Kitine: Nchi sasa yaongozwa kienyeji

Yaani Kitine aliyeiba US$64,000 mwaka 1997 akishirikiana na Mkapa leo ana nguvu za kusema nchi inaongozwa kienyeji? Huyu ndie alitakiwa apelekwe kisutu faster faster kwa kuiba na kutumia madaraka vibaya....tunapoteza muda kuwajadiri akina Masha wakati ushahidi wa wizi wa Kitine ni more convincing.

Kwanza Kitine atueleze jitihada alizofanya kuzirudisha US$64,000 alizoiba ndipo atupe msimamo wake juu ya mapungufu ya serikali ya sasa. Vinginevyo anakuwa kama padre anayehubiri kuacha usherati baada ya kushinda tuzo kadhaa za usherati.

Kama ndiyo hivyo basi hakuna kiongozi yeyote mstaafu ambaye ana sifa ya kuongea kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu maana wote ambao wako hai wana tatizo moja au jingine. Mzee Rukhsa tunajua ufisadi wa Mama Siti na yeye mwenyewe kugawa viwanja kwa ndugu, jamaa na marafiki. Cleopa Msuya aliwahi kutwambia kwamba kila mtu atabeba msalaba wake mwenyewe, Malecela tunajua matatizo yake mbali mbali hata Mwalimu alishamuona hastahili kuwa Rais wa nchi yetu. Salim Ahmed ataambiwa ni Mwarabu alikaa nje ya nchi miaka mingi hajui lolote kuhusu Tanzania hivyo hana wajibu wa kutia neno lolote kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu. Sumaye naye ni fisadi alitumia nafasi yake kama PM kujikusanyia utajiri wa hali ya juu ambao hakuwa nao kabla ya kuwa Waziri Mkuu, Kawawa naye ni mwasherati alikuwa na wake zaidi ya mmoja.

Wote wakae kimya tu na kuiacha Tanzania ikiendelea kuangamia kutokana na kuongozwa na watu wasiokuwa na hata chembe ya maadili ya uongozi, wasio na ujasiri na waliojaa woga wa hali ya juu na siku zote wataweka mbele maslahi yao, ya marafiki zao ambao ni mafisadi na chama chao cha kifisadi badala ya yale ya nchi.

Mungu inusuru Tanzania maana badala ya kupima uzito wa maneno yaliyosemwa sasa tunaangalia nani kayasema na kama aliyesema si mtu safi basi hayana sifa ya kujadiliwa na kuyatafakari maana ni upupu tu!!!! :confused::confused:

Si ajabu viongozi wengi wastaafu wameamua kukaa kimya huku nchi ikiendelea kuangamia maana wakiamua kukemea hali ya uongozi ndani ya nchi yetu basi mafisadi, watetezi wao na hata baadhi ya Watanzania wataamua kuwachafua tena na kuwaambia kaa kimya wewe hustahili kusema lolote wewe na matokeo yake nchi inaendelea kuangamia na matokeo yake mafisadi wanaendelea kupata nguvu na kushamiri kila kukicha!!!!

Oh! Tanzania unaelekea wapi nchi yangu!!!!! :( :(
 
Last edited:
Sio viongozi wote wastaafu ni mafisadi. Bado wapo baadhi ya viongozi ambao ni typical Nyerere type, waadilifu na bold. Yupo Mzee Ibarahim Kaduma, yupo Joseph Butiku na wengine wengi. Simtaji Jaji Joseph Warioba kwa sababu ameponza na taaluma yake ya sheria na Law chamber yake na Mahalu lakini ni mwadilifu wa kweli na bold.
 
Kama ndiyo hivyo basi hakuna kiongozi yeyote mstaafu ambaye ana sifa ya kuongea kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu maana wote ambao wako hai wana tatizo moja au jingine. Mzee Rukhsa tunajua ufisadi wa Mama Siti na yeye mwenyewe kugawa viwanja kwa ndugu, jamaa na marafiki. Cleopa Msuya aliwahi kutwambia kwamba kila mtu atabeba msalaba wake mwenyewe, Malecela tunajua matatizo yake mbali mbali hata Mwalimu alishamuona hastahili kuwa Rais wa nchi yetu. Salim Ahmed ataambiwa ni Mwarabu alikaa nje ya nchi miaka mingi hajui lolote kuhusu Tanzania hivyo hana wajibu wa kutia neno lolote kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu. Sumaye naye ni fisadi alitumia nafasi yake kama PM kujikusanyia utajiri wa hali ya juu ambao hakuwa nao kabla ya kuwa Waziri Mkuu, Kawawa naye ni mwasherati alikuwa na wake zaidi ya mmoja.

Wote wakae kimya tu na kuiacha Tanzania ikiendelea kuangamia kutokana na kuongozwa na watu wasiokuwa na hata chembe ya maadili ya uongozi, wasio na ujasiri na waliojaa woga wa hali ya juu na siku zote wataweka mbele maslahi yao, ya marafiki zao ambao ni mafisadi na chama chao cha kifisadi badala ya yale ya nchi.

Mungu inusuru Tanzania maana badala ya kupima uzito wa maneno yaliyosemwa sasa tunaangalia nani kayasema na kama aliyesema si mtu safi basi hayana sifa ya kujadiliwa na kuyatafakari maana ni upupu tu!!!! :confused::confused:

Si ajabu viongozi wengi wastaafu wameamua kukaa kimya huku nchi ikiendelea kuangamia maana wakiamua kukemea hali ya uongozi ndani ya nchi yetu basi mafisadi, watetezi wao na hata baadhi ya Watanzania wataamua kuwachafua tena na kuwaambia kaa kimya wewe hustahili kusema lolote wewe na matokeo yake nchi inaendelea kuangamia na matokeo yake mafisadi wanaendelea kupata nguvu na kushamiri kila kukicha!!!!

Oh! Tanzania unaelekea wapi nchi yangu!!!!! :( :(

Saafi kabisa BAK, soon Tanzania will go to the dogs!!!
Na hao dogs wakisemwa basi itabidi uwe malaika maana ukinyanyua mdomo tu nawee data zako bwelele, kitu ambacho si kibaya lakini mradi ukweli utoke.
Rostam yuko kwenye scandals za Umeme,kwenye BOT,TRL na hivi karibuni amejitokeza kwenye scandals za wakulima wa Chai Rungwe.
Vile vile ni kiongozi wa Chama. Sasa compare ufisadi huu na $64,000 za Kitine.
Kesi zilizom mahakamani za kina Mramba ni za Mabilioni sio $64,000.
Where is our sense of logic?
Itabidi malaika watelemke ,watusemee kuwa jamani tunahitaji kujisahihisha maana kwa mwendo huu baada ya miaka 10-20 tunajitengenezea bomu la tabaka ambazo ni irreconcilable.
Hatuna haja ya kwenda mbali kupata mifano.Kenya tosha
Chama kutoyazungumzia mambo haya ni woga tu wa kuogopana, au mafisadi wana nguvu sana.Kwamba fisadi hawezi kuchukuliwa hatua mpaka athibitike mahakamani , kwa chama chenye maadili ni kichekesho cha juha kalulu.
 
Kitine anaiona hatari ya "mbaya" wake Membe kuwa Rais 2015. Sioni atamzuiaje kwa kauli zinazojirudia kama hizi.
 
Last edited:
Kama ndiyo hivyo basi hakuna kiongozi yeyote mstaafu ambaye ana sifa ya kuongea kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu maana wote ambao wako hai wana tatizo moja au jingine. Mzee Rukhsa tunajua ufisadi wa Mama Siti na yeye mwenyewe kugawa viwanja kwa ndugu, jamaa na marafiki. Cleopa Msuya aliwahi kutwambia kwamba kila mtu atabeba msalaba wake mwenyewe, Malecela tunajua matatizo yake mbali mbali hata Mwalimu alishamuona hastahili kuwa Rais wa nchi yetu. Salim Ahmed ataambiwa ni Mwarabu alikaa nje ya nchi miaka mingi hajui lolote kuhusu Tanzania hivyo hana wajibu wa kutia neno lolote kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu. Sumaye naye ni fisadi alitumia nafasi yake kama PM kujikusanyia utajiri wa hali ya juu ambao hakuwa nao kabla ya kuwa Waziri Mkuu, Kawawa naye ni mwasherati alikuwa na wake zaidi ya mmoja.

Wote wakae kimya tu na kuiacha Tanzania ikiendelea kuangamia kutokana na kuongozwa na watu wasiokuwa na hata chembe ya maadili ya uongozi, wasio na ujasiri na waliojaa woga wa hali ya juu na siku zote wataweka mbele maslahi yao, ya marafiki zao ambao ni mafisadi na chama chao cha kifisadi badala ya yale ya nchi.

Mungu inusuru Tanzania maana badala ya kupima uzito wa maneno yaliyosemwa sasa tunaangalia nani kayasema na kama aliyesema si mtu safi basi hayana sifa ya kujadiliwa na kuyatafakari maana ni upupu tu!!!! :confused::confused:

Si ajabu viongozi wengi wastaafu wameamua kukaa kimya huku nchi ikiendelea kuangamia maana wakiamua kukemea hali ya uongozi ndani ya nchi yetu basi mafisadi, watetezi wao na hata baadhi ya Watanzania wataamua kuwachafua tena na kuwaambia kaa kimya wewe hustahili kusema lolote wewe na matokeo yake nchi inaendelea kuangamia na matokeo yake mafisadi wanaendelea kupata nguvu na kushamiri kila kukicha!!!!

Oh! Tanzania unaelekea wapi nchi yangu!!!!! :( :(
BAK,
Umesema vema kabisaaa.
Hakuna binadamu mkamilifu.Kwa vile huo ndiyo ukweli itabidi watu watambue kuwa wa kurekebisha siyo malaika bali ni binadamu hawahawa ( wewe, mimi, yeye) wenye mapungufu.Ndiyo maana mtu akianguka habaki chini bali hunyanyuka na kujikung'uta na kuendelea na safari.Wakina Kitine na wengineo waliowahi kuanguka bado wanayo nafasi kusimama, kujikung'uta na kuendelea na mapambano.Isitoshe hata kwenye maandiko si ajabu wale waliokuwa wabaya zaidi ndio waliofunuliwa wakaja wakawa wakombozi wa wengine.
Kwa hali tuliyokuwa nayo sasa watanzania, tatizo ni kwamba kwa vile watu waliogopa au kuona haya kukemea kwa kuogopa nao watakosolewa ndiyo tumejikuta tumefikia pabaya.Umefika muda tuwakubali akina Kitine, Mwinyi, Kawawa,Butiku,Malecela,Mbilinyi na wengine.....wakosoe na wanaokosolewa wakubali kukosolewa, na sisi tuunge mkono jitihada hizi za kujikosoa na kukosolewa.Kwani baba mlevi huwa hakosoi na kurudi watoto wake?
 
Kama ndiyo hivyo basi hakuna kiongozi yeyote mstaafu ambaye ana sifa ya kuongea kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu maana wote ambao wako hai wana tatizo moja au jingine. Mzee Rukhsa tunajua ufisadi wa Mama Siti na yeye mwenyewe kugawa viwanja kwa ndugu, jamaa na marafiki. Cleopa Msuya aliwahi kutwambia kwamba kila mtu atabeba msalaba wake mwenyewe, Malecela tunajua matatizo yake mbali mbali hata Mwalimu alishamuona hastahili kuwa Rais wa nchi yetu. Salim Ahmed ataambiwa ni Mwarabu alikaa nje ya nchi miaka mingi hajui lolote kuhusu Tanzania hivyo hana wajibu wa kutia neno lolote kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu. Sumaye naye ni fisadi alitumia nafasi yake kama PM kujikusanyia utajiri wa hali ya juu ambao hakuwa nao kabla ya kuwa Waziri Mkuu, Kawawa naye ni mwasherati alikuwa na wake zaidi ya mmoja.

Wote wakae kimya tu na kuiacha Tanzania ikiendelea kuangamia kutokana na kuongozwa na watu wasiokuwa na hata chembe ya maadili ya uongozi, wasio na ujasiri na waliojaa woga wa hali ya juu na siku zote wataweka mbele maslahi yao, ya marafiki zao ambao ni mafisadi na chama chao cha kifisadi badala ya yale ya nchi.

Mungu inusuru Tanzania maana badala ya kupima uzito wa maneno yaliyosemwa sasa tunaangalia nani kayasema na kama aliyesema si mtu safi basi hayana sifa ya kujadiliwa na kuyatafakari maana ni upupu tu!!!! :confused::confused:

Si ajabu viongozi wengi wastaafu wameamua kukaa kimya huku nchi ikiendelea kuangamia maana wakiamua kukemea hali ya uongozi ndani ya nchi yetu basi mafisadi, watetezi wao na hata baadhi ya Watanzania wataamua kuwachafua tena na kuwaambia kaa kimya wewe hustahili kusema lolote wewe na matokeo yake nchi inaendelea kuangamia na matokeo yake mafisadi wanaendelea kupata nguvu na kushamiri kila kukicha!!!!

Oh! Tanzania unaelekea wapi nchi yangu!!!!! :( :(

Umesema yote Mkuu. Kama ulikuwa kwenye mind yangu.:)

Mimi nadhani kila mtu anayo haki ya kutoa maoni yake. Hakuna mtu ambae hajawahi kufanya makosa katika maisha yake yote. Inawezekana hata hapa JF kuna watu ambao wameshafanya makosa makubwa sana tu (kila mmoja anajijua), ila hiyo haiwezi kuwazuia kutoa maoni yao.

Kitine ametoa maoni yake. Kama kuna hoja ya kuyapinga, ni vyema tukazisikia.

Ukweli ni kwamba historia ya nchi inaonyesha aliyosema Kitine ni sahihi kabisa. Hajasema kuwa hakuna waliokosea miaka ya nyuma au katika serikali zilizopita. Alichosema ni kwamba, sasa yamezidi. Hata hao wanaosema yeye mwenyewe alitumia pesa nyingi za umma kinyume cha sheria, wanajua pia kuwa pesa hizo hazikuwa nyingi kama zinazoibiwa sasa, na hatua madhubuti zilichukuliwa dhidi yake, ikiwa ni pamoja na kumpotezea wadhifa aliokuwa nao (Uwaziri). Je haya yanafanyika sasa hivi kwa wale walioonekana kutumia rasilimali za umma?

Kuna ambao wamedai kuwa washutumiwa wa uhalifu wenye nyadhifa mbalimbali katika Bunge na chama wanyang'anywe nyadhifa zao. Nani anaeweza kufanya hivyo? Maana Katiba ya nchi inatamka wazi kuwa Mbunge atapoteza wadhifa wake atakapohukumiwa Mahakamani kwa kufanya kosa la jinai au kuhukumiwa kufungo jela (kitu kama hicho). Wabunge wenye kesi Mahakamani hawawezi kunyang'anywa Ubunge wao bila sharti hilo kutimia.
 
Anakosea tu pale anaposema NCHI inaendeshwa kienyeji. Hapo anakuwa ameitukana pia mihimili mingine miwili yaana BUNGE na MAHAKAMA. Anahoji pia TEUZI zinazofanywa na Rais ambazo zinafanyika kwa mujibu wa KATIBA tulionayo.
 
Anakosea tu pale anaposema NCHI inaendeshwa kienyeji. Hapo anakuwa ameitukana pia mihimili mingine miwili yaana BUNGE na MAHAKAMA. Anahoji pia TEUZI zinazofanywa na Rais ambazo zinafanyika kwa mujibu wa KATIBA tulionayo.

hapa hakukkosea kabisa utawala wa sheria hakuna kabisa tanzania, mahakama zinatenda haki kwa kubagua tu. watu wangapi wana kesi za mauaji lakini hawawezi kushughulikiwa kama alivyoshughulikiwa marehemu Ditopile.
Liyumba kapeleka mahakamani vielelezo fake kabisa lakini kapewa dhamana na masharti nafuu
bunge linaegemea upande mmoja tu, mfano angalia wizara imepeleka bungeni bajeti yake including ununuzi wa mashangingi na seminars na wabunge wote wakapitisha hiyo bajeti akiwepo mkuu wa bunge (Waziri mkuu), baada ya muda waziri mkuu ambaye alikuwako bungeni na alipitisha hiyo bajeti anasimama jukwaani na kutangaza mashangingi na seminar ni marufuku na bunge linakaa kimya bila kumuuliza chochote
bwana Zitto alishasimamishwa bungeni kwa sababu ya ujinga wa kubagua upinzani, lakini mwisho wa siku ilionekana wabunge ndio waliochemsha,
KWA KIFUPI UTAWALA WA SHERIA TANZANIA HAKUNA, NA TUKIWEZA KUISIMAMISHA HII WIZARA NA KUFANYA KAZI YAKE VIZURI HII NCHI INGEFIKA MBALI SANA, MAANA NI AJABU KAMA HATA MWANASHERIA MKUU NAYE YUPO MSTARI WA MBELE KUVUNJA SHERIA NI HATARI
 
Naelekea kufikiri kuna kiongozi/mwanasiasa/mwanazuoni mmoja tu mwenye sifa alizozitaja Kitine katika Historia ya CCM na Tanzania-'Mzee wa Mikasi'
 
Kitine na wenzie wa aina yake wana DENI KUBWA katika ustawi wa demokrasia na uhuru nchini. kwa kipindi kirefu wamekuwa vinara wa KUBAKA demokrasia kwa kutumia mfumo wao wa KIDUMU CHAMA.

Ametumika ipasavyo na amefaidi kibinafsi vema. kuamka kwake sasa kuhusu hali ya kiutawala na kisiasa nchini ni kuungama na kujaribu kutibu maumivu yake ya ndani hasa yaliyomsibu baada ya utawala usiomtambua kuwemo.

walishiri kujenga mfumo mbovu unaokiangamiza chama chao ccm leo na kuendelea. tumebadilika na tunawagundua janja yao ila kelele zao pia zitasaidia kiasi kuamsha umma kuhusu ubovu wa mfumo uliopo.

watu aina ya kitine hasa viongozi waliopita wapo wengi na unafiki wao kwa sasa upo dhahiriiiiiii....
wamsaidie kijana wao JK ili kunusuru taasisi yao ccm waliyoitumia kwa muda mrefu kukandamiza wenye mawazo mbadala na kulinda heshima ya ukuu bila utendaji dhahiri.

namtarajia aendelee kutoa maoni hadharani kwamba KATIBA YA SASA HAIENDANI NA MABADILIKO YA KISIASA, KIUCHUMI NA KIJAMIII YANAYOHITAJIKA NCHINI....

TUSIENDELEE KUONGOZA KWA MAZOEAAAAA.........
 
SIKU moja baada ya Mkurugenzi mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa nchini, Dk. Hassy Kitine, kudai nchi inaendeshwa kienyeji na kukilalamikia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuendelea kuwakumbatia wanachama wake wanaokabiliwa na kesi za ufisadi, chama hicho kimesema hakiwezi kuwavua nyadhifa hizo, kwa sababu kesi zao bado ni tuhuma tu.

Sambamba na hilo, CCM imesema kauli ya Dk. Kitine kwamba nchi inaendeshwa kienyeji ni maoni yake binafsi, kwani hayana ukweli.

Msimamo huo wa CCM ulitolewa jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati, alipozungumza na Tanzania Daima, akijibu shutuma nzito zilizotolewa juzi na Dk. Kitine dhidi ya serikali.

“Sisi tunasema, yeye kama raia ana haki ya kutoa mawazo yake, na hiyo ndiyo demokrasia. Lakini si lazima kila anayetoa mawazo yake yawe sahihi. Mtu anaweza kujiuzulu nafasi yake kupisha uchunguzi ufanyike, hiyo haimaanishi kwamba hilo jambo amelifanya kweli.

“Uchunguzi unapofanyika kuna mambo mawili yanaweza kutokea, la kwanza huyo mtu anaweza kubainika alifanya hicho kitu na la pili anaweza kuonekana hana hatia.

“Hatuwezi kuwavua watu uanachama au nyadhifa zao ndani ya chama kwa sababu hiyo tu. Yeye aliyesema hivyo atutajie ni kiongozi gani wa serikali ambaye pia ni kiongozi wa chama, ameshathibitika kuwa hana maadili halafu kama chama tumeendelea kumwacha. Atuambie…..hakuna,” alisema Chiligati.

Alipoulizwa kwanini CCM isiwafukuze uanachama na kuwavua nyadhifa zao za kichama na ubunge, baadhi ya viongozi wake, ambao tayari serikali ya chama hicho ilisharidhika kwamba walikiuka maadili ya uongozi kwa kutumia vibaya madaraka yao, hata ikaamua kuwafungulia kesi, alisema: “Hatuwezi kuwachukulia hatua kwa sababu kesi zao bado ni tuhuma tu. Wakithibitika kama kweli walifanya hivyo, hatutawaacha,” alisema Chiligati.

Chiligati alipinga madai ya nchi kuongozwa kienyeji na kusisitiza kuwa kauli ya Dk. Kitine, haina ukweli wowote.

Alisema nchi inaongozwa vizuri kwa kufuata utawala wa sheria na mihimili yote ya dola, ikiwemo utawala, Bunge na Mahakama, inafanya kazi zake vizuri.

Alibainisha kuwa kielelezo kuwa nchi haiongozwi kienyeji, ni amani na utulivu vilivyopo nchini, kwani kama nchi ingekuwa inaongozwa kienyeji kusingekalika.

“Kwa mfano, hilo alilosema nchi inaongozwa kienyeji, maana yake nini? Nchi kuongozwa kienyeji maana yake hakuna mfumo wa utawala kabisa, hakuna utawala wa sheria. Mahakama hazipo wala Bunge halipo…serikali haipo.

“Kungekuwa na hali hiyo, ingekuwa sawa na kusema nchi inaongozwa kienyeji. Lakini sisi hatujafikia hatua hiyo. Bunge lipo, Mahakama ipo, Serikali ipo. Utawala wa sheria. Nchi haiongozwi kienyeji, ndiyo maana kuna amani na utulivu,” alisema Chiligati.

Mbali ya CCM kutoa kauli hiyo, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), aliunga mkono kauli ya Dk. Kitine.

“Mzee Kitine ameongea jambo ambalo ninaliongea kila siku kwamba, kuna tatizo kubwa serikalini. Tuhuma za ufisadi zimeshamiri sana, watendaji hawachukui maamuzi, wanasiasa wenye nyadhifa serikalini wamejaza nafasi na hawako tayari kuwajibika. Tunahitaji muafaka wa kitaifa kwenye mambo mengi,” alisema Zitto.

Alisema ili mambo yaende vizuri, Tanzania inahitaji kelele za wazee wastaafu kama Dk. Kitine, wasimamie kunena na kushauri na hata kukemea na wananchi wawapigie kura wabunge wengi wa upinzani ili Bunge liwe na meno.

Juzi, Dk. Kitine alisema taifa linakabiliwa na tatizo la uongozi, ambalo halijawahi kutokea katika historia ya nchi.

Kada huyo wa siku nyingi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), aliyewahi kuwa mbunge wa Makete, mkoani Iringa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, chini ya uongozi wa Rais mstaafu Benjamin Mkapa, alisema nchi imekuwa ikiendeshwa kienyeji, kwa sababu ya kuporomoka kwa maadili ya uongozi.

“Hali tuliyofikia si nzuri, tena niseme ni mbaya sana. Kuna kuporomoka kwa kiasi kikubwa kwa maadili ya uongozi. Na hii nawaambia, nchi haijawahi kuwa katika hali mbaya huko nyuma kama ilivyo sasa. Kwa hali tuliyofikia ni ngumu kurekebisha maadili ya uongozi.

“Tatizo kubwa ni viongozi kukosa integrity (uadilifu). Kwanza ni integrity ya viongozi wenyewe, pili ni commitment (wito), tatu ni nationalism (utaifa). Haya ndiyo yalikuwepo wakati wa Mwalimu,” alisema Dk. Kitine.

Alisema baadhi viongozi wa serikali wamepoteza sifa kuu tatu za uongozi ambazo ni kuwa na uadilifu, wito na kuweka mbele utaifa, sifa ambazo alisema ndizo zilikuwa nguzo ya uongozi wakati wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, chini ya Baba wa Taifa, hayati, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Alisema uteuzi mbaya wa viongozi hususan uteuzi wa mawaziri, umechangia kupatikana kwa viongozi wasio waadilifu, wengi wao wakijihusisha na vitendo vya rushwa
 
Niwahi sema humu ndani kuwa tatizo la watz ni wasomi wetu kutokuwa wakweli kwa boss wao wa mwanzo, wangelikuwa wakweli na kuthubutu kusimama ktk line hiyo ya ukweli nchi hii ingelikuwa mbali sana
 
Kama ndiyo hivyo basi hakuna kiongozi yeyote mstaafu ambaye ana sifa ya kuongea kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu maana wote ambao wako hai wana tatizo moja au jingine. Mzee Rukhsa tunajua ufisadi wa Mama Siti na yeye mwenyewe kugawa viwanja kwa ndugu, jamaa na marafiki. Cleopa Msuya aliwahi kutwambia kwamba kila mtu atabeba msalaba wake mwenyewe, Malecela tunajua matatizo yake mbali mbali hata Mwalimu alishamuona hastahili kuwa Rais wa nchi yetu. Salim Ahmed ataambiwa ni Mwarabu alikaa nje ya nchi miaka mingi hajui lolote kuhusu Tanzania hivyo hana wajibu wa kutia neno lolote kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu. Sumaye naye ni fisadi alitumia nafasi yake kama PM kujikusanyia utajiri wa hali ya juu ambao hakuwa nao kabla ya kuwa Waziri Mkuu, Kawawa naye ni mwasherati alikuwa na wake zaidi ya mmoja.

Wote wakae kimya tu na kuiacha Tanzania ikiendelea kuangamia kutokana na kuongozwa na watu wasiokuwa na hata chembe ya maadili ya uongozi, wasio na ujasiri na waliojaa woga wa hali ya juu na siku zote wataweka mbele maslahi yao, ya marafiki zao ambao ni mafisadi na chama chao cha kifisadi badala ya yale ya nchi.

Mungu inusuru Tanzania maana badala ya kupima uzito wa maneno yaliyosemwa sasa tunaangalia nani kayasema na kama aliyesema si mtu safi basi hayana sifa ya kujadiliwa na kuyatafakari maana ni upupu tu!!!! :confused::confused:

Si ajabu viongozi wengi wastaafu wameamua kukaa kimya huku nchi ikiendelea kuangamia maana wakiamua kukemea hali ya uongozi ndani ya nchi yetu basi mafisadi, watetezi wao na hata baadhi ya Watanzania wataamua kuwachafua tena na kuwaambia kaa kimya wewe hustahili kusema lolote wewe na matokeo yake nchi inaendelea kuangamia na matokeo yake mafisadi wanaendelea kupata nguvu na kushamiri kila kukicha!!!!

Oh! Tanzania unaelekea wapi nchi yangu!!!!! :( :(

Sikubaliani nawe kwa msingi kuwa hata ukiangalia alichokisema Kitine, hakuna jipya sana... haya yameshawahi kusemwa sana huko nyuma. hatua tuliyofikia sasa haitakiwi kurudiarudia wimbo huu, Aidha tuseme mapya, au tuchukue hatua. Kuna siri ngapi tusizozijua ambazo Kitine anazifahamu lakini hakuzisema siku hiyo? Kuna mambo mangapi anayoyafahamu ambayo akiyatamka yatakuwa ni clue kwa mambo mengi yaliyojificha?
 
Bora Chiligati anaanza kututhibitishia mapema kabisa kuwa harakati za kuwapandisha Kisutu Mafisadi ni SINEMA tu mwishowe tutaambiwa zilikuwa tuhuma tu na zimeshindwa kuthibitishwa mbele ya sheria!
 
Physically sijawahi kumuona Dr.Kitine,lakini nimetokea kumpenda na kumheshimu sana kwa jinsi anavyosimama imara kupambana na ufisadi na maovu mengine katika jamii.Yote aliyowahi kuongea Dr.Kitine ni sahihi kabisa, including hili la kuingoza nchi kienyeji.Kwani kuingoza nchi kienyeji maana yake ni nini,nadhani ni hili tu kwamba hakuna muongozo wowote wa wazi na uliokubalika na wadau wote as to how the country should be run.Ni mafisadi wachache tu walio jikusanya na wakajiita serikali na chama ndio kusema kweli wanao ongoza nchi,tena jinsi wanavyotaka wao na kwa maslahi yao.Bad luck indeed.Hapana hii haikubaliki, na namshukuru Dr.Kitine kwa kusimama imara na kusema no,things can't go on like that.Viva mpiganaji Mzee Dr.hassy Kitine,mapambano yanaendelea.
 
Upande wa pili: Hawa akina Kitine walitakiwa waweke utaratibu wa kimaadili na utaifa ili kina JK wafuate. Sio kama natetea haya manyang'au ya EPA n.k. Ila ninasikitika kusikia watu ambao walikuwa na nafasi za kuubadilisha mfumo wa uongozi kuwa wa kisasa na kisheria hawakufanya hivyo ila sasa ndio wa kwanza kulalamika. Wamemuachia JK Katiba ile ile Presidential Powers zile zile sasa hapo unategemea nini. Nina hakika hii timu ya JK miaka ijayo nayo italalamika vivi hivi.
 
1. Kama ndiyo hivyo basi hakuna kiongozi yeyote mstaafu ambaye ana sifa ya kuongea kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu maana wote ambao wako hai wana tatizo moja au jingine.

2. Mzee Rukhsa tunajua ufisadi wa Mama Siti na yeye mwenyewe kugawa viwanja kwa ndugu, jamaa na marafiki.

3. Cleopa Msuya aliwahi kutwambia kwamba kila mtu atabeba msalaba wake mwenyewe,

4. Malecela tunajua matatizo yake mbali mbali hata Mwalimu alishamuona hastahili kuwa Rais wa nchi yetu.

5. Salim Ahmed ataambiwa ni Mwarabu alikaa nje ya nchi miaka mingi hajui lolote kuhusu Tanzania hivyo hana wajibu wa kutia neno lolote kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu.

6. Sumaye naye ni fisadi alitumia nafasi yake kama PM kujikusanyia utajiri wa hali ya juu ambao hakuwa nao kabla ya kuwa Waziri Mkuu,

7. Kawawa naye ni mwasherati alikuwa na wake zaidi ya mmoja.

- Mkulu BAK yaani hii yako ni the best ever excuse nimewahi kusikia kutoka kwa mwananchi wa Tanzania akijaribu kukwepa responsibilities za taifa lake, Tanzania sasa hivi tunasumbuliwa na tatizo moja tu katika uongozi nalo ni wizi wa viongozi wetu kwa taifa, taifa letu limedumaa kwa sababu yua wizi, hatuwezi kukwepa kuchukua sheria kwa sababu eti sisi binadam wote ni wapungufu.

- Tanzania tuna sheria aginst wezi, yaani wananchi wezi it does not matter kama ni viongozi au wananchi, sasa kwa maneno yako hapo juu una maana tufike mahali tusichukue sheria kwa sababu viongozi wote ni wapungufu maana sisi binadam wote ni wapungufu, is that so?

- Kitine ni mwizi, yeye na mkewe serikali isingempa dola $ 64,000 kama asingekua mke wa Kitine, kamati ya bunge ya taifa ilikutana na kuchunguza na kubainisha kisheria kwamba mke wa Kitine ni mwizi, sasa kilichotakwia ni yeye na mkewe kutinga kwenye sheria, na bado mpaka leo tunaweza kumtingisha huko, sasa wewe unasema kwamba hao viongozi uliowataja hapo juu wameshawahi kufikia hii line ya wizi wa Kitine?

- Hao viongozi uliowataja hapo juu kama kuna mmoja mwenye ishus za kisheria, kwa sababu sijui kama tuna sheria za kukamata waasherati, au tuna sheria kwamba kiongozi aliyekaa nje muda mrefu anatakiwa kufungwa, au sheria inayosema kama Mwalimu alisema hufai basi unatakiwa kwenda kwenye sheria, au kwamba kiongozi alisema utabeba mzigo wako basi unatakiwa kufika kwenye sheria,

- lakini one thing huwezi changanya hapa ni kwamba Kitine ni mwizi, Mwalimu alimfukuza kazi uwt kwa sababu ya wizi, mkewe amekamatwa na kuhukumiwa na kamati ya bunge kwa sababu ya wizi, hapo juu inaelekea Mwinyi naye ana tuhuma za wizi, viongozi wote wa namna hii hawana moral authority ya kutuambia anything kuhusu viongozi wengine wezi na mafisadi.

- Good shot, lakini mkuu wangu hoja yako ina-fall short tena mbali sana, viongozi wezi ndio tatizo letu sasa hivi, sasa yeyote mwenye tuhuma za wizi akae pembeni, na wala binafsi sitaki kusikia akisema eti wengine ni wezi wakati yeye ni mwizi, sheria zetu ziko very clear kuhusu wananchi wezi wanatakiwa kwenye sheria, sheria zetu ziko wazi mkuu wizi sio mapungufu ni wizi na unatakiwa kwenye sheria, Kitine ni mwizi na ushahidi upo wazi, tena yeye na mkewe, hao viongozi wastaafu kama kuna mwizi lazima anatakwia kwenye sheria, sio kwenye majukwaa ya siasa, Malecela angekuwa mwizi asingekwua na ubavu wa kumuondoa Lowassa, kiongozi mwizi ni mwizi tu hakuna cha mapungufu wala uasherati, ni mwizi period na sheria zetu ziko very clear kuhusu hilo la viongozi wezi kama Kitine.

Thanxs!
 
Gentlemen (and Ladies) wa JF lets try not to get too personal on these discussions, we will lose the context.When it gets too personal wengine inakuwa vigumu kuchangia!
 
Mimi sidhani kama kuna kipya kitatoka ccm, hata ungeamshwa usingizini na kuambiwa ccm wamemjibu kitine ungeweza kuyaandika majibu yoooooote bila hata kuisoma hiyo habari
 
Back
Top Bottom