KKKT labariki unywaji wa Pombe

KKKT labariki unywaji wa Pombe

Iki tukuelewe vizuri kwamba humchukii na huna bifu na Malasusa na kwamba hujatumwa

Hebu tuambie haya:-

Hiyo Tuhuma ya ngono kumuhusu Malasusa ni Ipi? Una ushahidi uuweke hapa?

Huo Ubaguzi wa Malasusa ni Upi? Hebu thibitisha hapa mfano wa ubaguzi wake.

Jibu hayo tu.

Mwanahalisi wana kampeni ya muda mrefu kumchafua Dkt Malasusa. Walipumzika kwa miezi michache sasa wamenza tena kumwandama askofu wa watu.
 
Quiet bold statement. Itakuwa vizuri ukiweka ushahidi ni wapi exactly ameruhusu. Hii itasaidia kuondoa mitanziko kwa watu wasio na uhakika juu ya hili!
Timotheo 5:23

Hiyo ni mistari baadhi tuu..Ila ipo mingi tuu

Rejea Harusi ya Kana na Yesu
 
Kama mmeweza kuhalalisha ushoga hats pombe mtahalalisha! Kkkt sio kabisa bali Ni NGO.
Wewe ni kijana wa bwn mudy sio bure.

Aliyehalalisha ushoga ni Sheikh maarufu mwenye misikiti na waumini wengi sana USA anaitwa

"Daaliye Abdullah"

Unamfahamu au nikuoneshe picha zake?
 

Attachments

  • 2016-10-10-19-17-04--1289213680.png
    2016-10-10-19-17-04--1289213680.png
    11.5 KB · Views: 50
KKKT labariki unywaji wa Pombe

ASKOFU Mkuu wa zamani wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa, amebariki rasmi unywaji wa pombe katika kanisa hilo kongwe nchini, anaripoti Mwandishi Wetu.

Akizungumza katika mkutano wa 33 wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, wiki iliyopita, huko Seminari ya Kisarawe, mkoani Pwani, Askofu Malasusa amesema, ” katazo la unywaji wa pombe lililetwa na wamisionari, lakini pombe kama pombe haina tatizo.”

Askofu Dk. Malasusa, ndiye askofu mkuu wa kanisa la KKKT, Dayosisi ya Mashariki na Pwani. Askofu Dk. Malasusa alikuwa akikamilisha majibu yaliyotolewa na Askofu Keshomshahara wa kanisa hilo, Dayosisi ya Bukoba aliyoyatoa kwa swali lilioulizwa na Prof. Mjema wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Katika swali lake, Prof. Mjema alihoji, nafasi ya pombe katika dhana ya Mtume Paulo anapozungumzia kutiwa unajisi kwa vyakula na vinywaji wanavyokunywa wakristo.
Alitaka kupata ufafanuzi wa msiamo wa kanisa juu ya msemo wa “kimuingiacho mtu na kimtokacho mtu.” Awali katika majibu yake, Askofu Keshomshahara amesema, “pombe ni kinywaji tu kama vinywaji na vyakula vingine” na kwamba pombe inapaswa kutumiwa kwa kiasi na kwamba “hata sakramenti takatifu ya Meza ya Bwana inayotumika kanisani mwao ni pombe.”

Baada ya majibu hayo, ndipo Askofu Dk. Malasusa aliposisitiza kuwa makatazo ya pombe kanisani ni “busara ya wamisionari wa kwanza walioleta injili Afrika baada ya kuona Waafrika walikuwa wakilewa bila kiasi na kukosa ustaarabu.”
Aliendelea kusisitiza kuwa “pombe itumike kwa kiasi na hasa kwa wakristo wachanga.”

Majibu hayo ya maaskofu yaliwachanganya wajumbe wengi na kusababisha mijadala baada ya mkutano. Mjumbe mmoja aliyeongea na gazeti hili huku machozi yakimlenga anasema, “nimesikitika sana kuona maaskofu wetu wanalipotosha kanisa. Hivi kweli sakramenti ni pombe?” Dayosisi ya Mashariki na Pwani kupitia katiba yake, inapiga marufuku wazee wa kanisa kutomiliki vitega uchumi vinavyouza pombe.

Aidha, sherehe zote za kanisa haziruhusiwi kuwa na pombe huku baadhi ya waumini wakipewa adhabu na wachungaji wao kwa kunywa pombe au kufanya biashara ya pombe. Msimamo wa maaskofu hawa wawili unaliweka kanisa Zima la KKKT katika njiapanda ya kulifafanua jambo hili huku waumini wengi wakitishia kuhamia makanisa ya kiroho kukimbia upotoshaji wa wazi wa maakofu wa KKKT. Mkutano huo wa 33 ulijaa vitimbi vingi vinavyoonyesha dayosisi hiyo haiko shwari.

Akiongea kwa uchungu kwenye mkutano huo, Mchungaji wa kanisa hilo usharika wa Kigogo, jijini Dar es Salaam, Richard Ananja alimtaka Askofu Dk. Malasusa kuachia kiti mara moja kwa kuwa amepoteza sifa kwa kashfa za ngono zinazomkabili.

Amesema Dk. Malasusa anakabiliwa na tuhuma nzito za matumizi ya madaraka, uvujaji wa fedha za dayosisi, hujuma kwa Benki ya Maendeleo, kugushi vyeti ya elimu, ukabila, chuki na visasi kwa wachungaji.

Hivyo basi, ili kulinda hadhi na heshima ya kanisa na yeye binafsi, ni vema Askofu Malasusa “akaachia ngazi kwa hiari, badala ya kusuburi kufukuzwa.”
Hoja hiyo ilipozwa na katibu mkuu wa Dayosisi hiyo, Godfrey Nkini aliyedai kuwa kamati ya maadili inashughulikia tuhuma hizo.

Siku moja kabla ya kufungwa kwa mkutano, mchungaji wa kanisa la KKKT, Usharika wa Kibaha, Amani Lyimo katika mahubiri ya ibada ya asubuhi, aliushambulia utendaji wa Askofu Dk. Malasusa kuwa ni wa uonevu, usijali kweli, uliojaa udhalimu, ubabe na matumizi mabaya ya madaraka.
Amesema uongozi wa Dk. Askofu Malasusa unakomoa watu kuliko uongozi wowote uliopita katika dayosisi hiyo.

Kabla ya kufungwa kwa mkutano huo, Mwenyekiti wa kamati ya maadili wa dayosisi hiyo, Ibrahim Kaduma, alidai kuwa tuhuma juu ya Askofu Dk. Malasusa, si za kweli na zinachochewa na gazeti moja (hakulitaja) lakini akadai ni chuki ya uislamu dhidi ya kanisa.

Maelezo hayo yalipingwa na wachungaji wengi hali inayoonyesha kuwa Askofu Malasusa hayuko vizuri na wachungaji wake. Wachungaji walidai kamati imeleta “majibu mepesi” kwa tuhuma za ngono zinazomkabili Dk. Malasusa na kwamba kinachobakia sasa wao kumwaga hadharani yaliyositiriwa kulilinda kanisa, alisisitiza mmoja wa wachungaji wa kanisa hilo mwenye taaluma ya sheria.

Katika hatua nyingine, ajenda ya marekebisho ya katiba ya dayosisi hiyo, iliburuzwa ili kumwepusha Askofu Malasusa na hoja ya ukomo wa madaraka yake. Siku za karibuni, Askofu Dk. Malasusa amekumbwa na tuhuma mfululizo, zikiwamo matumizi mabaya ya madaraka, ngono na ubaguzi.

Hata hivyo, Dk. Malasusa amekuwa akijibu tuhuma hizo kwa kuwanyooshea kidole waumini wanaotoka mikoa ya Kaskazini kuwa wanamsakama kwa vile katika uchaguzi mkuu uliyopita, limuunga mkono Rais Magufuli na kumsaliti swahiba wake wa miaka mingi, Edward Lowassa.

Chanzo: Mwanahalisionline
Nimejaribu kuisoma habari hii, ila naona tatizo sio pombe au vitendo vya kitabia vya Askofu tatizo ni NAFASI YA UASKOFU, jamani wachungaji wa KKKT wengi wanafahamika wapo kweli wa kiroho lakini wapo waliowengi ambao wanajulikana fika nitashangaa kama hao ndiyo miongoni mwa wanaonyoosha vidole na kujitweza utakatifu, nafikiri kilichopo hapo ni hoja iliyopo kuhusiana na POMBE je bibilia inasemaje kuhusu pombe? Je sakrament inayotumiwa na KKKT haina kilevi? kama kipo kwanini Kanisa waruhusu kitu chenye kilevi kitumike kama sakramenti? Tupate majibu kutoka biblia ili kuanzia hapo tumuulize Askofu hicho anachosema amekipata wapi? Kilichomponza Askofu huenda ni kuwa mkweli,siamini kama Askofu hajui maandiko kwa kiasi hicho.
Nimepita tu jamani
 
1kor 6:9-10 walevi mbinguni si kwao
waefeso 5:19-21 matendo amboyo ni dhambi ni pamoja na ulevi wa mvinyo.

Ndio maana ninawaambia muache unafiki...

Nirudie Mara ngapi kuwa Biblia imekataza ulevi na sio pombe..??
Kuna tofauti kubwa kati ya Kunywa pombe na kunywa pombe kupitiliza mpaka ulewe...

Tusipende kujitoa ufahamu jamani.. DAAAH

HUKUNA sehemu yeyote ya kuverify kwamba timotheo aliambiwa anywe pombe kwa kutibu tumbo.
Unaposema hakuna sehemu ya ku-verify unamaanisha nini..?

Tim 5:23 hebu soma uone...
 
Tumemwambia mleta mada atupe ushahidi wa hayo yote ameshindwa.

Hii inadhihirisha Umbea wake.
 
Kwa kuwa pombe inasabisha ULEVI na ulevi huondoa ufahamu kwa mlevi basi haifai kunywewa.

Ukisoma Biblia vizuri mizizi ya dhambi imeorodheshwa mingi sana...Kuna Ulevi, ulafi, uzinzi nk nk nk..

Unajua kila kitu ni kwa kiasi..Ulafi ni kula kupita kiasi...Kwa hiyo tuache kula maana chakula kinasababisha ulafi..?? Maana umesema pombe inasababisha ulevi...

Ulevi hutokea au ni matokeo ya kunywa kupita kiasi kama ilivyo kula kupita kiasi..

Sasa sijui kwanini umeamua kuchagua ulevi kama dhambi na kuacha ulafi angali zote zimeorodheshwa sawa kwenye Biblia kama dhambi..??

Hebu tuambizane mkuu!
 
Kama mmeweza kuhalalisha ushoga hats pombe mtahalalisha! Kkkt sio kabisa bali Ni NGO.
Acha hizo. Kwani kuna Waluteri walikuta unalawitiwa wakakuacha na kusema unachofanyiwa ni sawa?
Msipende kuchanganya mambo yenu ya kupotosha, tunazungumzia pombe ambayo pia mathehebu mengine ya kikristo yanaruhusu. Ingawa hayaruhusu ulevi
 
Muhudumu niongeze balimi baridiii..
Kuna thamthilia Naifuatilia hapa..teh teh teh
 
Hui in mtwzamo waki wala so wa Kanisa kama taasisi.
 
Acha hizo. Kwani kuna Waluteri walikuta unalawitiwa wakakuacha na kusema unachofanyiwa ni sawa?
Msipende kuchanganya mambo yenu ya kupotosha, tunazungumzia pombe ambayo pia mathehebu mengine ya kikristo yanaruhusu. Ingawa hayaruhusu ulevi
Hakuna watu wanafiki kama hao...hata pombe wanayoipinga wao wameahidiwa wakifaulu kuingia peponi kule kuna mito inayotiririsha maziwa na mvinyo.
 
Nimejaribu kuisoma habari hii, ila naona tatizo sio pombe au vitendo vya kitabia vya Askofu tatizo ni NAFASI YA UASKOFU, jamani wachungaji wa KKKT wengi wanafahamika wapo kweli wa kiroho lakini wapo waliowengi ambao wanajulikana fika nitashangaa kama hao ndiyo miongoni mwa wanaonyoosha vidole na kujitweza utakatifu, nafikiri kilichopo hapo ni hoja iliyopo kuhusiana na POMBE je bibilia inasemaje kuhusu pombe? Je sakrament inayotumiwa na KKKT haina kilevi? kama kipo kwanini Kanisa waruhusu kitu chenye kilevi kitumike kama sakramenti? Tupate majibu kutoka biblia ili kuanzia hapo tumuulize Askofu hicho anachosema amekipata wapi? Kilichomponza Askofu huenda ni kuwa mkweli,siamini kama Askofu hajui maandiko kwa kiasi hicho.
Nimepita tu jamani
Kabla ya kujua kama sakramenti ya walutheri ina kilevi au la...

je soda tunayokunywa ya cocacola haina kilevi?

Je chai ya rangi?

Too much of anything we take is harmful.
 
Hakuna watu wanafiki kama hao...hata pombe wanayoipinga wao wameahidiwa wakifaulu kuingia peponi kule kuna mito inayotiririsha maziwa na mvinyo.
Ha ha ha, kumbe ndio wale wanaosema Kitimoto haramu kwa wafuasi wao lakini wenyewe kwa siri wanapeleka kg3 home na mkwara mzito "ikaushe sana mama Juma usisahau kuweka pilipili"
 
Ulevi ni pombe kama ulafi ilivyo kwa chakula.
Katazo la pombe ni ushauri au tuseme agizo la kibinadamu zaidi na wala sijaona hilo katazo kibiblia.Najua ulevi umekatazwa na pia ulafi umekatazwa.sijaona popote chakula kilipokatazwa kwa sababu husababisha ulafi na vivyo hivyo kwa pombe.
 
Ha ha ha, kumbe ndio wale wanaosema Kitimoto haramu kwa wafuasi wao lakini wenyewe kwa siri wanapeleka kg3 home na mkwara mzito "ikaushe sana mama Juma usisahau kuweka pilipili"
Hao hao
 
Back
Top Bottom