Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 371,652
- 860,937
Mimi ni SIMBA damu najuikana hivyo.. Na kama mtani wa jadi wa Yanga! Inapopata madhila nafurahi.. Ila kwa hili la kuchangia million mia moja nawatetea hawajafanya hivyo
Vilabu vyetu hivi vya soka vingi vinaongozwa na wafadhili na wadhamini, hawana vyanzo vya uhakika vya kuwaingizia mapato binafsi kama wao
Kilichotokea kwenye ile harambee ni michezo michafu ya kisiasa kupitia makundi yanayosigana kuelekea uchaguzi mkuu ili kuonesha kuungwa mkono kwenye kila kaliba
Kundi maarufu la wanamtandao waliopewa jina la wahuni ndio wamecheza mchezo huo mchafu kupitia kada wa CCM ambaye pia ni rais wa YANGA.
Huyu kwa kujua ama la akatwishwa zigo la kutangaza kiwango tajwa kuwa kimechangwa na Yanga (Young African Sports Club)
Nina hakika hakuna mwana Yanga kupitia viongozi wao aliyeshirikishwa kwenye hili.. Wote walishangaa tu kama wengine
Rai yangu kwa wana Yanga
Msiharibu mali za club, msichome moto jezi zenu kuonesha hasira na kutokubaliana na kilichofanyika.. Klabu yenu ni nzuri sana ikikaa mbali na wanasiasa.. Michezo ni furaha.. Siasa ni fadhaa!
Jipangeni mshikamane mumuwajibishe rais wenu! Huyu ndiye mchawi wenu.. Mumbane kupitia njia sahihi aseme alipata wapi hizo hela na ni nani alimpa mamlaka ya kuihusisha klabu na harambee ya kisiasa
Kwenye hili sisi SIMBA tunaweza kushirikiana nanyi kukomesha tabia hii mbovu ya wanasiasa wachovu kuvitumia vilabu vyetu kwa maslahi binafsi
Sisi SIMBA tunaojitambua tuko na Wana Yanga wote waliokasirishwa na tukio la harambee na tutakuwa nao bega kwa bega mpaka wanasiasa wakae mbali na michezo
Vilabu vyetu hivi vya soka vingi vinaongozwa na wafadhili na wadhamini, hawana vyanzo vya uhakika vya kuwaingizia mapato binafsi kama wao
Kilichotokea kwenye ile harambee ni michezo michafu ya kisiasa kupitia makundi yanayosigana kuelekea uchaguzi mkuu ili kuonesha kuungwa mkono kwenye kila kaliba
Kundi maarufu la wanamtandao waliopewa jina la wahuni ndio wamecheza mchezo huo mchafu kupitia kada wa CCM ambaye pia ni rais wa YANGA.
Huyu kwa kujua ama la akatwishwa zigo la kutangaza kiwango tajwa kuwa kimechangwa na Yanga (Young African Sports Club)
Nina hakika hakuna mwana Yanga kupitia viongozi wao aliyeshirikishwa kwenye hili.. Wote walishangaa tu kama wengine
Rai yangu kwa wana Yanga
Msiharibu mali za club, msichome moto jezi zenu kuonesha hasira na kutokubaliana na kilichofanyika.. Klabu yenu ni nzuri sana ikikaa mbali na wanasiasa.. Michezo ni furaha.. Siasa ni fadhaa!
Jipangeni mshikamane mumuwajibishe rais wenu! Huyu ndiye mchawi wenu.. Mumbane kupitia njia sahihi aseme alipata wapi hizo hela na ni nani alimpa mamlaka ya kuihusisha klabu na harambee ya kisiasa
Kwenye hili sisi SIMBA tunaweza kushirikiana nanyi kukomesha tabia hii mbovu ya wanasiasa wachovu kuvitumia vilabu vyetu kwa maslahi binafsi
Sisi SIMBA tunaojitambua tuko na Wana Yanga wote waliokasirishwa na tukio la harambee na tutakuwa nao bega kwa bega mpaka wanasiasa wakae mbali na michezo