Kosa la Rugemalira ni nini ?

Kosa la Rugemalira ni nini ?

FACTS:

1. James rugemalira alikuwa anamiliki 30% ya IPTL kupitia kampuni yake ya VIP. Asingeziuza hizo hisa, mpaka leo angekuwa bado anamiliki 30% ya IPTL KIHALALI kabisa, hivyo kuwa mbia mwenza wa PAP.
2. James rugemalira aliuza hizo share zake kwa kampuni ya PAP kwa dola milioni 75. Uuzaji wa hizi hisa ulifuata taratibu zote kisheria including ulipaji kodi.

MASWALI:
1. Huyu ndugu anaitwa mwizi kivipi? Amelipwa fedha kutokana na kuuza hisa, tatizo liko wapi hapo? Kisheria angeweza kumuuzia yoyote yule tofauti na PAP hizo hisa kama wangeafikiana bei! PAP wamefikia dau na yeye kawauzia, where is the problem hapo? IPTL sio kampuni ya umma, PAP sio kampuni ya umma, VIP sio kampuni ya umma. This is purely a private sector transaction. Mbona Rostam aliuza share zake vodacom kwa mabilioni tena kupitia nje ya nchi lakini hakuitwa mwizi (kwa kukwepa kodi among other things), badala yake akasherehekewa kwa front-page news? Naomba kufahamishwa kwa hoja tafadhali, uharamia wa James Rugemalira upo wapi.

Ni mchezo mchafu tu wa kisiasa kupakana matope lengo lao lilikuwa ni mama Tibaijuka. Rugemarila kapewa fedha zake kalipa kodi tatizo lipo wapi hata akiamua kumwaga fedha zake baharini. Tusubiri ripoti tuone kama itamuhukumu kama viny@go wengine wanavyosema.
 
Ni mchezo mchafu tu wa kisiasa kupakana matope lengo lao lilikuwa ni mama Tibaijuka. Rugemarila kapewa fedha zake kalipa kodi tatizo lipo wapi hata akiamua kumwaga fedha zake baharini. Tusubiri ripoti tuone kama itamuhukumu kama viny@go wengine wanavyosema.


Ruge is a nobody in a scheme of things, anaonekana wazi anatumika na wanasiasa, ili wajifanikishie malengo yao, na hilo liko wazi, mtu gani in 3 days una payroll ya wanasiasa ndefu kuliko ofisi za bunge?

bora ukae kimya ndugu. Muda wa kupindisha ukweli umeshakwisha.
 
1.Ndugu, hiyo IPTL iliwekwa chini ya mufilisi kutokana na kesi ya RUGEMALIRA HUYU HUYU! Ruge alitaka IPTL ifilisiwe ili alipwe fedha zake 30% ya assets. Hivyo hata singasinga asingetokea, bado IPTL ingepigwa mnada Ruge angekula chake pale pale! Mitambo ya IPTL ubungo pale inakubalika kuwa na thamani around $250mil usd. so unaweza kuona bado angekula vijisenti vingi tu. Sasa hapo kuna rushwa gani mpaka eti ahonge watu wa serikali?
Unayosema ni sawa... sasa inakuaje tena maofisa wa RITA wanaonekana kweney paylist? Maofisa wa serikali chini ya RITA wamefanya biashara gani na Ruge hata walipwe millions of money? Ni bahati mbaya sana sina stimu kwa sasa baada ya kusikia mahakama imezui mjadala bungeni kuendelea vinginevyo ningekutafutia gazeti la mwaka 2009 ambalo lilimtaja afisa wa RITA ambae anaonekana kwenye statement ya Ruge! Tuseme hakuna, rushwa, why paying them?Unless kama statements zinazoonekana kwenye mitandao ni feki otherwise, there's no any explanation on that!
2. VIP iliuza hisa zake kwa PAP mwezi september, na deal nzima ilikuwa concluded then! Rugemalira alitoa press statement around August akielezea dili nzima ilivyokwenda. From then onwards, ndipo PAP ikapata uhalali wa kuingilia fedha za escrow. So you see by the time PAP inashughulika na escrow, James Rugemalira alikuwa hayupo!
Wait... pesa ya Escrow ilikuwa in favor of IPTL... tunaposema IPTL, ina maana 70% ni Mechmar na 30% ni VIP! Hivyo basi, ikiwa hata kama PAP wangenunua hisa 70% kwa njia za halali basi angekuwa amenunua 70% ya IPTL including mali na madeni ya IPTL! Katika mazingira ya kawaida, 70% ya pesa za Escrow zingekuwa ni mali ya PAP na 30% zingerudi kwa VIP kwa kuwa nae alikuwa na mwanahisa! Na endapo VIP wasingechukua 30% ya pesa za Escrow basi thamani ya 30% ya hisa za VIP ingekuwa ime-include na fedha zilizopo Escrow kwavile nazo zilikuwa ni mali yake! Hivyo basi, VIP nao walikuwa na share kwenye pesa za Escrow.
3. kuhusu escrow account, hii dili ilikuwa kati ya PAP na Tanesco, wote wakakubaliana kuhamisha fedha kwenda PAP. Sasa hapo James rugemalira anahusika vipi tena? Kama kuna ubatili wowote wanatakiwa kufuatiliwa watu wa serikali na PAP sio JR! c'mon; tanesco kuna bodi nzima, wakurugenzi, mameneja, serikalini kuna waziri, naibu waziri, katibu, AG, BOT, Mbona wote hawa hawafuatiliwi anafuatiliwa mtu ambaye kosa lake ni kuuza mali yake kihalali?
Nimeshasema hapo juu kwamba pesa za Escrow zilikuwa ni mali ya Ruge vilevile kupitia hisa zake 30% kwahiyo nae LAZIMA alipata mgao wake wa 30% unless kama 30% yake ya Escrow money ilikuwa ndani ya hisa alizouza ambazo kimsingi ni kitu kile kile tu!
Vile vile swali rahisi tu: fedha za escrow ni malipo ya umeme toka IPTL kwenda Tanesco, sasa leo watu wanapodai kuwa actually fedha zote ni za Tanesco na bado Tanesco inadai, maana yake ni nini? kuwa IPTL muda wote huo toka 2006 ilikuwa inazalisha umeme bure?
BInafsi sijasema kwamba pesa zote ni mali ya TANESCO ingawaje inawezekana vile vile kwamba zote ni mali ya TANESCO!Hapa kilichokuwa kinatakiwa kufanyika kabla ya pesa kuwa drawn ni kufanya accounting tangu the first transaction to Escrow hadi ya mwisho! Mathalani, Mahakama ilitoa hukumu na kusema IPTL ilikuwa ina-overcharge! Kama ndivyo, kabla ya chochote, any excess amount ambayo ilizidi ilitakiwa kuondolewa kwa muda wote ambao IPTL ili-overcharge kwavile hii ilikuwa ni mali ya TANESCO sawa na radar deal... hapa kulikuwa na change ya TANESCO... je, Mechmar + VIP walirudisha change? Huo ni mfano mmoja tu kukuonesha kwamba si kwamba the whole amount ilikuwa ni mali ya IPTL(VIP+Mechmar)
4. Kuhusu fedha kampa nani, rejea namba 2. Kuwa fedha zake ni halali na ana uwezo wa kumpa yoyote yule.
Mosi, nimeshakuonesha kwamba pesa sio halali kwavile hizo za Escrow ndani yake kuna za VIP ambazo nae kalipwa... sio halali kwavile ndani ya fedha za Escrow kuna za TANESCO resulting from overcharging kama ilivyokuwa imethibitishwa na mahakama! Pili, kama nilivyosema awali, kwa vile pesa ni "zake" ana haki ya kumpa yeyote anayemtaka lakini inapogundulika kwamba among the payees ni government and ex-government officials ambao wanahusika moja kwa moja ama kwenye sekta ya nishati , IPTL saga (like RITA), TRA... hakika, ingawaje ana haki na uhuru wa kumpa yeyote amtake, ulipaji huu una-rise suspicion!!!!
Na zaidi ya hapo kuna USHAHIDI GANI KUWA hivi vielelezo vilivyosambaa humu JF ni vya kweli? Kilichopo ni karatasi reeefu lenye majina ya watu, aliyelitoa hajulikani! Lakini zaidi ya yote hata kama tukifanya wamepewa fedha na JR, je wanahusika vipi katika transaction ya VIP na PAP mwezi september? Kumbuka orodha ina majina kama ya askofu kilaini, watoto na mkwe wa rugemalira, etc, how on earth do these people fit in on all this
Mkuu jMali... post yako ambayo nilii-quote ingawaje haikuwa ndefu kama yangu lakini nayo ilikuwa ndefu vilevile! Labda nikung'ate sikio... ilibaki kidogo tu nikuambie kwamba "nitakujibu baadae" kwa sababu wakati nasoma post yako, begi lilikuwa begani tayari kwa kuondoka... nilikuwa na safari. Pamoja na yote hayo, bado nilijitahidi kuvumilia nikakusoma hatua kwa hatua na nikakujibu hatua kwa hatua! Je, nawe ulinisoma hatua kwa hatua? Kama hukunisoma, rudia post yangu uliyoi-quote hapo juu... usisome post mzima, soma kipengele namba 1 hadi 3!!!
 
Last edited by a moderator:
Ndugu chige...asante kwa majibu yako, naomba niendele na mjadala.

Unayosema ni sawa... sasa inakuaje tena maofisa wa RITA wanaonekana kweney paylist? Maofisa wa serikali chini ya RITA wamefanya biashara gani na Ruge hata walipwe millions of money? Ni bahati mbaya sana sina stimu kwa sasa baada ya kusikia mahakama imezui mjadala bungeni kuendelea vinginevyo ningekutafutia gazeti la mwaka 2009 ambalo lilimtaja afisa wa RITA ambae anaonekana kwenye statement ya Ruge! Tuseme hakuna, rushwa, why paying them?Unless kama statements zinazoonekana kwenye mitandao ni feki otherwise, there's no any explanation on that!

Assuming hiyo list iliyosambaa kwenye mtandao ni kweli. Bado ni private matter! Hata tukifanya Rugemalira ametoa rushwa RITA (na sijui kwa nini atoe) hilo linakuwa suala la wanahisa wa IPTL walioshitakiana na kusababisha IPTL iwekwe chini ya RITA. IPTL SIYO YA SERIKALI! Sasa hapo mimi na wewe tunaingiaje? IPTL kuwa chini mufilisi (RITA) inahusiana vipi na umma wa watanzania? At most hili ni suala la Rugemalira na PAP ndio wanaotakiwa kushikana mashati kama kuna rushwa ilienda RITA.


Wait... pesa ya Escrow ilikuwa in favor of IPTL... tunaposema IPTL, ina maana 70% ni Mechmar na 30% ni VIP! Hivyo basi, ikiwa hata kama PAP wangenunua hisa 70% kwa njia za halali basi angekuwa amenunua 70% ya IPTL including mali na madeni ya IPTL! Katika mazingira ya kawaida, 70% ya pesa za Escrow zingekuwa ni mali ya PAP na 30% zingerudi kwa VIP kwa kuwa nae alikuwa na mwanahisa! Na endapo VIP wasingechukua 30% ya pesa za Escrow basi thamani ya 30% ya hisa za VIP ingekuwa ime-include na fedha zilizopo Escrow kwavile nazo zilikuwa ni mali yake! Hivyo basi, VIP nao walikuwa na share kwenye pesa za Escrow.
Nimeshasema hapo juu kwamba pesa za Escrow zilikuwa ni mali ya Ruge vilevile kupitia hisa zake 30% kwahiyo nae LAZIMA alipata mgao wake wa 30% unless kama 30% yake ya Escrow money ilikuwa ndani ya hisa alizouza ambazo kimsingi ni kitu kile kile tu!

katika maelezo yako hapo juu: ni kweli kuwa kwa kumiliki 30% ya IPTL Rugemalira alikuwa na claim katika fedha za escrow kwa kulingana na hisa zake. Ni kweli kuwa hisa za kampuni yoyote zinajumuisha assets na liabilities za kampuni. Sina shaka yoyote kuwa bei aliyolipwa ya $75m usd, ilizingatia mambo yote including uwapo wa fedha za IPTL katika escrow account na mchanganuo wake (kwa sababu fedha yote ile sio faida tu) kwa kukubaliana na sigh sethi. Na sio kwamba (kama nimekuelewa) kuwa alilipwa kwanza some money minus 30% ya escrow, halafu eti akaja kulipwa tena 30% za escrow baada ya kuwa zimetolewa. HAKUNA KITU KAMA HICHO! Pili hata Kama singh sethi baadae ataona kuwa bei aliyomlipa Rugemalira ili-consider kimakosa kuwa fedha za escrow ni mali ya IPTL wakati sivyo, hapo kesi itakuwa kati ya Sing sethi na Rugemalira kurudishiana chenji. BADO UMMA HAUJAINGIA HAPO hayo ni mambo ya private sector.

BInafsi sijasema kwamba pesa zote ni mali ya TANESCO ingawaje inawezekana vile vile kwamba zote ni mali ya TANESCO!Hapa kilichokuwa kinatakiwa kufanyika kabla ya pesa kuwa drawn ni kufanya accounting tangu the first transaction to Escrow hadi ya mwisho! Mathalani, Mahakama ilitoa hukumu na kusema IPTL ilikuwa ina-overcharge! Kama ndivyo, kabla ya chochote, any excess amount ambayo ilizidi ilitakiwa kuondolewa kwa muda wote ambao IPTL ili-overcharge kwavile hii ilikuwa ni mali ya TANESCO sawa na radar deal... hapa kulikuwa na change ya TANESCO... je, Mechmar + VIP walirudisha change? Huo ni mfano mmoja tu kukuonesha kwamba si kwamba the whole amount ilikuwa ni mali ya IPTL(VIP+Mechmar)
Hukumu ya mahakama imetoka wakati VIP sio mwanahisa wa IPTL. Madeni yote ya IPTL yanaelekezwa kwa wamiliki wapya wa IPTL. Sioni hapo VIP inaingiaje wakati yenyewe ilishajitoa siku nyingi. Ikigundulika kuwa fedha za escrow zinatakiwa zirudi, VIP hahusiki.

lakini inapogundulika kwamba among the payees ni government and ex-government officials ambao wanahusika moja kwa moja ama kwenye sekta ya nishati , IPTL saga (like RITA), TRA... hakika, ingawaje ana haki na uhuru wa kumpa yeyote amtake, ulipaji huu una-rise suspicion!!!!

Rugemalira hayuko chini ya uchunguzi wa chombo chochote kile cha kisheria as far as i know. Sasa hao "imegundulika" na nani? Hao tunaoambiwa kuwa "amewalipa" mpaka sasa ni tetesi tu, na hazina msingi wowote ule. Hivyo suspicions zozote zile zinakuwa hazina mashiko. Especially ukizingatia kuwa hakuna connection yoyote ile kati ya wanaotajwa na sing sethi. Labda kama baadhi wangekuwa na udugu na sigh sethi, tungesema anawalipa kwa sababu walimshawishi sing sethi kununua hisa za VIP. Si busara kujadili tetesi na uvumi, hiyo list inaweza kuwa photoshop afterall, aliyeitoa hasemi yeye ni nani mpaka ameipata, hakuna uthibitisho wowote ule...anybody could have made it. Humu JF kuna mtu alipewa ubalozi wa china juzi juzi hapa...akajadiliwa weee mpaka serikali ikatoa tamko....
 
Last edited by a moderator:
Assuming hiyo list iliyosambaa kwenye mtandao ni kweli. Bado ni private matter! Hata tukifanya Rugemalira ametoa rushwa RITA (na sijui kwa nini atoe) hilo linakuwa suala la wanahisa wa IPTL walioshitakiana na kusababisha IPTL iwekwe chini ya RITA. IPTL SIYO YA SERIKALI! Sasa hapo mimi na wewe tunaingiaje? IPTL kuwa chini mufilisi (RITA) inahusiana vipi na umma wa watanzania? At most hili ni suala la Rugemalira na PAP ndio wanaotakiwa kushikana mashati kama kuna rushwa ilienda RITA.
Man, are you serious? Suala la rushwa tangu lini likawa ni private matter? Hivi wewe (achilia mbali kampuni) leo hii ukienda hospitali kasha ukampa rushwa daktari ili uhudumiwe hiyo itakuwa ni private matter? RITA yenyewe ni serikali… kuna sheria zinazoongoza RITA na pia kuna sheria pale kampuni inapowekwa chini ya mufilisi wa RITA… si kwamba kwavile ni kampuni binafsi then wenye nayo wanaweza tu kwenda RITA na kusema "we want our company back, itoe kwenye kundi la mufilisi coz' we already have a buyer…!" Hakunakitu kama hicho. Sasa je, sheria zilifuatwa katika kuiondoa IPTL kwenye faili ya mufilisi na kuiuza? Je, ikithibitika kwamba zile statements ni genuine bado huwezi kujiuliza ni namna gani Yule Yule ambae IPTL ilikuwa chini yake amelipwa millions of shillings na wenye kampuni yao!! Hii haiwezi kuwa issue private ya wana-hisa coz' hao wanahisa ni associates kwa maana ikiwa kuna maofisa wa serikali wamehongwa basi hao wanahisa wote watakuwa wamehusika! Hakuna private matter hapo… rushwa ni rushwa tu!
katika maelezo yako hapo juu: ni kweli kuwa kwa kumiliki 30% ya IPTL Rugemalira alikuwa na claim katika fedha za escrow kwa kulingana na hisa zake. Ni kweli kuwa hisa za kampuni yoyote zinajumuisha assets na liabilities za kampuni. Sina shaka yoyote kuwa bei aliyolipwa ya $75m usd, ilizingatia mambo yote including uwapo wa fedha za IPTL katika escrow account na mchanganuo wake (kwa sababu fedha yote ile sio faida tu) kwa kukubaliana na sigh sethi. Na sio kwamba (kama nimekuelewa) kuwa alilipwa kwanza some money minus 30% ya escrow, halafu eti akaja kulipwa tena 30% za escrow baada ya kuwa zimetolewa. HAKUNA KITU KAMA HICHO! Pili hata Kama singh sethi baadae ataona kuwa bei aliyomlipa Rugemalira ili-consider kimakosa kuwa fedha za escrow ni mali ya IPTL wakati sivyo, hapo kesi itakuwa kati ya Sing sethi na Rugemalira kurudishiana chenji. BADO UMMA HAUJAINGIA HAPO hayo ni mambo ya private sector.
Kwanini amlipe kwanza? Sidhani kama ndicho nilichosema! Nilichosema ni kwamba, hisa za IPTL ambazo ni 70%, Seith alizinunua kwa few thousand dollars wakati 30% ya VIP ziliuzwa kwa millions of dollar… does it make it any sense? Sasa basi nilichosema ni kwamba, kuna uwezekano mkubwa kwamba kuna ukwepaji wa kodi… nadhani unafahamu kwamba panapotokea mauziano kuna kodi ya capital gain. Hivyo basi, assume kodi halali ambayo Seith alitakiwa kulipa TRA ni 50 billion lakini akalipa 5 million, hapo maana yake ni kwamba, kiasi alicho-save kwenye kulipa kodi halali ndicho hicho ambacho ametumia kulipa some of 30% shares za VIP! Na kwavile huwezi kukwepa kodi kama hii pasipo kuishirikisha TRA, ndipo pale haishangazi kuona kwenye list ya Ruge kuna maofisa wa TRA!

Labda mtu anaweza kujiuiza: Ikiwa hapo muhongaji ni PAP, kwanini basi majina ya maofisa wa TRA yatokee kwenye list ya Ruge! Kuna various possibilities, moja inawekana kabisa kwamba Seith na Ruge walishakubaliana nani a-deal na nani? Ruge yeye alikuwa tayari kwa lolote ili pesa yake aipate, na huwezi juwa… inawekena vile vile kwamba, pesa ambayo Seith aliipata kwa kukwepa kulipa kodi aligawana na Ruge, huku role ya Ruge katika kupata mgao wa ukwepaji kodi huo ikiwa ni kufanya biashara na maofisa wa TRA!
Hukumu ya mahakama imetoka wakati VIP sio mwanahisa wa IPTL. Madeni yote ya IPTL yanaelekezwa kwa wamiliki wapya wa IPTL. Sioni hapo VIP inaingiaje wakati yenyewe ilishajitoa siku nyingi. Ikigundulika kuwa fedha za escrow zinatakiwa zirudi, VIP hahusiki.
Hukumu ipi? Hii ambayo ilipelekea account ya Escrow kuwa freezed, au? Kama ndiyo, tunafahamu IPTL ilikuwa 70% Mechmar… je, hiyo 30% ilikuwa ya nani kama haikuwa ya VIP? Kama hazikuwa za VIP, sasa kwanini PAP ilitaka ku-settle na VIP? Kwahiyo unataka kusema VIP walikuwa wameshauza 30% ya hisa zake wakati kulikuwa na kesi mahakaman?
Rugemalira hayuko chini ya uchunguzi wa chombo chochote kile cha kisheria as far as i know. Sasa hao "imegundulika" na nani? Hao tunaoambiwa kuwa "amewalipa" mpaka sasa ni tetesi tu, na hazina msingi wowote ule. Hivyo suspicions zozote zile zinakuwa hazina mashiko. Especially ukizingatia kuwa hakuna connection yoyote ile kati ya wanaotajwa na sing sethi. Labda kama baadhi wangekuwa na udugu na sigh sethi, tungesema anawalipa kwa sababu walimshawishi sing sethi kununua hisa za VIP. Si busara kujadili tetesi na uvumi, hiyo list inaweza kuwa photoshop afterall, aliyeitoa hasemi yeye ni nani mpaka ameipata, hakuna uthibitisho wowote ule...anybody could have made it. Humu JF kuna mtu alipewa ubalozi wa china juzi juzi hapa...akajadiliwa weee mpaka serikali ikatoa tamko....
Kuhusu kwamba hizo ni tetesi nimeshasema mara kadhaa kwamba, ikishathibitika statements zinazoonekana kwenye mitandao ni genuine then there MUST be something! Kila mtu anafahamu kwamba haijakuwa confirmed! Lakini ikishakuwa confirmed, huwezi kusema kwamba hakuna connection yoyote na PAP… hao walio chini ya tetesi ni government officials ambao moja kwa moja wanahusika kwenye sakata hili! Sion sababu ya kurudia rudia role ya watu wa TRA, sioni sababu ya kurudia rudia role ya watu wa RITA, sioni sababu ya kurudia rudia role ya mawaziri wa zamani wa wizara ya nishati, sioni sababu ya kurudia rudia role ya mtu kama Chenge ambae kama kumbukumbu zangu zipo sawa, wakati Escrow account inafunguliwa yeye alikuwa ndie Mwanasheria Mkuu wa serikali! Sitaki kuamini kwamba bado hapo huoni connection yoyote kati ya hao maofisa wa serikali na PAP!

Mwisho unasema si busara kujadili tetesi lakini sitakii kuamini eti unachomaanisha ni kwamba hakuna maofisa wa serikali waliohongwa unless kama unataka kusema kwamba hata kauli za Zitto kwamba kuna maofisa kadhaa wamehongwa nazo no tetesi! Je, Zitto nae anaongelea tetesi? Kama sio tetesi na kweli kuna watu wamehongwa, ni ajabu gani miongoni mwa hao waliohongwa kuwa ni hao wanaoonekana kwenye statement ya Ruge? Good enough, majority ya wale wanaoonekana ni wale wale ambao they have some roles in this whole thing! Kwamba humu JF kuna mtu alishapewa ubalozi na baadae kugundulika kwamba si kweli haiwezi kuwa sababu tosha kuhalalisha kwamba kila kisemwacho JF uongo kwavile kuna mambo mengi ambayo yalianzia hapa hapa JF na watu wakabisha lakini hatimae ikabainika kwamba ni KWELI, UKWELI MTUPU!
 
Last edited by a moderator:
acha hizo wewe...ingia PM kwa malumbano binafsi, hapa tunazungumzia ishu serious. Wewe unaionaje? kama mtanzania half-cast?

half-cast my foot. Usiingilie siasa za watanzania. Labda kama watanzania wanakubali dual-citizenship. Njoo kwenye jukwaa letu huku.
 
Man, are you serious? Suala la rushwa tangu lini likawa ni private matter? Hivi wewe (achilia mbali kampuni) leo hii ukienda hospitali kasha ukampa rushwa daktari ili uhudumiwe hiyo itakuwa ni private matter? RITA yenyewe ni serikali… kuna sheria zinazoongoza RITA na pia kuna sheria pale kampuni inapowekwa chini ya mufilisi wa RITA… si kwamba kwavile ni kampuni binafsi then wenye nayo wanaweza tu kwenda RITA na kusema "we want our company back, itoe kwenye kundi la mufilisi coz' we already have a buyer…!" Hakunakitu kama hicho. Sasa je, sheria zilifuatwa katika kuiondoa IPTL kwenye faili ya mufilisi na kuiuza? Je, ikithibitika kwamba zile statements ni genuine bado huwezi kujiuliza ni namna gani Yule Yule ambae IPTL ilikuwa chini yake amelipwa millions of shillings na wenye kampuni yao!! Hii haiwezi kuwa issue private ya wana-hisa coz' hao wanahisa ni associates kwa maana ikiwa kuna maofisa wa serikali wamehongwa basi hao wanahisa wote watakuwa wamehusika! Hakuna private matter hapo… rushwa ni rushwa tu!
Kwanini amlipe kwanza? Sidhani kama ndicho nilichosema! Nilichosema ni kwamba, hisa za IPTL ambazo ni 70%, Seith alizinunua kwa few thousand dollars wakati 30% ya VIP ziliuzwa kwa millions of dollar… does it make it any sense? Sasa basi nilichosema ni kwamba, kuna uwezekano mkubwa kwamba kuna ukwepaji wa kodi… nadhani unafahamu kwamba panapotokea mauziano kuna kodi ya capital gain. Hivyo basi, assume kodi halali ambayo Seith alitakiwa kulipa TRA ni 50 billion lakini akalipa 5 million, hapo maana yake ni kwamba, kiasi alicho-save kwenye kulipa kodi halali ndicho hicho ambacho ametumia kulipa some of 30% shares za VIP! Na kwavile huwezi kukwepa kodi kama hii pasipo kuishirikisha TRA, ndipo pale haishangazi kuona kwenye list ya Ruge kuna maofisa wa TRA!

Labda mtu anaweza kujiuiza: Ikiwa hapo muhongaji ni PAP, kwanini basi majina ya maofisa wa TRA yatokee kwenye list ya Ruge! Kuna various possibilities, moja inawekana kabisa kwamba Seith na Ruge walishakubaliana nani a-deal na nani? Ruge yeye alikuwa tayari kwa lolote ili pesa yake aipate, na huwezi juwa… inawekena vile vile kwamba, pesa ambayo Seith aliipata kwa kukwepa kulipa kodi aligawana na Ruge, huku role ya Ruge katika kupata mgao wa ukwepaji kodi huo ikiwa ni kufanya biashara na maofisa wa TRA!
Hukumu ipi? Hii ambayo ilipelekea account ya Escrow kuwa freezed, au? Kama ndiyo, tunafahamu IPTL ilikuwa 70% Mechmar… je, hiyo 30% ilikuwa ya nani kama haikuwa ya VIP? Kama hazikuwa za VIP, sasa kwanini PAP ilitaka ku-settle na VIP? Kwahiyo unataka kusema VIP walikuwa wameshauza 30% ya hisa zake wakati kulikuwa na kesi mahakaman?

Kuhusu kwamba hizo ni tetesi nimeshasema mara kadhaa kwamba, ikishathibitika statements zinazoonekana kwenye mitandao ni genuine then there MUST be something! Kila mtu anafahamu kwamba haijakuwa confirmed! Lakini ikishakuwa confirmed, huwezi kusema kwamba hakuna connection yoyote na PAP… hao walio chini ya tetesi ni government officials ambao moja kwa moja wanahusika kwenye sakata hili! Sion sababu ya kurudia rudia role ya watu wa TRA, sioni sababu ya kurudia rudia role ya watu wa RITA, sioni sababu ya kurudia rudia role ya mawaziri wa zamani wa wizara ya nishati, sioni sababu ya kurudia rudia role ya mtu kama Chenge ambae kama kumbukumbu zangu zipo sawa, wakati Escrow account inafunguliwa yeye alikuwa ndie Mwanasheria Mkuu wa serikali! Sitaki kuamini kwamba bado hapo huoni connection yoyote kati ya hao maofisa wa serikali na PAP!

Mwisho unasema si busara kujadili tetesi lakini sitakii kuamini eti unachomaanisha ni kwamba hakuna maofisa wa serikali waliohongwa unless kama unataka kusema kwamba hata kauli za Zitto kwamba kuna maofisa kadhaa wamehongwa nazo no tetesi! Je, Zitto nae anaongelea tetesi? Kama sio tetesi na kweli kuna watu wamehongwa, ni ajabu gani miongoni mwa hao waliohongwa kuwa ni hao wanaoonekana kwenye statement ya Ruge? Good enough, majority ya wale wanaoonekana ni wale wale ambao they have some roles in this whole thing! Kwamba humu JF kuna mtu alishapewa ubalozi na baadae kugundulika kwamba si kweli haiwezi kuwa sababu tosha kuhalalisha kwamba kila kisemwacho JF uongo kwavile kuna mambo mengi ambayo yalianzia hapa hapa JF na watu wakabisha lakini hatimae ikabainika kwamba ni KWELI, UKWELI MTUPU!

Mkuu...huyu jMali hawezi kuelewa hata ukimueleweshaje. Unajua kwa nini? Ni mnyarwanda mwenzangu anaejiita mtanzania. Muonee huruma
 
Last edited by a moderator:
Man, are you serious? Suala la rushwa tangu lini likawa ni private matter? Hivi wewe (achilia mbali kampuni) leo hii ukienda hospitali kasha ukampa rushwa daktari ili uhudumiwe hiyo itakuwa ni private matter? RITA yenyewe ni serikali… kuna sheria zinazoongoza RITA na pia kuna sheria pale kampuni inapowekwa chini ya mufilisi wa RITA… si kwamba kwavile ni kampuni binafsi then wenye nayo wanaweza tu kwenda RITA na kusema "we want our company back, itoe kwenye kundi la mufilisi coz' we already have a buyer…!" Hakunakitu kama hicho. Sasa je, sheria zilifuatwa katika kuiondoa IPTL kwenye faili ya mufilisi na kuiuza?
Kwa maelezo yako nahisi inawezekana hujui kazi ya RITA na jinsi inavyofanya kazi, naomba ufuatilie na kujiongezea ufahamu how RITA works. Kuna hatua za ufilisi na si kila kampuni inayowekwa chini ya RITA maana yake imefisilika au ndio inafilisiwa. IPTL iliwekwa RITA katika level ya uangalizi, hawakuwekwa katika hatua ya ufilisi. katika hatua iliyowekwa IPTL iliruhusu kuondolewa hadhi ya kuwa chini ya RITA na kurudishwa kwa wenyewe pale ambapo financial affairs zake zitatengemaa. Na ndicho hicho kilichofanyika. Amri ya mahakama kutokana na maombi ya James Rugemalira akidai haki yake, ndio yaliyoweka IPTL chini ya RITA, na amri ya mahakama kutokana na maombi ya James Rugemalira huyu huyu baada ya kulipwa chake na Sing sethi, ndio yaliyoondoa IPTL chini ya RITA. Mbona kila kitu kiko straight forward?


Je, ikithibitika kwamba zile statements ni genuine bado huwezi kujiuliza ni namna gani Yule Yule ambae IPTL ilikuwa chini yake amelipwa millions of shillings na wenye kampuni yao!! Hii haiwezi kuwa issue private ya wana-hisa coz' hao wanahisa ni associates kwa maana ikiwa kuna maofisa wa serikali wamehongwa basi hao wanahisa wote watakuwa wamehusika! Hakuna private matter hapo… rushwa ni rushwa tu!
Again, kama hujui kazi ya RITA lazima utatuhumu rushwa, lakini once ukijua, utagundua kuwa there is ABSOLUTELY NOTHING OF THE SORT. kampuni zinawekwa chini ya RITA kwa amri ya mahakama na zinaondolewa kwa amri ya mahakama. kama kuna mtu wa RITA amelipwa amelipwa kwa ishu zingine, vinginevyo thibitisha (ukionyesha ni jambo gani ambalo ofisa wa RITA kafanya kumsaidia JR).

Kwanini amlipe kwanza? Sidhani kama ndicho nilichosema! Nilichosema ni kwamba, hisa za IPTL ambazo ni 70%, Seith alizinunua kwa few thousand dollars wakati 30% ya VIP ziliuzwa kwa millions of dollar… does it make it any sense? Sasa basi nilichosema ni kwamba, kuna uwezekano mkubwa kwamba kuna ukwepaji wa kodi… nadhani unafahamu kwamba panapotokea mauziano kuna kodi ya capital gain. Hivyo basi, assume kodi halali ambayo Seith alitakiwa kulipa TRA ni 50 billion lakini akalipa 5 million, hapo maana yake ni kwamba, kiasi alicho-save kwenye kulipa kodi halali ndicho hicho ambacho ametumia kulipa some of 30% shares za VIP! Na kwavile huwezi kukwepa kodi kama hii pasipo kuishirikisha TRA, ndipo pale haishangazi kuona kwenye list ya Ruge kuna maofisa wa TRA!
Mkuu unachanganya mambo, there is no doubt kuwa sethi kakwepa kodi kwenye transaction ya kununua 70% za IPTL. Lakini hoja yangu ni kuwa hilo HALIMHUSU Rugemalira. Sethi alianza kwanza kumnunua Rugemalira kwa 75mil usd mwezi september! By the time sethi ananegotiate hizo 70%, alikuwa tayari anamiliiki 30% aliyonunua kwa Ruge. Ukwepaji kodi wa Sethi unamhusisha vipi Rugemalira tena? Kama Ruge alitumwa na sethi kuwalipa TRA ili wafoji kodi ya sethi hilo ni jambo lingine, lakini huwezi tu kudai Ruge anahusika na ukwepaji kodi wa Sethi mpaka uonyeshe uhusiano. Na hilo litahitaji uchunguzi wa vyombo vya sheria sio conspiracies za JF! Lakini kwangu itakuwa ngumu kuamini hivyo kwa kuwa Rugemalira hakuwa na shida kiasi hicho. Hisa zake zilikuwa pale pale, na mitambo ya IPTL ilikuwa pale pale, haki yake angepata tu hata iweje! In fact ni sethi ndio alikuwa na shida ya IPTL sio Ruge alikuwa na shida ya fedha za sethi. Hivi unajua kuwa Ruge mbali na bei ya hisa za VIP pia alitoa masharti kwa yoyote atakayenunua juu ya bei ya umeme?

Labda mtu anaweza kujiuiza: Ikiwa hapo muhongaji ni PAP, kwanini basi majina ya maofisa wa TRA yatokee kwenye list ya Ruge! Kuna various possibilities, moja inawekana kabisa kwamba Seith na Ruge walishakubaliana nani a-deal na nani? Ruge yeye alikuwa tayari kwa lolote ili pesa yake aipate, na huwezi juwa… inawekena vile vile kwamba, pesa ambayo Seith aliipata kwa kukwepa kulipa kodi aligawana na Ruge, huku role ya Ruge katika kupata mgao wa ukwepaji kodi huo ikiwa ni kufanya biashara na maofisa wa TRA!
Hii ni conspiracy, tetesi, uvumi ambao kwa great thinkers hatupaswi ku-entertain. Viko vyombo vya sheria, na ripoti inasomwa leo, let's hear them. Sethi ni kweli amekwepa kodi na TRA wanawajibika, lakini kujifanya sisi ni wachunguzi kiasi cha kuchafua majina ya watu sio vizuri. Wacha sheria ichukue mkondo wake.
Hukumu ipi? Hii ambayo ilipelekea account ya Escrow kuwa freezed, au? Kama ndiyo, tunafahamu IPTL ilikuwa 70% Mechmar… je, hiyo 30% ilikuwa ya nani kama haikuwa ya VIP? Kama hazikuwa za VIP, sasa kwanini PAP ilitaka ku-settle na VIP? Kwahiyo unataka kusema VIP walikuwa wameshauza 30% ya hisa zake wakati kulikuwa na kesi mahakamani?
Kutokana na kesi ya VIP, IPTL iliwekwa chini ya mufilisi (RITA) katika mchakato wa kuanza kufilisiwa (ingawa haikufikia stage hiyo), ili PAP anunue IPTL ilibidi aanze kwanza ku-deal na VIP ili IPTL itoke kwenye status ya mufilisi, na ndipo iwe na uwezo wa kuuza hisa zake.

Kuhusu kwamba hizo ni tetesi nimeshasema mara kadhaa kwamba, ikishathibitika statements zinazoonekana kwenye mitandao ni genuine then there MUST be something! Kila mtu anafahamu kwamba haijakuwa confirmed! Lakini ikishakuwa confirmed, huwezi kusema kwamba hakuna connection yoyote na PAP… hao walio chini ya tetesi ni government officials ambao moja kwa moja wanahusika kwenye sakata hili! Sion sababu ya kurudia rudia role ya watu wa TRA, sioni sababu ya kurudia rudia role ya watu wa RITA, sioni sababu ya kurudia rudia role ya mawaziri wa zamani wa wizara ya nishati, sioni sababu ya kurudia rudia role ya mtu kama Chenge ambae kama kumbukumbu zangu zipo sawa, wakati Escrow account inafunguliwa yeye alikuwa ndie Mwanasheria Mkuu wa serikali! Sitaki kuamini kwamba bado hapo huoni connection yoyote kati ya hao maofisa wa serikali na PAP!

Mpaka sasa hakuna ushahidi, hivi nikikuuliza hayo majina yametoka wapi utanijibu nini? Huwezi kuanza kujenga hoja juu ya kitu ambacho hakijathibitishwa wala hakijulikani usahihi wake. Akaunti tunaambiwa ni ya rugemalira, je aliyetoa hiyo statement ni nani? Mwanae, mkewe? Majina yaliyoko sawa ni ya viongozi wa zamani wa serikali. so what? Msingi mzima wa hoja yako umejengwa kwenye assumption kuwa Ruge katumiwa na sigh sethi kukwepa kodi! msingi ambao kwangu hauwezekani. Orodha ina majina mengi zaidi ya raia wa kawaida kuliko hao viongozi wa serikali, je mtu kama waziri tibaijuka amehusikaje? wakati wa hiyo escrow yeye alikuwa nani?

Anyway naomba tusitishe mjadala mpaka baada ripoti itakapotolewa leo, tujue mengi zaidi.
 
Mkuu jMali,

Nilichukua uamuzi wa kutokukujibu post yako ya mwisho si tu kwamba nilijisikia uvivu kurudia kitu kile kile kila wakati huku ukijifanya hutaki kuelewa, bali pia busara ilinishawishi kuacha ili ujibiwe na Kamati ya PAC!

Je, unaweza kuniambia kati ya yale yote niliyosema hapo kabla, ni lipi ni la uongo? Nilikupa hata uwezekano wa kwamba ni pesa za Escrow ndizo zilitumika kumlipa Ruge, bado ulikataa...!! Je, PAC nao ni waongo?

 
Last edited by a moderator:
Mkuu murutongore,

With due respect, naomba uniitie jMali popote alipo maana naona ameikimbia thread yake!!!!
 
Last edited by a moderator:
Kosa lake ni kuwa na roho nzuri na kuanza kuzigawa hizo pesa kwa mpangilio maalum.
Cha kushangaza pesa za escrow!
Namna pesa zilivyolipwa, 40.425, 80.8, 16.1,80.850,1.617, 323.400, hii maana yake nini?
 
FACTS:
IPTL sio kampuni ya umma, PAP sio kampuni ya umma, VIP sio kampuni ya umma. This is purely a private sector transaction... Naomba kufahamishwa kwa hoja tafadhali, uharamia wa James Rugemalira upo wapi.

Tangu lini dalali wa biashara katika sekta binafsi akawa waziri wa serkali katika ofisi za serkali??
 
Mkuu murutongore,

With due respect, naomba uniitie jMali popote alipo maana naona ameikimbia thread yake!!!!

mkuu chige , sisi tumechamzoea huku.. anajua kulianzisha lakini kumaliza huwa hawezi..msamehe bure.. kakutana na intellectual
 
Last edited by a moderator:
Kama si mwizi mbona kaweka mawakili mpaka wa ulaya?
Huyu jMali bhana, hadi ameninfanya nishindwe kutekeleza majukumu yangu vizuri leo manake tangu asubuhi, kila ninachomwelewesha hataki matokeo yake, yale yale niliyomwambia ndiyo yaliyosemwa na PAC... alivyoona kibao kimemgeukia, amekula kona!!!
 
Last edited by a moderator:
Sijajua kwa ishu nzito kama hii anaibuka MTU kutetea moja kati ya mafisadi. Siku zote fisadi ni mkwepaji na ndio maana hata huyu Singa Seth though alijua anafisadise lakini alitengeneza mfumo kuhakikisha analinda maslah na usalama wake kisheria!
 
Majibu nadhani umeyapata kwenye ripoti ya PAC.
 
Back
Top Bottom