Ni kwanini ccm mna tabia ya kujibu hoja bila kuweka data? Zitto kaja na data anazoziamini ambazo zinapinga data zilizotolewa na serikali, ni kwanini basi badala ya kutaja mlolongo wa miradi msiseme juu ya madeni ya nje na ndani mmeyalipa kwa kiwango gani kutokana na makusanyo yenu?Zito hujui kuwa bajeti ya serikali mapato yake hutokana na makusanyo ya ndani na mapato ya Nje?
Kosa la rais kutekeleza kwa pesa za kukopa si kuvunja Sheria. Uchumi wa Nchi yetu bado haujafikia hatua ya kujitosheleza kulipia bajeti yote.
Kauli ya Mhe rais kuhusu kuongezeka kwa makusanyo ya ndani ni kweli acha kupotosha takwimu za serikali.
Naamini sasa umebaki unalia kama debe tupu huku ukidhani utaendelea kuwadanganya watanzania hutaweza
Kama kweli kwa uhalisia wa ukusanyaji mnaotamba kuwa nao lipeni madeni ya walimu na pensheni za wastaafu basi kwa kasi hiyohiyo ya ukusanyaji!
Hiyo miradi si ipo kibajeti au kuna ya dharura?
Zitto might be right kama majibu ndiyo yale ya jana!