View attachment 1680616
Jamani hapa ni juzi tarehe 6 Jan huyo mnayemwona katikati kama hapa kwetu ni waziri kukuu Kasim Mjaliwa bungeni Dodoma, wanausalama wakijaribu kuokoa maisha yake mbele ya waandamanaji wenye democrasiya ya kutosha duniani.
View attachment 1680626
Hawa si FBI au US Army, hawa ni raia wema ambao wanatimiza haki yao ya kidemocrasia wakiwa wamebeba siraha za kivita fulu magazini ktk maandamano, wakati huku kwetu kwa Magu hata gusa tu barabara ugusi.
View attachment 1680627
Waandamanaji wakiwa nje ya jengo la serikali huku wakiwa na siraha za kijeshi na nzito tayari kwa lolote lile kutimiza haki ya ya kidemocrasia.
View attachment 1680628
Hapa muandamanaji akichukuwa selfii kwa ajiri ya kuwatumia jamaa zake huku yeye na mwenzake wakiwa na siranzito kuliko zile tulizotumia mwaka 1978 kule Mutukula Uganda kumwondoa Idi amini.
Jamani zimebaki siku tatu 2 kufutika kwa taifa ambalo lilikuwa linapigiwa mfano kila kuitwapo leo kuwa mababa wa democrasia duniani Marekani. Tangia mwaka 1992 milango ilipofunguliwa tume kuwa tukiubiliwa na sisi tuwe na democrasia kama ya Marekani mpaka tumechoka.
Sijui kama nyakati za mwisho zimefika, wakati mimi ukusanyaji wa sadaka bado haujanitosha. Naelekeza swali kwa wanaharakati wa Tanzania ambao wamekuwa wakisisitiza kwa miongo kadha sasa kuwa tufuate siasa na democrasia za Marekani leo wanahoja gani kwani siwaoni wala kuwa sikia kanakwamba hawapo au awaoni chochote.
Maduka ya siraha yanafanya biashara kuliko wakati wowote tangia kuruhusiwa kununua sira nchini humu, kila raia anajaribu kununu mkwasa wake hili kunukishiana kama ilivyotokea kwa Wahutu na Watusi na sasa leo ngoma imeamia kwao.
Bwana mmoja ambaye yeye alikuwa anataka kununua lile la kuweka begani lakini ilishindikana hivyo wameamua kwenda wekshopu kutengeneza wenyewe, taarifa sisizo rasmi lakini zenye ukweli kuwa siku hiyo ya kuapishwa Biden ndiyo huo mchezo wa kuchezea moto juu ya tanki la petroli utaanza kuchezwa nchini Marekani
View attachment 1680690
Macho ya dunia nzima yatakuwa yakishuhudia mwisho wa kitu kinanachitwa democrasia duniani.
Taarifa tulizopata ni kuwa kilakitu kitalipwa hapa hapa duniani kwani sitaki kusema mengi ila wafuasi wa Trump na Biden wanapishana katika maduka ya siraha kuhakikisha wanapata bunduki nzuri na risasi za kutosha kwa kazi ya siku hiyo.
Taasisi za kidini pia nazo zimemiminika katika viwanda na maduka hili kuweza kujipatia siraha kwaajili ya kuwa tayari kwa chochote siku hiyo kwani hawana hakika na maombi tupu.
Tayari watu 5 akiwemo polisi mmoja wamekwisha fariki dunia wakati wa maandamano ya kuvamia bunge wakitimiza haki yao ya kidemocrasia ya kuandamana kama Lisu na Mbowe walivyokuwa wakisisitiza ndiyo maana leo nimeelewa kauli ya Mtu huru aliyekuwa anasherehekea sikukuu zote Segerea aliwai kusema Tanzania lazima ibebe majeneza wakifa watu 100 au 200 tutapata haki. Kumbe alijifunza huko na leo Mungu kaweka wazi Wamerekani wanatafuta haki na bundiki.
Vijana wa Tanzania na wana harakati Mungu wa baba zetu Afrika na atusaidi tujikwamue kutoka katika utumwa wa kiakili.
Na aimidiwe Mungu wa baba zetu Afrika kwani majibu yameanza kupatika.
Mtoto wa mchungaji nawasilisha.