KKKT yasitisha matamasha yote yanayoambatana na maadhimisho ya Pasaka ili kuepuka maambukizi ya Covid-19

denooJ

JF-Expert Member
Mar 31, 2020
18,511
68,141
Askofu-Shoo.jpg

Askofu Dkt. Frederick Shoo
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dkt. Frederick Shoo, ametangaza kusitisha matamasha yote yanayoambatana na maadhimisho ya Pasaka, lengo likiwa ni kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19.

Alitoa agizo hilo katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Arthur Shoo.

"Hata tunapoelekea katika kipindi cha Pasaka najua huwa kuna mikesha, mikutano ya injili, makongamano mengi. Haya yote nafikiri kwa hali tunayopitia sasa, tusitishe wimbi hili lipite", alisema.

Askofu shoo pia amesema panahitajika elimu sahihi ya kujikinga na ugonjwa huo, akiwataka watanzania kuacha kufanya mzaha, huku akikemea tabia ya baadhi ya watu kushangilia pale viongozi wa kitaifa wanapopata ugonjwa huo.

Pia ametoa angalizo kwa wanaotengeneza na kuuza dawa za asili kutofanya kwa maslahi binafsi tu.

"Mnaotoa dawa za asili, msitumie kama fursa y kutengeneza biashara kwa kuwa tu, watu wanataka kupona na kujikinga"

Amewataka Watanzania kuacha mizaha na kushirikiana na wataalamu wa afya pamoja na kumuomba Mungu.

"Katika janga la Corona hatari sio kwa wale waliokwishafariki bali ni sisi hapa tunaopumua na kukohoa ndio wenye hatari ya kuambukizana. Nawaombeni sana, isiwe aibu wala isionekane ni kosa la imani kuvaa barakoa" alisema

====

EvhxLpNXcAU-9QB.jpg
 
Happ Dar kwa kada mtiifu atasitisha? Maana jamaa simuelewagi toka ile Kashfa ya kula mke wa mtu
SHoo amesitisha kwa Tanzania nzima mkuu yeye kwa sasa ndiye mkuu wa kanisa. means KKKT nchi nzima ndio wamesitisha hivyo.
huyo wa Dar ni sehehmu ya KKKT
 
SHoo amesitisha kwa Tanzania nzima mkuu yeye kwa sasa ndiye mkuu wa kanisa. means KKKT nchi nzima ndio wamesitisha hivyo.
huyo wa Dar ni sehehmu ya KKKT
Kwa mfumo wa KKKT Askofu wa dayosisi husika bado ana sauti. Ndo maana mwaka jana huku Mashariki na Pwani waligoma kusoma barua ya Makao Makuu.
 
Askofu-Shoo.jpg

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dkt. Frederick Shoo, ametangaza kusitisha matamasha yote yanayoambatana na maadhimisho ya Pasaka, lengo likiwa ni kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19.

Alitoa agizo hilo katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Arthur Shoo.

"Hata tunapoelekea katika kipindi cha Pasaka najua huwa kuna mikesha, mikutano ya injili, makongamano mengi. Haya yote nafikiri kwa hali tunayopitia sasa, tusitishe wimbi hili lipite", alisema.

Askofu shoo pia amesema panahitajika elimu sahihi ya kujikinga na ugonjwa huo, akiwataka watanzania kuacha kufanya mzaha, huku akikemea tabia ya baadhi ya watu kushangilia pale viongozi wa kitaifa wanapopata ugonjwa huo.

Pia ametoa angalizo kwa wanaotengeneza na kuuza dawa za asili kutofanya kwa maslahi binafsi tu.

"Mnaotoa dawa za asili, msitumie kama fursa y kutengeneza biashara kwa kuwa tu, watu wanataka kupona na kujikinga"

Amewataka Watanzania wataacha mizaha na kushirikiana na wataalamu wa afya pamoja na kumuomba Mungu.

"Katika janga la Corona hatari sio kwa wale waliokwishafariki bali ni sisi hapa tunaopumua na kukohoa ndio wenye hatari ya kuambukizana. Nawaombeni sana, isiwe aibu wala isionekane ni kosa la imani kuvaa barakoa" alisema
 
Si tumekubaliana Corona aichagui mtu wala dini jamani?

Lakini Tanzania viongozi wengi wa dini moja kubwa wamekufa sana kwa Corona kuliko viongozi wa dini zingine,hivi ni kwanini tena jamani?
 
Hay
Jabali hana pa kutokea..
Acheni sifa za kijinga kama wako serious wafunge makanisa huko ndio hakuna utaratibu wa kukaa distance, wawambie watu wakasari majumbani.

Hayo matamasha yana beba watu wangapi?

Wawazuie watu kwenda kanisani ndi watakuwa wametibu tatizo lakini haya mengine ni uongo tu.

Matamasha watu ni walewale na kanisani watu ni walewale sasa hapo wanamaanisha nini?
 
Misa vipi nazo?
Kama sadaka tupewe namba za wakala,tutazituma,ila tusalie nyumbani.
 
Wanatoa huduma kwa Wagonjwa ya sakramenti ya wagonjwa. Wana mahospitali mengi nchini ambako watawa wanafanya kazi .
 
Hay

Acheni sifa za kijinga kama wako serious wafunge makanisa huko ndio hakuna utaratibu wa kukaa distance, wawambie watu wakasari majumbani.

Hayo matamasha yana beba watu wangapi?

Wawazuie watu kwenda kanisani ndi watakuwa wametibu tatizo lakini haya mengine ni uongo tu.

Matamasha watu ni walewale na kanisani watu ni walewale sasa hapo wanamaanisha nini?
Ni wajinga tu mkuu!

Ni upuuzi kujisifu umezuia tamasha la siku 1 huku ukiendelea kuruhusu watu kukusanyana ibadan.
 
Back
Top Bottom