Kodi ya simu yapingwa rasmi mahakamani

Kodi ya simu yapingwa rasmi mahakamani

Wadau nimepokea taarifa Kuwa Umoja wa Chama cha Kampuni za simu (MOAT) sio kile cha baba Mengi. . . Leo wanaenda mahakama ya Kodi kuweka pingamizi kwa kila Mtanzania kukatwa shilingi 1000 kuanzia Mwezi Julai. Sasa niko njiani kwenda kuwaunga Mkono hawa jamaa...... Mimi nina Laini tatu inamaana nadaiwa elfu 9. Mungu anisaidie. Watanzania tunaumizwa si mchezo.



Misaada mnasema hamuitaki mnamtukana Rais eti ombaomba, kulipa kodi hamtaki, huduma za bule mnataka saaaaaaaaaaana!! hivi serikali mnataka ipate wapi kodi?

Naunga mkono hiyo kodi ianze mara moja ili wenzetu wa vijijini nao wapate umeme maana hii pesa yote inaenda REA kusambaza umeme vijijini.

Nyie wa mjini umeme mnaopata toka mtela, kidatu na kwingineko mjue kuna walipa kodi wenzetu walilipa kodi tukapata huu msaada na sisi tulipe vijijini wapate umeme.
Acheni mawazo ya kisiasa.
 
Siungi mkono kampuni za simu kuweka pingamizi,wao ni wakusanyaji tu wa hii kodi iweje leo wawahurumie wateja wa simu waliozoea kukuibia!!
Great Thinkers nataka mjue siri iliyojificha hapo,kampuni za simu zimekuwa wakwepaji wakubwa wa kodi na sasa imefika mwisho wao,serikali itakuweka system mpya ya kupata kodi na hivyo kampuni hizi hazitaweza kuweka kodi kama waliozoea.
Tusikubali kudanganyika,tulipe hiyo kodi na tuibane serikali katika matumizi yake.

Hapo kwenye red mkuu njia za kuibana ndo kaz.
 
Hii kodi ya shilingi elfu 12 kwa mwaka ni kubwa sana kwa mtanzania. Naunga mkono juhudi hizo kwa kuwa mchakato wa kuanzisha hiyo kodi haukushirikisha wadau, imeletwa kibabe, pia kodi hiyo itawahusu hata watoto wadogo wa umri chini ya miaka 18, wazee na wagonjwa. Kodi ya simu haikubaliki. Usaliti wa January Makamba huu.

ni ccm yote kwa ujumla kwani ndo wanaotumia wingi wao bungeni kuwaletea waTZ majanga
 
tatizo si kodi tatizo ni matumizi mabovu ya serikali..... hizo zitatumika kugharamia safari za hawara zao tu ni vyema kupinga hiyo kodi.

Kweli mkuu kwani kama zingekuwa na faida kwetu sidhani kama kungekuwa na matatizo kamwe
 
wanaenda kwa nia njema?? Ni kwasababu wanawapenda ama kuwahurumia watanzania?? Gharama za tozo za simu wameziangalia kwanza?? Na hii serikali ndio maana watu wanasema kiongozi wake ni dhaifu...Mengi/manji/lowasa akatwe 1000 sawa na juma wa kwamtogole ama mzee manywele wa sitimbi?

Yaani hii siri kali yetu imezoea kumuibia mtz wa kipato cha chin zaidi haiwezekani kodi atoayo m .Mengi/manji/lowasengi/manji/lowasa waweze kutozwa sawa na mtu anayeweka 500 kwa mwezi wa huko NAMANYERE.
 
Kweli mkuu kwani kama zingekuwa na faida kwetu sidhani kama kungekuwa na matatizo kamwe

Hata maandamano mnafanya kwenye barabara za lami siku hizi, halafu mnasema hazina faida?
 
Hata maandamano mnafanya kwenye barabara za lami siku hizi, halafu mnasema hazina faida?

Ni kweli faida zipo..Maana hata mkuu safari zimeongezeka na magari ya kifahari..Tulipe KODI...
 
Ni kweli faida zipo..Maana hata mkuu safari zimeongezeka na magari ya kifahari..Tulipe KODI...

Ushasema "Mkuu" na yule katibu wa magwanda anaendesha siasa zake za porojo JF ushaona siku hizi anakwenda kula bata na mke wa mtu kwa fedha za ruzuku? sasa kama hamtaki kulipa kodi mchumba atasusa.
 
Wadau nimepokea taarifa Kuwa Umoja wa Chama cha Kampuni za simu (MOAT) sio kile cha baba Mengi. . . Leo wanaenda mahakama ya Kodi kuweka pingamizi kwa kila Mtanzania kukatwa shilingi 1000 kuanzia Mwezi Julai. Sasa niko njiani kwenda kuwaunga Mkono hawa jamaa...... Mimi nina Laini tatu inamaana nadaiwa elfu 9. Mungu anisaidie. Watanzania tunaumizwa si mchezo.

kwa uelewa wangu mdogo haya makampuni ya simu si kweli kwamba yana onea huruma watumiaji, bali wanaogopa kupoteza customers kwa sababu nature ya telecom biz hapa bongo ina husisha mteja mmoja kumiliki lain zaidi ya moja. so unavoona tcra wamedisplay labda voda ina subcribers 6m we jua kua kati ya hao 6m kuna wengine pia wamehesabiwa kwa tigo vile vile na airtel. so kodi ikipita obvious mtu atapunguza idadi ya line anazomiliki kitu ambacho kitavuruga faida yao.
 
MAKAMPUNI Ya simu wanahuruma sana. Inashangaza ilitakiwa watumiaji ndio washitaki sio makampuni ya simu. Jambo la muhimu ni serikali kukusana kpodi VAT and Corporate Tax ipasavyo kwenye haya makampuni sio kuwabebesha mzigo wananchi. Tunapenda kuona kodi kutoka huko inaongezeka anagalau tuwafikie hata RWANDA tu.
 
To me iyo 12000 kwa kila line sio issue shida inakuja kwenye nidhamu ya matumizi ya iyo ela ndo apo ata moyo wa kuchangia unakufa kabisa.
Alafu ninyi mnaoshangaa mtu kuwa na line 3 ivi kweli mko Tanzania au mwaishi nje kuna mahala Tanzania unakuta kuna mtandao mmoja tuu mingine haipatikani au siku nzima mtandao fulani haupatikani unless kama uko na back up au second line ndo unaweza communicate na wadau!Huwezi ukarely on one line Tz ipo siku itakuja kula kwako unless kama wewe ni mtu wa kuishi DSM hutembei mikoani ambako network huwa issue
 
Nawashangaa Watanzania mnabeba simu tatu halafu mnakataa kulipia kodi.

Hii kodi iwepo na nnaikubali kwa roho kunjufu kabisa.

Na hizo kampuni za simu zitashindwa hii kesi na kila zitakavyochelewesha kuanza kukata hii kodi ndivyo tutalimbikiza kodi na tutaumia sisi zaidi na wao watajichotea humohumo. Ni wajanja tu hao.

Serikali iwaambie kama wanahuruma sana na wananchi wapunguze bei zao kufidia hii kodi.

Na Mitanzania ijinsi tulivyo mingine itaingia kichwachwa na kuwaunga mkono hizi kampuni ambazo hazitazami maslahi ya Mtanzania zaidi ya bishara yao tu.
Naunga mkono baadhi ya sehemu za comments zako ... tangu lini haya makampuni yakatuonea huruma? kila siku wanaibua promotion ambazo zimejaa wizi ... wanatuhadaa eti kifurushi sms 300 ili hali hata kumi kwa siku hutumi na wanalijua hilo fika ... kati ya makampuni ambayo ni wezi na wanyonyaji wakuu wa mtz ni haya ya simu ... alipoteuliwa January nkajua tumepona kumbe laa ...
 
Yaani hata kama ni kilaza, umejitahid sana kueleza.Watu wengine huwa wanapost hapa jf just for the sake of posting. Suala la kuwa na line zaidi ya moja ni la kawaida sana kwa sasa. Kuuliza laini tatu ni za nini ni kuonesha ujinga wake tu. Ni bora ukae kimya kuliko kuongea ukajitangaza kuwa wewe ni zuzu. Bravo mkuu kwa kuelimisha
 
nahisi mfumo wa kutuma barua alafu unatumbukiza kwenye basi unataka kurudi taratibu
tulipokubari utandawazi hatukujua kama ipo siku moja tutaikumbuka posta na simu
 
  • Thanks
Reactions: awp
Kweli mkuu kwani kama zingekuwa na faida kwetu sidhani kama kungekuwa na matatizo kamwe

mpaka mfanya biashara anakimbilia mahakamani kupinga ilhali si yeye anakatwa bali mteja ujue kuna jambo nyuma ya pazia
 
usiwe KILAZA jaribu kujifikirisha,sio kila kitu utafuniwe.Haya meza basi ngoja nikutafunie.
Mimi kwa sasa nipo Dar kwa bussines zangu na bussines partiners wengi wanatumia sim card za tigo,hivyo kuepusha gharama za kupiga kati ya voda(line yangu )na tigo{partiners} itanibidi niachane na voda kwa muda ili hamie tigo,licha ya hayo Nimeiacha familia yangu mtwe mafi,kigoma mwisho tena kijijini kabisa,kule nertwork inayo patikana ni airtel pekee na wao(my family)kwa kigezo kilekile cha kuepusha gharama itabidi wanipigie kuptia line yangu niliyo tokanayo huko shamba(airtel).
Sasa hapo tayari ninakuwa na line ngapi?
Iwapo kampuni za mitandao yoote Tanzania zingekuwa na gharama moja ya kupiga kwenda mtandao wowte hapa Tz,naamini tusingekuwa tunabeba line 3'3
Umenisoma wee KILAZA.
Mwambie huyo anayeishi zama za mawe kuwa pia una modem ya Vodacom,unatumia kwenye laptop yako huko uliko amabapo siku hizi ofisi sio lazima iwe kwenye jengo maalumu bali hata nyumbani na ukafanya kazi zote huku ukisubiri chakula cha nyumbani anachopika mamsap ukiwa home na kazi ikaendelea kufanyika .tena kazi zenyewe zikiwa mbali hata zikiwa kwa Obama
 
Nawashangaa Watanzania mnabeba simu tatu halafu mnakataa kulipia kodi.

Hii kodi iwepo na nnaikubali kwa roho kunjufu kabisa.

Na hizo kampuni za simu zitashindwa hii kesi na kila zitakavyochelewesha kuanza kukata hii kodi ndivyo tutalimbikiza kodi na tutaumia sisi zaidi na wao watajichotea humohumo. Ni wajanja tu hao.

Serikali iwaambie kama wanahuruma sana na wananchi wapunguze bei zao kufidia hii kodi.

Na Mitanzania ijinsi tulivyo mingine itaingia kichwachwa na kuwaunga mkono hizi kampuni ambazo hazitazami maslahi ya Mtanzania zaidi ya bishara yao tu.

Sikutegemea FF kuwa ungekuwa na majibu mepesi namna hiyo,mi nina laini 2 moja natumia kwenye modem ambapo ikiwa kwenye modem hainiwezeshi kupiga wala kupokea simu zaidi ni msg tu ,kwa kuwa siwezi kuitumia kwa kupiga na kupokea simu inabidi niwe na laini nyingine kwa jili ya kupiga na kupokea kwa hiyo kuwa na hitaji la laini ya pili,kumiliki laini zaini ya moja sio UPEDESHEE bali ni hitaji muhimu katika zama hizi za usasa
 
Back
Top Bottom