GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 4,695
- 6,398
Nimeamua kuuleta huu uzi kutokana na mada kadhaa nilizoziona humu JF zinazoongelea vituo vya watoto yatima kwa mtazamo hasi. Baadhi ya watu wametamani hata hivyo vituo visipewe misaada au vifutwe kabisa.
Uzi ulionichochea hasa ni wa Bexb alioutoa 04/10/2023 wenye kichwa, NIFAHAMISHE KITUO CHA WATOTO YATIMA CHENYE UHITAJI MKUBWA SANA.
Ingawa mleta mada alionekana kuwa na shauku ya kutaka kuhakikisha kuwa msaada husika utaelekezwa mahali sahihi, kuna baadhi ya wachangiaji waliomkejeli na wengine kuonesha hali ya kutokuwa na imani na vituo vya kulelea watoto, maarufu kama vituo vya watoto yatima.
Kwa kuwa kuna ninayoyafahamu yaliyo mazuri yanayotendwa na vituo vya watoto, nimeona niyashirikishe humu jukwaani kwa lengo la kuwatia moyo Watanzania wenzangu , na watu wengine pia, wasione tashwishwi kuvisaidia vituo hivyo kulingana na uwezo waliojaliwa na Mungu.
Ni kweli kuwa kuna baadhi ya vituo vinavyotenda isivyo sahihi, lakini si sababu ya msingi kuhukumu kuwa vituo vyote vya kulelea watoto ni vya kimagumashi.
Na hata vinavyotumika vibaya, kuvifungia au kukataa kuvisaidia si suluhisho. Kufanya hivyo ni kuwatesa zaidi watoto wanaolelewa humo. Watoto wanaweza kuumia zaidi kuliko wamiliki wa hivyo vituo. Ni kuwahukumu (watoto) kwa kosa lisilowahusu.
Ikitokea ikabainika kuna vituo vinatumika ndivyo sivyo, badala ya kuchukua maamuzi yatakayowaumiza watoto, ni bora wahusika wachukuliwe hatua stahiki, ikilazimu, wanyang'anywe hivyo vituo, na kukabidhiwa kwa watu watakaoweza kuviendesha kwa kuzingatia sheria za nchi na maslahi ya watoto.
Huu ni utangulizi. Nitakuja na sehemu ya kwanza, ya pili, ya tatu, n.k. kwa kadiri nikakavyokuwa nikipata muda.
Lakini narudia kutazamisha, kuwa pamoja na kuweko kwa vituo vya "kimchongo" vya kulelea watoto, kuna vingine vingi tu vinavyofanya kazi nzuri sana ya kuwahudumia watoto "wetu" kwa moyo wa upendo.
Ndiyo, ni watoto wetu kwa sababu ama wamezaliwa na Watanzania, au basi wamezaliwa nchini mwetu, Tanzania. Ni sahihi kusema, ni watoto wetu, ni ndugu zetu, ni wenzetu! Tuwasaidie kwa hali na mali, kwa kadiri ya uwezo wetu.
Tukutane tena baadaye kidogo!
Asante.
NB: Niyaelezayo ni ushuhuda binafsi uliotokana na uzoefu wa kufanya kazi kwa miaka kadhaa (katika ngazi ya utawala) kwenye kituo cha kulelea watoto. Hata hivyo , isichukukliwe kuwa vituo vyote vipo hivyo. Ukweli utaendelea kubaki kuwa kuna vitu vinavyotoa huduma kwa uaminifu na kuna vya kimagumashi.
Sitataja jina la kituo wala mkoa isije ikaleta mtazamo kuwa pengine ninawapigia kampeni.
Uzi ulionichochea hasa ni wa Bexb alioutoa 04/10/2023 wenye kichwa, NIFAHAMISHE KITUO CHA WATOTO YATIMA CHENYE UHITAJI MKUBWA SANA.
Ingawa mleta mada alionekana kuwa na shauku ya kutaka kuhakikisha kuwa msaada husika utaelekezwa mahali sahihi, kuna baadhi ya wachangiaji waliomkejeli na wengine kuonesha hali ya kutokuwa na imani na vituo vya kulelea watoto, maarufu kama vituo vya watoto yatima.
Kwa kuwa kuna ninayoyafahamu yaliyo mazuri yanayotendwa na vituo vya watoto, nimeona niyashirikishe humu jukwaani kwa lengo la kuwatia moyo Watanzania wenzangu , na watu wengine pia, wasione tashwishwi kuvisaidia vituo hivyo kulingana na uwezo waliojaliwa na Mungu.
Ni kweli kuwa kuna baadhi ya vituo vinavyotenda isivyo sahihi, lakini si sababu ya msingi kuhukumu kuwa vituo vyote vya kulelea watoto ni vya kimagumashi.
Na hata vinavyotumika vibaya, kuvifungia au kukataa kuvisaidia si suluhisho. Kufanya hivyo ni kuwatesa zaidi watoto wanaolelewa humo. Watoto wanaweza kuumia zaidi kuliko wamiliki wa hivyo vituo. Ni kuwahukumu (watoto) kwa kosa lisilowahusu.
Ikitokea ikabainika kuna vituo vinatumika ndivyo sivyo, badala ya kuchukua maamuzi yatakayowaumiza watoto, ni bora wahusika wachukuliwe hatua stahiki, ikilazimu, wanyang'anywe hivyo vituo, na kukabidhiwa kwa watu watakaoweza kuviendesha kwa kuzingatia sheria za nchi na maslahi ya watoto.
Huu ni utangulizi. Nitakuja na sehemu ya kwanza, ya pili, ya tatu, n.k. kwa kadiri nikakavyokuwa nikipata muda.
Lakini narudia kutazamisha, kuwa pamoja na kuweko kwa vituo vya "kimchongo" vya kulelea watoto, kuna vingine vingi tu vinavyofanya kazi nzuri sana ya kuwahudumia watoto "wetu" kwa moyo wa upendo.
Ndiyo, ni watoto wetu kwa sababu ama wamezaliwa na Watanzania, au basi wamezaliwa nchini mwetu, Tanzania. Ni sahihi kusema, ni watoto wetu, ni ndugu zetu, ni wenzetu! Tuwasaidie kwa hali na mali, kwa kadiri ya uwezo wetu.
Tukutane tena baadaye kidogo!
Asante.
NB: Niyaelezayo ni ushuhuda binafsi uliotokana na uzoefu wa kufanya kazi kwa miaka kadhaa (katika ngazi ya utawala) kwenye kituo cha kulelea watoto. Hata hivyo , isichukukliwe kuwa vituo vyote vipo hivyo. Ukweli utaendelea kubaki kuwa kuna vitu vinavyotoa huduma kwa uaminifu na kuna vya kimagumashi.
Sitataja jina la kituo wala mkoa isije ikaleta mtazamo kuwa pengine ninawapigia kampeni.