Kodi ya simu yapingwa rasmi mahakamani

Kodi ya simu yapingwa rasmi mahakamani

MATATIZO SABA

Member
Joined
Sep 28, 2011
Posts
8
Reaction score
4
Wadau nimepokea taarifa Kuwa Umoja wa Chama cha Kampuni za simu (MOAT) sio kile cha baba Mengi. . .

Leo wanaenda mahakama ya Kodi kuweka pingamizi kwa kila Mtanzania kukatwa shilingi 1000 kuanzia Mwezi Julai. Sasa niko njiani kwenda kuwaunga Mkono hawa jamaa...... Mimi nina Laini tatu inamaana nadaiwa elfu 9.

Mungu anisaidie. Watanzania tunaumizwa si mchezo.
ZIKIWA zimebakia siku mbili kabla ya serikali kuanza kuwatoza kodi ya laini (sim card) watumiaji wa simu, Taasisi ya Watumiaji wa Bidhaa na Huduma imefungua kesi Mahakama Kuu kupinga sheria hiyo.

Taasisi hiyo ya Consumers of Goods and Services Across the Country ilifungua kesi hiyo juzi Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam chini ya hati ya dharura na kuanza kusikilizwa jana mbele ya jopo la majaji watatu.


Majaji waliosikiliza kesi hiyo ni Lawrence Kaduri, Aloysius Mujuluzi na Salvatory Bongole.

Katika kesi hiyo walalamikaji wanaiomba mahakama itangaze kwamba sheria iliyopitishwa na Bunge inayotaka kila mtumiaji wa simu ya mkononi kukatwa sh 1,000 kila mwezi ni kandamizi.


Walidai kwamba watumiaji wengi wa simu za mkononi hawana uwezo wa kukatwa fedha hiyo kwa mwezi, huku wakisisitiza kuwa itawaathiri watumiaji wa huduma hiyo.


Kwa mujibu wa madai ya walalamikaji hao, sheria hiyo inakiuka matakwa ya katiba ya nchi ya uhuru wa kupashana habari na kuiomba mahakama kuifuta sheria hiyo waliyoiita kuwa kandamizi.


Mawakili wa walalamikaji kutoka Kampuni ya uwakili ya Rex, Lugano Mwandamo na Merkizedeki Lutema walidai kuwa wateja wao wanataka mahakama imzuie Waziri wa Fedha kupitia Mamlaka ya Mapato (TRA) kutoza kodi hiyo hadi hapo maombi yao yatakapotolewa uamuzi.


"Kuanzia sasa hivi mahakama itoe amri ya muda kuzuia utekelezaji wa sheria hiyo usitendeke," alidai Mwandamo.

Kutokana na maombi hayo, jopo la majaji liliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 3 mwaka huu, likimtaka wakili wa serikali, Kelley Mwitasi kuwasilisha maelezo yake kwa njia ya maandishi.

Wakati huo huo, majaji hao waliutaka upande wa walalamikaji kujibu maelezo ya upande wa serikali kwa njia ya maandishi na kuyawasilisha mahakamani hapo kabla ya Oktoba 7, ambapo kesi hiyo itaanza kusikilizwa saa saba mchana siku hiyo.


Kufunguliwa kwa kesi hiyo kutasitisha utekelezaji wa utozaji wa kodi hiyo unaotakiwa kuanza Septemba 30 mwaka huu, baada ya TRA kuziandikia kampuni za simu waraka wa kuzitaka zianze utekelezaji wa sheria hiyo.


Sheria hiyo iliyopingwa na wanasiasa wengi bila kujali itikadi za vyama vyao, ilipitishwa kwa nguvu ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa Bunge la Bajeti na kutaka utekelezaji wake uanze Julai 30.

Bunge kupitia Kamati ya Bajeti inayoongozwa na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM) lilitaka kuwapo kwa kodi hiyo ili kusaidia shughuli za bajeti ya serikali kuu.

Kupitishwa kwa kodi hiyo kuliibua malalamiko ya wanasiasa hata wa CCM dhidi ya Chenge anayelazimisha kuwapo kwa kodi hiyo, huku akishindwa kuamini kwamba kuna Mtanzania anayekosa sh 1,000 kwa mwezi kwa ajili ya laini ya simu.


Malalamiko hayo, yalimlazimu Rais Jakaya Kikwete kukutana na wadau wa mawasiliano ambao ni wamiliki wa kampuni za simu Tanzania (MOAT), Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba na Waziri wa Fedha, William Mgimwa, kisha kuwaagiza waiondoe kodi hiyo.

"Nakuombeni kaeni pamoja, wekeni bongo zenu pamoja, wekeni akili yenu pamoja tutafute namna gani tutajaza pengo hili la sh bilioni 178 endapo tutakubaliana kuwa kodi hii inawabebesha wananchi mzigo mzito na kuwa pengine menejimenti ya kodi yenyewe ni ngumu," alisema rais kwenye kikao hicho.

Licha ya agizo la rais kutekelezwa kwa MOAT kutakiwa kuongeza kodi nyingine iitwayo ‘Excise duty' kutoka asilimia 14 hadi 17 bila kujali kwamba katika Bunge la bajeti kodi hiyo iliongezwa kutoka asilimia 12 hadi asilimia 14, kodi ya laini za simu haijaondolewa.

Wachambuzi wa masuala ya siasa na mawasiliano walisema kutojadiliwa kwa mabadiliko ya kodi hiyo ya simu ni dalili kwamba Waziri wa Fedha amezidiwa nguvu na kiti cha spika kinachounga mkono hoja hiyo ya Chenge na kushindwa kutekeleza agizo la rais.


Takwimu zilizotolewa na kampuni za simu zinaonyesha kuwa miongoni mwa wamiliki wa laini za simu milioni 22; milioni nane wanatumia chini ya sh 1,000 kwa mwezi.


Tanzania Daima
 
Hii kodi ya shilingi elfu 12 kwa mwaka ni kubwa sana kwa mtanzania. Naunga mkono juhudi hizo kwa kuwa mchakato wa kuanzisha hiyo kodi haukushirikisha wadau, imeletwa kibabe, pia kodi hiyo itawahusu hata watoto wadogo wa umri chini ya miaka 18, wazee na wagonjwa. Kodi ya simu haikubaliki. Usaliti wa January Makamba huu.
 
Una line tatu zote hizo za nni?

wadau nimepokea taarifa kuwa umoja wa chama cha kampuni za simu (moat) sio kile cha baba mengi. . . Leo wanaenda mahakama ya kodi kuweka pingamizi kwa kila mtanzania kukatwa shilingi 1000 kuanzia mwezi julai. Sasa niko njiani kwenda kuwaunga mkono hawa jamaa...... Mimi nina laini tatu inamaana nadaiwa elfu 9. Mungu anisaidie. Watanzania tunaumizwa si mchezo.
 
Hii kodi ya shilingi elfu 12 kwa mwaka ni kubwa sana kwa mtanzania. Naunga mkono juhudi hizo kwa kuwa mchakato wa kuanzisha hiyo kodi haukushirikisha wadau, imeletwa kibabe, pia kodi hiyo itawahusu hata watoto wadogo wa umri chini ya miaka 18, wazee na wagonjwa. Kodi ya simu haikubaliki. Usaliti wa January Makamba huu.

Kodi siyo kubwa ila "DIRECT TAX" is always painful. Mbona kuna "INDIRECT TAX" - excise ya 14% hiyo hatulalamiki?
 
Hii kodi ya shilingi elfu 12 kwa mwaka ni kubwa sana kwa mtanzania. Naunga mkono juhudi hizo kwa kuwa mchakato wa kuanzisha hiyo kodi haukushirikisha wadau, imeletwa kibabe, pia kodi hiyo itawahusu hata watoto wadogo wa umri chini ya miaka 18, wazee na wagonjwa. Kodi ya simu haikubaliki. Usaliti wa January Makamba huu.

Huyo Makaamba hamna kitu mbona!!
 
Una line tatu zote hizo za nni?
usiwe KILAZA jaribu kujifikirisha,sio kila kitu utafuniwe.Haya meza basi ngoja nikutafunie.
Mimi kwa sasa nipo Dar kwa bussines zangu na bussines partiners wengi wanatumia sim card za tigo,hivyo kuepusha gharama za kupiga kati ya voda(line yangu )na tigo{partiners} itanibidi niachane na voda kwa muda ili hamie tigo,licha ya hayo Nimeiacha familia yangu mtwe mafi,kigoma mwisho tena kijijini kabisa,kule nertwork inayo patikana ni airtel pekee na wao(my family)kwa kigezo kilekile cha kuepusha gharama itabidi wanipigie kuptia line yangu niliyo tokanayo huko shamba(airtel).
Sasa hapo tayari ninakuwa na line ngapi?
Iwapo kampuni za mitandao yoote Tanzania zingekuwa na gharama moja ya kupiga kwenda mtandao wowte hapa Tz,naamini tusingekuwa tunabeba line 3'3
Umenisoma wee KILAZA.
 
Nawashangaa Watanzania mnabeba simu tatu halafu mnakataa kulipia kodi.

Hii kodi iwepo na nnaikubali kwa roho kunjufu kabisa.

Na hizo kampuni za simu zitashindwa hii kesi na kila zitakavyochelewesha kuanza kukata hii kodi ndivyo tutalimbikiza kodi na tutaumia sisi zaidi na wao watajichotea humohumo. Ni wajanja tu hao.

Serikali iwaambie kama wanahuruma sana na wananchi wapunguze bei zao kufidia hii kodi.

Na Mitanzania ijinsi tulivyo mingine itaingia kichwachwa na kuwaunga mkono hizi kampuni ambazo hazitazami maslahi ya Mtanzania zaidi ya bishara yao tu.
 
Nawashangaa Watanzania mnabeba simu tatu halafu mnakataa kulipia kodi.

Hii kodi iwepo na nnaikubali kwa roho kunjufu kabisa.

Na hizo kampuni za simu zitashindwa hii kesi na kila zinatakavyochelewesha kuanza kukata hii kodi ndivyo tutalimbikiza kodi na tutaumia sisi zaidi na wao watajichotea humohumo. Ni wajanja tu hao.

Serikali iwaambie kama wanahuruma sana na wananchi wapunguze bei zao kufidia hii kodi.

Na Mitanzania ijinsi tulivyo mingine itaingia kichwachwa na kuwaunga mkono hizi kampuni ambazo hazitazami maslahi ya Mtanzania zaidi ya bishara yao tu.

hizo kodi wanazotoa watanzania. je zinaendana na kipato chao? hivi unajua watanzania wanaishi chini ya dolla 1 kwa siku? nenda uko vijijin uone hali ilivyo ngumu. kupata elfu tu ni kazi kubwa.

pia usiangalie wachache angalia watanzania walio wengi.
hivi unajua serikali ina misamaha mingi ya kodi kwa matajiri na sekta kama madini.

kwenye madini serikali ya botswana inapata zaidi ya asilimia 40 ya kodi pia kuna sheria za kuwalazimisha wajenge miundo mbinu sehemu wanakochimba.

uku Tanzania serikali inachukua asilimia 3.
ujinga sana huuu
 
Nawashangaa Watanzania mnabeba simu tatu halafu mnakataa kulipia kodi.

Hii kodi iwepo na nnaikubali kwa roho kunjufu kabisa.

Na hizo kampuni za simu zitashindwa hii kesi na kila zitakavyochelewesha kuanza kukata hii kodi ndivyo tutalimbikiza kodi na tutaumia sisi zaidi na wao watajichotea humohumo. Ni wajanja tu hao.

Serikali iwaambie kama wanahuruma sana na wananchi wapunguze bei zao kufidia hii kodi.

Na Mitanzania ijinsi tulivyo mingine itaingia kichwachwa na kuwaunga mkono hizi kampuni ambazo hazitazami maslahi ya Mtanzania zaidi ya bishara yao tu.

Lakini FaizaFoxy mtu wa mwisho anayeumia ni mtanzania,siamini kama serikali haina uwezo wa kuwabana
hao wawekezaji wa simu wakapunguza gharama,lakini badala ya kusaidia na serikali nayo inamuongezea mzigo
mtanzania hapohapo kwenye gharama kubwa za wawekeji hao kwa kumdai mwananchi kodi,wakati kiukweli
ukifuatilia hata hao wenye makampuni ya simu hawalipi kodi kama inavyotakiwa kulipwa kwa kisingizio cha uwekezaji
,hapa wa kulaumiwa ni serikali yetu na viongozi wake wanafiki'
 
nahisi mfumo wa kutuma barua alafu unatumbukiza kwenye basi unataka kurudi taratibu
 
Nawashangaa Watanzania mnabeba simu tatu halafu mnakataa kulipia kodi.

Hii kodi iwepo na nnaikubali kwa roho kunjufu kabisa.

Na hizo kampuni za simu zitashindwa hii kesi na kila zitakavyochelewesha kuanza kukata hii kodi ndivyo tutalimbikiza kodi na tutaumia sisi zaidi na wao watajichotea humohumo. Ni wajanja tu hao.

Serikali iwaambie kama wanahuruma sana na wananchi wapunguze bei zao kufidia hii kodi.

Na Mitanzania ijinsi tulivyo mingine itaingia kichwachwa na kuwaunga mkono hizi kampuni ambazo hazitazami maslahi ya Mtanzania zaidi ya bishara yao tu.
serikali ina huruma kw wananchi wake?... kila mtu hapa ni mwizi tu! tayari kodi ya simu inakuwa imeisha katwa sasa hii tene kulipia line inatoka wapi, mbaya zaidi unakuta hii pesa tunayo lipa ndiyo inatumika wakati wa uchaguzi ili kuchakachua matokeo. hivyo tunakuwa tume kaangwa kwa mafuta yetu, huu ni utmbo mtupu!
 
Wadau nimepokea taarifa Kuwa Umoja wa Chama cha Kampuni za simu (MOAT) sio kile cha baba Mengi. . . Leo wanaenda mahakama ya Kodi kuweka pingamizi kwa kila Mtanzania kukatwa shilingi 1000 kuanzia Mwezi Julai. Sasa niko njiani kwenda kuwaunga Mkono hawa jamaa...... Mimi nina Laini tatu inamaana nadaiwa elfu 9. Mungu anisaidie. Watanzania tunaumizwa si mchezo.

MAHAKAMA YA KODI??!! iko wapi hiyo mkuu?
 
Nakuunga mkono, mguu, kichwa na kila kitu Money Stunna, siku zote mi hujiuliza hivi kwanin watawala wa nchi hii hawatak kuiga yaliyo mazur kw wenzetu, mf kwenye sector ya madin kwani hao investors tukiwawekea kodi yenye manufaa kwetu itakuw dhambi?
 
Last edited by a moderator:
waongeze ifke buku hata 5 kwa mwezi.baadhi ya watanzania mambulula yanayoendelea kung'ang'ania ccm yapate kujifunza manafk wakubwa.
 
Back
Top Bottom