Kuachwa kunauma jamani

Kuachwa kunauma jamani

Nilikuwa na mpenzi kwa muda wamiaka miwili lakini alikua aniambii ukweli.Siku moja nikaamua kumuuliza hivi nini malego yetu akajibu ninamsichana mwingine tena anarudi hivi karibuni kwahiyo tusitishe mahusiano.Naombeni ushauri wana JF

Sasa si umeuliza malengo...na ukajibiwa! Hujatuambia kama umekubaliana na malengo au la..tushauri nini?!
 
akomae tu najua now atakuwa nalia balaaa ila ndiyo kashaamua tu nenda mwana kwenda

miaka miwili katembezewa bakora, na anajua kichwa wazi wa jamaa alivyo mkali, leo amuachie kirahisirahisi!!!?

usimshauri mwenzio awe chizi baada ya siku moja
 
pole shoga ila wanawake inabidi tujielewe na tujue kujipenda kwanza sisi wenyewe. we mtu hujazaliwa nae hafu unampa moyo wako wote wa nini. siku zote mwanamke penda kwa kutumia akili sio moyo wala hutapata shida ya kuumizwa ukishafunga ndoa ndio ufungue moyo wako kwa 50% zingine baki nazo. hafu mtu anae kupenda kwa dhati utamuona tu atakuwa yupo makini kupanga mipango na ww atakushirikisha mambo yk na kadhalika.
 
Watu wa namna hii waache waende zao tena kwa wemaa...kuwa muungwana kwake ile mbaya...halafu baadae litakapo geuka huko alipo...akikujia mkubali na wewe muache kama alivyokuacha wewe....Atasikilizia utamu...atalia kuliko wewe

aiseeee mimi nilishindwa hii kitu aiseee
 
Pole best kubali kabisa kwamba ndiyo mwisho,mshukuru Mungu kwa kukuepusha na janga hilo,sasa jipende mwenyewe sana kuliko ulivyokuwa unajipenda mwanzo,kula vizuri,piga pamba za uhakika,fanya kazi kwa bidii jipe muda mzuri wa kupumzika na ukipumzika usimuwaze kabisa mawazo yakikuzidi jichanganye na watu,fanya ibada sana, Kamwe kamwe usifanye haraka ya kuwa na mpenzi mpya,Mungu akujaze amani na furaha kuu usahau machungu yote

Yaan mwenyezi mungu ampe moyo wa kusahau na mwepesi pia maana yataka moyo. Kikubwa atulie kwanza.
 
kubali tu yaishe ndiyo viumbe hawa .. wewe hukuona dalili za kuachwa? wala usilazimishe mwache aende tena mwache kabisa wala usijutie hata kidogo mshukuru Mungu kukuepushia ushwetwaini wa huyo mwanaume .....

kuumia itauma ila mwache nasema tena mwacheeee kula raha bibie wala usiwaze....

tena mwambie sikupendi

Duuh ushauri mzito na maneno makali but sadly ndo ukweli huo ambao anatakiwa kuufanyia kazi miss chagga..
Muwe mnatumia vichwa mnapoangukia kwenye mapenzi badala ya mioyo..
 
Last edited by a moderator:
nilikuwa najitahidi kuficha ila siku zinavyozuidi kwenda naona unalipuka na unakuja kwa kasi kwa namna navyo yaona maovu yenu yanaongezeka

kwan unafikir kuvunjika kwa mahusiano chanzo n mwanaume tu?
 
miaka miwili katembezewa bakora, na anajua kichwa wazi wa jamaa alivyo mkali, leo amuachie kirahisirahisi!!!?

usimshauri mwenzio awe chizi baada ya siku moja

aje nimpe maujanja yakula raha
 
Mwache aende zake let him go for good, hawa viumbe ni viumbe wazito, yaani hawa bebeki kwa khanga,kitenge wala kaniki yaani sawa na zigo la mavi hata ufanyeje litatoa harufu tu.
 
kwani ulikua huna kidumu...

kubali tu yaishe ndiyo viumbe hawa .. wewe hukuona dalili za kuachwa? wala usilazimishe mwache aende tena mwache kabisa wala usijutie hata kidogo mshukuru Mungu kukuepushia ushwetwaini wa huyo mwanaume .....

kuumia itauma ila mwache nasema tena mwacheeee kula raha bibie wala usiwaze....

tena mwambie sikupendi

Miss u
 
Pole! wakati wengine wanatafuta wake na wengine wanatafuta wanaume, wengine wanaacha na kuachwa!!
 
pole sana kuanza upya si ujinga achana nae malipo ni hapa hapa
 
kwan unafikir kuvunjika kwa mahusiano chanzo n mwanaume tu?

Bwana wanaume ndio mara nyingi wanaanza. Ila inauma jamani, kwanini mnapenda kutuumiza. Ukipata tu kitu kipya changes zinaanza fasta hata kuficha ficha, Jaribuni kuwa wabunifu.
 
Back
Top Bottom