KKKT yatahadharisha kuhusu COVID19

KKKT yatahadharisha kuhusu COVID19

Wasubuti kumfungia Rais wetu uone kama watabaki hata na muumini mmoja, makanisa yao yatabaki magofu .JPM ananguvu sana na amejijengea ufalme ndani ya mioyo ya mamilioni ya watanzania, afrika na dunia kwa ujumla. JPM ametuambia tutegemee Mungu na tumuombe atuepushe corona isiingie katika miili yetu. God bless our President and live long JPM
Kwa hiyo huko makanisani watu wanaenda kumwabudu Magufuli na sio Mungu.!!

Mpumbavu kama wewe ukifiwa na baba yako mzazi na anazikwa siku moja na Magufuli bila shaka utaenda kumzika Magufuli. Huna akili kabisa wewe.
 
Uko sahihi badala ya kutujazia mikelele yao ya nyaraka wafunge tu makanisa yao tumechoka minyaraka kutwa
Kama wanasoma corona ipo wafunge makanisa waache ubabaishaji
Umechoka wewe na Basha wako, ondoa upuuzi wa kudharau viongozi wa dini za wenzio. Sisi tuliokusudiwa kusikia maonyo ya viongozi wetu tumeelewa na tutazingatia, wewe ulimfanya Magufuli kiongozi wako wa kiroho hujazuiwa kumuabudu.
 
Basi miongoni mwa tahadhari na wafunge Kanisa lao ili waumini wao wasiambukizwe na mikusanyiko.
Baba askofu Dr Frederick Shoo amewaambia Wachungaji na viongozi wa Kanisa; Wapeni tahadhari "Watu wa Mungu". Nyie watu wa Magufuli mnaumia nini wakati hamuambiwi nyie bali wanaambiwa watu wa Mungu?
 
Viongozi wa kidini wa ukweli wamefunuliwa na kuanza kuona jinsi ambavyo rais anatumia nafasi yake kinafiki kwa kumuhusisha Mungu na vitu vya kipuuzi.

Yeye anafikiri akili ya mwanadamu kuvumbua hizo chanjo hawajawezeshwa na Mungu au anafikiri walioanzisha tiba ya hospitali walifanya hivyo kwa akili zao wenyewe bila kuwezeshwa na Mungu.

Tatizo kuna watu wana fikra za kijinga kwa kufikiria kwamba mtu akiwa rais basi yeye ndio mwenye akili kushinda wote. Hovyo kabisa.
 
Na wala hawaongozwi na Corona

Mungu hakuwatuma kuhubiri habari za Coronaa bali za Yesu Wamepotoka wanahemuka na Corona badala ya kuhemka na Injili
Wasipofanya hivyo na waumini wao wakafa kwa ugonjwa wa Corona hizo habari za Yesu watamuubilia nani?.
 
Wasipofanya hivyo na waumini wao wakafa kwa ugonjwa wa Corona hizo habari za Yesu watamuubilia nani?.
Injili ina uwezo wa kufanya vyote kuokoa na kuponya ikiwemo kuokoa watu wasipate corona na kuponya Corona wajikite kwenye spiritual solutión ya Corona eneo la physical solutions wawaachie wenyewe wabobezi ni upotofu kuamini kuwa ukijikita kwenye injili watu watakufa!!!! Yesu alikuja ili watu wawe na uzima tele sio vifo tele viwe vya Corona au chochote
 
Kila mtu ana imani yake, Mungu aliyewajusha wana wa Israel wakavuka bahar anashindwaje haka ka covd? Iman yako itakuponya
 
Wasipofanya hivyo na waumini wao wakafa kwa ugonjwa wa Corona hizo habari za Yesu watamuubilia nani?.
Sasa wanafuata hzo sheria za distance kwel? Au ndo kiki tuu nao kuongeza umaarufu maana bongo nyoso😂😂
 
Basi miongoni mwa tahadhari na wafunge Kanisa lao ili waumini wao wasiambukizwe na mikusanyiko.
Mwendawazimu wewe. Umekuwepo JF kwa bahati mbaya. JF ilikusudiwa kuwa mahali pa wenye akili timamu kujadili mambo muhimu.
 
Wasubuti kumfungia Rais wetu uone kama watabaki hata na muumini mmoja, makanisa yao yatabaki magofu .JPM ananguvu sana na amejijengea ufalme ndani ya mioyo ya mamilioni ya watanzania, afrika na dunia kwa ujumla. JPM ametuambia tutegemee Mungu na tumuombe atuepushe corona isiingie katika miili yetu. God bless our President and live long JPM
Huo ufalme ameujenga ndani ya mioyp ya wajinga na waliokosa akili (CCM INAPENDWA NA WATU WAJINGA - TWAWEZA) na siyo ndani ya mioyo ya wenye akili.
 
Injili ina uwezo wa kufanya vyote kuokoa na kuponya ikiwemo kuokoa watu wasipate corona na kuponya Corona wajikite kwenye spiritual solutión ya Corona eneo la physical solutions wawaachie wenyewe wabobezi ni upotofu kuamini kuwa ukijikita kwenye injili watu watakufa!!!! Yesu alikuja ili watu wawe na uzima tele sio vifo tele viwe vya Corona au chochote
Huyajui maandiko.

Mara ngapi Mungu aliwatuma manabii kwenda kuwaonya wafalme kwenye mambo yanayohusu uongozi wao?
 
Sasa mtu anataka waumini wachukue tahadhari ya namna gani? Akiachia watu waende kanisani utakuwa ni unafiki kama unafiki mwingine.

Kuna wale wengine wanasema kujikinga na corona mchana fanyeni kazi ila usiku jiwekeni lockdown. Kana kwamba kirusi kinalala mchana na kuamka usiku.
Makanisa mengi sasa hivi yanachukua tahadhari dhidi ya corona. Ndiyo maana unakuta wameweka viti nje ya majengo kwa sababu ndani ya jengo, viti vimewekwa katika umbali wa tahadhari.
 
Huyajui maandiko.

Mara ngapi Mungu aliwatuma manabii kwenda kuwaonya wafalme kwenye mambo yanayohusu uongozi wao?
Enzi hizo dini ilikuwa moja nchi nzima ya Israel na kiongozi mkuu wa dini alikuwa nabii na ndiye aliyekuwa akiweka mfalme madarakani hawa wa KKKT kwanza sio manabii na hawaamini huduma za manabii

Yohana mbatizaji alimkemea herode ambaye hakuwa muumini wale akakatwa kichwa
 
Nasikitika Sana kwa Nini makanisa haya tangu 2015 lile jukwa la wakristo Tanzani" limepotea ghafla, nakumbuka wakati wa "sakata la nani achinje, mauaji, mchakato wa katiba mpya, mahakama ya kadhi nk yalitoa nyaraka nzito tena kwa umoja wao.

Ilifaa zaidi Kama nyaraka hizi zingetolewa na "Jukwaa la wakristo Tanzania" na si kila kanisa kutoa nyaraka yake, huu ni udhaifu wa umoja wa makanisa.

Tunasubiri nyaraka ya warokole kuhusu Corona, ikikumbukwa kwamba kanisa lao lilitoa tuzo kwa kiongozi wa malaika kwa kuishinda covid'19.
"" TUSIMJARIBU MUNGU"
 
Yetu macho na masikio! Tunaangamia kwa kujifanya wajuaji kwa kila jambo. Uviko-19 ipo tujitahadhali wakuu.
Screenshot_20210130-190027.png
 
Ngoja tusubiri kiongozi mkuu wa dini zote atasemaje kuhusu hizi tahadhari.
 
Mwaka jana Magufuli kalaumiwa sana na kuambiwa kuwa alikuwa anawatowa wananchi wake kafara kwenye corona ila leo tunasema mwaka jana Tz tulifanikiwa kudhibiti corona,lawama kwa Magufuli zimeanza tena kwamba anasema hakuna corona wanasahau kuwa huku kusema hakuna corona ni tokea mwaka jana.
 
Basi miongoni mwa tahadhari na wafunge Kanisa lao ili waumini wao wasiambukizwe na mikusanyiko.
Him barua no Kali sana, mbona Tanzania imeacha kuchukua tahadhali tangu April mwaka Jana na bado watu wa Mungu wako salama! Bado hatuonyeshi appreciation hata kama ugonjwa umerudi ilitakiwa barua iandikwe kwa upole na kwa kumshukuru Mungu kutulinda kipindi cha kwanza na sasa tungeendelea kumuomba Mungu aendelee kuipigania Tanzania huku wana was Mungu wakiendelea kujikinga hii ingependeza sana kuliko ile kusema kumjaribu Mungu.
 
USIMJARIBU BWANA MUNGU WAKO; among the best answers ever!
 
Tunajirusha toka kwenye kinara cha hekalu.makusudi kisa Mungu ameifuta corona Tanzania? Kwamba tuna Mungu kuliko maeneo mengine yote ya dunia? Let's be serious jamani!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom