Yeah_i wonder why some people wana bother na dar.....see them in heaven.
Watu waliokuja mjini juzi hao, hawajaona Dar enzi za Halmashauri ya Jiji inazoa taka.
Enzi hizo unaenda Posta half of the kids you meet you know from School, libraries (Tanganyika, British Council, American mpaka Russian Centre next to Diamond - sio Diamond Platinum, Diamond Jubilee - kuchukua vitabu vya Propaganda za Kirusi etc), mpira etc.
Dar enzi hizo mtu akikwambia anapenda muziki maana yake anaenda kuchukua music lessons Jumba la Wakorea, watu wanafanya performing arts Russian Cultural Centre mnaenda kukutana na kina Natasha huko. Mashindano ya breakdancing Chuche, Lauli na Omary. Kabla ya mambo ya pool side na ghorofa ya saba na "Yo Rap Bonanza" na marehemu Abdulakim Mgomelo.
Dar parties za kwa Che Mfaume Rd, hapo sijakurudisha enzi za Dar ina Zimamoto inayofanya kazi pale Mwembetogwa.
Dar unamzaba kofi mtoto wa rais (wakati kila mtu jambajamba) halafu unampiga beat akisema kwa mwalimu utamuuilia mbali kabisa, kisha kakuringishia sura ya baba yake kwenye shilingi (lord forgive me, even though I am a non-believer). Such childish impunity!
Leo walugaluga wamekuja wamekuta Dar wenyewe tumewapisha wahemee wanajifanya wanaijua Dar, wakati watu tunaipata na familia zimo katika historia kabla ya kujengwa "nyumba ya saa".
Walugaluga wakisema wanaijua Dar na wajukuu wa Jumbe Tambaza watasemaje?
Nilivyofika NYC zama hizo an old gentleman once told me, akaniambia wale old school New Yorkers ambao wapo hapa long time wanaelewa vitu hawana matatizo.
Ogopa sana walugaluga waliohamia juzi hawajapoteza hata accents wanavyoringia u-New Yorker.
Ndio kitu kile kile kinaendelea hapa.
Watu wa Dar wenyewe wenye viunga kuanzia Upanga, Obay, Kijitonyama, Sinza, Tabata, Mbezi Beach mpaka Mkuranga, Mbezi na kwenda Chanika na Kisarawe huko tunajua debonair ya Dar na decorum inayotakiwa kwa mtoto wa mjini.
Mtoto wa mjini hawezi kuchafua jina kwa deni, hususan la kitoto kama hilo la 200,000. Ukimwambia Mussa Malori "nimetoa sadaka 200,000" atakwambia "hujatoa bado".
Hiyo ni tip tu anapewa doorman anayefungua mlango au bartender a-keep champagne baridi kwa centrigrade inayotakiwa.
Huyo mlugaluga tu, anaharibia debonairs wa Dar.
Ulugaluga as well as being urbanite are both states of mind more than attributes of origin.