Mnaishadadia Iran kama vile ni nchi yenye nguvu za kijeshi kweli, mlifanya vilevile kwa Iraq ambayo ilikuwa inaonekana kuwa babe zaidi, sasa hivi iko wapi? USA kwa investment yake ya kijeshi na akili nyingi mtaona siku za usoni kitakachomtokea Iran. Itatafutiwa sababu halafu kichapo kinafuata. Unakumbuka jinsi watalaam wa nyuklia wa Iran walivyouawa? Na ikalalamika kuwa ni njama za Marekani?
Huo uwezo mnaoibambika Iran, haina. Imekuwa ikisupport magaidi yote yanayoshambulia Israel na kutisha kuwa itaifuta kwenye ramani ya dunia lakini ni mikwara tu kama yenu humu. Missiles za waarabu wakiwa na backup ya waajemi, Iran, zimekuwa hazifui dafu Gaza na miji ya Israel kwa kudakwa na Iron Dome. Sasa Iran kama ina uwezo huo, imeshindwaje kuifuta Israel kwa kuwasupport waarabu?
Kitu kingine kinachotokea ni aibu, kuna watu kama
Elungata anaamini kila kilichoondikwa kwenye internet, utamsikia akisema, Google au anakuletea Google link. Google ni search engine inayo index chochote kilichopo kwenye internet hata blog ya Mambe Kimambi na kukuletea results. Lazima ujue kuwa siku hizi kila mtu ana uwezo wa kuandika chochote kwenye internet, kama vile kwenye forums, blogs, websites, wiki n.k. Habari zilizo nyingi ni biased. Sisi kwenye research huwa tunacalculate bias error na confidence interval na kutreat parameters zingine scientifically tunapopublish kitu ambacho ni intensively researched kwa kutumia reliable sources. Halafu kujifanya unajua habari ya tech ya kivita pia unadanganya. Tech ya kivita ni kati ya top secrets. Ili uone kuwa tech hiyo sio mchezo, Tanzania mkiletewa bila kuiteka Stealth F-35B na kuambiwa mfanye reverse engineering, kwa akili zenu itawachukua karne na hamtaweza kutoa hata copy.
Mtu yeyote asichukulie maelezo ya watu humu kama absolute truth au genuine, chukulia upo kwenye kijiwe cha kahawa na kila mtu anaeleza chai zake.