Kongamano la Utimiaji wa Mambo ya Kisasa kwa Njia ya Kichina na Fursa kwa Afrika lafanyika

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
1678353304118.png

Kongamano la Utimiaji wa Mambo ya Kisasa kwa Njia ya Kichina na Fursa kwa Afrika lililoandaliwa na Idara ya Asia na Afrika ya Shirika Kuu la Utangazaji la China (CMG) limefanyika kwa njia ya mtandao, na kuwashirikisha wahariri na wanahabari wa vyombo muhimu vya habari vya nchi za Afrika Mashariki zikiwemo Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

1678352114473.png

Mfanyakazi wa Idhaa ya Kiswahili ya Idara ya Asia na Afrika ya CMG kutoka Tanzania Fadhili Mpunji, amefafanua yaliyomo na maana ya utimiaji wa mambo ya kisasa kwa njia ya Kichina, na kusema kama jambo muhimu zaidi, wazo la maendeleo ya amani na ustawi wa pamoja la China limeoneshwa kupitia mapendekezo yaliyotolewa na China kuhusu usalama wa kimataifa na na maendeleo ya kimataifa.

1678352143125.png

Mwanahabari wa Shirika la Habari la Umma la Tanzania Ephrahim Bahemu ambaye yuko China kuripoti mkutano wa Bunge la Umma la China na mkutano wa Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la China, ameeleza maoni yake kuhusu utimiaji wa mambo ya kisasa kwa njia ya Kichina, na maana yake kwa maendeleo na ustawi wa Afrika. Amesema njia ya Kichina ina tofauti ya kimsingi na ile ya nchi za Magharibi, kwani inazingatia zaidi ustawi wa pamoja wa wananchi wote, na maendeleo ya utamaduni na maadili sambamba.

1678352169248.png

Mwanahabari wa Shirika la Utangazaji la Kenya (KBC) Eric Biegon anayefuatilia sana masuala ya China amebainisha kuwa, njia maalumu ya China katika kutimiza mambo ya kisasa imepanua wazo na chaguo la nchi nyingine zinazoendelea duniani, na nchi za Afrika zinapaswa kuiga uzoefu unaofaa wa China, ili kutimiza mambo ya kisasa kwa njia inayoendana utamaduni na mawazo maalumu ya Kiafrika kuhusu thamani.
 
Back
Top Bottom