jMali
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 8,412
- 5,013
- Thread starter
- #201
mkuu kwanza nikusahihishe, zitto hajaeleza ROLE yoyote ambayo hawa watu wamecheza kwenye wizi wa singh sethi, kataja tu vyeo vyao, ambavyo ni common knowledge kwa kila mtanzania. Who doesn't know kuwa Chenge aliwahi kuwa attorney general? au tibaijuka ni waziri? Tatizo la Zitto ni lile lile uliokuwa nalo wewe, sensationalism! Majina makubwa yana-attract nzi! Ndio maana nikikuomba unipe theory ya kwa nini Methodious kilaini "kalipwa" sidhani kama utanieleza (well may be you can try hahaha,) Sasa yeye zitto kamtaja ili iweje? wametajwa ili kunogesha ripoti otherwise hakuna ROLE yoyote ambayo Zitto ameiainisha, badala yake amedai kuwa majina yao yamepelekwa takukuru sio kwa mashtaka BALI UCHUNGUZI! Swali ni je uchunguzi wa nini, kwa nini takuru hao wasiwe wamekamilisha huo uchunguzi mpaka leo? Je was that fair kuwataja wakati for now hakuna chochote cha maana kinachowakabili? jibu ni kuwa wametajwa kwa kuwa wanafahamika that's all!Kama bado unaendelea kukanusha na kudai alichosema Zitto ndicho ulichosema wewe basi unanifanya niamini una interest fulani!
Zitto ameelezea mashaka ya government officials and ex-officials kulipwa na Ruge na akaelelezea role ya kila mmoja kv Chenge kuwa ex-AG, yule jamaa wa RITA n.k mambo ambayo nilikueleza na wewe ukakana... hapa tena unadai alichosema Zitto ndicho ulichosema wewe!!
- Nilikuambia wazi kwamba ingawaje Ruge pesa ni zake na ana haki ya kutumia apendavyo lakini bado matumizi yaliyoonekana yanatishia shaka na wewe ukapinga na hicho ndicho alichosema Zitto!
Pili, Zitto hajaweka shaka yoyote kuwa VIP wamelipwa kiharamu. Hiyo ndio pointi ya msingi, ndio maana its pointless kutaja majina ya watu waliopewa pesa ambayo HUNA SHAKA NAYO KUWA NI HALALI! Let me ask you this simple question. Kama Rugemalira asingegawa hizi pesa, labda mpaka sasa zingekuwa tu pale Mkombozi, Je mashtaka yako dhidi yake yangekuwa nini? Ukijibu hili suala ndio utakuwa umemaliza mzizi wa fitna! The only thing kinachowavutia watu kumchafua rugemalira ni orodha ya watu aliowapa pesa, cha ajabu some of them kwa uwazi kabisa kama mama tibaijuka.
i must have missed that part au labda wewe umetafsiri vingine. Ngoja tupate file la ripoti ili tuwe tunafanya reference moja kwa moja, kwa sababu kwa sasa hivi tunatumia memory zetu tu ya kuona kwenye TV, so i reserve this nitajibu nikijipanga kwa file.Nikakueleza kwamba kuna uwezekano mkubwa kwamba Seith na Ruge wamecheza mchezo pamoja na kuna uwezekano hata pesa alizolipwa Ruge zimetokana na huo mchezo na nikakueleza kuna uwezekano mkubwa kwamba ingawaje issue ni ya PAP lakini inawezekana walipeana majukumu ya nani a-deal na nani lakini wewe ukapinga na Zitto amethibitisha hilo baada ya kusema kuna wale ambao walilipwa kupitia a/c ya Ruge na kuna wale waliolipwa kupitia a/c ya PAP... inashangaza hapa unapodai kwamba ulichosema wewe ndicho alichosema Zitto!!
Ruge na waliopokea fedha zake wameripotiwa takukuru FOR WHAT EXACTLY? Hawajashitakiwa! wameripotiwa! tusubiri kama uchunguzi utawatia hatiani for anything ndipo tujadili. Ndio maana narudia tena, watanzania tunapenda cheap politics za majina majina badala ya substance. Mi nasubiri kusikia how methodious kilaini alivyokuwa muhimu katika kuiba fedha za escrow mpaka kutajwa bungeni kuwa "kalipwa" na rugemalira....Unadai hakuna mahala Zitto alipomtuhumu Ruge... labda tu nikukumbushe kwamba moja ya mapendekezo ya PAC ni kwamba pesa ambazo Ruge na mwenzake waligawa kama njugu zinapaswa kurudishwa na pesa za Escrow pia zinapaswa kurudishwa... na ninaposema za Escrow maana yake ni pamoja na zile alizochukua Ruge... na kama hukusikia vizuri, suala la Ruge limeachwa kwa TAKUKURU na sidhani kama ulitarajia ahukumiwe bungeni... hapa bado unasema huoni tatizo liko wapi! Taratibu za kibenji zipi unazodai zimekiukwa?
Iko hivi, Ruge alishagombana na IPTL at the time anawatonya Tanesco. Elewa kuwa kama minority share holder hakuwa na nguvu za maamuzi juu ya IPTL ingawa kweli yeye ni mwanahisa. Wakati wanaelewana na Mechmar bei haikuwa ile, Mechmar walikuja kupandisha baada ya kugombana naye, so sio kweli kwamba aliwazunguka. Rudia timeline of events. Ndio maana alishitaki mahakamani ili iwekwe chini ya ulinzi na yeyey apate haki yake. Yeye kama mbia-mzawa alifanya jambo la kizalendo kwa kuitonya Tanesco, hata hapo napo unamlaumu?Kwamba eti Ruge ndie kawatonya TANESCO wala sio hoja ya msingi na kama alikuwa na nia njema asingebadilika na kuiibia serikali! Ruge anaonesha wazi kwamba ni mbinafsi... fuatlia hata kwenye issue za Mabibo Wine... kila siku kupelekana kwenye vyombo vya sheria na vikampuni vidogo vidogo ili mradi tu awe na sole right ya ku-import ama bia hii au ile! Na katika hili la IPTL, kuna uwezekano mkubwa sana lengo la Ruge kuwatonya TANESCO wala haikuwa kwa ajili ya kuipenda nchi yake lakini bila shaka alifanya hivyo ili Mechmae imwage manyanga kisha VIP wafanye biashara na TANESCO peke yao vinginevyo, sioni maana yake, ikiwa yeye ni share partner wa IPTL, ilikuwaje IPTL wapange chaji kubwa against TANESCO kisha na yeye aridhiane na wenzake kwamba watachaji XYZ lakini baadae anawazunguka na kuwaambia TANESCO kwamba eti IPTL wanatoza pesa kubwa wakati na yeye ni sehemu ya IPTL! Hapa Ruge alitaka kuwazunguka wenzake ili biashara ya umeme afanye peke yake sawa na jinsi anavyohangaishana na vikampuni vidogo ku-demand exlussive right ya kuagiza baadhi ya bia hapa nchini!
Ndio maana nasema mwarobaini utakuwa tupate copy ya ripoti humu ili tuonyeshane EXACTLY nini kilisemwa badala ya kupambana vita vya kumbukumbu. Mimi nilichosikia na kuona ni zitto akisema kauli inafanana hivi: "James rugemalira aliitwa na muhongo na kuulizwa ulipwe shilingi ngapi ili ufute kesi na IPTL " au kitu kinafanana na hicho. Sethi ndio alimu-approach rugemalira via Muhongo na ku-offer kununua hisa za VIP. Na ndio maana nikasema argument ya ushirikiano wa Rugemalira na sethi kwenye escrow is ridiculous! Sasa sijui mwenzangu umesikia ripoti ipi tena. Na hata zitto mwenyewe the only hoja aliyonayo against rugemalira ni kuwa kawapa fedha watu wanaojulikana na majina kayapeleka takukuru ili waangalie kama "yaliyomo yamo". NOTHING ON THE DEAL BETWEEN VIP AND PAP.Mwisho unauliza inawezekana vipi Ruge huyo huyo acheze mchezo na IPTL kuiba fedha za Escrow! Kwanza, Ruge hakucheza mchezo na wale ambao aligombana nao bali alicheza mchezo na mpiga deal mwingine anayeenda kwa jina la Seith! Ingawaje unasema kwamba my argument is ridiculous, nakushauri waulize waliomsikia vizuri wakati Zitto anasoma ripoti maana ake inaelekea ama hukuisikiliza au ulisikiliza lakini hutaki tu kukubali ukweli!