Kizuri Kula na Mwenzio: Burger Za 'McDonalds' Bongo!.

Kizuri Kula na Mwenzio: Burger Za 'McDonalds' Bongo!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,221
Reaction score
128,982
Ule msemo wa Kizuri kula na wenzio unamaanisha ukiona jambo jema, zuri, wajulishe na wenzio!.

Hii ni kwa wenzetu mliopo ughaibuni, msosi rahisi ni fast food. Wale wa Mcdonalds, Kentucky or Tenesse etc, mkirudi nyumbani bongo, sasa mambo hayo yapo!. Karibu kila petrol station kubwa jirani kuna kibanda cha burger, tatizo ni hizo burger zenyewe!.

Miongoni mwa wanaojitahidi sana kufanania na Mcdonalds angalau angalau ni kile kibanda pale Petrol Station ya Morocco!.

Mkirejea nyumbani, ukijiona umemiss sana burger, karibu hapo Morroco you'll never regireti!.
 
Ile ya Morocco- Kinondoni ndiyo the best..

Nadhani inafuatiwa na ya pale Bamaga...
 
Pasco ndugu yangu, zile hamburg kwa kweli wanajitahidi.
Kuna siku jamaa yangu alimpeleka demu pale wa chuo flani opposite na mahakama ya kazi, demu alizifinya chicken burger mbili na vichips akazifuta zote then akashushia na sprite ya kopo! Mimacho ilimtoka jamaa! Toka siku ile anamuita MUNGIKI.
 
pasco

yaani umenidisturb appetite yangu kwa chakula kingine, ile burger ipo vizuri
 
Kwa Tanzania huwezi kuita junk food, bado hatujafikia kuwa na machakula kama ya ulaya. Otherwise ni kweli kwa ulaya ni junk food ila hapa watu tunakula kama kitu kipya kwenye Tanzania cuisines haipo hii. Tushajizoelea mbuzi choma!
 
Junk food kwa bongo yetu ni CHIPS MAYAI NA MSHIKAKI right?
 
Ule msemo wa Kizuri kula na wenzio unamaanisha ukiona jambo jema, zuri, wajulishe na wenzio!.

Hii ni kwa wenzetu mliopo ughaibuni, msosi rahisi ni fast food. Wale wa Mcdonalds, Kentucky or Tenesse etc, mkirudi nyumbani bongo, sasa mambo hayo yapo!. Karibu kila petrol station kubwa jirani kuna kibanda cha burger, tatizo ni hizo burger zenyewe!.

Miongoni mwa wanaojitahidi sana kufanania na Mcdonalds angalau angalau ni kile kibanda pale Petrol Station ya Morocco!.

Mkirejea nyumbani, ukijiona umemiss sana burger, karibu hapo Morroco you'll never regrate!.


Sasa hilo ni tangazo la Biashara au..?
 
Sasa hilo ni tangazo la Biashara au..?
Kiagata, hili sio tangazo la biashara, hii ni taarifa ya kizuri ule na mwenzio!. Lingekuwa tangazo ningetaja kuanzia jina la petrol station, jina la hiyo burger hut, ningekutajia mpaka mmiliki wa kibanda, na kukutajia vibanda vyake vingine ili kukuza biashara yake!. Kwa vile burger sio msosi wa asili yetu, walengwa wa taarifa hii ni wale wa maburger burger, sisi wa ugali tunaendelea na ugali wetu!.
 
Haaa ile ya pale Moroco ni kiboko....alafu bei yao si kubwa kihivyo.
Huwa sikosekani mitaa ile siku mojamoja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom