Kozi zitakazokuwezesha kujiunga kirahisi na JWTZ

Kitu pekee kilichonifanya kutokujiunga jeshi ni kukosa uhuru binafsi wa maisha yangu.

" You dont have you own time"

Sent using Jamii Forums mobile app
Ukiangalia vizuri, hata huko unakodhani una uhuru, kuna muda lazima ujiamrishe tuu wewe mwenyewe kufanya mambo flani yanayokuhusu, unajipa amri wewe mwenyewe na usipoitekeleza basi mambo yako lazima yaende kombo. Bado ni mle mle tuu kwamba kuwajibika na kutii amri yako mwenyewe (kama wanajeshi wanavyotii amri za makamanda wao) ni lazima. Hata uhuru wako una mipaka kwa hiyo ni yale yale tuu.
 
hapo kwenye short course ya miezi mitatu ni fiksi mzee, Jeshi hata uwe na elimu gani lazima uhenye depo na sio mchezo baada ya kambi ndio kila mmoja anajisogeza kwenye kitengo chake.

kwa kifupi ukimuona mtu yoyote kavaa kombati ya Jeshi jua kaisotea hiyo mpe saluti zake maana depo ya jeshi hasa JWTZ sio mchezo, kuna mazoezi makali sana na kila anaevaa kombat

Kwa sasa nimeshaajiliwa ila kusema kwel siwezi kumpata kwa kipato hata niunganishe mishahara yangu ya miezi miwili
Jeshini wanalipa vizuri hasa hawa maofisa asikwambie mtu
.....
 
Huyo waziri lazima alindwe na askari kijana. Mwenyezi Mungu amempatia karama tofauti kila mmoja wetu, wote tukiwa mawaziri nani atailinda nchi yako dhidi ya uvamizi wa adui ? Nani atatibu wagonjwa ? Nani atakuwa raia ? N.k Ndio hivyo wewe unavyopenda uwaziri, wenzio wanapenda jeshi. Wengine wanapenda upadre, uchungaji n.k ndio mpango wa Mungu huu.
Unawaza kulinda tu thinkwide, tafuta fursa za kimataifa acha kuwaza uaskari wenzio wasomi jeshi ni ajira ya muda wanacheki michongo ya kimataifa i.e UN,UK,US
 
uko sawa kabisa jeshini kuna wasomi walibobea kinyume na wanavyofikiri watu.Yuko mwanajeshi mmoja ni Professor,Dr Brigadier general Yadon ana taaluma ya udaktari.Hakuna taaluma uraiani jeshini haipo.Mnakumbuka muhimbili ma dr waligoma wanajeshi wakaenda kukamata usukani? mnakumbuka waongoza ndege airpot dar waligoma wanajeshi wakaenda kushikilia.Mnao dhani wanajeshi ni vilaza mnapotea sana.Hata Marekani wanaanga wengi wa NASA waliokwenda mwezini walikuwa ni wanajeshi.Pia gunduzi nyingi za kitabibu marekani zinafanywa na jeshi.Haa Lockheed Martin ina mkono wa jeshi
-Umesema jeshini Kuna wasomi waliobobea nikadhani utaleta orodha ya wanajeshi wenye PhD kumbe Yuko mmoja wakati Polisi juzi tu Kwenye mahafali ya Assistant inspector kulikuwa na PhD 1, na unaweza kukuta pengine Polisi kuna PhD nyingi kuliko Jeshi
-Kwa akili yako ule mgomo wanajeshi madaktari wangeuweza endapo mgomo ungekuwa Siriaz? Jeshini Kuna SPECIALIST wengi kuliko Muhimbili? Automatically Muhas ndiyo Kuna wabobezi wa kutosha jeshini mabingwa wako wachache ukilinganisha na MUHIMBILI
-Ona unavyopotea unafananisha JESHI LA US na Jeshi la Tz wenzenu wanaunda Zana za Vita,Magari Vita Kama AFV,MFUMO WA KUZUIA MAKOMBORA nyie mmebuni zana gani duniani ambayo mnajivunia? au magari ya Nyumbu
-Umesema gunduzi nyingi za kitabibu huko US zinafanywa na Jeshi sio kwa Tanzania huku gunduzi za kitabibu zinafanywa na KCMC,Muhas,bugando,nimr, umejiuliza kwa Nini huko US gunduzi nyingi zimefanywa na Jeshi? Jibu ni kwamba US wanaajiri kwa meritocracy na sio mediocracy
 
-Umesema jeshini Kuna wasomi waliobobea nikadhani utaleta orodha ya wanajeshi wenye PhD kumbe Yuko mmoja wakati Polisi juzi tu Kwenye mahafali ya Assistant inspector kulikuwa na PhD 1, na unaweza kukuta pengine Polisi kuna PhD nyingi kuliko Jeshi
-Kwa akili yako ule mgomo wanajeshi madaktari wangeuweza endapo mgomo ungekuwa Siriaz? Jeshini Kuna SPECIALIST wengi kuliko Muhimbili? Automatically Muhas ndiyo Kuna wabobezi wa kutosha jeshini mabingwa wako wachache ukilinganisha na MUHIMBILI
-Ona unavyopotea unafananisha JESHI LA US na Jeshi la Tz wenzenu wanaunda Zana za Vita,Magari Vita Kama AFV,MFUMO WA KUZUIA MAKOMBORA nyie mmebuni zana gani duniani ambayo mnajivunia? au magari ya Nyumbu
-Umesema gunduzi nyingi za kitabibu huko US zinafanywa na Jeshi sio kwa Tanzania huku gunduzi za kitabibu zinafanywa na KCMC,Muhas,bugando,nimr, umejiuliza kwa Nini huko US gunduzi nyingi zimefanywa na Jeshi? Jibu ni kwamba US wanaajiri kwa meritocracy na sio mediocracy
Huwa siwaelewi watu ambao kila kitu lazima wajifananishe na America au Magharibi!
Kwa akili yako tu ya kawaida unadhani kuna haja ya kujifananisha na America!?
Na unatumia misingi ipi kujifananisha na America!?
 
Huwa siwaelewi watu ambao kila kitu lazima wajifananishe na America au Magharibi!
Kwa akili yako tu ya kawaida unadhani kuna haja ya kujifananisha na America!?
Na unatumia misingi ipi kujifananisha na America!?
- Anza kusoma mada ilipoanzia, aliyefananisha Jeshi la Tanzania na la US ni mwingine
 
hapo kwenye short course ya miezi mitatu ni fiksi mzee, Jeshi hata uwe na elimu gani lazima uhenye depo na sio mchezo baada ya kambi ndio kila mmoja anajisogeza kwenye kitengo chake.

kwa kifupi ukimuona mtu yoyote kavaa kombati ya Jeshi jua kaisotea hiyo mpe saluti zake maana depo ya jeshi hasa JWTZ sio mchezo, kuna mazoezi makali sana na kila anaevaa kombati kayapitia.
Sasa unabishana na mimi??
Wamepiga spesho kozi ya miezi 3 tuu watu maalumu /taaluma maalumu na wamekula kiapo.
Na sio hiyo tuu jata mwaka 2012 waliwahi hukuliwa tena madereva tuu uraiani wakala kozi miezi 3 tuu na kombati wakavaa .
 
Huwezi kumshauri mtu hobbie sasa hapo ndipo unapokosea
Lengonsio kushauri mtu awe na hobbie ya kitu fulani hapana,bali lengo ni kumuamsha mtu mwenye hobbie afanye vitu vya ziada katika hobbie yake,pengine yeye haoni fursa zaidi katika hobbie hiyo.
Huwezi kumshauri mtu hobbie sasa hapo ndipo unapokosea,
Lakini hata wewe umewashauri watu wai gie kwenye kazi au fani za kuongoza nchi,sio kila mtu ana hobbie ya kusomea fani hizo,kama wwe una hobbie hizo kuna wengine hawana so usiwashauri na wewe watu waingie kwenye hobbie unayoiona wewe ina maana.

Watu kama akina einstein,newtons,telsa n.k wqngewaza kuongoza nchi tu leo hii kuna vitu tungevikosa,hivyo nawewe naona unawashauri watu juu ya hobbie wakati
Sasa unaweza kumshauri mtu hobbie???
Wewe umetoa ushauri wa watu kusomea fani za kuongoza nchi,wakati huo huo hizo fani kusomea ni hobbie lakini hapohapo umetoa ushahuri na wewe.
Kwamba umshauri mtu apende kucheza, karata wakati sio hobbie yake. Hobbie huwa haishauriwi
Narudia kwa kusema wewe umewashauri watu wasomee fani za uongozi( na technology kama dikosei)wakatii kusomea hizo fanii ni hobbie pia.
 
Natumai mu wazima wa afya. Pole kwa wanaoumwa, Mungu awajaalie mkapate afya njema.

Nimeona niwashauri kuhusu kozi na taaluma za kuwa nazo, vijana wetu wenye lengo la kwenda kujitolea JKT ili baadae waje kupata nafasi ya kuandikishwa JWTZ kwa urahisi.

Kijana, kama una nia ya kuja kulitumikia taifa letu hili pendwa la Tanzania kupitia kuwa mwanajeshi JWTZ, soma kozi hizi ili ukienda kujitolea JKT ikuwie rahisi kuandikishwa kufanya kozi ya jeshi la wananchi JWTZ.

1. Kozi zote za afya. Udaktari, unesi, ufamasia, radiographia n.k pata certificate, diploma, degree, masters mpaka PhD ya taaluma za afya, hutajutia.

2. Urubani. Ukisoma kozi hii, hata JKT unaweza usipite, ila sasa hakikisha kwenu muwe mna hela ya kutosha sio ya kubababisha maana urubani si mchezo, mpaka milioni 200 +.

Hizi ndio kozi za uhakika, ukiwa na hizo fani, ukaenda JKT, siku JWTZ wakija kuwafanyia usaili hutakosa kupata nafasi kwenda kuvaa bakabaka.

Mbali na hapo, jiandae kutoboa mkataba na kurudi nyumbani, au ujiandae kwenda polisi, Magereza, uhamiaji au wanyamapori (ukibahatika).

Ni hayo tuu kwa leo, nakaribisha michango ya wengine. Muwe na muda mwema sana
Mbona nasikia hata darasa la saba Wana pendwa sana huko kikosin ...

Yaan akisimama Bachelor holder na STD 7 graduate nasikia STD 7 graduate anapita
 
Mbona nasikia hata darasa la saba Wana pendwa sana huko kikosin ...

Yaan akisimama Bachelor holder na STD 7 graduate nasikia STD 7 graduate anapita
Kwasababu jeshi lina maofisa wengi hivyo halitaki tena maofisa linataka nguvu kazi ndio maana hupendelea la saba maana hawa wengi wanaishia kua ma private au vyeo vya mabegani basi ( koplo,meja,sajenti ,rcm,nk)

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom