MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,223
- 22,299
Nimekuwa nikisoma mashambulizi mbalimbali mitandaoni dhidi ya chama kilichobeba matumaini ya watanzania wote wakiwemo wanaokiponda hasa CHADEMA na kujikuta wakati mwingine niwaze kitakachoitoa CCM madarakani. Ukisoma maandishi ya wapinzani unaweza ukatishika na kudhani mwisho wa CCM ndo umewadia. Baada ya kutafakari nikagundua jambo pekee litakalofanya CCM ianguke ni kama itashindwa kudhibiti migogoro na migawanyiko ndani ya chama kwa haraka.
Mwaka 2015 sisi wanaCCM tulipata funzo ambalo hatutakaa tulisahau. Uchaguzi ulikuwa mgumu sana kutokana na kuchelewa sana kudhibiti vikundi vilivyoleta mgawanyiko mkubwa chamani kiasi kwamba kwenye uchaguzi ule tulishuhudia mwanachama akiwa na nguvu kubwa kisiasa huenda zaidi ya mwenyekiti wa chama. Kura zetu nyingi zillienda upinzani kupitia mwanachama yule na wafuasi wake waliokihama chama wakati wanahitajika sana. Isitoshe usaliti ulikuwa wa hali ya juu kwenye uchaguzi. Kwa sababu CCM inajua umuhimu wa kuwa madarakani haikurudia kosa 2020 na inazidi kujirekebisha.
Shukrani kwa waasisi wa chama waliohakikisha Rais anakuwa pia mwenyekiti wa CCM. Hizi kofia mbili zinamfanya mwenyekiti wa chama na Rais kupata urahisi wa maamuzi yenye tija. Kwa wale wanaojipa ujasiri wa kutumia lugha mbaya zilizokosa ustaarabu dhidi ya Rais niwakumbushe kuwa mnapiga ukuta ngumi na mtaumia wenyewe. Rais wa Tanzania ana namna nyingi sana za kudili nanyi. Wakati wa Magufuli mlisema kwanini anafanya maamuzi kivyake bila kushirikisha bunge ila sasa hivi Rais anashirikisha bunge mnalia na kudai bunge la CCM wakati mna wabunge 19 viti maalum CHADEMA na mmoja wa kuchaguliwa kupitia CHADEMA.
Ninatoa wito kwa wale ambao hawana kadi za CCM hakikisheni mnazipata. CCM bado sana iko madarakani kwa miaka mingi sana ijayo. Vitukuu vyetu wataikuta CCM iliyo imara.
Mwaka 2015 sisi wanaCCM tulipata funzo ambalo hatutakaa tulisahau. Uchaguzi ulikuwa mgumu sana kutokana na kuchelewa sana kudhibiti vikundi vilivyoleta mgawanyiko mkubwa chamani kiasi kwamba kwenye uchaguzi ule tulishuhudia mwanachama akiwa na nguvu kubwa kisiasa huenda zaidi ya mwenyekiti wa chama. Kura zetu nyingi zillienda upinzani kupitia mwanachama yule na wafuasi wake waliokihama chama wakati wanahitajika sana. Isitoshe usaliti ulikuwa wa hali ya juu kwenye uchaguzi. Kwa sababu CCM inajua umuhimu wa kuwa madarakani haikurudia kosa 2020 na inazidi kujirekebisha.
Shukrani kwa waasisi wa chama waliohakikisha Rais anakuwa pia mwenyekiti wa CCM. Hizi kofia mbili zinamfanya mwenyekiti wa chama na Rais kupata urahisi wa maamuzi yenye tija. Kwa wale wanaojipa ujasiri wa kutumia lugha mbaya zilizokosa ustaarabu dhidi ya Rais niwakumbushe kuwa mnapiga ukuta ngumi na mtaumia wenyewe. Rais wa Tanzania ana namna nyingi sana za kudili nanyi. Wakati wa Magufuli mlisema kwanini anafanya maamuzi kivyake bila kushirikisha bunge ila sasa hivi Rais anashirikisha bunge mnalia na kudai bunge la CCM wakati mna wabunge 19 viti maalum CHADEMA na mmoja wa kuchaguliwa kupitia CHADEMA.
Ninatoa wito kwa wale ambao hawana kadi za CCM hakikisheni mnazipata. CCM bado sana iko madarakani kwa miaka mingi sana ijayo. Vitukuu vyetu wataikuta CCM iliyo imara.