Kosa la Rugemalira ni nini ?

Kosa la Rugemalira ni nini ?

aliuza hisa kwa kampuni bandia. akalipwa fedha zisizomilikiwa na kampuni hiyo kisheria. otherwise hana makosa ktk kugawa hela aliyodhani niyake.

Wewe angalau umetoa hoja. Kwa hiyo tunakubaliana kuwa akirudisha hela na yeye anarudishiwa hisa zake au sio?
 
Labda tukuulize wewe umesikiliza kituo gani... Kama ukusikia jinsi Zitto alivyowahusisha hata government officials na Ruge then am afraid there's something behind your critics!

all he did was mention people who were given money by Ruge and that some of them were ex-gov officials. Kitu ambacho tumekuwa tukijadili humu JF for days now! Taarifa ipi mpya kuhusu hawa watu ambao wewe umeipata katika ripoti ya zitto ambayo hukuwa unajadili humu JF toka juzi?
 
namba mbili. wewe ulidai IPTL ilikuwa imefilisiwa kwa maana ya dissolved.
NI wapi nilisema IPTL imefilisiwa? Hivi nilisema imefilisiwa au imewekwa chini ya mfilisi? Hiki hapa ndicho nilichosema:

Man, are you serious? Suala la rushwa tangu lini likawa ni private matter? Hivi wewe (achilia mbali kampuni) leo hii ukienda hospitali kasha ukampa rushwa daktari ili uhudumiwe hiyo itakuwa ni private matter? RITA yenyewe ni serikali… kuna sheria zinazoongoza RITA na pia kuna sheria pale kampuni inapowekwa chini ya mufilisi wa RITA… si kwamba kwavile ni kampuni binafsi then wenye nayo wanaweza tu kwenda RITA na kusema “we want our company back, itoe kwenye kundi la mufilisi coz’ we already have a buyer…!” Hakunakitu kama hicho. Sasa je, sheria zilifuatwa katika kuiondoa IPTL kwenye faili ya mufilisi na kuiuza? Je, ikithibitika kwamba zile statements ni genuine bado huwezi kujiuliza ni namna gani Yule Yule ambae IPTL ilikuwa chini yake amelipwa millions of shillings na wenye kampuni yao!! Hii haiwezi kuwa issue private ya wana-hisa coz’ hao wanahisa ni associates kwa maana ikiwa kuna maofisa wa serikali wamehongwa basi hao wanahisa wote watakuwa wamehusika! Hakuna private matter hapo… rushwa ni rushwa tu!
Sasa utasemaje kwamba nilisema imefilisiwa wakati maelezo yanaonesha wazi kwamba nimeseme ilikuwa chini ya RITA?
 
subiri aende pale kisutu, kama msafi sheria itamsafisha. ila kwa ninavyojua, hautaamini macho yako kwasababu kenye hii issue kuna forgeries nyingi sana, money laundering amefanya sana huyu hasa kwa kusafishia hela chafu kwa kugawa kwa watu, kukwepa kodi amekwepa, ..yaani kuna makosa mengi hadi utamwonea huruma. we tuliza mtima subiri apelekwe mahakamani halafu utaona mziki wake.

na ikijulikana kuwa hao waliopokea pesa pia walikuwa na knowledge kuwa pesa hizo zilikuwa ni chafu, wote wanaingia kwenye money laundering.kosa ambalo halina dhamana. huyo mhindi singasinga ndio kabisa hatakuwa na dhamana hivyo ajiandae kwenda kukaa lupango na wezi wa manzese.

VIP haijafoji chochote, ilikuwa inamiliki hisa zake kiuhalali. VIP sold the shares to PAP...anyway kama unavyosema tusubiri tu chief time will tell.
 
subiri akifikishwa mahakamani utafahamu makosa yake, anafanya mzaha ndani ya kumi na nane za watu?

sina tatizo akifikishwa mahakamani. lakini nikuonye tu kuwa nchi hii kuna watu kama chenge na dr idris ambao DHAHIRI walikula rushwa ya rada, lakini hawakwenda mahakamani hata siku moja, Kagoda mpaka leo haijapatikana na imekula 40bil, majengo pacha dili looote lile la mabilioni wametoswa watu wawili tu liyumba na mwenzie, iddi simba na UDA......Hao wote wana kesi dhahiri za kujibu lakini nothing has been done, sembuse huyu ambaye watu mnataka asulubiwe tu bila hata kunyoosha maelezo kaiba vipi?
 
Wewe angalau umetoa hoja. Kwa hiyo tunakubaliana kuwa akirudisha hela na yeye anarudishiwa hisa zake au sio?
hapo ameshapoteza kila kitu, kama ulikuwa unamsikia ruge wa kipindi cha nyuma kuanzia leo ameshakuwa mpya, alikuwa na knowledge kuwa anadili na kampunihewa, kupitia hilo amepata pesa nyingi, akaanza kuzisafisha kwa kuwapatia watu kama zawadi. jambo hili ni baya kuliko wizi wenyewe, money laundering offence is a very serious offence ambalo halina dhamana hivyo jamaa atakaa dhani hata miaka minne hadi kesi iishe, na kwasababu inasemekana ushahidi upo mzuri, mali zake zote zitataifishwa, naamisha zote ambazo zimepatikana kipindi tangu aanze kujihusisha na ufiadi.
 
all he did was mention people who were given money by Ruge and that some of them were ex-gov officials. Kitu ambacho tumekuwa tukijadili humu JF for days now! Taarifa ipi mpya kuhusu hawa watu ambao wewe umeipata katika ripoti ya zitto ambayo hukuwa unajadili humu JF toka juzi?
Unataka nirudie kitu ambacho nimeshakisema kabla ya kuwasilishwa kwa ripoti na nikarejea tena baada ya kuwasilishwa na ndicho Zitto alichokisema! Ikiwa shule inatuhumiwa ku-cheat kwenye mtihani wa taifa halafu a/c ya Headteacher ikakutwa kuna pesa kibao zimetoka ambazo baadhi ziliingizwa kwenye a/c za wasimamizi wa mitihani, zingine zimeingizwa kwenye a/c za askari waliokuwa wanasimamia usalama kwenye eneo la mtihani halafu bado hapo usione uhusiano uliopo kati ya kuvuja kwa mitihani na pesa zilizotoka kwa headteacher na kuingia kwenye akaunt za invigilators na askari, basi sitakuwa na la ziada zaidi ya kusema tuna safari ndefu ikiwa tunashindwa hata such simple arithmetic!
 
Wewe angalau umetoa hoja. Kwa hiyo tunakubaliana kuwa akirudisha hela na yeye anarudishiwa hisa zake au sio?
Bado atakuwa na kesi ya ku-corrupt government officials unless atoe ushahidi wa biashara halali aliyofanya na hao maofisa wa serikali!!!!!
 
VIP haijafoji chochote, ilikuwa inamiliki hisa zake kiuhalali. VIP sold the shares to PAP...anyway kama unavyosema tusubiri tu chief time will tell.
unalijua kosa la money laundering mzee? hivi ulishawahi kuona nani tangu uzaliwe anagawa mabilioni kwa watu kama njugu? hizo pesa zote ni suspecious kuwa ni proceeds of crime. hivyo, watamfanyia unyumbufu yakinifu hapo hadi itaonekana hela hizo ni chafu, na zikiwa chafu tu amepoteza kila kitu. na bahati mbaya account zake zote zitafungwa muda si mrefu, na akijaribu kwenda kuhamisha haraka sasaivi atakuwa anatengeneza ushaidi kuwa kama aliona hela zake safi kwanini alihamisha harakaharaka hivi...yaani kama ana watoto, ajabiru kuwapa wosia mapema la sivyo atawapa wosia wakimfuata lupango. sidhani kama hadi sasa hajakamatwa.
 
unalijua kosa la money laundering mzee? hivi ulishawahi kuona nani tangu uzaliwe anagawa mabilioni kwa watu kama njugu? hizo pesa zote ni suspecious kuwa ni proceeds of crime. hivyo, watamfanyia unyumbufu yakinifu hapo hadi itaonekana hela hizo ni chafu, na zikiwa chafu tu amepoteza kila kitu. na bahati mbaya account zake zote zitafungwa muda si mrefu, na akijaribu kwenda kuhamisha haraka sasaivi atakuwa anatengeneza ushaidi kuwa kama aliona hela zake safi kwanini alihamisha harakaharaka hivi...yaani kama ana watoto, ajabiru kuwapa wosia mapema la sivyo atawapa wosia wakimfuata lupango. sidhani kama hadi sasa hajakamatwa.

Okay lets see....
 
sina tatizo akifikishwa mahakamani. lakini nikuonye tu kuwa nchi hii kuna watu kama chenge na dr idris ambao DHAHIRI walikula rushwa ya rada, lakini hawakwenda mahakamani hata siku moja, Kagoda mpaka leo haijapatikana na imekula 40bil, majengo pacha dili looote lile la mabilioni wametoswa watu wawili tu liyumba na mwenzie, iddi simba na UDA......Hao wote wana kesi dhahiri za kujibu lakini nothing has been done, sembuse huyu ambaye watu mnataka asulubiwe tu bila hata kunyoosha maelezo kaiba vipi?
Ameiba vipi? Huyu ana tuhuma mbili... moja ya kushirikiana na tapeli Seith hadi wakafanaikiwa kuchukua pesa za Escrow na kugawana huku wakifahamu fika kwamba sehemu ya pesa hiyo ni mali ya TANESCO na tuhuma ya pili ni ku-corrupt government officials as seen in his bank statement!! Na hata asipofikishwa mahakamani bado haiondoi ukweli kwamba, mosi ameshirikiana na Seith kuuibia serikali na pili ame-corrupt maofisa wa serikali... na wala haitashangaza asipofikishwa mahakamani kwa sababu amehonga sehemu mbali mbali including kwa majaji... kama ambavyo kutopelekwa mahakamani kwa Chenge in radar saga hakujafuta ukweli unaofahamika kwamba Chenge alikula rushwa kwenye deal la radar, ndivyo hivyo hivyo itakavyoacha kufuta ukweli kwamba Ruge ameshirikiana na Seith kuiibia serikali na kuhonga maofisa wa serikali bila kujali kama amepelekwa mahakamani au lah!
 
Bado atakuwa na kesi ya ku-corrupt government officials unless atoe ushahidi wa biashara halali aliyofanya na hao maofisa wa serikali!!!!!

hapo ndipo ninapopataka, corruption! enhee, mujulizi kapewa fedha ya nini? chenge? Ngeleja? hawa wamemsaidia vipi rugemalira?
 
Ameiba vipi? Huyu ana tuhuma mbili... moja ya kushirikiana na tapeli Seith hadi wakafanaikiwa kuchukua pesa za Escrow na kugawana huku wakifahamu fika kwamba sehemu ya pesa hiyo ni mali ya TANESCO na tuhuma ya pili ni ku-corrupt government officials as seen in his bank statement!! Na hata asipofikishwa mahakamani bado haiondoi ukweli kwamba, mosi ameshirikiana na Seith kuuibia serikali na pili ame-corrupt maofisa wa serikali... na wala haitashangaza asipofikishwa mahakamani kwa sababu amehonga sehemu mbali mbali including kwa majaji... kama ambavyo kutopelekwa mahakamani kwa Chenge in radar saga hakujafuta ukweli unaofahamika kwamba Chenge alikula rushwa kwenye deal la radar, ndivyo hivyo hivyo itakavyoacha kufuta ukweli kwamba Ruge ameshirikiana na Seith kuiibia serikali na kuhonga maofisa wa serikali bila kujali kama amepelekwa mahakamani au lah!

si kweli, at this point, ruge hawezi kupelekwa mahakamani, hata huko takuru kwenyewe nahisi faili watalikalia tu kama mafaili mengine. You see, hata ile kumhoji tu mtu unatakiwa kuwa na reasonable doubts. tukirudi kwenye ule mfano wangu wa mimi kukuhoji umepata wapi fedha ya kununua gari wakati kazi yako muuza karanga. Unadhani usiponijibu nikaenda kukushitaki takuru utakamatwa? JR anaweza akaamua kutumia haki yake ya kisheria ya kutojibu chochote huko takuru (kama hata akihojiwa) mpaka pale takuru watakapokwenda mahakamani. Sasa swali linakuja Takuru watamtuhumu JR kwa kitu gani? Sawa kawapa fedha kina chenge, mahakama itauliza so? shida yenu? watajibu nini?
Hakuna sehemu yoyote ile ambapo mtu analazimishwa kusema kwa nini kampa fedha fulani MPAKA PALE swali hilo likiwa ndani ya tuhuma kubwa zaidi, ambazo mpaka sasa hivi HAKUNA!
 
jMali ana roho ngumu. anasema wakina tibaijuka wametajwa kapamba ripoti. inamaana hajasikia deo akisema wanabanwa na sheria ya utakatishaji pesa.

deo ana maoni yake na mimi nina yangu. mimi najenga hoja zangu. deo sio mungu.
 
JMali, what's your comment kuh hii quotation kutoka ripoti ya PAC "Kampuni ya PAP haikuwa na uhalali wowote wa umiliki wa IPTL wakati inalipwa fedha za kutoka Akaunti ya Tegeta ESCROW."



sina tatizo hapo, hiyo ni kweli kabisa. Lakini rejea kichwa cha thread yangu: hoja yangu ni rugemalira vs sethi/PAP na sio PAP na escrow.
 
Bado atakuwa na kesi ya ku-corrupt government officials unless atoe ushahidi wa biashara halali aliyofanya na hao maofisa wa serikali!!!!!

hawawezi kujenga kesi kwa kutumia hiyo bank statement kirahisi rahisi hivyo mpaka wathibitishe kuwa waliolipwa pia waliprovide service fulani katika uhalifu. Vinginevyo akisema zilikuwa ni zawadi na wewe huna tuhuma mbadala utamkataliaje?
 
PAP walitoa wap hizo hela?, kama siyo kwenye hiyo escrow AC, na ndio kiti kinachozungumziwa hapa

PAP walimlipa Ruge KABLA hawajaiba fedha za escrow! Fedha za PAP kwenda VIP hazikutoka escrow account.
 
Back
Top Bottom