Kuihusisha ACT na udini kisa imechagua siasa safi ni mwendelezo wa matusi kwetu

THE BIG SHOW

JF-Expert Member
Feb 28, 2012
16,365
12,823
Friends and Our Enemies,

This is the last kick of the dying horse,

Chadema, wanaharakati uchwara, wafia dini na wapinga maendeleo ya nchi wamefikia hatua ya mwisho sasa.

Wameona kuwa hila zao, uongo wao na lugha zao chafu baada ya kukataliwa na wananchi wameona sasa waanze choko choko na vyama vingine vya upinzani ambavyo vimeamua kujitenga nao katika upuuzi wao usio na mbele wala nyuma.

ACT WAZALENDO NA CUF siyo vyama pekee vya upinzani ndani ya taifa hili ambavyo vimeamua kujitenga na chagadema na hao maaskofu katika suala hili, la hasha hata kidogo, vipo vyama vingi sana vya siasa ndani ya nchi hii ambavyo vimeona kinachoendelea siyo uzalendo, bali ni maslahi ya tumbo na siasa chafu za watu wachache tuh wasio na akili timamu.

(i) ACT, CUF na vyama vingine vitashiriki vipi na chadema na hao wanaojiita maaskofu katika suala hili ili hali toka mwanzo wa sakata hili wameonesha nia ya kuvunja muungano kwa kuingiza utanganyika na uzanzibar?

(ii)ACT, CUF na vyama vingine watashiriki vipi na wao ili hali mwanzao tuh wa sakata hilo wamejiingiza katika siasa chafu za kumkashifu kiongozi wa nchi mara wampe lugha zisizo na staha eti mara mvaa ushungi na kadhalika?

(iii) ACT, CUF na vyama vingine wataungana nao vipi hawa chadema na hawa wanaharakati uchwara ili hali mwanzo tuh wameshaonesha kuligawa taifa kwa kushirikisha viongozi wa dini i.e hao maaskofu kwenye majukwaa ya kisiasa huku wote kwa pamoja wakiacha kuzungumza hoja na kuegemea kuitukana serikali?

Ni mtu mjinga tuh ambae anaweza kukubali kushirikiana na watu wanaonuka harufu mbaya ya kila aina ya siasa chafu na zilizofeli kama chadema na hao maaskofu hao.

Sasa kwa hali ilipofikia wanazidi kujiharibia kwani wanafikia hatua ya kuunasibisha uislam na mtu kama Zitto Kabwe au Prof Lipumba eti ya kwamba wamesusa kushiriki harakati zao mfu eti kisa wanapigania imani, wanatutaka nini waislam hawa chadema na vibaraka wao?

Hawawezi kufanya siasa zao bila kushirikisha kivuli cha dini ndani ya nchi hii?

Kama ACT & CUF wamegoma kushirikiana nao, kwanini wasitafute angle nyingine ya kuwatazma nayo wakimbilie kwenye angle ya udini?

Nichukue fursa yangu kuwapongeza ACT, CUF na vyma vingine vya upinzani kwa kuukwepa huu mtego,na kwa hakika mtego huo wamejitegea wenyewe na wamenasa wenyewe, sisi wananchi ndiyo ambao tutawahukumu panapo majaliwa ya uhai ifikapo hapo 2025 Insha Allah.

Wajifunze namna ya kuendesha siasa safi za kuunganisha nchi,na siyo siasa chafu za kuzigawa nchi kisha wakatarajia kuwa watu wenye akili zao timamu watawaunga mkono.
 
Ku mute huku mikataba ya rasilimali za Taifa ikiwa haina tija kwa Taifa huyo ni... Mnufaika 👇👇

Screenshot_20210420-100928.png
 
ACT ni chama cha Waislamu. Mikutano yao wanajaa maustaaz.
Chadema ni chama cha Wakirsto. Mikutano yao wanajaa wachungaji.

Razima tuambiane ukweri.
 
ACT ni chama cha Waislamu. Mikutano yao wanajaa maustaaz.
Chadema ni chama cha Wakirsto. Mikutano yao wanajaa wachungaji.

Razima tuambiane ukweri.
na majiz ya kura ya ccm ni lichama la warabu na waislam tunaomba wakristu walimimbie hilo lichama.
 
Back
Top Bottom