Kova: Maandamano ya DOWANS kesho marufuku!

Kova: Maandamano ya DOWANS kesho marufuku!

Tungoje mpaka dec na hayo maazimisho yao 50yrs pia kama watayaahirisha au itakuwaje??
 
Inanisikitisha sana, kwa nini kitengo cha intelijensia kinashindwa kuwakamata wanaowahisi ni alshabab kwamba wapo nchini na lhrc wakiandamana wao watafanya vurugu? Na kwa nini tutishwe? Ina maana vyombo vyetu vya usalama ni dhaifu sana? Na kama ni hivyo kwa nini mechi ya simba na yanga haiairishwi? Inanisnonesha sana mwisho nawashauri watanzania huu ni mwanzo na tusikate tamaa watabana mwisho wataachia ila spendi hatua wanayotaka tuichukue ya nguvu ya umma
 
Polisi wana source nyingi za kujua hatari inayoweza kujitokeza. Tusipuuze kwa ajili ushabiki tu.
Yes, Al shabaab tupo hapa nchini lakini napemda kuwahakikishia kwamba maandamano haya sisi Al shabaab tumeyaridhia na hatutofanya lolote negatively, na tumekubaliana kuyalinda kwa juhudi zote maandamano haya ya dowans-hivyo kama Kova wasiwasi wake ni sisi Al Shabaab, bac ayaruhusu tu wala asiwe na wasiwasi, sisi huwa tunaharibu kwenye uharibifu(bar/casino/danguro na upuuzi wa namna hizo) Oyaa, dogo Kova, ruhusu tu mzee-surely hatulipui ktk hayo maandamano. Tchao, HM
 
Nadhani kuna haja ya kuahirisha maazimisho ya miaka 50 ya uhuru, mechi ya simba na yanga na mikusanyiko mingine mingi itayojumuisha viongozi wa taifa na kimataifa kwa kuhofia Al Shabab!
wewe kweli mzee rula maana umenyoosha maneno yako kama rula,umenena ukweli mtupu,kwa hakika tzania naweza sema ni nchi ya kiabunuwasi.
 
Atakuwa anaunga mkono Mafisadi, basi nae atakuwa ni fisadi siku zke za kuwa madarakani zinahesabika.
 
Tanzania ni zaidi ya tuijuavyo..na inawenyewe..na wenyewe ni mafisadi..
 
Polisi wana source nyingi za kujua hatari inayoweza kujitokeza. Tusipuuze kwa ajili ushabiki tu.
Wewe acha kutuletea siasa za Polisi za mwaka 47! Unafikiri Polisi wa Gaddafi hawakuwa na source za kuwajulisha hatari? Lenye mwanzo lina mwisho! Iko siku nchi hii itakombolewa, na siku hiyo, wewe sugu1; kama ilivyokuwa kwa Gaddafi, tutakutoa shimoni ulikojificha kama panya. SHAME ON U !
 
Tuwache ushabiki jamani. Mwenzenu ANANILEA NKYA kisha pokea chake sasa anataka kutuingiza vitani. Hivi huyu mama kasomea sheria kweli?. Basi vurugu zikianza na awe Mbele kabisa ili aoneshe uzalendo wake. Hili Deni lazima lilipwe tu tulishafanya makosa tena yaliosababishwa na siasa zetu za kupakana matope. Hivi kweli tumefika huko ambako sasa tunajifanya hatutaki kuheshimu sheria za kimataifa?
Huyo Marekani anayezitengeneza sheria za kimataifa haziheshimu wala kuzijali. Wewe mchovu (tz) unafaidika nini na sheria hizo zaidi ya kunyonywa? Ninyi ni wa kuwalipa wanaume wenzenu kila siku, niambie llini nanyi mtalipwa eti kwa vile haki zenu zimekiukwa? Sheria za kimataifa za upande mmoja, ovyooooo! Yapasa tuzikatae.
 
kwa mara ya kwanza ninakubaliana na Polisi ktk hili sababu kwa kipindi hiki ambacho hali ni tete hawa jamaa Al shabab wanaweza kutupiga ktk maandamano na kusababisha mass casualty,tukikumbuka uganda jinsi walivyoshambuliwa wakati wakiangalia world cup.Kifupi kwa kipindi hiki tujiepushe na mikusanyiko siyo ya lazima.

Maandamano ya watu kudai haki zao na kujaribu kuzuia kile kidogo kilichobaki kisiibiwe na mafisadi unaita mikusanyiko isiyo na lazima? Na hiyo mikusanyiko inayoendelea kila kukicha ya kusherehekea miaka 50 ya uhuru ambao hatuujui ndiyo mikusanyiko ya lazima? Kila kukicha pesa zinaendelea kuliwa na watu wanaacha kazi za ujenzi wa Taifa kusherehekea miaka 50 ya uhuru, kila wizara ina wiki yake, na pengine kila shirika la umma lina siku yake. Mpaka hiyo tarehe 9 Desemba itakapofika mikusanyiko mingapi itakuwa imeshafanyika? Na hizo mechi za ligi kuu, na mabonanza, na washindani wa Vodacom Miss wanaokusanyika kila kukicha, hayo yote ni ya lazima? Ama kwako wewe kwa kuwa wananchi wanasimama kupinga azma ya serikali ya ccm kuilipa kampuni ambayo hata jk amedai kuwa hamjui mwenyewe ni nani, pamoja na kwamba itawazidishia ugumu wa maisha watanzania unaona si jambo la lazima? Amka utazame, mbiu imeshalia, Afrika ya jana siyo ya leo. Kuna waliofikiri Hosni Mubarak hataondoka, kuna waliofikiri Ghadaffi hataondoka. Ole wao wanaolala wakifikiri wataendelea kuwanyanyasa watanzania kwa kutokubali kusikia sauti ya wanyonge!
 
Hivi Al shabab walipolipua kenya kulikuwa na maandamano, naomba kujulishwa.
 
baadhi ya polisi wa tanzania wataendelea kufa na umaskini wao
waige ya wenzao wa lIibya na Misri kama wanataka ukombozi ktk maisha yao
au kwa vile wanaishi kwa rushwa?? mfano wale wanaolinda mipakani kama himo ,tarakea hai nk wana mali za kufa mtu, majumba ya kumwaga
fuso na Noah huyu utamwambia kuna umaskini atakuelewaje huyu??? na kila mwezi fungu linatumwa kwa Wema na KOva hawana njaa hawa
Inabidi watu kuamua cha kufanya sasa.
 
tutake tusitake,dowanz italipwa,so cha kufanya ni kilikabili deni mapema kuliko kupiga kelele zisizo na maana wakati linakua tu..NA TUSIWASIKILIZE HAO WANAOITISHA MAANDAMANO ILI KUKUUZA MAJINA yAO KWA POLITICAL INTEREST ZAO HAPO BADAE WAKATI SI TWAUMIA..
 
Kamanda Kova amezuia maamndamano yaliyoandaliwa na wanaharakati kwa kile alichodai kuwa ni kuepuka uwezekano wa kushambuliwa na Al Shabab eti ni kusanyiko na kwamba ikitokea maafa jeshi la polisi litalaumiwa (source ITV)

Namuunga Mkono

Lakini sijamsikia kamanda akikataza makusanyiko mengine kama yale yanayofanyika makanisani, misikitini ama mikutano yoyte mikubwa. Kwa mimi nilitegemea makusanyo mengine yote yapigwe marufuku kwa sababu hizo hizo alizozitoa kamanda ili kuepusha kile alichodai ni mashambulizi ya Al Shabab.

Kwa mtazamo wangu mimi naona hizi ni mbinu za mafisadi yanayohusika na Richmond/Dowans yaliyotengeza mpango ambao unaonekana kushirikisha viongozi wa ngazi za juu akiwemo Kamanda.

Je tutafika salama?
 
Teh teh teh teh teh teeeeeh! Nilitaka kushangaa haya maandamano interejensia hawajayaona au kwa sababu sio chadema, na hao al shabab ndo akina nani tz au walioandaa maandamano? Nitaendelea kusema na nitarudia kusema kila siku, hii nchi bila kumwagana vinyesi hatutakaa tuheshimiane hata kidogo
 
Kova umeshusha hadhi yako, kwa kiasi cha kutisha! Tanzania hakuna Intelijensi yoyote. Kama ingekuwako, mgao wa giza usingekuwako! Ni usalama wa kutafuta kula! Ndiyo maana Polisi wamejaa vitambi tu! Sijui watapiganaje na Al-Shabab, huku wakiwa na vitambi! Ngoja tuone!
 
Hukitaka kulala na hasira, soma habari za Tanzania usiku. Zinatia kinyaa. Hii nchi kweli imeoza. Huyu Kova anasema utumbo kama huu na hakuna atakayemfanya chochote hata magazeti kuhoji hakuna.
 
Back
Top Bottom