Desprospero
JF-Expert Member
- Feb 1, 2023
- 887
- 2,201
Wakati mwingine tuongee ukweli. Mimi ni muumini wa demokrasia. Kuna mtu nchi hii asiyeeleweka. Ni Mwandishi Bollen Ngetti. 2010 huyu Dk. Slaa alimtuhumu kutumiwa na TISS na kuhadharisha viongozi wa Chadema wasimpe ushirikiano.
Wiki tatu zilizopita alisambaza clipu ya video akiliomba Jeshi la Polisi kuwakamata wote wanaomkebehi na kushambulia mkataba wa DP World.
Jana ameandika na kusambaza andiko akimuomba Rais Samia kuwaachia huru bila masharti Dk. Slaa na wenzake. Tunashuhudia leo Slaa akiachiwa na wenzake.
Huyu ni rafiki wa viongozi wengi sana wa Upinzani akiwemo Zitto Kabwe, James Mbatia, Mbowe, Mdee. Ifike mahali, tumshuku, tukae naye mbali. Si Mwema Kwa upinzani Tanzania. Chukueni hilo.
Wiki tatu zilizopita alisambaza clipu ya video akiliomba Jeshi la Polisi kuwakamata wote wanaomkebehi na kushambulia mkataba wa DP World.
Jana ameandika na kusambaza andiko akimuomba Rais Samia kuwaachia huru bila masharti Dk. Slaa na wenzake. Tunashuhudia leo Slaa akiachiwa na wenzake.
Huyu ni rafiki wa viongozi wengi sana wa Upinzani akiwemo Zitto Kabwe, James Mbatia, Mbowe, Mdee. Ifike mahali, tumshuku, tukae naye mbali. Si Mwema Kwa upinzani Tanzania. Chukueni hilo.