Eiyer kuna kisa kilitokea mtaa mmoja wa Dar mwaka juzi ilikuwa kulia huwezi, kucheka huwezi.
kuna jamaa alikuwa anamtaka sana mke wa mtu ambaye bwanake alimwezesha kuwa na kijigrosare mahala. kwa hiyo jamaa ikawa anaenda hapo kunywa mara kwa mara nilielezwa. ikasukwa njia TUKIO lifanyike hapohapo grosare. inasemekana ikawa sasa mazowea.
mwizi anakuja grosare, anajifanya anaingia choo, mke wa mtu anamfuata chooni, wanajua wenyewe walikuwa wanafanyaje huko jamaa anamaliza haja zake bila kelele. kumbe kuna kina shigongo weshajua mpango huu.
siku moja jamaa wakamtonya mume wa mtu. naye akaja maeneo jirani kusubiri mchezo uanze. mara, jamaa kazunguka chooni. haijapita dakika mamtoto wa jamaa naye huyooo, chooni. jamaa akaambiwa tayari njoo... Mume wa mtu kachukua njemba haooo, grosare. kufika chooni jamaa hajamaliza.
Walimnyang'anya nguo zake zote akawa uchi wa mnyama kama alivotoka kwa mamake. Baada ya hilo wakamwambie sasa wewe tunakurudisha kwako tunaiambie familia yako wewe si mwaminifu kwa mkeo. Walimtembeza kilometa karibia mbili uchi mchana kweupeeee kumpeleka kwake.
Cha ajabu sasa. yule mwanamke kumbe alikuwa na mtoto ambaye bado alikuwa ananyonya nyumbani kamwachia mfanyakazi. Ndoa ya mwenye grosare ilivunjika.
Kwa kifupi ni kweli wanaume wanawaadhibu wezi wao wa kiume.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.