Mwanangu usiniletee single maza

Mwanangu usiniletee single maza

Yukwapi

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2024
Posts
500
Reaction score
644
Habari Wana JF
Mwanangu usiniletee single maza🙏
Hii nikauli iliyotoka kwenye kunywa Cha baba yangu nilipomueleza kua nataka kuoaa.

Ipo hivi nilipata kazi mwanza miaka miwili iliyopita na katika harakati za kazi nilikutana na bint aliezalishwa mtoto mmoja,tulikua marafiki na meishowe tuliingia kwenye mahusiano

Mpaka kufikia Sasa tuna mwaka mmoja kwenye mahusiano na tumeafikiana kufunga ndoaa.
Siku ya Jana nilipata wasaa wakuongea na baba kumueleza mipango yangu na huyo mwanamke pamoja na jinsi alivyo lakini alipojua kua ni single maza alimkataa katukatuu.

Roho iliniumaa ila nikasema ngoja nimsikie mama nayeye anasemaje inshort naye alipita mulemule alipopita baba😭

Sikukata tamaa Leo hasubuhi nilimpigia tena baba simu nakumweleza sifaa za huyu mwanamke ila alikataa nakuniambia "wewe nimwanangu wakiume ulietoka kwenye kiuno changu na katika ufalmewangu Nina uzao wakwanza kwenye tumbo la mama Yako hii nibaraka katika ufalme wangu na himaya yangu ,mama Yako ameheshimisha ukoo wetu na wazazi wangu pamoja na wazee wa ukoo wanalifahamu hiloo .

Wewe pekee ndiokijana unaetaka kutuletea malkia kutoka ufalmee mwingine asiekua na sifa yakua na uzao wako wa Kwanzaa .

Mwanangu hatakama umempendasana muachee uzao wa kwanza kutoka kwa mwanamke ni aganoo tena agano lisiloweza kufutikaa sina chakukueleza sana ila tafuta muda usomee maandiko juu ya mzaliwa wa Kwanzaa.
Tunajua unampenda ila kwenye familia yetu hatumtaki na kwanza umenizarau sana kwakutaka kutuletea mkee wa mtuu tema mate chini nauombee msamahaa kwa zarau ulizonionesha natamani ufalmee wako usiwenamtuu wakuuteteresha vizazi na vizazi kama umeshindwa kupata mwanamke nitakutafutia wapo wengi wazuri.

Naskuzote usitumie hisia kufanya maamuzi wanaume hatupo hivyo 😭😭

Aseee haya ndiomaneno niliyoambiwa ila nachotaka kujua naombeni anaejua umuhimu wa mzaliwa wa Kwanza 🙏
 
Baba yake lamine yamal wa kambo hawezi kukuelewa na hiyo kauli Yako.

Enjoy good life mr

Huyo mwenye koti jeusi anateleza na Ganda la ndizi, kitonga
 

Attachments

  • Screenshot_20260507-200207.jpg
    Screenshot_20260507-200207.jpg
    83.7 KB · Views: 7
Kwani hiyo mada ya yeye kutaka niwe na uzao wakwanza kwa mwanamke anamaanisha Nini au kunamazara Gani uzao wakwanza kutoka kwa mtuu mwingine?
Apo issue iko ivi kaka mwanamke yoyote hawezi kuzaa na mwanaume asiyempenda ivo mpaka umeona amezaa na mwanaume uyo ujue amempenda ipo siku watatafutana tu kupitia malezi ya mtoto na wewe ukiwa naye katika ndoa sio kwamba mtaishi muda wote na furaha na amani kuna mapito pia apo ndo utamjua vizuri uyo single maza na mfano mwingine mdogo nakupa kwa wanyama ushawai tazama kipindi cha wanyama ukaona simba anaua watoto sasa wale sio watoto wake ni watoto wa dume aliloshinda nguvu eiza kamuua au kamkimbiza baada ya mapigano,Simbq kafanya vile ili aanzishe uzao wake
 
Unaoa wewe ,haoi baba yako ,fuata kile moyo wako unahitaji achana na stori za mtaani na imani potofu juu ya hao akina mama waliozalishwa .

Dunia ina pande nyingi na kila mtu ana historia nzuri na mbaya ya kile kilichomfikisha pale alipo ,acha mara moja kuwaona hao wadada /wamama waliozalishwa kama wakosefu ,dunia imewapitisha huko ikiwa na makusudi maalumu ambayo mimi na wewe hata wao wanaweza wasiyajue .

Nakuomba kama unampenda na mnapendana muoe huyo dada achana na ngano za baba yako ,naye ni mtu na anayo haki ya kupendwa tena na kuishi kifamilia tena .

Kwaheri ila muoe huyo dada hakupenda kuwa single ni hatma za kidunia 😪😪
 
Kwani hiyo mada ya yeye kutaka niwe na uzao wakwanza kwa mwanamke anamaanisha Nini au kunamazara Gani uzao wakwanza kutoka kwa mtuu mwingine?
Mtoto wa kwanza ndie msimamizi wa mirathi na mwangalizi wa familia wewe utakapokufa au utakapozeeka. Kitendo cha mwanamke kuja kwenye mji wako na mtoto ambae ashazaa na mwanaume mwingine italeta mgongano wa kimasilahi wa nani anaestahili haki ya mzaliwa wa kwanza ndani ya nyumba yako.

Vilevile kwa sababu mwanamke hana uhakika kama mwanae atakuwepo kwenye mirathi yako au ya baba mzazi kuna uwezekano akatumia jasho lako kumwandalia mwanae future yake kimya kimya. Hii itafanya mume na mke muwe mnajenga miji miwili tofauti.
 
Siku moja nilikuwa naangalia TV na bimkubwa maigizo maigizo pale.Aliniambia na wewe siku moja uje uniambiee eti mwanamke kama huyo ndio unataka kuoa.Namshukuru Nimeoa mwanamke ambaye ndugu na Jamaa wamekubali.
 
Wazazi wapo sahihi.

Single mothers Sio wabaya ila kwa kijana unayejitafuta, jiepushe na single mothers
 
Single mother wanalogwa sana na wanaume ambao huwa wanakuwa nao, ni hivyo single father nao wanalogwa.. Na wanalogana vibaya wakwame kuwa kweny mahusiano mapya au hata wakipata watu mambo yasiende na waonekane wabayaa..
 
Watu baada ya kuachana hutupiana uchawi na kila aina ya mikosi.. ili wakwame waendapo
 
Hakupenda???, kwani siku hiyo mimba inaingia ulishiriki kushika paja?
Mkuu wangu Mnyenz na leo unataka tugombane tena ?
Hapana wewe ni jamaa yangu ,tubishane kwa hoja sio matusi ila ikifika hatua ya kupimana nguvu ,PM yangu ipo wazi namba nitatoa ili tukutane walau ijulikane nani zaidi upande wa ngumi ila kwa matusi mimi mweupe kaka mkubwa .
 
Kwani hiyo mada ya yeye kutaka niwe na uzao wakwanza kwa mwanamke anamaanisha Nini au kunamazara Gani uzao wakwanza kutoka kwa mtuu mwingine?
Washkaji ndo wamekuja kukutembelea, unaanza utambulisho sasa.

"Huyu ndio shem wetu, na huyu dogo ndio mtoto wetu wa kwanza "
 
Back
Top Bottom