Kwa maelezo yako nahisi inawezekana hujui kazi ya RITA na jinsi inavyofanya kazi, naomba ufuatilie na kujiongezea ufahamu how RITA works. Kuna hatua za ufilisi na si kila kampuni inayowekwa chini ya RITA maana yake imefisilika au ndio inafilisiwa. IPTL iliwekwa RITA katika level ya uangalizi, hawakuwekwa katika hatua ya ufilisi. katika hatua iliyowekwa IPTL iliruhusu kuondolewa hadhi ya kuwa chini ya RITA na kurudishwa kwa wenyewe pale ambapo financial affairs zake zitatengemaa. Na ndicho hicho kilichofanyika. Amri ya mahakama kutokana na maombi ya James Rugemalira akidai haki yake, ndio yaliyoweka IPTL chini ya RITA, na amri ya mahakama kutokana na maombi ya James Rugemalira huyu huyu baada ya kulipwa chake na Sing sethi, ndio yaliyoondoa IPTL chini ya RITA. Mbona kila kitu kiko straight forward?
Again, kama hujui kazi ya RITA lazima utatuhumu rushwa, lakini once ukijua, utagundua kuwa there is ABSOLUTELY NOTHING OF THE SORT. kampuni zinawekwa chini ya RITA kwa amri ya mahakama na zinaondolewa kwa amri ya mahakama. kama kuna mtu wa RITA amelipwa amelipwa kwa ishu zingine, vinginevyo thibitisha (ukionyesha ni jambo gani ambalo ofisa wa RITA kafanya kumsaidia JR).
Mkuu unachanganya mambo, there is no doubt kuwa sethi kakwepa kodi kwenye transaction ya kununua 70% za IPTL. Lakini hoja yangu ni kuwa hilo HALIMHUSU Rugemalira. Sethi alianza kwanza kumnunua Rugemalira kwa 75mil usd mwezi september! By the time sethi ananegotiate hizo 70%, alikuwa tayari anamiliiki 30% aliyonunua kwa Ruge. Ukwepaji kodi wa Sethi unamhusisha vipi Rugemalira tena? Kama Ruge alitumwa na sethi kuwalipa TRA ili wafoji kodi ya sethi hilo ni jambo lingine, lakini huwezi tu kudai Ruge anahusika na ukwepaji kodi wa Sethi mpaka uonyeshe uhusiano. Na hilo litahitaji uchunguzi wa vyombo vya sheria sio conspiracies za JF! Lakini kwangu itakuwa ngumu kuamini hivyo kwa kuwa Rugemalira hakuwa na shida kiasi hicho. Hisa zake zilikuwa pale pale, na mitambo ya IPTL ilikuwa pale pale, haki yake angepata tu hata iweje! In fact ni sethi ndio alikuwa na shida ya IPTL sio Ruge alikuwa na shida ya fedha za sethi. Hivi unajua kuwa Ruge mbali na bei ya hisa za VIP pia alitoa masharti kwa yoyote atakayenunua juu ya bei ya umeme?
Hii ni conspiracy, tetesi, uvumi ambao kwa great thinkers hatupaswi ku-entertain. Viko vyombo vya sheria, na ripoti inasomwa leo, let's hear them. Sethi ni kweli amekwepa kodi na TRA wanawajibika, lakini kujifanya sisi ni wachunguzi kiasi cha kuchafua majina ya watu sio vizuri. Wacha sheria ichukue mkondo wake.
Kutokana na kesi ya VIP, IPTL iliwekwa chini ya mufilisi (RITA) katika mchakato wa kuanza kufilisiwa (ingawa haikufikia stage hiyo), ili PAP anunue IPTL ilibidi aanze kwanza ku-deal na VIP ili IPTL itoke kwenye status ya mufilisi, na ndipo iwe na uwezo wa kuuza hisa zake.
Mpaka sasa hakuna ushahidi, hivi nikikuuliza hayo majina yametoka wapi utanijibu nini? Huwezi kuanza kujenga hoja juu ya kitu ambacho hakijathibitishwa wala hakijulikani usahihi wake. Akaunti tunaambiwa ni ya rugemalira, je aliyetoa hiyo statement ni nani? Mwanae, mkewe? Majina yaliyoko sawa ni ya viongozi wa zamani wa serikali. so what? Msingi mzima wa hoja yako umejengwa kwenye assumption kuwa Ruge katumiwa na sigh sethi kukwepa kodi! msingi ambao kwangu hauwezekani. Orodha ina majina mengi zaidi ya raia wa kawaida kuliko hao viongozi wa serikali, je mtu kama waziri tibaijuka amehusikaje? wakati wa hiyo escrow yeye alikuwa nani?
Anyway naomba tusitishe mjadala mpaka baada ripoti itakapotolewa leo, tujue mengi zaidi.