Siku nikifukuzwa kazi au biashara ikiyumba nibaki na pakulala na familia yangu.

Sababu hapo juu nyingi ni za maana kabisa ila tatizo ni kwamba njia zilizotumika kutatua hizo changamoto zinaongeza changamoto zaidi, kivipi?. Ngoja tujadili mambo machache kuhusiana na maisha ya watu wengi hususani mijini (e.g. Dar):

  • Wengi wananunua viwanja maeneo ya mbali kutoka mahali wanapofanyia shughuli zao zinazowapa kipato.
  • Baadhi ya hayo maeneo yana changamoto za miundombinu ya maji, umeme, barabara na hata kiusalama.
  • Wengi wanajenga kwa kuunga unga sana, unaweza jenga nyumba hata miaka sita au zaidi. Kuna msemo wanasema "nyumba haiishi".
  • Nyumba nyingi wanazojenga watu kukaa zinakuwa ni kubwa na za kifahari bila kukumbuka lengo la mwanzo lilikuwa ni makazi tu na sio jengo la maonesho (Hapo utajibiwa kuwa tunajenga mara moja ya kuzeekea)

Kuzingatia hizo hoja hapo juu, yafuatayo yanakuwa ni matokeo ya gharama za maisha baada ya huyu mtu kuhamia kwake:

  • Gharama za usafiri au mafuta zinakuwa juu ukilinganisha na awali.
  • Mazingira yanakuwa sio rafiki kwa familia kuishi, maana nyumba nyingi zinakuwa bado hazijaisha (Wengine wanasema unakuwa unaishi site).
  • Kama una gari, gharama za matengenezo zinakuwa juu kwa sababu ya pengine barabara kuwa mbaya, lakini kwa kuwa unasafiri umbali mrefu kila siku, basi hata service ya gari utafanya mara nyingi zaidi.
  • Pia kama una gari utalazimika kuendesha gari umbali mrefu kila siku, hii si nzuri kwako kiafya.
  • Gharama za umeme na maji pia zinaweza kuongezeka kwa kuwa nyumba ni kubwa sasa na pengine maji hayajafika.
  • Maeneo mengine hata watu hawajahamia wengi hivyo hata usalama unakuwa hatarini.
  • Mara nyingi unaweza ukajikuta mbali na huduma bora za kijamii ikiwemo hospitali, shule, n.k.

***NOTE: Gharama zinaweza kuongezeka ukilinganisha na mwanzo.

Kwanini kuna hofu ya kuwekeza hizo pesa?

Tujiulize swali hili la msingi. Ni kweli baadhi ya watu wanatamani sana kuffanya biashara, lakini wengi wanasema, BIASHARA HAZITABIRIKI. Ni kweli kabisa, lakini ukweli ni kwamba hilo sio tatizo la watu kutokuwekeza.
SHIDA KUBWA NI WATU KUTOKUWA NA ELIMU YA FEDHA. Hili ni jambo la muhimu sana kwa vijana kupata elimu. kwanza kabisa sio kweli kwamba ukitaka kuwekeza ni lazima ukafanye biashara fulani kama kuuza nguo, vinywaji au duka la mangi. Unaweza ukafanya uwekezaji kwa njia nyingi sana ambazo hazitahitaji your active time kuweza kusimamia ila mwisho wa siku ukaja kuwa na uchumi mkubwa kabisa. Uwekezaji huu ni kama mifano ifuatayo:

  • Kununua viwanja na mashamba (Kumba muda unavyokwenda ardhi inapanda thamani lakini nyumba inashuka thamani)
  • Kununua hisa za makampuni
  • Tressury Bonds and Bills
  • Mifuko ya uwekezaji ya pamoja (e.g. UTTAMIS)
  • Fixed deposits accounts
  • Kuwekeza kwenye elimu (Hii sio lazima zile za darasani, inaweza kuwa hata kujiendeleza katika fani flani)
  • N.k.

La muhimu ni kupata elimu sahihi ya mambo ya fedha ili ujue jinsi ya kufanya maamuzi ni vipi utumie pesa yako.


Ngoja nitoe mfano halisi mmoja ulio hai kabisa kwa lengo la kupata uhalisia wa ninacho kisema:

Mwaka 2013 niliajiriwa mahali na tulikuwa kama waajiriwa sita wapya katika hiyo kampuni, mwenzetu mmoja alikuwa na uelewa mkubwa sana wa mambo ya fedha, na mara nyingi alikuwa anatushauri kuhusu haya mambo lakini tulikuwa tunamuona kama kachanganyikiwa: Mimi na wenzangu wengine wa tano tulikwenda mahali tukanunua viwanja na kuanza kujenga kwa kasi sana na badae tukachuku na mikopo kuongeza kasi hiyo. Kwa haraka haraka kwa wastani tuliweza kutenga kama milioni moja kwa mwezi kila mmoja wetu kwa ajiri ya miradi ya ujenzi. Mungu si athumani baada ya miaka mitatu paka minne wote watano tukawa tumehamia kwenye site zetu huku tukiendelea na finishing.

Jamaa alikuwa kila mwezi anaweka milioni moja kwenye mfuko mmoja wa uwekezaji wa pamoja na alikuwa anapata average interest kama ya 11.85% kwa mwaka. Badae akawa ananunua na bond za serikali pamoja na mambo ya kununua mashamba mbali kidogo na mji yakichangamka anakata na kuyauza. Kiufupi jamaa ana zaidi ya milioni 200 kwenye mfuko anaoweka pesa pamoja na kuwa na asset ya viwanja na mashamba na benki ana pesa chafu.

Turudi kwetu tuliojenga na sasa tuna mikoko yetu, umbali wa kwenda na kurudi nyumbani ni 50 Km kila siku. Na pia siwezi pata picha ile hofu ya kwamba nikiachishwa kazi bado ipo maana siwezi nikala nyumba.

Kwa ajili ya muda niishie hapa kwa leo, nipate mawazo ya watu wengine pia. Kiufupi mimi naona kuna mitaji mingi ya biashara na uwekezaji inapotea kwa huu mwamvuli wa kujenga na kununua hii mikoko.

Ahsanteni!!!
Huu uzi ni fantastic!!
Financial Education ndo kila kitu katika kukuza uchumi. Pesa humheshimu mmiliki pale ambapo allocation yake italenga kuzarisha zaidi. Money formula ya 20%,30%,50% ni nzuri sana ikitumika vyema.
 
Back
Top Bottom