Kubadili matokeo IV 2012: Prof. Mukandala aivimbia serikali!

Kwa kweli maamuzi yaliyofanywa na kamati ilyoundwa kufuatilia suala la matokeo mabovu ya kidato cha nne yalikuwa ni ya kukurupuka, na yalifanywa bila kufikiriwa sawasawa. Najaribu kuwaza concept ya kustandardize matokeo, ni kwa faida ya nani? Kujifurahisha kwa kuona tunarekodi za vijana wengi waliofaulu bila kuzingatia ubora wa elimu na uwezo wa hao wanafunzi wenyewe? Si haya aliyosema Richard Mabala kuwa ni sawa na kupanua goli ili mtu afunge!!! Haya ni Maamuzi yasiyo na tija. Nampongeza sana Prof. Mkandala kama kweli atasimamia msimamo huo.

Tatizo la matokeo mabaya haliko kwenye kustandardize wala hizo grades mpya, tatizo ni mfumo mbovu wa elimu nchini. Na matatizo haya si mageni, maana yalishazungumzwa sana. Matatizo ni kama kukosa nyenzo za kufundishia, uhaba wa walimu, uhaba wa vifaa vya maabara, maslahi duni ya walimu, mazingira magumu ya kufundishia, ukosefu wa majengo ya kutosha, ubovu na uchakavu wa madarasa na nyumba za walimu, nk nk
Serikali ilipaswa iyatatue haya na si kukimbilia kkwenye kufuta matokeo na kustandardize matokeo maana matokeo haya ni kuwa na WASOMI wasio wasomi ambao kimsingi NDIYO hao wanaotuletea MATATIZO kwenye hii SERIKALI yetu ya sasa. Baadhi ya viongozi wetu ni vihiyo wa kutupwa, wana PHD ama Masters za magumashi na matokeo yake ndiyo haya kukurupuka kutoa maamuzi ambayo hayana tija kwa watanzania.

Hii ndio shida ya kuchanganya taaluma na siasa. Wanasiasa wamezoea uongo kila kitu wanataka kudanganya na kujidanganya wenyewe. Kama walitaka kuona hayo matokeo ya kupeana pasipo taaluma kuzingatiwa bora wangetoa maagizo mapema ili waliosahihisha na kupanga hayo matokeo wafuate viwango vya hao wanasiasa na si viwango vya kitaaluma. Tatizo wanasiasa wa nchi hii kila kitu wao wanaweza tuwaachie wanataaluma wafanye yao nanyi mfanye siasa zenu
 
Wakijiuzulu itakuwa shangwe, vifijo na nderemo kwa Waislam. Nawashauri wasijiuzulu kwa sababu wakijiuzulu tu JK atawateua Waislam kuongoza nafasi hizo.

Mkuu tafadhali sana hebu ondoa maswala yako ya udini kwan hapa sisi tupo tunajadiliana maswala ya kitaaluma ambayo yanawagusa wananchi directly bila kujali itikadi zao za kisiasa na kidini.
 
Binafsi sihafiki kubadili matokeo,kikubwa ni kupanga mikakati madhubuti ya kuhakikisha matokeo yajayo ufaulu unaongezeka maradufu.

Sawa wanaweza fanya hivyo ili kujilizisha na kuwaridhisha wazazi na vijana waliofeli,lakini hapo mbeleni vijana hawa watapata tabu sana na kikubwa zaidi itawabwetesha walioko mashuleni kwa kudhani kuwa hata wao watafanyiwa hivyo pindi matokeo yao yakiwa mabaya.Na ikumbukwe kuwa muendelezo huu wa huruma za kitaaluma katika elimu utaijenga jamii tegemezi kifikra na kimtazamo na matokeo yake ni kukosa wataalamu waliobobea katika nyanja mbalimbali za uzalishaji mali.
 
Kwa hiyo tunafurahi hawa watoto wakafanye kazi za u house girl na house boy,na shamba boy?Na pia waew vibaka ,ukipaki gari yako uibiwe vitu vya gari?fikirieni sana.


mkuu hatuwezi kuondoa tatizo la ajira mbaya kwa kuwapa maksi za bure watoto wetu tutaua taifa letu...taifa linaitaji wataalamu wenye ujuzi na uwezo sio wa kupewa maksi za bure...tukiwapa mafunzo mazuri hawa watoto uko mashuleni watafaulu tu,hatutaitaji kuwapa nyongeza ya marks.
 
Mama Ndalichako linda heshima yako, usitake wanasiasa wakushushe chini. Wao wanaacha kutimiza wajibu wao wa kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora halafu wanataka wewe uwawekee mambo sawa. Wao si wako na mambo ya bora elimu ambayo hakuna waalim, vitendea kazi, maslahi mabovu halafu iweje? Ukiachia ngazi vyo vingi vikuu viko vingi vitakupokea kwa shangwe. Wewe mama ni mwalimu bora na very strict.Umeiweza NECTA, umefanikisha kuzuia kuvuja kwa mitihani. Na ndiyo maana wakiingia chumba cha mtihani wanaona nyota maana jana yake wanakuwa wamesoma paper fake. Ha ha ha!!
 
Bora Prof Mukandara ajiuzuru. huyu kawambwa kashindwa kabisa kuendesha ile wizara . sidhani kama bajeti yake itapita bila kujiuzuru yeye mwenyewe
 
Mwenyekiti wa Baraza la Mitihani la Taifa-NECTA ambaye pia ni Makamu Mkuuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,Prof.Rwekaza Sympho Mukandala amesema hayuko tayari kubadili matokeo ya Kidato cha Nne.

Chanzo cha karibu cha Prof.Mukandala kinadai kuwa mara baada ya kutolewa taarifa ya Serikali inayotaka 'kuboreshwa' kwa matokeo hayo,Prof.Mukandala ameonesha kukataa amri hiyo hadi sasa. 'Sisi tulipitisha matokeo hayo mbele yao na kwa idhini yao.

Iweje leo Baraza libadili matokeo?.Tunafanya hivi kwa faida ya nani na kwa ustawi wa elimu ya wapi?' alinukuliwa akihoji Prof.Mukandala.

Habari za kuaminka zinadai kuwa Prof.Mukandala pamoja na Katibu Mtendaji Dr.Joyce Ndalichako wanajiandaa kuachia ngazi kama Serikali itasimamia uamuzi wake huo.

Mengi yatafuata. Kaeni chonjo! VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam (sasa Dodoma)

Wana kila sababu ya kusimamia uamuzi wao.Haiingii akilini 21% uite ni kufaulu kama kweli una nia njema na Elimu.
Wadau wanatakiwa kuwa unga mkono katika uamuzi huo.
Kinachoendelea ni Mawaziri husika kujikwamua na zogo lakutakiwa kujiuzulu.
Waziri Kawambwa atupe majibu kwanini Ripoti hii haikuwahi kutolewa wala kufanyiwa kazi?


 
binafsi ningependa kusimama upande wa msimamo wa prof. Mkandara, haya mapungufu yooote yanajulikana fika, si ya leo wala jana, tatizo kubwa ni hao tunaowapa/wanaopewa hizo nafasi, baadhi yao hata taaluma zao ni za kutia shaka, wameshindwa kuwa wabunifu,ni watu wanye fikra za maisha ya leo bora liende pasi na kufikiria kesho itakuwaje, matokeo yake ni kama tunabahatisha sasa,suala la mitaala bado ni kizungumkuti na hakuna hata anayestuka
 
Wazira ifumuliwe na Baraza livunje na tuwe na mitaala yenye kueleweka.

Mtindo wa kujichimbia na matokeo baada ya mtihani kusahihishwa ili kupanga matokeo pale baraza uishe.

Yule Padri mkuu wa kitengo cha kupanga matokeo apewe mafao yake na asiganyage tena pale Baraza la Mitihani.

Mukandala,Kawamwa na Ndalichako sio wajiuzuru bali wafukuzwe kazi,hakuna kuwapa kazi sehemu nyingine yoyote mpaka wakalime nyanya ili liwe fundisho kwa wengine



mkuu mie naona kama wakienda kulima nyanya itakuwa ni bora kuliko kufanya kazi na vilaza kama Lukuvi....by the way kilimo cha nyanya ukiwa siriaz kinalipa kuliko ivyo vyeo vyao ni wewe tu zao la Mulugo haujui ilo na sikulaumu,nailaumu system.
 
Akiachia ngazi Ndalichako itakuwa sawa na Kuvuja kwa Pakacha. Huyu mama amelalamikiwa sana, hata kama ni mtendaji mzuri lakini lawama zikizidi ni bora kutafuta ustaarabu mwingine. Mbona elimu yake ni nzuri tu aachane na hiyo kazi ya NECTA ni kama imemshinda vile. Sifa ya kiongozi mzuri ni pamoja na ku_manage Public Relations
Amelaumiwa na nani mkuu? Au na wewe ni mmoja mmoja wanaolaumu? Unaweza kunipa sababu gani za msingi za kiutendaji unazodhani kwamba zinamfanya aonekane ni tatizo? taja tatu tu!
 
Kawambwa na Mulugo wanamatatizo sana, yakibadilishwa bora wakamatwe na kupelekwa rumande, ni wanafunzi wangapi wamejiua kwa matokeo hayo? napata shida kuelewa uwezo mdogo walionao viongozi hawa na kupewa nyadhifa nzito walizonazo!
 
mkuu mie naona kama wakienda kulima nyanya itakuwa ni bora kuliko kufanya kazi na vilaza kama Lukuvi....by the way kilimo cha nyanya ukiwa siriaz kinalipa kuliko ivyo vyeo vyao ni wewe tu zao la Mulugo haujui ilo na sikulaumu,nailaumu system.

Unataka wafanye kazi na Sugu,Lema na Mbowe?Ok nyie ndio wale munaopewa mitihani kule kwenye shule zenu,munakuja na point 7 lakini munaburuzwa na wenye point 25.

Wizara na Baraza vioza hivyo basi zifumuliwe na tuwe na mitaala yenye kuelewa si double standard ya sasa,mtihani mmoja mitaala tofauti poor mind

Watu watimuliwe huko wakalime nyanya wasipewe kazi sehemu nyingine yoyote.
 
Unataka wafanye kazi na Sugu,Lema na Mbowe?Ok nyie ndio wale munaopewa mitihani kule kwenye shule zenu,munakuja na point 7 lakini munaburuzwa na wenye point 25.

Wizara na Baraza vioza hivyo basi zifumuliwe na tuwe na mitaala yenye kuelewa si double standard ya sasa,mtihani mmoja mitaala tofauti poor mind

Watu watimuliwe huko wakalime nyanya wasipewe kazi sehemu nyingine yoyote.


wapi uko au mum? mtaishia kujifariji ivyo ivyo..lakini ukweli mnaujua ni kina nani ndio cream ya nchi hii.


kilimo cha nyanya kinalipa sana mkuu mara milion nyingi ya kuuza kahawa na kashata,sema unadharau tu bure.
 
kama mwl mstaafu hili tamko la kurekebisha matokeo haliniingii akilini kabisa,ila kwa vile liko kisiasa zaidi nawatakia kila la heri.
 
Back
Top Bottom