kongamano la katiba UDSM Lahujumiwa

ZAma za propaganda zimepita, hizi ni zama za kutumia kichwa kufikiri. Nashangaa watu wanavitengo vya propaganda eti kuwashawishi waamini uongo kuwa ukweli. Uhuru, Habari leo, Tambwe Hiza na hata hao Waislam waandae Kongamano lao na mazimio yao yatakuwa yao. Lkn naamini kunawaislamu kibao wanauelewa na macho na masikio yao MKURUMA kesho.
 
Kama waislamu hawatasimama na kuamua mambo yao wenyewe ipo siku watakuwa njia panda, maana tukiutafuta usafi a hao wanaowatumia kiukweli haupo, na hapa hata mafundisho ya uislamu wanakuwa wameyasaliti.
Huu udini tunaouona ukiletwa kwetu kwa njia hii ya ajabuajabu iko siku utatucost.
 
Stupit this udinism, yani kla mara wanafikiri watanzania ni wapumbavu kiasi cha kuamini fulani anahujimiwa kisa ni wa dini fulani. Huu ni ujinga ambao watanzania lazima tuuepuku.

mbona kipindi cha mkapa mambo mengi ya kutisha yalikuwepo kama kuzama kwa MV Bukoba. Nahakika nao wangesema wamehujumiwa. wakati mambo mengine ni uongozi mbovu.

Enyi waislam wenzangu msikubali kununulika na kuanza propoganda chafu na mkashindwa kumkosoa mtu eti kisa ni dini yako. Kwenye serikali hatuangalii dini tunaangalia mtu safi asifiwe na mchafu akemewe.

Wakristo kwa waislam. Kemeeni uovu mkiuona hata kama mtu ni wa dini yako, na msifieni mtu pale anapostahili sio kutumiwa na wanasiasa kuleta pumba huku familia zenu zikibaki masikini.

King Suleiman, ninakuunga mkono sana. Haya mambo ya wachovu wa kisiasa na watafuta maslahi binafsi yataleta balaa nchini mwetu. Wananchi tuangalie maisha yetu na mustakabali wa taifa letu na kizazi chetu cha baadaye.

Mtu anayetumia dini kwa ajili ya kujikinga na sauti ya umma juu ya uovu wake anaoufanya analeta balaa kabisa katika nchi hii. Tusikubali kudanganganywa na siasa za udanganyifu. Mungu epusha shida hii kwa watanzania.
 
huu ndio mchezo wa JK, ku divert attention ya kungamano la Katiba hapo UDSM, kama
vile Arusha eti wana CCM wanaomba kuandamana kumsifu meya wa Arusha, then kuweka
movie sawa polisi wamewanyima ruhusa hadi siku nyingine, all this ni kuchaganyanya na
kuwatoa ktk attention, ila watu wanajua, huu ni FIRST DEGREE YA UJINGA as they are nothing they have.
 
ZAma za propaganda zimepita, hizi ni zama za kutumia kichwa kufikiri. Nashangaa watu wanavitengo vya propaganda eti kuwashawishi waamini uongo kuwa ukweli. Uhuru, Habari leo, Tambwe Hiza na hata hao Waislam waandae Kongamano lao na mazimio yao yatakuwa yao. Lkn naamini kunawaislamu kibao wanauelewa na macho na masikio yao MKURUMA kesho.

Word!
 
Waislamu wanahaki ya kukutana na kama wanashutumu maaskofu wache wafanye hivyo na ni vema vyombo vya habari vikaandika mambo yote watakayoto!!!
Mwisho wa siku itajulikana kama ni ya kweli!!!
Kikwete alianza kusema hayo wakati wa uzinduzi wa bunge , akasema kuna udini , lakini mpaka sasa hana ushahidi wa mambo aliyosema !!!
Ametia aibu mbele ya jamii!!!
Kama kikwete kawatuma waislamu watamwaibisha !!!
Jambo ni moja ,tunataka viongozi wanaojari maaendeleo ya wananchi na siyo maendeleo ya rostam!!
Je, sabodo mustafa ni dini gani?? Mbona anachangia chadema???
Sabodo katoa mchango wa 10m kwa familia ya denis mkristo aliyeuawa arusha , lakini hajatoa kwa ismail ambaye ni muislamu mwenzake!!!
 
Stupit this udinism, yani kla mara wanafikiri watanzania ni wapumbavu kiasi cha kuamini fulani anahujimiwa kisa ni wa dini fulani. Huu ni ujinga ambao watanzania lazima tuuepuku.

mbona kipindi cha mkapa mambo mengi ya kutisha yalikuwepo kama kuzama kwa MV Bukoba. Nahakika nao wangesema wamehujumiwa. wakati mambo mengine ni uongozi mbovu.

Enyi waislam wenzangu msikubali kununulika na kuanza propoganda chafu na mkashindwa kumkosoa mtu eti kisa ni dini yako. Kwenye serikali hatuangalii dini tunaangalia mtu safi asifiwe na mchafu akemewe.

Wakristo kwa waislam. Kemeeni uovu mkiuona hata kama mtu ni wa dini yako, na msifieni mtu pale anapostahili sio kutumiwa na wanasiasa kuleta pumba huku familia zenu zikibaki masikini.

Heshima kwako mkuu. It's encouraging to have objective thinkers in our society.
 
katika hali ya kushitua na kushangaza,kesho wakati UDSM wakiwa wameamua kuwa na kongamano kubwa la kujadili uwepo wa katiba mpya,lipo kundi la watu ambao wanadai kuwa ni waislamu na wao wameamua kuitisha kongamano lao kesho ktk ukumbi wa karimjee na wanategemea kutoa matamko mbalimbali lengo ni kuhakikisha kuwa media itaondoa attention kwenye katiba. pia watatoa matamko controversial sana juu ya utawala kuwa JK na serikali yake inahujumiwa na wakristo. pindi tamko likikamilika litawekwa hapa jamvini kwani ndio draft ya kwanza imekuwa tayari. ukumbi wa karimjee umelipiwa na mnene mmoja serikalini. leo mahubiri kwenye misikiti kadhaa DSM yamekuwa yakionyesha kuwa kila mara anapokuwa rais muislam basi anawekewa vikwazo na hata kudhalilishwa na wametoa mifano mingi ya Mwinyi na sasa JK.More 2 come later

Huo ni mkono wa JK, maana wote tunajua kuwa karata ya udini ndio mtaji wake maana ndg zetu hawa wanapenda sana kuegemea ktk masuala ya dini kama uwanja wao wa kujengea hamasa.
 
Waislamu wapendwa, ikumbukwe kuwa Kikwete huyo huyo mwaka 2005, alishinda kwa zaidi ya asilimia 80%. Wakati ule alipigiwa kura na watu wa dini zote. Leo anapo pigwa madongo, anapigwa na watu wa dini zote. Anapigwa madongo kwa sababu ya kuvurunda kwake, na si kwa sababu ya uislamu wake.

Anaporususu askari wake kupiga risasi, anawaamrisha wapige risasi (nyingi tu) kwenye kundi walipo watu wa dini zote. Risasi imemwua Mkristo na nyingine ikamwua Muislamu. Risasi nyingine zimejeruhi viungo vya watu wa dini zote na jinsia zote.

Mwaka 2005, alisema kuwa atahakikisha kuwa katika uongozi wake ataboresha miundo mbinu ya umeme ili nishati hii ipatikane kwa unafuu kwa wananchi walio wengi hususan wa vijijini. Leo, anaanza tu awamu ya pili, anakula matapishi yake mwenyewe kwa kubariki ongezeko la mgao wa umeme (ambao hata upatikanaji wake ni kwa kimtandao) la asilimia zaidi ya 18. Watu wakimshukia, utaambiwa kuwa, wanafanya hivyo kwa kuwa Rais ni Muislamu. Aaaaaaah jamani!!!

Udini haupo Tanzania, kilichopo ni kikundi cha watu wachache, waliopungukiwa sera kichwani, ambao wamejificha chini ya mwamvuli wa UDINI ambao pindi wananchi wakiwa kwenye mikakati ya kujadili mambo muhimu ya nchi yao; wao huibua masuala ya UDINI. Na kwa bahati mbaya, hutumia baadhi ya viongozi wa Kiislamu.

Tuwapotezee watu hawa, hawatufai hata kidogo. Wasituondoe katika mstari wetu wa kudai mabadiliko Aluta continua!!!
 
Naomba waislamu msinielewe vibaya kwa maneno nitakayoandika hapa kwani ndivyo ninavyoamini mimi binafsi.
1. Binafsi naamini Waislamu kama watanzania wengine wana uchungu na uzalendo na nchi yao
2. Naamini waislamu kwa misingi na maamrisho ya dini yao, hawana nia ya kuvuruga amani wala kubagua watanzania wenzao kwa misingi ya dini
3. Naamini waisalmu wanapata haki kwa mgao sawa na wanavyopata wananchi wa dini zingine

Tatizo ninaloliona ndugu zangu ni kuwa kwa siku za karibuni (baada ya mchakato wa uchaguzi kuanza), waislamu wameanza kuchafuliwa kwa maksudi na watu wenye malengo ya kisiasa, kwa maslahi binafsi ya watu hao. Kwa bahati mbaya nahisi kuna udhaifu fulani katika system ya uislamu, inayosababisha wawe vulnerable na kurubuniwa kirahisi
1. Nahisi kuna ukosefu wa hirachy katika uongozi wa dini ya kiislamu. hapa namaanisha kuwa ni rahisi sana akajitokeza anayejiita shehe, Bakwata, au sijui nani akasema au kutenda kitu fulani kwa 'niaba' ya waislamu leo, na kesho akatokea mwangine, akawa kinyume nae, pia kwa niaba ya waislamu. Unaweza kuona mfano wa maandamano na mauji ya Arusha
2. Nina wasiwasi na nia ya BAADHI ya viongozi wa dini ya waislamu kuwa za kibinafsi zaidi
3. Nina wasiwasi na uaminifu wa BAADHI ya viongozi wa waislamu, kuwa na dalili ya kurubuniwa kirahisi na wanasiasa
4. Nina wasiwasi na elimu ya BAADHI ya viongozi wa waislamu, kwani pamoja na busara na uwezo wa asili juu ya masuala ya uongozi, lakini hatuwezi ku-underestimate umuhimu wa elimu katika uongozi

Kutokana na hayo, naona sasa kwa kuona kuwa wamezidiwa kila idara, CCM (au kikundi fulani ndani ya CCM), kimefanikiwa kuwarubuni baadhi ya viongozi wadhaifu wa waislamu, katika matukio tofauti, lakini katika mpango endelevu, na kuutumia uislamu kama ngao yao dhidi ya harakati za wanachi za kujikomboa kutoka katika udhalimu wa CCM

Nawaasa waislamu wote wenye nia njema kupinga na kulaani mpango huu wa kishetani wa CCM, wa kuwatumia kama ngao. Mtu yeyote ajue kuwa katika nchi ambayo hakuna dini yenye majority katika population representation, then hakuna chance kuwa move za udini na kidini zitakazowesha kundi lolote kupata maslahi yake, kinyume na matakwa ya walio wengi.

Waislamu wakumbuke kwamba, hata kama raisi atawapendelea katika nafasi za uteuzi, au mambo fulani madogo, hiyo naina maana ikilinganishwa na wanyanyaso wanayopata kama wananchi wengine katika nynja za kuichumi, afya, elimu n.k

Waislamu wakumbuke kuwa, kama wataamua kuisapoti serikali kwa kila kitu, eti kwa sababu raisi ni muislamu, ipo siku raisi huyom ataondoka madarakani, afafu wataona aibu kupinga mambo ambayo, ama leo wanayatetea, au yameanzishwa na raisi wa sasa.

Waislamu wakumbuke kuwa hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu anayempinga Kikwete kwa eti ni muislamu, bali anapingwa kwa kuwa ni dhaifu kiuongozi na kiutawala.

CCM wakumbuke kuwa wanapandikiza mbegu ambayo muda sio mrefu itawaangamiza hata wao

Hali kadhalika CCM wajue pia kuwa hata kama wana taarifa zozote zi 'kiintelijensia' kuwa pengine wapo wakristo wanaompinga JK kwa udini au wenye hila za maslahi ya kidini, njia muafaka ya kukabiliana nao sio kuzidi kupandikiza udini, bali ni kuukemea

Naamini wanaokuza udini ndani ya CCM ni wale wanaohitaji maslahi ya muda mfupi bila kujali mustakabali wa ama CCM au Tanzania katika siku zijazo.

Wanaowatumia rafiki zangu waislam ni wale wasio WaTanzania halisi. Hawana uchungu na nchi. Majambazi wakubwa.....nk. Wanajua hata mkipigana, hola, wao wanasepa zao huko na kutuacha tunauana kipumbavu. Shame on them. Waislaam makini hawawezi kukubali kutumiwa. Pumbavu sana wanaowatumia wapendwa wangu aislaam. Mwizi ni mwizi, ni mwizi awe budha, mpagani, mkristu, mwislaam au hana dini. Hali kadhalika, mwadilifu anaweza toka dini yeyote ile, tena anaweza kuwa shekhe, padre, au hana dini kabisa......

WAKE UP BELOVED MOSELEMS, DO NOT BE USED BY HULIGANS.....
 
Naona mengi yameshasemwa na ni yale yale kwa humu' Uislamu ni udini". Naomba kuuliza yafuatayo:
1. Jee kongamano hili ili lipiku lile la Katiba limetangazwa kiasi gani kama lilivyokwishatangazwa hilo la mlimani?
2. Hivyo kwa hilo kongamano la Mlimani shughuli zote zitazuiliwa hata hawa Waislamu wasifanye shughuli yao?
Hivyo waislamu kama sehemu ya jamii hawana haki ya kufanya kongamaqno lao?
3. Hivyo kwenye uchaguzi uliopita watu wote walikuwa wapinzani wa Serikali ya Kikwete?
4. Hivyo katika hili kongamano la Waislamu maazimio watakayotowa yatakuwa maaazimio ya Waislamu wote na kongamano la mlimani litatowa msimamo wa kila mtu humu Tanzania? Ikiwa hivyo nahisi hatuna haja ya vyama kwani misimamo yetu si iko sawa?
5. Kwanini lazima Waislamu wapangiwe wakati fulani wafanye wanavyotaka?
6. Na kwanini Udini ni pale viongozi wa Kiislamu wanapotowa hoja zao wakati kila wakati viongozi wa Kikristo wanatowa matangazo kwa utashi wao? Wanawasiliana na wenzao wa Kiislamu kabla ya kutowamatamshi kama wadau kama tunavyotaka Waislamu wafanye?
Nafikiri hili la udini ni la Wakiristo kwani wao ndio wako sensitive na Waislamu wao huwa wanadai haki zao ambazo yeyote anaenyimwa ana haki ya kufanya hivyo. JF wacheni ukiristo (kwenu udini ni uislamu)
 
Wanaowatumia rafiki zangu waislam ni wale wasio WaTanzania halisi. Hawana uchungu na nchi. Majambazi wakubwa.....nk. Wanajua hata mkipigana, hola, wao wanasepa zao huko na kutuacha tunauana kipumbavu. Shame on them. Waislaam makini hawawezi kukubali kutumiwa. Pumbavu sana wanaowatumia wapendwa wangu aislaam. Mwizi ni mwizi, ni mwizi awe budha, mpagani, mkristu, mwislaam au hana dini. Hali kadhalika, mwadilifu anaweza toka dini yeyote ile, tena anaweza kuwa shekhe, padre, au hana dini kabisa......

WAKE UP BELOVED MOSELEMS, DO NOT BE USED BY HULIGANS.....
Hivyo unaweza ukaniambia eti nani ana uchungu wa nchi kati ya Wanasiasa wa pande zote mbili (CCM na upinzani)? Hebu nieleze panapo masilahi yao umesikia wakipingana? Mamilioni ya shilingi wanalipana na huku sisi tukilala hoi. Eti uchungu wa nchi yakguju Si chochote bali ni mapambano ya masilahi basi. Wakiristo na Waislamu wa kawaida ni watoto wa bandia tu!!
 
Ndiyo tatizo la wadogo zetu. Watakuwa wameambiwa kuwa kongamano litaambatana na kahawa, kashata, pilau, n.k maana hicho ndicho wanachokiabudu na kukitumikia siku zote.
 
Back
Top Bottom