#COVID19 Mwitikio wa China wa miaka mitatu wa COVID-19 ni endelevu, wa utaratibu na unaendana na nyakati

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
Ripoti iliyotolewa wiki hii na kituo cha Yuyuantantian, kinachomilikiwa na shirika kuu la Habari la China (CMG) inaonyesha kuwa Mwitikio wa China wa miaka mitatu wa COVID-19 ni endelevu, wa kimfumo na unaendana na nyakati na pia umeokoa maisha ya watu.

Pamoja na hatua za kuzuia na kudhibiti janga hilo zinazotekelezwa katika maeneo mbalimbali, uzuiaji na udhibiti wa janga la kitaifa umeingia katika hatua mpya.

Watu wengi hawakuweza kukabiliana na mabadiliko hayo mara moja na walikuwa na wasiwasi katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

China imepitia miaka mitatu ya kazi ngumu dhidi ya janga hili, lakini pia imefanikiwa ndani ya awamu tatu za kukabili virusi hivyo.

Awamu ya kwanza ni wakati virusi vilipokuwa vipya kabla ya kubadilika kutoka Delta hadi Omicron, pamoja na uharibifu wake.

Kipindi cha pili ni cha dirisha la kutafiti na kutengeneza dawa za dalili za ugonjwa huo, haswa uzinduzi mkubwa wa dawa za jadi za Kichina zenye hati miliki.

1671449312859.jpeg


Na awamu ya kutoa chanjo kwa idadi kubwa ya watu.

Virusi vya Corona vimeendelea kubadilika katika miaka mitatu iliyopita. Aina za Alpha, Beta, Gamma, Delta na Omicron zimeleta changamoto mpya katika kuzuia na kudhibiti janga hili.

Aina ya Alpha, ambayo iligunduliwa kwa mara ya kwanza nchini Uingereza Septemba 2020, ilikuwa ndio aina kuu nchini kote katika miezi michache.

Uchunguzi umeonyesha kuwa virusi vya aina ya Alpha vinaambukiza kwa asilimia 43 hadi 90 kuliko aina nyingine na ndani ya muda mfupi aina hiyo ilienea na kuwa ndiyo kuu kote duniani.

Utafiti wa Uingereza ulionyesha kuwa idadi ya vifo kutokana na kuambukizwa kwa aina ya Alpha ilikuwa mara 1.64 ikilinganishwa na aina ya awali.

Kuanzia Januari hadi Machi 2021, ilikuwa moja ya vipindi ambapo idadi ya vifo nchini Uingereza iliongezeka haraka sana ikiwa na wastani wa vifo 17,000 kwa mwezi.

Wakati huo huo, aina ya Beta iligunduliwa.

Ikilinganishwa na aina zingine, aina ya Beta inasambaa kwa haraka.

Watafiti wamegundua kuwa aina ya Beta inaambukiza kwa asilimia 50 kuliko aina ya asili, na waathiriwa mara nyingi hulazwa hospitalini na hatari ya juu ya kufa.

Baadaye, aina ya Gamma iligunduliwa. Wakati huo, nchi zote ulimwenguni zilikuwa mbioni kupata chanjo ya kupigana na virusi hivyo.

Katika nusu ya pili ya 2021, aina ya Delta ilienea kote Marekania. Idadi ya kesi za kila siku zilizidi 100,000, na idadi ya vifo vya kila siku kutokana na virusi vilizidi 1,000.

Takwimu za Shirika la Afya Ulimwenguni zinaonyesha kuwa mnamo 2021, idadi ya vifo kutokana na COVID-19 ilikuwa karibu milioni 3.5.

Kuibuka kwa aina ya Omicron mwishoni mwa 2021 kulileta changamoto mpya.

Nchini Marekani wiki tatu tu baada ya Omicron kuwa aina kuu , karibu kesi mpya milioni 1.5 zilithibitishwa kwa siku moja.

Baada ya kuibuka kwa aina ya Omicron, Uingereza ilikuwa na kesi mpya milioni 1.227 zilizothibitishwa katika wiki ya kwanza ya 2022.

Wakati aina ya Omicron ilipoonekana kwa mara ya kwanza, Wu Weilin, mtaalam wa zamani wa Shule ya Matibabu ya Harvard, alifanya hesabu ya kisayansi na kugundua kuwa kulingana na utafiti wa mapema, maambukizi ya Omicron yalikuwa mara 4.2 zaidi kuliko ya Delta, na Delta iko juu mara 1,260 kuliko ile ya aina ya asili ya coronavirus; Hivyo ni kusema, kasi ya maambukizi ya Omicron inaweza kuwa mara elfu zaidi kuliko aina ya awali.

Wakati nchi zingine zikiichukulia Omicron kama homa", China haikulegeza hatua zake za kukabili janga hilo na ilikuwa inafanya kila juhudi kufikisha chanjo kwa kundi la watu walio hatarini.

1671449365238.jpeg


Kufikia mwisho wa 2021, zaidi ya dozi milioni 2.8 za chanjo ya COVID-19 zilikuwa zimetolewa nchini China.

Kufikia Desemba 2022, China ilikuwa imetoa zaidi ya dozi milioni 3.4 za chanjo.

Dozi 614,912,000 za chanjo hiyo zilitolewa kwa wazee na watoto.

Na sasa iko mbioni kuwachanja zaidi ya watu bilioni 1.4.

Hadi sasa, kuna ufahamu bora wa ugonjwa na makali ya Omicron, hii imetuwezesha sisi kama China kutengeneza dawa za kukabili makali yake, haswa dawa za jadi za Kichina zenye hati miliki, na wakati huo huo kutoa chanjo.Serikali ya China pia imerekebisha sera ya kuzuia janga hilo.

Hizo ni juhudi za China za kupambana na Covid-19 katika miaka mitatu iliyopita.

China imechagua mbinu tofauti ya kupambana na janga tofauti na nchi za Magharibi kwani China siku zote imekuwa ikifuata mtazamo unaozingatia watu.
 
Back
Top Bottom