Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,581
- 18,124
Muda mfupi uliopita kamati ya Nidhamu ya chama cha ANC imemfungia Julius Malema kwa mika mitano na kumvua madaraka ya Urais wa Vijana pamoja na Msemaji wa ANCYL Floyd Shivambu. Malema ameonekana kwamba amechochea mgawanyiko ndani ya chama na serikali
Kilichomponza Julius Malema ni msimamo wake wa kupigania maslahi ya vijana na class ya chini ambayo haioni fursa ya kusonga mbele kwa matumaini huku uchumi wa nchi ukiendelea kuwa mikononi mwa Makaburu. Bado vijana wa Afrika kusini kama walivyo vijana wa Tanzania wanaishi kwa matumaini na hofu juu ya kesho yao. Hoja alizokuwa akipigania Malema za kufanya reforms katika sekta ya madini na Ardhi kwa maslahi ya maskini walio wengi iliungwa mkono kwa nguvu
Hoja nyingine ya kuangusha serikali vibaraka kama Botswana na kumuunga mkono Robert Mugabe imetumika kama chambo tu ili kughilibu matakwa na maslahi ya vijana na maskini wa Afrika kusini ili kukwepa kuwajibika kufanya reforms.Madai ya Julius Malema ni ya Msingi sana kama kweli Afrika kusini inataka Taifa lisonge mbele na kuepuka mapambano ya kitabaka yaani class struggle ambazo zitachochea ubaguzi zaidi.
Kitendo cha kumfukuza Julius Malema ni mwendelezo wa viongozi dhaifu na usaliti kwa umma huku wakijitahidi kukimbia matatizo yanayohitaji suluhisho. Mwenyekiti wa chama Jacob Zuma atawaambia nini au atawapa majibu gani vijana wa Afrika Kusini walioandamana juzi tu tarehe 28-29 mwezi uliopita wakiongozwa na Julius malema katika ku-address matatizo yao? Je kumfukuza Malema na viongozi waandamizi wa ANCYL ni suluhisho au jibu la msingi kwa yale waliyokuwa wanayasimamia?
Inaeleweka wazi sasa viongozi wa Afrika wanapokuwa madarakani hugeuka kuwa masultani na miungu mtu huku wakijitungia kanuni zilizoandikwa au ambazo hazijaandikwa kunyamazisha,kutisha na kuminya demokrasia pale maslahi yao ya kisiasa na kijamii yanapoguswa. Jacob Zuma na viongozi wenzake wanadhihirisha kwamba kuna mstari mwembamba kati ya hulka zao na zile za makaburu na pia mtazamo wao juu ya wananchi wa Afrika kusini na Hatima yao. Jacob Zuma anaonekana kuweka mkakati wa wazi wazi kwa kuhofia uwepo wa Malema ndani ya chama hicho ungemfanya awe one term president kwa sababu Malema alishatangaza kutomuunga mkono Mwenyekiti wake Uchaguzi ujao ndani ya Chama. Zuma anahofia kilichomkuta Thabo mbeki yeye akiwa Kapteni iliyomghilibu Mbeki pamoja na Malema aliyefanya kazi kubwa kwa imani kwamba Zuma angesimamia maslahi ya vijana na wananchi maskini.
Vijana wa Tanzania hatuna tofauti na vijana maskini wa Afrika kusini na pia viongozi wetu ingea si wote katika vyama vyetu vya siasa hawana tofauti na Jacob zuma wa Afrika Kusini. Wote wanataka kuwatumia vijana kwa ajili ya maslahi yao au kama Daraja. Tusikubaliane na hilo ni lazima tuingie mezani tuangalie ni kitu gani ambacho kila mmoja analeta. Najua kwa tabia za kuiga hata mambo yasiyo na faida hata viongozi wetu kwenye vyama vya siasa watakurupuka kuiga na kuifanya ANC kuwa Role model wao katika kunyamzisha sauti zinazohoji au zisizotaka kuburuzwa bila kujua ANC ya sasa ni ya makaburu weusi si ile ya akina Mandela tena.Sasa succeccion battle imekuwa too bitter, ANC itakuwa even more divided. Ni jukumu la Julius Malema na vijana kusimama kidete sasa hadi msaliti wa vijana na maskini wa Afrika Kusini Jacob Zuma aondoke!
Vyama vya siasa vishughulikie matatizo ya msingi na visikilize sauti za vijana. Makosa yarekebishwe, vijana wanastahili kusikilizwa na kusaidiwa na sio kutishwa. ANC itachochea mgawanyiko zaidi na kama vyama vya siasa Tanzania tunataka kutatua migogoro kwa njia hii basi igeni muone
Kilichomponza Julius Malema ni msimamo wake wa kupigania maslahi ya vijana na class ya chini ambayo haioni fursa ya kusonga mbele kwa matumaini huku uchumi wa nchi ukiendelea kuwa mikononi mwa Makaburu. Bado vijana wa Afrika kusini kama walivyo vijana wa Tanzania wanaishi kwa matumaini na hofu juu ya kesho yao. Hoja alizokuwa akipigania Malema za kufanya reforms katika sekta ya madini na Ardhi kwa maslahi ya maskini walio wengi iliungwa mkono kwa nguvu
Hoja nyingine ya kuangusha serikali vibaraka kama Botswana na kumuunga mkono Robert Mugabe imetumika kama chambo tu ili kughilibu matakwa na maslahi ya vijana na maskini wa Afrika kusini ili kukwepa kuwajibika kufanya reforms.Madai ya Julius Malema ni ya Msingi sana kama kweli Afrika kusini inataka Taifa lisonge mbele na kuepuka mapambano ya kitabaka yaani class struggle ambazo zitachochea ubaguzi zaidi.
Kitendo cha kumfukuza Julius Malema ni mwendelezo wa viongozi dhaifu na usaliti kwa umma huku wakijitahidi kukimbia matatizo yanayohitaji suluhisho. Mwenyekiti wa chama Jacob Zuma atawaambia nini au atawapa majibu gani vijana wa Afrika Kusini walioandamana juzi tu tarehe 28-29 mwezi uliopita wakiongozwa na Julius malema katika ku-address matatizo yao? Je kumfukuza Malema na viongozi waandamizi wa ANCYL ni suluhisho au jibu la msingi kwa yale waliyokuwa wanayasimamia?
Inaeleweka wazi sasa viongozi wa Afrika wanapokuwa madarakani hugeuka kuwa masultani na miungu mtu huku wakijitungia kanuni zilizoandikwa au ambazo hazijaandikwa kunyamazisha,kutisha na kuminya demokrasia pale maslahi yao ya kisiasa na kijamii yanapoguswa. Jacob Zuma na viongozi wenzake wanadhihirisha kwamba kuna mstari mwembamba kati ya hulka zao na zile za makaburu na pia mtazamo wao juu ya wananchi wa Afrika kusini na Hatima yao. Jacob Zuma anaonekana kuweka mkakati wa wazi wazi kwa kuhofia uwepo wa Malema ndani ya chama hicho ungemfanya awe one term president kwa sababu Malema alishatangaza kutomuunga mkono Mwenyekiti wake Uchaguzi ujao ndani ya Chama. Zuma anahofia kilichomkuta Thabo mbeki yeye akiwa Kapteni iliyomghilibu Mbeki pamoja na Malema aliyefanya kazi kubwa kwa imani kwamba Zuma angesimamia maslahi ya vijana na wananchi maskini.
Vijana wa Tanzania hatuna tofauti na vijana maskini wa Afrika kusini na pia viongozi wetu ingea si wote katika vyama vyetu vya siasa hawana tofauti na Jacob zuma wa Afrika Kusini. Wote wanataka kuwatumia vijana kwa ajili ya maslahi yao au kama Daraja. Tusikubaliane na hilo ni lazima tuingie mezani tuangalie ni kitu gani ambacho kila mmoja analeta. Najua kwa tabia za kuiga hata mambo yasiyo na faida hata viongozi wetu kwenye vyama vya siasa watakurupuka kuiga na kuifanya ANC kuwa Role model wao katika kunyamzisha sauti zinazohoji au zisizotaka kuburuzwa bila kujua ANC ya sasa ni ya makaburu weusi si ile ya akina Mandela tena.Sasa succeccion battle imekuwa too bitter, ANC itakuwa even more divided. Ni jukumu la Julius Malema na vijana kusimama kidete sasa hadi msaliti wa vijana na maskini wa Afrika Kusini Jacob Zuma aondoke!
Vyama vya siasa vishughulikie matatizo ya msingi na visikilize sauti za vijana. Makosa yarekebishwe, vijana wanastahili kusikilizwa na kusaidiwa na sio kutishwa. ANC itachochea mgawanyiko zaidi na kama vyama vya siasa Tanzania tunataka kutatua migogoro kwa njia hii basi igeni muone